Ramadhan Special Thread
Ameachika Kisha Mume Kamuingilia Baada Ya Mwezi Bila Ya Kumtamkia, Itakuwa Ni Talaka Rejea?
Maswali: Talaka - Eda
SWALI

Assalamu 'alaykum warahmatullah wabarakatu. Mwanamke kuachwa na mume wakatengana kwa muda wa mwezi mmoja baadaye mume akaja akakuingilia bila ya kukutamkia je! Atakuwa amekurejea?



JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu talaka rejea. Hapa dada yetu hukututajia kamwe hiyo talaka ni ya ngapi. Je, ni talaka ya kwanza, ya pili, au ya tatu? Kawaida mwanamke akipatiwa talaka anafaa akae palepale nyumbani kwa mumewe mpaka amalize eda yake.



Kukaa eda pale nyumbani ni kuyarudisha mambo katika hali ya kawaida na pengine kila mmoja aone kuwa amekosa ili hao wawili wapate kurudiana. Ikiwa mume atamwingilia mkewe kabla ya eda kumalizika katika talaka ya kwanza au ya pili, atakuwa mume tayari amemrudia. Lakini ikiwa ni talaka ya tatu hao wanandoa hawawezi kurudiana hivyo itakuwa ni haramu wao kukutana kimwili.



Ikiwa amekuingilia baada ya talaka ya kwanza au ya pili basi atakuwa amekurudia, nawe ni mkewe tena. Linalotakiwa ni mfanye bidii msiwe ni wenye kuachana kwani talaka zikifuatana huenda ikawapeleka nyinyi katika hali hamuwezi tena kurudiana (yaani talaka ya tatu) mpaka uolewe na mume mwingine kisha uachwe.



Na Allaah Anajua zaidi
 
Ameachika Talaka Tatu Bado Anampenda Mumewe Aolewe Na Kuachika Ili Warudiane?
Maswali: Talaka - Eda


SWALI:

Kwanza napenda kumshukuru Allaah kwa kunipa afya na uzima, na la pili napenda kukushukuruni nyote mloiandaa website hii inshAllaah Allaah atakupeni kheir nyingi hapa duniani na akhera ameen.

Napenda kuuliza kwamba mimi ni mwanamke nilieachwa talaka tatu na mume wangu hawezi tena kunirejea tena, hivyo imepita muda sasa na eda yangu imemaliza, kwa bahati nzuri nimepata mume anataka kunioa sasa, lakini mimi bado nampenda sana yule mume wangu wa mwanzo na amesema hata nikiachwa yeye yupo tayari kunioa, hivyo nikubali kuolewa na huyu mume mpya halafu nitake kuachwa kwa ajili ya kurejeana na mume wangu wa mwanzo, jee ndoa hii inasihi? Tafadhali naomba majibu kutoka kwenu (Wabillah tawfiq)




JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Shukrani zetu za dhati kwa swali lako hilo kuhusu talaka. Hatuelewi kabisa mume au mke anayesema ninapendana sana na mwenzangu lakini zikawa talaka zinatoka ya kwanza, ya pili. Baada ya kwamba ya pili imetoka wanandoa hao hawakuweza kutatua matatizo waliyonayo mpaka na ya tatu nayo ikatolewa! Je, kweli hapo kuna mapenzi? Tufahamu kuwa talaka ya tatu inapotolewa wanandoa hao wawili hawawezi kabisa kurudiana mpaka mke aolewe na mume mwengine wakutane kimwili, waachane kikawaida bila ya mkono mwingine kuingia kati. Kwa haya, Allaah Aliyetukuka Anatueleza:

“Talaka ni mara mbili. Kisha ni kukaa kwa wema au kuachana kwa vizuri” (2: 229).



Aayah inayofuata tunaelezwa yafuatayo: “Na kama amempa talaka (ya tatu) basi si halali kwake baada ya hayo mpaka aolewe na mume mwengine. Na akiachwa basi hapana ubaya kwao kurejeana wakiona kuwa watashikamana na mipaka ya Allaah. Na hii ni mipaka ya Allaah Anayoibainisha kwa watu wanaojua” (2: 230).

Tufahamu kuwa si halali kwa mume kumtaka mwanamume mwingine amuoe mtalaka wake kisha amuache. Jambo hilo limelaaniwa kabisa katika sheria, na anayehalalisha na yule anayehalalishiwa wote wana laana ya Allaah Aliyetukuka.

Ama kauli yako ya kuwa ukubali kuolewa na mtu aliyekuja kukuposa kisha utake talaka haifai kabisa kwani kwa kufanya hivyo utakuwa umefanya makosa kadhaa. Mojawapo ni kuwa umemdanganya huyo mume mpya yeye akitarajia kuwa ni mkewe wa kudumu kumbe niya yako ni nyingine. Pia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametahadharisha: “Mwanamke yeyote atakayeomba talaka bila ya sababu yoyote ile hatasikia hata harufu ya Peponi” (Abu Daawuud kutoka kwa Thawbaan [Radhiya Allaahu ‘anhu]).

Ushauri wetu kwako ni kuwa usifanye hivyo bali ikiwa kweli unataka kuolewa na huyo anayekuposa, basi kuwa na niya na kuishi naye milele. Ikiwa itatokea kuwa mume huyo amekuacha basi mume wako akija kukuposa tena utatoa idhini ya yeye akuoe.

Pia inawabidi mjifunze umuhimu wa talaka na si kuichezea kama mlivyofanya kwani matokeo yake ndio haya mahangaiko mliyonayo.

Twakutakia kila la kheri na fanaka.

Na Allaah Anajua zaidi
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب التقوى

006 – Mlango Wa Taqwa – Kumkhofu Allaah



Alhidaaya.com





يَقُولُ اللهُ تَعَالَى:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلَا تَمُوتُنَّ إِلَّا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ

Enyi walioamini! Mcheni Allaah kama apasavyo kuogopwa na wala msife isipokuwa nyinyi (mmeshakuwa) ni Waislaam (wanaojisalimisha kwa Allaah). [Aal-‘Imraan: 102]

فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُم

Basi mcheni Allaah muwezavyo. [At-Taghaabun: 16]



يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا

Enyi walioamini! Mcheni Allaah na semeni kauli nyoofu ya haki. [Al-Ahzaab: 70]



وَمَن يَتَّقِ اللَّـهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا

Na yeyote anayemcha Allaah; Humjaalia njia ya kutoka (shidani).

وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ

Na Atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii. Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza. [At-Twalaaq: 2-3]



يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن تَتَّقُوا اللَّـهَ يَجْعَل لَّكُمْ فُرْقَانًا وَيُكَفِّرْ عَنكُمْ سَيِّئَاتِكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ۗ وَاللَّـهُ ذُو الْفَضْلِ الْعَظِيمِ

Enyi walioamini! Mkimcha Allaah Atakupeni upambanuo wa haki na batili, na Atakufutieni maovu yenu, na Atakughufurieni. Na Allaah ni Mwenye fadhila adhimu. [Al-Anfaal: 29]



Hadiyth – 1



عن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قِيلَ: يَا رسولَ الله، مَنْ أكرمُ النَّاس؟ قَالَ: ((أَتْقَاهُمْ)). فقالوا: لَيْسَ عن هَذَا نسألُكَ، قَالَ: ((فَيُوسُفُ نَبِيُّ اللهِ ابنُ نَبِيِّ اللهِ ابنِ نَبيِّ اللهِ ابنِ خليلِ اللهِ)) قالوا: لَيْسَ عن هَذَا نسألُكَ، قَالَ: ((فَعَنْ مَعَادِنِ العَرَبِ تَسْأَلوني؟ خِيَارُهُمْ في الجَاهِليَّةِ خِيَارُهُمْ في الإِسْلامِ إِذَا فقُهُوا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa: Yaa Rasula-Allaah, ni nani bora katika watu? Akajibu: “Ni yule aliyewazidi kwa kumcha Allaah.” Wakamwambia: Hatukuulizi kuhusu hili. Akawaambia: “Basi ni Yuwusuf Nabiy wa Allaah, Ibn Nabiy wa Allaah, ibn Nabiy wa Allaah, Ibn Khaliyl wa Allaah.” Wakasema: Hatukuulizi kuhusu hili. Akasema: “Mwaniuliza kuhusu koo za Waarabu? Wabora wao katika ujahiliyyah ndio wabora wao katika Uislamu iwapo watafahamu Dini.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth -2



