Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,744
- 25,446
Kariakoo leo asubuhi
Piga picha wakuvamie, wanahasira hao balaa tupu
Nimeona Mwananchi digital wamepost Kariakoo kuna barabara imekuwa nyeupe,vibanda vimetupiliwa mbali.
Sent using Jamii Forums mobile app
Safi.wafanye usafi sasa
Yaani kwa haraka inaonyesha jinsi gani wamachinga walivyochafua jiji, usafi ufanyike jiji liwe safi na barabara zibaki nyeupe sasa Makala kweli wewe ni kiongozi tunakushukuru kwa hili.
Unakumbuka nyumba zilizobomolewa kimara ili kupisha barabara? Mbezi je? Unakumbuka nyumba ya profesa jay ilivyobomolewa?Pumzika kwa amani Jemedari chuma JPM, mzalendo na kiongozi madhubuti.
Mabeberu na Mafisi yamekuondoa mapema sana ingali taifa linahitaji uchapa-kazi wako.
Kila siku naikumbuka ile sauti yako yenye mngurumo wa radi. Kiongozi mwenye kinywa kilichojaa mamlaka na AMRI.
You have gone too soon John!
Mimi nipo huku majimoto mkuu, hapo ni wapi?
Hapo ulipopiga picha kote kulikuwa vibanda?View attachment 1992354
Mbagala Zakiem na Rangi tatu nako mwitikio ni mkubwa
Mwanzaa kazi enaendelea ya kujenga vibanda eneo la dampooView attachment 1995802View attachment 1995803
Upande tu Bus uje ujionee,Habari za humu wanajamii,
Direct madani,
Baada ya songombingo la serikali ya mama samia kusafisha jiji la dar kwa kuwaondoa wamachinga waliokuwa wamejibanza kandokando ya barabara kujitafuta riziki zao kuisha, tunaona asilimia kubwa ya wana dar es salaam kusifia mandhari masafi ya muonekano mpya wa jiji hilo.
Sasa basi, kwa shauku yangu binafsi na ya watu wengine ambao hawapo dar, tunaomba wana dar mtuoneshe kwa mtindo wa picha mandhari mapya na usafi wa dar, baada ya wamachinga kutolewa.
Nawasilisha.
Marashi ya karafuuUpande tu Bus uje ujionee,
Jiji sio tu limekua safi kimuonekano hadi Marashi ya Karafuu tunayapata.
Viva Serikali, Viva Tanzania.