عن أبي سعيد الخدري رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّ الدُّنْيَا حُلْوَةٌ خَضِرةٌ، وإنَّ اللهَ مُسْتَخْلِفُكُمْ فِيهَا فَيَنْظُرَ كَيفَ تَعْمَلُونَ، فَاتَّقُوا الدُّنْيَا وَاتَّقُوا النِّسَاء؛ فإنَّ أَوَّلَ فِتْنَةِ بَنِي إسرائيلَ كَانَتْ في النِّسَاءِ)). رواه مسلم

Abuu Sa’iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika dunia ni tamu rangi ya kijani, Hakika Allaah Amewatawalisha humo ili Awatazame mtakayotenda. Basi ogopeni dunia na waogopeni wanawake; hakika fitnah (mtihani) ya mwanzo kwa wana wa Israiyl ilikuwa ni katika wanawake.” [Muslim]





Hadiyth – 3

عن ابن مسعودٍ رضي الله عنه: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يقول: ((اللَّهُمَّ إنِّي أَسألُكَ الهُدَى، وَالتُّقَى، وَالعَفَافَ، وَالغِنَى)). رواه مسلم

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba: “Ee Rabb, nakuomba uongofu na taqwa na kuepuka mabaya na ukwasi.” [Muslim]





Hadiyth – 4

عن أبي طريفٍ عدِيِّ بن حاتمٍ الطائيِّ رضي الله عنه، قَالَ: سمعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ ثُمَّ رَأَى أتْقَى للهِ مِنْهَا فَليَأتِ التَّقْوَى)). رواه مسلم

Abuu Twariyf ‘Adiyyi bin Haatim At-Twaaiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Atakayeapa yamini kisha akaona linalomridhisha zaidi Allaah kulikoni aliloliapia, basi afanye linalomridhisha Allaah.” [Muslim]





Hadiyth – 5

عن أبي أُمَامَةَ صُدَيّ بنِ عجلانَ الباهِلِيِّ رضي الله عنه قَالَ: سَمِعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يَخْطُبُ في حجةِ الوداعِ، فَقَالَ: ((اتَّقُوا الله وَصلُّوا خَمْسَكُمْ، وَصُومُوا شَهْرَكُمْ، وَأَدُّوا زَكاةَ أَمْوَالِكُمْ، وَأَطِيعُوا أُمَرَاءكُمْ تَدْخُلُوا جَنَّةَ رَبِّكُمْ)). رواه الترمذي، في آخر كتابِ الصلاةِ، وَقالَ: (حديث حسن صحيح)

Abuu Umaamah, Swudayy bin ‘Ajlaan Al-Baahiliyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akikhutubia katika Hajjatil-Widaa’i akasema: “Mcheni Allaaah, swalini Swalaah zenu tano, fungeni Swawm mwezi wenu, toeni Zakaah za mali yenu na watiini viongozi wenu, mtaingia Jannah ya Rabb wenu.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan Swahiyh]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب في اليقين والتوكل

007 - Mlango Wa Yakini Na Kutawakali Kwa Allaah



قَالَ اللهُ تَعَالَى:

وَلَمَّا رَأَى الْمُؤْمِنُونَ الْأَحْزَابَ قَالُوا هَـٰذَا مَا وَعَدَنَا اللَّـهُ وَرَسُولُهُ وَصَدَقَ اللَّـهُ وَرَسُولُهُ ۚ وَمَا زَادَهُمْ إِلَّا إِيمَانًا وَتَسْلِيمًا ﴿٢٢﴾

Basi Waumini walipoona makundi, walisema: “Haya ndio yale Aliyotuahidi Allaah na Rasuli Wake, na Amesema kweli Allaah na Rasuli Wake; na haikuwazidishia isipokuwa iymaan na kujisalimisha. [Al-Ahzaab: 22]





الَّذِينَ قَالَ لَهُمُ النَّاسُ إِنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعُوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إِيمَانًا وَقَالُوا حَسْبُنَا اللَّـهُ وَنِعْمَ الْوَكِيلُ﴿١٧٣﴾

Wale walioambiwa na watu: “Hakika watu wamejumuika dhidi yenu, basi waogopeni” (Haya) Yakawazidishia iymaan; na wakasema: “Allaah Anatutosheleza, Mzuri Alioje Mdhamini Anayetegemewa kwa yote.”



فَانقَلَبُوا بِنِعْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ وَفَضْلٍ لَّمْ يَمْسَسْهُمْ سُوءٌ وَاتَّبَعُوا رِضْوَانَ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ ذُو فَضْلٍ عَظِيمٍ ﴿١٧٤﴾

Basi wakarudi na neema kutoka kwa Allaah na fadhila; halijawagusa ovu lolote; na wakafuatilia radhi za Allaah. Na Allaah ni Mwenye fadhila adhimu. [Aal-‘Imraan: 173-174]



قَالَتْ لَهُمْ رُسُلُهُمْ إِن نَّحْنُ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَمُنُّ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ ۖ وَمَا كَانَ لَنَا أَن نَّأْتِيَكُم بِسُلْطَانٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١١﴾

Rasuli wao wakawajibu: “Sisi si chochote isipokuwa ni watu kama nyinyi, lakini Allaah Anamfadhilisha Amtakaye miongoni mwa waja Wake. Na haikutupasa sisi kukujieni kwa ushahidi isipokuwa kwa idhini ya Allaah. Na kwa Allaah watawakali Waumini. [Ibraahiym: 11]



فَبِمَا رَحْمَةٍ مِّنَ اللَّـهِ لِنتَ لَهُمْ ۖ وَلَوْ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ الْقَلْبِ لَانفَضُّوا مِنْ حَوْلِكَ ۖ فَاعْفُ عَنْهُمْ وَاسْتَغْفِرْ لَهُمْ وَشَاوِرْهُمْ فِي الْأَمْرِ ۖ فَإِذَا عَزَمْتَ فَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ ۚ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُتَوكِّلِينَ ﴿١٥٩﴾

Basi ni kwa rahmah kutoka kwa Allaah umekuwa mpole kwao (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم). Na lau ungelikuwa mjeuri mwenye moyo mgumu wangelitawanyika mbali nawe (wakakukimbia). Basi wasamehe na waombee maghfirah na washauri katika mambo. Na unapoazimia basi tawakali kwa Allaah. Hakika Allaah Anapenda wanaotawakali. [Aal-‘Imraan:159]



وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لَا يَحْتَسِبُ ۚ وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ فَهُوَ حَسْبُهُ ۚ إِنَّ اللَّـهَ بَالِغُ أَمْرِهِ ۚ قَدْ جَعَلَ اللَّـهُ لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا﴿٣﴾

Na Atamruzuku kutoka njia ambayo hatizamii. Na yeyote anayetawakali kwa Allaah, basi Yeye Humtosheleza. Hakika Allaah Anatimiza kusudio Lake. Allaah Amejaalia kwa kila kitu makadirio. [Atw-Twalaaq: 3]



إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ الَّذِينَ إِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَجِلَتْ قُلُوبُهُمْ وَإِذَا تُلِيَتْ عَلَيْهِمْ آيَاتُهُ زَادَتْهُمْ إِيمَانًا وَعَلَىٰ رَبِّهِمْ يَتَوَكَّلُونَ﴿٢﴾

Hakika Waumini ni wale ambao anapotajwa Allaah nyoyo zao, zinajaa khofu na wanaposomewa Aayaat Zake huwazidishia iymaan, na kwa Rabb wao wanatawakali. [Al-Anfaal: 2]



Hadiyth – 1

عن ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((عُرِضَتْ عَلَيَّ الأُمَمُ، فَرَأيْتُ النَّبيّ ومَعَهُ الرُّهَيطُ، والنبي وَمَعَهُ الرَّجُلُ وَالرَّجُلانِ، والنبيَّ ولَيْسَ مَعَهُ أَحَدٌ إِذْ رُفِعَ لي سَوَادٌ عَظيمٌ فَظَنَنْتُ أَنَّهُمْ أُمَّتِي فقيلَ لِي: هَذَا مُوسَى وَقَومُهُ، ولكنِ انْظُرْ إِلَى الأُفُقِ، فَنَظَرتُ فَإِذا سَوادٌ عَظِيمٌ، فقيلَ لي: انْظُرْ إِلَى الأفُقِ الآخَرِ، فَإِذَا سَوَادٌ عَظيمٌ، فقيلَ لِي: هذِهِ أُمَّتُكَ وَمَعَهُمْ سَبْعُونَ ألفًا يَدْخُلُونَ الجَنَّةَ بِغَيرِ حِسَابٍ ولا عَذَابٍ))، ثُمَّ نَهَضَ فَدخَلَ مَنْزِلَهُ فَخَاضَ النَّاسُ في أُولئكَ الَّذِينَ يَدْخُلُونَ الجَنَّةَ بِغَيْرِ حِسَابٍ ولا عَذَابٍ، فَقَالَ بَعْضُهُمْ: فَلَعَلَّهُمْ الَّذينَ صَحِبوا رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، وَقالَ بعْضُهُمْ: فَلَعَلَّهُمْ الَّذِينَ وُلِدُوا في الإِسْلامِ فَلَمْ يُشْرِكُوا بِالله شَيئًا- وذَكَرُوا أشيَاءَ- فَخَرجَ عَلَيْهِمْ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: ((مَا الَّذِي تَخُوضُونَ فِيهِ؟)) فَأَخْبَرُوهُ فقالَ: ((هُمُ الَّذِينَ لا يَرْقُونَ، وَلا يَسْتَرقُونَ، وَلا يَتَطَيَّرُونَ؛ وعَلَى رَبِّهِمْ يَتَوكَّلُون)) فقامَ عُكَّاشَةُ بنُ محصنٍ، فَقَالَ: ادْعُ الله أنْ يَجْعَلني مِنْهُمْ، فَقَالَ: ((أنْتَ مِنْهُمْ)). ثُمَّ قَامَ رَجُلٌ آخَرُ، فَقَالَ: ادْعُ اللهَ أنْ يَجْعَلنِي مِنْهُمْ، فَقَالَ: ((سَبَقَكَ بِهَا عُكَّاشَةُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Nilionyeshwa ummah mbali mbali. Nikamuona Nabiy ana kipote, Nabiy mwengine ana mtu mmoja na wawili, na Nabiy mwengine hana mfuasi. Mara kwa ghafla, nikaonyeshwa kundi kubwa, nikadhani kuwa ni ummah wangu. Nikaambiwa: Huyu ni Muwsaa na Qawmu yake, lakini tazama upande huu. Nikatazama, nikaona kundi kubwa. Nikaambiwa: Tazama upande mwengine. Nikaona kundi kubwa, nikaambiwa: Huu ni Ummah wako, pamoja nao kuna watu sabini elfu wataingia Jannah bila hisabu wala adhabu.” Halafu akainuka na kuingia nyumbani kwake. Watu wakaanza kuzungumza na kujadiliana kuhusu wale watakaoingia Jannah bila hisabu wala adhabu. Baadhi yao wakasema: Labda hao ni wale waliosuhubiana na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Wengine wakasema: Labda hao ni wale waliozaliwa katika Uislamu na wala hawakumshirikisha Allaah na chochote. Wakaongea mambo mengi. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawatokea, akawauliza: “Mlikuwa mnazungumza kuhusu nini?” Wakamueleza. Akawaambia: “Hao ni wale ambao hawazingui (hawafanyi Ruqyyah) wala hawataki kuzinguliwa kutoka kwa mwengine, wala hawapigi ramli na wameegemea kwa Rabb wao tu.” Akasimama ‘Ukaashah bin Mihswan akasema: Muombe Allaah Anijaalie katika wao. Akamwambia: “Wewe ni katika wao.” Kisha akasimama mtu mwengine, akamwambia: Muombe Allaah Anijaalie miongoni mwao. Akamwambia: “Amekutangulia ’Ukaashah (daraja hiyo).” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2

عن ابن عباس رضي الله عنهما أيضًا: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم كَانَ يقول: ((اللَّهُمَّ لَكَ أَسْلَمْتُ، وَبِكَ آمَنْتُ، وَعَليْك تَوَكَّلْتُ، وَإِلَيْكَ أنَبْتُ، وَبِكَ خَاصَمْتُ. اللَّهُمَّ إِنِّي أعُوذُ بعزَّتِكَ؛ لا إلهَ إلا أَنْتَ أنْ تُضلَّني، أَنْتَ الحَيُّ الَّذِي لا يَمُوتُ، وَالجِنُّ والإنْسُ يَمُوتُونَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ، وهذا لفظ مسلم واختصره البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiomba: “Ee Allaah, kwa ajili Yako nimejisalimisha, Kwako tu nimeamini, Wewe pekee nimekutegemea, Kwako tu nimerejea, kwa ajili Yako tu nakhasimiana. Ee Allaah, hakika mimi najilinda kwa utukufu Wako, hakuna Muabudiwa wa haki isipokuwa Wewe, Usinipoteze. Wewe ni Hai Usiekufa, majini na wana-Aadam watakufa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]







Hadiyth – 3

عن ابن عباس رضي الله عنهما أيضًا، قَالَ: حَسْبُنَا اللهُ وَنِعْمَ الوَكِيلُ، قَالَهَا إِبرَاهيمُ صلى الله عليه وسلم حِينَ أُلقِيَ في النَّارِ، وَقَالَها مُحَمَّدٌ صلى الله عليه وسلم حِينَ قَالُوا: إنَّ النَّاسَ قَدْ جَمَعوا لَكُمْ فَاخْشَوْهُمْ فَزَادَهُمْ إيْمانًا وَقَالُوا: حَسْبُنَا الله ونعْمَ الوَكيلُ. رواه البخاري.

وفي رواية لَهُ عن ابن عَبَّاسٍ رضي الله عنهما، قَالَ: كَانَ آخر قَول إبْرَاهِيمَ صلى الله عليه وسلم حِينَ أُلْقِيَ في النَّارِ: حَسْبِي الله ونِعْمَ الوَكِيلُ

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Allaah Anatutosha. Naye ni Mdhamini bora kabisa, neno hili alisema Nabiy Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) alipotumbukizwa motoni, na alisema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) pale watu (walipokodiwa na Maquraysh) walipowaambia (Waislaam): “Maquraysh wamewakusanyikia, kwa hiyo waogopeni. Lakini maneno hayo yaliwazidishia Iymaan (Waislamu) wakasema: Allaah Anatutosha Naye ni Mdhamini bora kabisa.” [Al-Bukhaariy]

Riwaayah nyingine; kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Neno la mwisho alilolitamka Nabiy Ibraahiym (‘Alayhis Salaam) wakati alipotumbukizwa kwenye moto ilikuwa ni kusema: “Allaah Ananitosha, Naye ni Mdhamini bora kabisa.”





Hadiyth – 4

عن أبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((يَدْخُلُ الجَنَّةَ أَقْوامٌ أفْئِدَتُهُمْ مِثلُ أفْئِدَةِ الطَّيرِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna watu wataingia Jannah nyoyo zao ni mithili ya ndege (Kwa ule ulaini wanyoyo za ndege namna zilivyo).” [Muslim]





Hadiyth – 5

عن جابر رضي الله عنه: أَنَّهُ غَزَا مَعَ النبي صلى الله عليه وسلم قِبلَ نَجْدٍ، فَلَمَّا قَفَلَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَفَلَ معَهُمْ، فَأَدْرَكَتْهُمُ القَائِلَةُ في وَادٍ كثير العِضَاه، فَنَزَلَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم وَتَفَرَّقَ النَّاسُ يَسْتَظِلُّونَ بالشَّجَرِ، وَنَزَلَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم تَحتَ سَمُرَة فَعَلَّقَ بِهَا سَيفَهُ وَنِمْنَا نَوْمَةً، فَإِذَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يَدْعونَا وَإِذَا عِنْدَهُ أعْرَابِيٌّ، فَقَالَ: ((إنَّ هَذَا اخْتَرَطَ عَلَيَّ سَيفِي وَأنَا نَائمٌ فَاسْتَيقَظْتُ وَهُوَ في يَدِهِ صَلتًا، قَالَ: مَنْ يَمْنَعُكَ مِنِّي؟ قُلْتُ: الله- ثلاثًا-)) وَلَمْ يُعاقِبْهُ وَجَلَسَ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية قَالَ جَابرٌ: كُنَّا مَعَ رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم بذَاتِ الرِّقَاعِ، فَإِذَا أَتَيْنَا عَلَى شَجَرَةٍ ظَلِيلَةٍ تَرَكْنَاهَا لرسول الله صلى الله عليه وسلم، فجاء رَجُلٌ مِنَ المُشْركينَ وَسَيفُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم معَلَّقٌ بالشَّجَرَةِ فَاخْتَرطَهُ، فَقَالَ: تَخَافُنِي؟ قَالَ: ((لا)). فَقَالَ: فَمَنْ يَمْنَعُكَ مِنِّي؟ قَالَ: ((الله)).

وفي رواية أبي بكر الإسماعيلي في صحيحه، قَالَ: مَنْ يَمْنَعُكَ مِنِّي؟ قَالَ: ((اللهُ)). قَالَ: فَسَقَطَ السيفُ مِنْ يَدهِ، فَأخَذَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم السَّيْفَ، فَقَالَ: ((مَنْ يَمْنَعُكَ مني؟)). فَقَالَ: كُنْ خَيرَ آخِذٍ. فَقَالَ: ((تَشْهَدُ أنْ لا إلهَ إلا الله وَأَنِّي رَسُول الله؟)) قَالَ: لا، وَلَكنِّي أُعَاهِدُكَ أنْ لاَ أُقَاتِلَكَ، وَلا أَكُونَ مَعَ قَومٍ يُقَاتِلُونَكَ، فَخَلَّى سَبيلَهُ، فَأَتَى أصْحَابَهُ، فَقَالَ: جئتُكُمْ مِنْ عنْد خَيْرِ النَّاسِ.

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia kuwa yeye alikwenda kupigana Jihaad sehemu za Najd akiwa pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliporejea, alirejea pamoja nao. Ikawakuta katikati ya mchana katika bonde lenye miti mingi ya miba. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akashuka. Wa nao wakaenea (huku na kule) wakitafuta vivuli vya miti. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alishuka chini ya mti wa samura (aina ya mti wenye miba), akautundika upanga wake, tukalala kidogo. Mara ghafla Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akatuita, akawa yupo na mbedui, akatuambia: “Mtu huyo kauchomoa upanga wangu nami nimelala, nikaamka nao upo mkononi mwake, akaniuliza: Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu? Nikamjibu: “Allaah mara tatu.” Wala hakumuadhibu, akaketi. [Al-Bukhaariy na Muslim]



Riwaayah nyingine inasema: “Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Tulikuwa pamoja na Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) huko Dhaatir-Riqaa’, tunapofika kwenye mti wenye kivuli, humuachia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Akaja mtu katika mushrikiyn na upanga wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) umetundikwa kwenye mti. Akauchomoa, akamuuliza: Unaniogopa? Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamjibu: “Hapana” Akamuuliza: Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu? Akamwambia: “Allaah”.



Riwaayah nyingine ya; Abuu Bakr Al-Ismaa’iyl katika sahihi yake, imesema: Akamuuliza: Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu? Akamwambia: “Allaah” Upanga ukamuanguka kutoka mkononi mwake. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akauchukua upanga ule. Akamuuliza: “Ni nani atakaye kuhami dhidi yangu?” Akamjibu: Mbora mwenye kuuchukua. Akamuuliza: “Unashuhudia kuwa hakuna Anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allaah na kuwa mimi ni Rasuli Wake?” Akajibu: Hapana. Lakini nakuahidi kuwa sitakupiga vita, wala sitokuwa pamoja na watu wanaopigana na wewe. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuacha aende zake. Akawaendea Maswahaba zake, akawaambia: “Nimewajia kutoka kwa mbora wa watu.”





Hadiyh – 6

عن عُمَر رضي الله عنه قَالَ: سمعتُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يقول: ((لَوْ أَنَّكُمْ تَتَوَكَّلُونَ عَلَى اللهِ حَقَّ تَوَكُّلِهِ لَرَزَقَكُمْ كَمَا يَرْزُقُ الطَّيْرَ، تَغْدُو خِمَاصًا وَتَرُوحُ بِطَانًا)). رواه الترمذي، وَقالَ: (حديث حسن)

‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nimemsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Lau mngelikuwa mnamtegemea Allaah ukweli wa kumtegemea, Angewaruzuku kama Anavyowaruzuku ndege. Wanatoka asubuhi wakiwa wana njaa na wanarudi wakiwa wameshiba.” [At-Tirmidhiy, na amesema: Hadiyth hii ni Hasan]





Hadiyth – 7

عن أبي عُمَارة البراءِ بن عازب رضي الله عنهما، قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا فُلانُ، إِذَا أَوَيْتَ إِلَى فراشِكَ، فَقُل: اللَّهُمَّ أسْلَمتُ نَفْسي إلَيْكَ، وَوَجَّهتُ وَجْهِي إلَيْكَ، وَفَوَّضتُ أَمْري إلَيْكَ، وَأَلجأْتُ ظَهري إلَيْكَ رَغبَةً وَرَهبَةً إلَيْكَ، لا مَلْجَأ وَلا مَنْجَا مِنْكَ إلا إلَيْكَ، آمنْتُ بِكِتَابِكَ الَّذِي أنْزَلْتَ؛ وَنَبِيِّكَ الَّذِي أَرْسَلْتَ. فَإِنَّ مِتَّ مِنْ لَيلَتِكَ مِتَّ عَلَى الفِطْرَةِ، وَإِنْ أصْبَحْتَ أَصَبْتَ خَيرًا)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية في الصحيحين، عن البراءِ، قَالَ: قَالَ لي رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا أَتَيْتَ مَضْجِعَكَ فَتَوَضَّأْ وُضُوءكَ للصَّلاةِ، ثُمَّ اضْطَجعْ عَلَى شِقِّكَ الأَيمَنِ، وَقُلْ... وذَكَرَ نَحْوَهُ ثُمَّ قَالَ: وَاجْعَلْهُنَّ آخِرَ مَا تَقُولُ))

Abuu ‘Umaarah Al-Baraa bin ‘Aazib (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia mtu: “Ee fulani utakapokiendea kitanda chako, sema: Ee Allaah, nimejisalimisha Kwako, uso wangu nimeuwelekeza Kwako, mambo yangu nimekuachia Wewe, nimekuegemeza Wewe kwa kutaraji thawabu Zako na kuogopa dhambi Zako, hakuna sehemu ya kuegemea wala kukuepuka ila ni Kwako. Nimekiamini Kitabu Chako Ulichokiteremsha na Rasuli Wako Uliyemtuma. Basi utakapofikwa na mauti usiku huo, utakuwa umekufa katika Uislamu, na ukipambaukiwa utapata khayr.” [Al-Bukhaariy na Muslim]



Riwaayah nyingine iliyomo katika Sahihi Al-Bukhaariy na Sahihi Muslim; kutoka kwa Al-Baraa imesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliniambia: “Unapokwenda sehemu yako ya kulala, tawadha wudhuu wa Swalaah, kisha ulale kwa upande wako wa kulia na usema: (Akajata mfano wake kama ilivyotangulia) “Maneno hayo ndiyo yawe ya mwisho utakayoyasema.”





Hadiyth – 8

عن أبي بكرٍ الصِّديق رضي الله عنه عبدِ اللهِ بنِ عثمان بنِ عامرِ بنِ عمر ابنِ كعب بنِ سعدِ بن تَيْم بنِ مرة بن كعبِ بن لُؤَيِّ بن غالب القرشي التيمي رضي الله عنه وَهُوَ وَأَبُوهُ وَأُمُّهُ صَحَابَةٌ رضي الله عنهم قَالَ: نَظَرتُ إِلَى أَقْدَامِ المُشْرِكينَ وَنَحنُ في الغَارِ وَهُمْ عَلَى رُؤُوسِنا، فقلتُ: يَا رسولَ الله، لَوْ أَنَّ أَحَدَهُمْ نَظَرَ تَحْتَ قَدَمَيهِ لأَبْصَرَنَا. فَقَالَ: ((مَا ظَنُّكَ يَا أَبا بَكرٍ باثنَيْنِ الله ثَالِثُهُمَا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Bakr As-Swidiyq, ‘Abdullaah ‘Uthmaan bin ‘Aamir bin ‘Umar bin Ka’b bin Sa’d bin Taym bin Murrah bin Ka’b bin Lu-ayy bin Ghaalib Al-Qurashiy At-Taymiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) yeye, baba yake na mama yake wote ni maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum) amesema: Niliitazama miguu ya mshirikina nasi tupo pangoni nao wapo juu yetu (wanatutafuta ili watuue). Nikamwambia: Yaa Rasula-Allaah, lau mmoja wao atautazama mguu wake atatuona! Akasema: “Ee Abuu Bakr, unadhaniaje watu wawili ambao watatu wao ni Allaah?” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 9

عن أم المُؤمنينَ أمِّ سَلَمَةَ وَاسمها هِنْدُ بنتُ أَبي أميةَ حذيفةَ المخزومية رضي الله عنها: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ إِذَا خَرَجَ مِنْ بَيتِهِ، قَالَ: ((بِسْمِ اللهِ تَوَكَّلتُ عَلَى اللهِ، اللَّهُمَّ إِنِّي أعُوذُ بِكَ أنْ أضِلَّ أَوْ أُضَلَّ، أَوْ أَزِلَّ أَوْ أُزَلَّ، أَوْ أظْلِمَ أَوْ أُظْلَمَ، أَوْ أجْهَلَ أَوْ يُجْهَلَ عَلَيَّ)) حديثٌ صحيح، رواه أبو داود والترمذي وغيرهما بأسانيد صحيحةٍ. قَالَ الترمذي: (حديث حسن صحيح). وهذا لفظ أبي داود

Mama wa Waumini, Ummu Salamah, jina lake ni Hindu bint Abiy Umayyah Hudhayfah Al-Makhzumiyyah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapotoka nyumbani kwake husema: “Kwa jina la Allaah, Nimeegemea kwa Allaah. Ee Allaah, kwa hakika najilinda Kwako nisije nikapotea au kupotezwa, au nikateleza au nikatelezeshwa, au nikadhumu au nikadhulumiwa au nikafanya ujinga au nikafanyiwa ujinga.” [Hadiyth hii, ni Sahihi imepokelewa na Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy na wengineo kwa isnaad Sahihi. At-Tirmidhiy amesema: Hadiyth hii ni Hasan Sahih]





Hadiyth – 10

عن أنس رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَالَ- يَعْني: إِذَا خَرَجَ مِنْ بَيتِهِ: بِسمِ اللهِ تَوَكَّلْتُ عَلَى اللهِ، وَلا حَولَ وَلا قُوَّةَ إلا باللهِ، يُقالُ لَهُ: هُدِيتَ وَكُفِيتَ وَوُقِيتَ، وَتَنَحَّى عَنْهُ الشَّيطَانُ)). رواه أبو داود والترمذي والنسائي وغيرهم. وَقالَ الترمذي: (حديث حسن)، زاد أبو داود: ((فيقول- يعني: الشيطان-- لِشيطان آخر: كَيفَ لَكَ بِرجلٍ قَدْ هُدِيَ وَكُفِيَ وَوُقِيَ؟))

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayesema anapotoka nyumbani kwake. Kwa jina la Allaah nimeegemea kwa Allaah, hakuna namna ya kuepuka maasi wala nguvu ya kufanya ‘Ibaadah ila kwa msaada wa Allaah. Ataambiwa: Umeshaongozwa, umeshatoshelezwa, na umeshakingwa, na shaytwaan hujitenga naye.” [Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na wengineo. At-Tirmidhiy amesema: Hadiyth hii ni Hasan]

Abuu Daawuwd ameongezea: Shaytwaan humueleza shaytwaan mwenzie: Utamuwezaje mtu aliyeongozwa, akatoshelezwa na akakingwa?







Hadiyth – 11

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: كَانَ أَخَوانِ عَلَى عهد النَّبيّ صلى الله عليه وسلم وَكَانَ أحَدُهُمَا يَأتِي النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم وَالآخَرُ يَحْتَرِفُ، فَشَكَا المُحْتَرِفُ أخَاهُ للنبي صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: ((لَعَلَّكَ تُرْزَقُ بِهِ)). رواه الترمذي بإسناد صحيحٍ عَلَى شرطِ مسلم

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Kulikuwepo ndugu wawili zama za Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), mmoja alikuwa akienda kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) (na kukaa naye), na mwengine anafanya kazi; yule anayefanya kazi akamshitakia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) dhidi ya ndugu yake, Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Pengine wewe unaruzukiwa kwa sababu yake.” [At-Tirmidhiy kwa isnaad Swahiyh]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

باب الاستقامة

008 - Mlango Wa Istiqaamah - Kuthibitika Imara (Kuwa Na Msimamo)



Alhidaaya.com



قَالَ اللهُ تَعَالَى:

فَاسْتَقِمْ كَمَا أُمِرْتَ

Basi thibitika imara kama ulivyoamrishwa. [Huwd: 112]



إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا تَتَنَزَّلُ عَلَيْهِمُ الْمَلَائِكَةُ أَلَّا تَخَافُوا وَلَا تَحْزَنُوا وَأَبْشِرُوا بِالْجَنَّةِ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿٣٠﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara; Malaika huwateremkia (wanapofishwa kuwaambia): “Msikhofu, na wala msihuzunike, na pokeeni bishara njema ya Jannah ambayo mlikuwa mkiahidiwa.”



نَحْنُ أَوْلِيَاؤُكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَشْتَهِي أَنفُسُكُمْ وَلَكُمْ فِيهَا مَا تَدَّعُونَ ﴿٣١﴾

“Sisi ni walinzi wenu katika uhai wa dunia na katika Aakhirah. Na mtapata humo yale yanayotamani nafsi zenu, na mtapata humo yale mtakayoomba. [Fusw-swilat: 30-31]



إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴿١٣﴾

Hakika wale waliosema: “Rabb wetu ni Allaah.” Kisha wakathibitika imara, basi hakutokuwa na khofu juu yao, na wala hawatohuzunika.



أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٤﴾

Hao ndio watu wa Jannah, ni wenye kudumu humo, jazaa kwa yale waliyokuwa wakitenda. [Al-Ahqaaf: 13-14]





Hadiyth – 1



وعن أبي عمرو، وقيل: أبي عَمرة سفيان بن عبد الله رضي الله عنه قَالَ: قُلْتُ: يَا رَسُول الله، قُلْ لي في الإسْلامِ قَولًا لا أسْأَلُ عَنْهُ أَحَدًا غَيْرَكَ. قَالَ: ((قُلْ: آمَنْتُ بِاللهِ، ثُمَّ استَقِمْ)). رواه مسلم

Abuu ‘Amru, au Abuu 'Amrah Sufyaan bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimwambia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam); niambie neno katika Uislamu ambalo sitamuuliza yoyote zaidi yako. Akasema: “Sema: Nimemuamini Allaah, kisha uthibitike imara.” [Muslim]





Hadiyth – 2



وعن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((قَارِبُوا وَسَدِّدُوا، وَاعْلَمُوا أَنَّهُ لَنْ يَنْجُوَ أَحَدٌ مِنْكُمْ بعَمَلِهِ)) قالُوا: وَلا أَنْتَ يَا رَسُول الله؟ قَالَ: ((وَلا أنا إلا أنْ يَتَغَمَّدَني الله برَحمَةٍ مِنهُ وَفَضْلٍ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Alisema: “Fanyeni wastani (msivuke mipaka) na muwe na msimamo. Jueni kwamba hakuna yeyote yule miongoni mwenu atakayeokoka na 'amali yake.” Maswahaba wakamuuliza: Hata wewe ee Rasuli wa Allaah? Akajibu: “Hata mimi, isipokuwa Allaah Anifunike kwa rahmah na fadhila Zake.” [Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب التفكر في عظيم مخلوقات الله تَعَالَى، وفناء الدنيا وأهوال الآخرة وسائر أمورهما وتقصير النفس، وتهذيبها وحملها عَلَى الاستقامة



009 – Mlango Wa Kutafakari Viumbe ‘Adhiym Vya Allaah, Dunia Kutoweka – Vitisho Vya Aakhirah Na Mambo Mengine Yanayohusiana Nayo Nafsi Kufanya Taqswiyr, Kuiadabisha Nafsi Na Kuifanya Iwe Na Msimamo



قَالَ اللهُ تَعَالَى:

قُلْ إِنَّمَا أَعِظُكُم بِوَاحِدَةٍ ۖ أَن تَقُومُوا لِلَّـهِ مَثْنَىٰ وَفُرَادَىٰ ثُمَّ تَتَفَكَّرُوا ۚ

Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika nakuwaidhini kwa jambo moja tu! Msimame kwa ajili ya Allaah wawili wawili, au mmoja mmoja kisha mtafakari.” [Sabaa: 46]



إِنَّ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَاخْتِلَافِ اللَّيْلِ وَالنَّهَارِ لَآيَاتٍ لِّأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿١٩٠﴾

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi, na mabadiliko (ya mfuatano) ya usiku na mchana; bila shaka ni Aayaat (ishara, dalili, zingatio n.k) kwa wenye akili.



الَّذِينَ يَذْكُرُونَ اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِهِمْ وَيَتَفَكَّرُونَ فِي خَلْقِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ رَبَّنَا مَا خَلَقْتَ هَـٰذَا بَاطِلًا سُبْحَانَكَ فَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴿١٩١﴾

Ambao wanamdhukuru Allaah (kwa) kusimama, na (kwa) kukaa na (kwa) kulala ubavuni mwao na wanatafakari katika kuumbwa mbingu na ardhi (wakisema): “Rabb wetu, Hukuumba haya bure. Subhaanak! (Utakasifu ni Wako!) Tukinge na adhabu ya moto. [Aal-‘Imraan: 190-191]



أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى الْإِبِلِ كَيْفَ خُلِقَتْ ﴿١٧﴾

Je, hawamtazami ngamia namna walivyoumbwa?



وَإِلَى السَّمَاءِ كَيْفَ رُفِعَتْ ﴿١٨﴾

Na mbingu vipi zilivyonyanyuliwa?



وَإِلَى الْجِبَالِ كَيْفَ نُصِبَتْ ﴿١٩﴾

Na majabali vipi yamekongomewa imara.



وَإِلَى الْأَرْضِ كَيْفَ سُطِحَتْ ﴿٢٠﴾

Na ardhi vipi ilivyotandazwa?



فَذَكِّرْ إِنَّمَا أَنتَ مُذَكِّرٌ ﴿٢١﴾

Basi kumbusha (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم); hakika wewe ni mkumbushaji tu. [Al-Ghaashiyah: 17-21]



أَفَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ

Je, hawakutembea katika ardhi wakatazama vipi imekuwa hatima ya ambao wa kabla yao? [Muhammad: 10]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب المبادرة إلى الخيرات، وحثِّ من توجه لخير على الإقبال عليه بالجد من غير تردد

010 – Mlango Wa Kukimbilia Mambo ya Khayr Na Kumuhimiza Anayefanya Khayr Kuielekea Kwa Jitihada Bila Kusitasita



Alhidaaya.com



قَالَ اللهُ تَعَالَى:

فَاسْتَبِقُوا الْخَيْرَاتِ ۚ

Basi shindaneni kwenye khayraat. [Al-Baqarah: 148]



وَسَارِعُوا إِلَىٰ مَغْفِرَةٍ مِّن رَّبِّكُمْ وَجَنَّةٍ عَرْضُهَا السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ أُعِدَّتْ لِلْمُتَّقِينَ ﴿١٣٣﴾

Na kimbilieni maghfirah kutoka kwa Rabb wenu na Jannah upana wake ni wa mbingu na ardhi imeandaliwa kwa wenye taqwa. [Aal-‘Imraan: 133]





Hadiyth – 1

عن أبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((بَادِرُوا بِالأعْمَال فتنًا كقطَعِ اللَّيْلِ المُظْلِمِ، يُصْبحُ الرَّجُلُ مُؤْمِنًا وَيُمْسِي كَافِرًا، وَيُمْسِي مُؤمِنًا ويُصبحُ كَافِرًا، يَبيعُ دِينَهُ بعَرَضٍ مِنَ الدُّنيا)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Zikimbilieni ‘amali njema kwani zitakuja fitnah (nyingi) kama mfano wa usiku na kiza. Mtu atapambaukiwa akiwa Muumin na akifikiwa na jioni hali ya kuwa ni kafiri, au atafikiwa jioni akiwa Muumin na atapambaukiwa akiwa kafiri, anaiuza Dini yake kwa thamani ya dunia.” [Muslim]





Hadiyth – 2

عن أبي سِروْعَة- بكسر السين المهملة وفتحها- عُقبةَ بن الحارث رضي الله عنه قَالَ: صَلَّيتُ وَرَاءَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم بالمَدِينَةِ العَصْرَ، فَسَلَّمَ ثُمَّ قَامَ مُسْرِعًا، فَتَخَطَّى رِقَابَ النَّاسِ إِلَى بعْضِ حُجَرِ نِسَائِهِ، فَفَزِعَ النَّاسُ مِنْ سُرْعَتِهِ، فَخَرَجَ عَلَيهمْ، فَرأى أنَّهمْ قَدْ عَجبُوا مِنْ سُرعَتهِ، قَالَ: ((ذَكَرتُ شَيئًا مِنْ تِبرٍ عِندَنَا فَكَرِهتُ أنْ يَحْبِسَنِي فَأمَرتُ بِقِسْمَتِهِ)). رواه البخاري.

وفي رواية لَهُ: ((كُنتُ خَلَّفتُ في البَيْتِ تِبرًا مِنَ الصَّدَقةِ فَكَرِهتُ أنْ أُبَيِّتَهُ)). ((التِّبْرُ))

Abuu Sirw’ah, ‘Uqbah bin Al-Haarith (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Niliswali nyuma ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Swalaah ya Al-‘Aswr Madiynah. Akatoa salaam kisha akainuka kwa haraka, akawa anaziruka shingo za watu kuelekea katika chumba cha mkewe. Watu wakapata mshangao kwa ile haraka yake. Kisha akawatokezea na kuwaona wamemstajabu kwa ile haraka yake, akawaambia: “Nilikumbuka kitu katika kipande cha dhahabu kilichokuwa kwetu, nikakichukua kisije kikanizuia, nikaamuru kigawanywe.” [Al-Bukhaariy]



Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema:

“Nilikuwa nimeacha nyumbani kipande cha dhahabu cha Swadaqah, nikachukia kisije kikapitiwa na usiku (nacho kipo nyumbani).”





Hadiyth – 3

عن جابر رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رجل للنبي صلى الله عليه وسلم يَومَ أُحُد: أَرَأيتَ إنْ قُتِلتُ فَأَيْنَ أَنَا؟ قَالَ: ((في الجنَّةِ)) فَأَلْقَى تَمَرَاتٍ كُنَّ في يَدِهِ، ثُمَّ قَاتَلَ حَتَّى قُتِلَ. مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: mtu mmoja alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) siku ya Vita vya Uhud: Niambie nikiuliwa nitakwenda wapi? Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamjibu: “Jannah.” Akazitupa tende chache alizokuwa nazo mkononi mwake, kisha akapigana mpaka akauliwa. [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 4

عن أبي هريرة رضي الله عنه، قَالَ: جاءَ رَجُلٌ إِلَى النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: يَا رسولَ الله، أيُّ الصَّدَقَةِ أعْظَمُ أجْرًا؟ قَالَ: ((أنْ تَصَدَّقَ وَأنتَ صَحيحٌ شَحيحٌ، تَخشَى الفَقرَ وتَأمُلُ الغِنَى، وَلا تُمهِلْ حَتَّى إِذَا بَلَغتِ الحُلقُومَ قُلْتَ لِفُلان كذا ولِفُلانٍ كَذا، وقَدْ كَانَ لِفُلانٍ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Mtu mmoja alikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza: Yaa Rasula-Allaah, ni swadaqah ipi yenye ujira mkubwa zaidi? Akajibu: “Utoe swadaqah nawe ni mzima, unatamani mali na unakhofia ufakiri na unatarajia utajiri, wala usichelewe mpaka roho ikafika kwenye koo, ukaanza kusema: Fulani ana haki kadhaa na fulani ana haki kadhaa, na fulani alikuwa ana haki kadhaa.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 5

عن أنس رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم أخذ سيفًا يَومَ أُحُدٍ، فَقَالَ: ((مَنْ يَأخُذُ منِّي هَذَا؟)) فَبَسطُوا أيدِيَهُمْ كُلُّ إنسَانٍ مِنْهُمْ يقُولُ: أَنَا أَنَا. قَالَ: ((فَمَنْ يَأخُذُهُ بحَقِّه؟)) فَأَحْجَمَ القَومُ فَقَالَ أَبُو دُجَانَةَ رضي الله عنه: أنا آخُذُهُ بِحَقِّهِ، فأخذه فَفَلقَ بِهِ هَامَ المُشْرِكِينَ. رواه مسلم

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) anaelezea kuwa: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alichukua upanga siku ya Vita vya Uhud. Akauliza: “Ni nani atakayeuchukua upanga huu kutoka kwangu?” Kila mmoja wao akanyoosha mkono akisema: Mimi, mimi. Akawauliza: “Ni nani atakayeuchukua kwa haki yake?” Watu wakasita. Abuu Dujaanah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: Mimi nitauchukua kwa haki yake. Akauchukua, akawa anakata vichwa vya washirikina (katika Jihaad). [Muslim]





Hadiyth – 6

عن الزبير بن عدي، قَالَ: أتينا أنسَ بن مالك رضي الله عنه فشكونا إِلَيْه مَا نلقى مِنَ الحَجَّاجِ. فَقَالَ: ((اصْبرُوا؛ فَإنَّهُ لا يَأتي عَلَيْكُم زَمَانٌ إلا والَّذِي بَعدَهُ شَرٌّ مِنهُ حَتَّى تَلقَوا رَبَّكُمْ)) سَمِعتُهُ مِنْ نَبِيِّكُمْ صلى الله عليه وسلم. رواه البخاري

Az-Zubayr bin ‘Adiyy amesema: Tulimuendea Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) tukamlalamikia hali tuliyoipata kwa Al-Hajjaaj. Akatuambia: Subirini, hakika haiji zama ila zama zilizokuja baadaye ni shari kulikoni zilizopita mpaka mkutane na Rabb wenu. Maneno haya nimeyasikia kutoka kwa Nabiy wenu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 7

عن أبي هريرة رضي الله عنه: أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((بادِرُوا بِالأَعْمَالِ سَبْعًا، هَلْ تَنْتَظِرُونَ إلا فَقرًا مُنسيًا، أَوْ غِنىً مُطغِيًا، أَوْ مَرَضًا مُفسِدًا، أَوْ هَرَمًا مُفْندًا، أَوْ مَوتًا مُجْهزًا، أَوْ الدَّجَّالَ فَشَرُّ غَائِبٍ يُنْتَظَرُ، أَوْ السَّاعَةَ فالسَّاعَةُ أدهَى وَأَمَرُّ)). رواه الترمذي، وَقالَ: (حديث حسن)

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Zikimbilieni ‘amali njema kabla haijawafikia mambo saba. Je, mnangoja mpaka mfikwe na ufukara wenye kusahaulisha, au utajiri unaopoteza, au maradhi yenye kufisidi, au uzee uletao udhaifu wa akili, au mauti ya ghafla, au Dajjaal ambaye ndio kiumbe muovu asiyepaswa kusubiriwa, au Qiyaamah, na Qiyaamah ndio chenye balaa kubwa na uchungu mwingi zaidi!” [A-Tirmidhiy, na amesema Hadiyth hii ni Hasan]





Hadiyth – 8

أن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ يَومَ خيبر: ((لأُعْطِيَنَّ هذِهِ الرَّايَةَ رَجُلًا يُحِبُّ اللهَ وَرَسُولَهُ يَفتَحُ اللهُ عَلَى يَدَيهِ)). قَالَ عُمَرُ رضي الله عنه: مَا أحبَبْتُ الإِمَارَة إلا يَومَئِذٍ، فَتَسَاوَرتُ لَهَا رَجَاءَ أنْ أُدْعَى لَهَا، فَدَعا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عليّ بن أبي طالب رضي الله عنه فَأعْطَاهُ إيَّاهَا، وَقالَ: ((امْشِ وَلا تَلتَفِتْ حَتَّى يَفتَح اللهُ عَلَيكَ)). فَسَارَ عليٌّ شيئًا ثُمَّ وَقَفَ ولم يلتفت فصرخ: يَا رَسُول الله، عَلَى ماذا أُقَاتِلُ النّاسَ؟ قَالَ: ((قاتِلْهُمْ حَتَّى يَشْهَدُوا أنْ لا إله إلا اللهُ، وَأنَّ مُحَمدًا رسولُ الله، فَإِذَا فَعَلُوا ذلك فقَدْ مَنَعوا مِنْكَ دِمَاءهُمْ وَأَمْوَالَهُمْ إلا بحَقِّهَا، وحسَابُهُمْ عَلَى الله)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema siku ya Vita vya Khaybar: “Kwa hakika bendera hii nitampa mtu anayempenda Allaah na Rasuli Wake, Allaah Ataleta ushindi kwa sababu yake.” ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) anasema: Sikuwahi kuupenda uamiri jeshi isipokuwa siku hiyo. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamuita ‘Aliy bin Abiy Twaalib, akampa bendera ile. Akamwambia: “Nenda wala usigeuke mpaka Allaah Akupe ushindi.” ‘Aliy akatembea kidogo. Kisha akasimama wala hakugeuka nyuma, akauliza kwa sauti ya juu: Yaa Rasula-Allaah, nipigane na watu juu ya nini? Akamwambia: “Pigana nao mpaka washuhudie kuwa hapana Muabudiwa wa haki ispokuwa Allaah, na Muhammad ni Rasuli wa Allaah. Wakifanya hivyo, wameshahifadhika kutokana na nawe katika damu zao na mali yao ila kwa haki yake, na hisabu yao ipo kwa Allaah.”
 
Hizi ni baadhi ya post zangu za zamani

JE QUR'AN NI NAKALA YA BIBLIA?

UUMBAJI WA MBINGU NA ARDHI


Ni mara nyingi Ulaya na humu JF watu wamekuwa wakileta hoja kuwa Muhammad amekopi Biblia katika Maandiko ya Qur'an, lakini kibaya Zaidi wanasema maneno Bila kuthibitisha. Kwahiyo hawana tofauti na watu ambao wanaweweseka Tu na mambo ambayo hawayajui.

Nimeona nilete hoja Kwa kuthibitisha kupitia Maandiko ili tuwatoe uchafu katika ubongo wao.
Sasa nitaanza na Biblia,katika biblia uumbaji wa Mbingu na Ardhi umeelezwa Kwa mfulululizo wa story,kwamba siku ya Kwanza kuliumbwa hiki na ya pili hiki na kadhalika. Tuone Maandiko yanasemaje:

Mwanzo 1:1-31
[1]Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
In the beginning God created the heaven and the earth.

[2]Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.
And the earth was without form, and void; and darkness was upon the face of the deep. And the Spirit of God moved upon the face of the waters.

[3]Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru.
And God said, Let there be light: and there was light.

[4]Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema; Mungu akatenga nuru na giza.
And God saw the light, that it was good: and God divided the light from the darkness.

[5]Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku moja.
And God called the light Day, and the darkness he called Night. And the evening and the morning were the first day.

[6]Mungu akasema, Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.
And God said, Let there be a firmament in the midst of the waters, and let it divide the waters from the waters.

[7]Mungu akalifanya anga, akayatenga yale maji yaliyo juu ya anga na yale maji yaliyo chini ya anga; ikawa hivyo.
And God made the firmament, and divided the waters which were under the firmament from the waters which were above the firmament: and it was so.

[8]Mungu akaliita lile anga Mbingu. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya pili.
And God called the firmament Heaven. And the evening and the morning were the second day.

[9]Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo.
And God said, Let the waters under the heaven be gathered together unto one place, and let the dry land appear: and it was so.

[10]Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
And God called the dry land Earth; and the gathering together of the waters called he Seas: and God saw that it was good.

[11]Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo.
And God said, Let the earth bring forth grass, the herb yielding seed, and the fruit tree yielding fruit after his kind, whose seed is in itself, upon the earth: and it was so.

[12]Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
And the earth brought forth grass, and herb yielding seed after his kind, and the tree yielding fruit, whose seed was in itself, after his kind: and God saw that it was good.

[13]Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tatu.
And the evening and the morning were the third day.

[14]Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka;
And God said, Let there be lights in the firmament of the heaven to divide the day from the night; and let them be for signs, and for seasons, and for days, and years:

[15]tena iwe ndiyo mianga katika anga la mbingu itie nuru juu ya nchi; ikawa hivyo.
And let them be for lights in the firmament of the heaven to give light upon the earth: and it was so.

[16]Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia.
And God made two great lights; the greater light to rule the day, and the lesser light to rule the night: he made the stars also.

[17]Mungu akaiweka katika anga la mbingu, itie nuru juu ya nchi
And God set them in the firmament of the heaven to give light upon the earth,

[18]na kuutawala mchana na usiku na kutenga nuru na giza; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
And to rule over the day and over the night, and to divide the light from the darkness: and God saw that it was good.

[19]Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya nne.
And the evening and the morning were the fourth day.

[20]Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu.
And God said, Let the waters bring forth abundantly the moving creature that hath life, and fowl that may fly above the earth in the open firmament of heaven.

[21]Mungu akaumba nyangumi wakubwa, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho, ambavyo maji yalijawa navyo kwa wingi kwa jinsi zao, na kila ndege arukaye, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
And God created great whales, and every living creature that moveth, which the waters brought forth abundantly, after their kind, and every winged fowl after his kind: and God saw that it was good.

[22]Mungu akavibarikia, akisema, Zaeni, mkaongezeke, mkayajaze maji ya baharini, ndege na wazidi katika nchi.
And God blessed them, saying, Be fruitful, and multiply, and fill the waters in the seas, and let fowl multiply in the earth.

[23]Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya tano.
And the evening and the morning were the fifth day.

[24]Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo.
And God said, Let the earth bring forth the living creature after his kind, cattle, and creeping thing, and beast of the earth after his kind: and it was so.

[25]Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
And God made the beast of the earth after his kind, and cattle after their kind, and every thing that creepeth upon the earth after his kind: and God saw that it was good.

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
And God said, Let us make man in our image, after our likeness: and let them have dominion over the fish of the sea, and over the fowl of the air, and over the cattle, and over all the earth, and over every creeping thing that creepeth upon the earth.

[27]Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
So God created man in his own image, in the image of God created he him; male and female created he them.

[28]Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.
And God blessed them, and God said unto them, Be fruitful, and multiply, and replenish the earth, and subdue it: and have dominion over the fish of the sea, and over the fowl of the air, and over every living thing that moveth upon the earth.

[29]Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;
And God said, Behold, I have given you every herb bearing seed, which is upon the face of all the earth, and every tree, in the which is the fruit of a tree yielding seed; to you it shall be for meat.

[30]na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo.
And to every beast of the earth, and to every fowl of the air, and to every thing that creepeth upon the earth, wherein there is life, I have given every green herb for meat: and it was so.

[31]Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.
And God saw every thing that he had made, and, behold, it was very good. And the evening and the morning were the sixth day.

Mwanzo 2:1-2

[1]Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.
Thus the heavens and the earth were finished, and all the host of them.

[2]Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.
And on the seventh day God ended his work which he had made; and he rested on the seventh day from all his work which he had made.

Mpaka hapo tumeona uumbaji upande wa Biblia.
Sasa tofauti na Biblia,katika Qura'n uumbaji umefanyika katika nyakati sita na hakuna maelezo ya mfuatano WA kutoka moja mpaka Sita juu ya uumbaji,Bali habar za uumbaji zimeelezwa katika Aya tofauti tofauti katika kipindi chote cha kushuka qura'n Kwa miaka 23. Na kama haitoshi maelezo ya qura'n juu ya uumbaji Yana dhibitishwa na hoja za Kisayansi ambazo ni sahihi kama ilivyoelezwa na Muhammad (s.a.w)
Qur'an inaeleza kuwa Mwenyezi Mungu aliumba ardhi Kwa siku mbili:

"Sema: Hivyo nyinyi mnamkataa aliye umba ardhi katika siku mbili, na mnamfanyia washirika? Huyu ndiye Mola Mlezi wa walimwengu wote."
41:9

Kisha Mwenyezi Mungu akailekea mbingu ambayo ilikuwa Moshi akaiita pamoja na ardhi zikaambatana pamoja.

"Kisha akazielekea mbingu, na zilikuwa moshi, akaziambia hizo na ardhi: Njooni, kwa khiari au kwa nguvu! Vyote viwili vikasema: Tumekuja nasi ni wat'iifu."
41:11

"Basi akazifanya mbingu saba kwa siku mbili, na akazipangia kila mbingu mambo yake. Na tukaipamba mbingu ya chini kwa mataa na kwa ulinzi. Hichi ndicho kipimo cha Mwenyezi Mungu Mwenye Kujua."
41:12

Mpaka hapo tunaona kwamba uumbaji WA mbingu na ardhi umefanyika nyakati nne au siku nne.

Qur'an inasema halafu mbingu ambayo ni Moshi ili ambatanishwa na ardhi Kwa pamoja zikawa zimeshikamana,tuangalie Maandiko:


"Je! Hao walio kufuru hawakuona kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabandua? Na tukajaalia kwa maji kila kilicho hai? Basi je, hawaamini?"
21:30

Kwahiyo mpaka hapa tunaona kwamba,uumbaji WA mbingu na ardhi Kwa mujibu wa Qur'an,ulikuwa kama ifuatavyo;

Mwenyezi Mungu aliumba ardhi kisha akaichukua mbingu ambayo ilikuwa Moshi akaziambatanisha pamoja zikawa zimeshikana kisha baadae akaziachanisha na kuumbwa Kwa mbingu Saba na viliomo baina ya mbingu na ardhi.

Ukija katika Sayansi inadhibitisha utaratibu ule ule ulio elezwa na Qur'an

Sayansi inasema katika uumbaji, kulikuwa na gaseous mass with fine particles ambazo Kwa kiarabu (dukan) ambao INA maanisha Moshi,ambapo Moshi unaundwa na gaseous substratum na fine particles ambazo zinakuwa katika Hali ya ugumu na Hali ya kimiminika katika high temperature or low temperature.

Halafu baadae zikaachana baada ya kutokea mlipuko mkubwa,ambao ulipelekea kurushwa Kwa materials mbali mbali angani na kuundwa Kwa mbingu na vitu vingine kama sayari na nyota na bodies nyingine mbali mbali,rejea kwenye Bing Bang Theory.
Na kwakuongezea Tu ndio maana ukiangalia sayar kama Jupiter utakuta kuna gaseous kama helium na hydrogen, nyota kama jua ni gaseous tupu,hizo Kwa uchache Tu.

Na vile vile Qur'an imeeleza dunia katika uwingi na hivyo ikamaanisha huenda kukawa na uwezekano WA kuwepo dunia nyingine kama yetu ingawa Sayansi bado haijagundua Hilo swala,ingawa wanasema uwezekano huo upo katika galaxy nyingine ambayo IPO nje ya galaxy yetu,waliosoma au ambao wanapenda kusoma mambo ya anga nadhani wanajua nikisema Milk way galaxy namaanisha nini?

Kwahiyo kuna mambo mengi ambayo yameelezwa katika Qur'an ambapo bado. Sayansi haija yagundua huenda yakaja kugundulika na vizazi vijavyo huko.

Kwahiyo maelezo haya ni Uongo mkubwa Sana kusema kwamba Muhammad amekopi Maandiko ya Biblia wakati kuna tofauti kubwa Sana ya uumbaji WA Biblia na Qur'an.

Basi Muhammad atakuwa ni mtu mwenye akili Sana aone Maandiko ya Biblia ambayo hayawezi kudhibitishwa na Sayansi halafu ayabadilishe na yawe mazuri kiasi kwamba Sayansi iweze kuyadhibitisha yashahabiane na Quran. Na kumbuka Muhammad aliishi Karne ya 14 na Sayansi imedhibitisha Karne ya 20 baada ya kuwepo kwa dhana za kisasa za kiutafiti.

Hakika huo ndio ukubwa wa Maneno ya Mwenyezi Mungu,na ukweli siku zote ni WA kudumu na unashinda changamoto zote.

Naomba atayekuja kuchallenge huu Uzi wangu asije na Maneno matupu,Bali athibitishe Kwa maandiko kama Mimi nilivyofanya,vinginevyo zitakuwa porojo Tu.

Panapo majaliwa inshallah nitakuja na muendelezo wa part (2), lengo ni kuweka mambo Sawa maana uzushi umezidi sana humu ndani
 
'Aqiyqah Afanye Nchi Za Nje Anakoishi Ambako Hakuna Jirani Waislamu Au Afanye Nyumbani Walipo Masikini?
Maswali: Uzazi - Malezi
SWALI:



ASALAM ALYKUM WARAHMATLLAH,



SUALI LANGU KUHUSIANA NA HAKIKI YA MTOTO KUIFANYA HAPA UK,



KWANI NINAVYO FAHAMU MIMI NIKWAMBA UCHINJE MBUZI MMOJA KWA MTOTO WAKIKE AU WAWILI KWA MTOTO WA KIUME NA UIGAWANYE NYAMA HIO MAFUGU MATATU MOJA UWAPATIE MAJIRANI ZAKO LAPILI UWAPATIE MASKINI NA LATATU LIWE KWA AJILI YAKO. SASA SUALI LANGU LIPO HAPA JUU YA KUWAPATA HAWA MASKINI KWA HAPA UK NA PIA HAWA MAJIRANI KUWEZA KUWAPELEKEA HIO NYAMA KWANI MAJIRANI ZANGU WOTE NI WAZUNGU ILA MMOJA TU NDIYE MUISLAMU MSWAHILI AMBAYE ANAWEZA KUPOKEA NYAMA HIYO. VILE VILE SITOWEZA KUPATA HAO MASKINI KWANI WOTE NI WATU WENYE UWEZO WAO. NAOMBA NIPATIWE MAFAHAMISHO ILI NIWEZE KUIFANYA HAPA AU NIFANYE KWETU VIJIJINI? NAOMBA UFAFANUZI JUU YA HILI TAFADHALINI.



JIBU:



Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu ‘Aqiyqah ambayo ni sadaqa inayofanywa pindi wanandoa wanapopata mtoto, wa kiume au wa kike. Hakika lengo ya sadaqa zote katika Uislamu ni kutolea katika mtaa na mji anaoishi mmoja wetu ila kama kutakuwa na haja itakayopelekea kuhamishwa.



Haifai sadaqa kuhamishwa kutoka mji mmoja hadi mwengine ila kwa dharura za kishari’ah.



Tukizungumzia kuhusu ‘Aqiyqah upo ufahamu wa makosa kuwa ni lazima igawanywe mafungu matatu. ‘Aqiyqah mtu ameachiwa uhuru kabisa, anaweza kula yeye kila kitu, anaweza akatoa nyama yote na anaweza kumpatia amtakaye. Muhimu ni kule kumwagwa damu ya mnyama kwa lengo hilo la kutekeleza maagizo ya Mtume wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).



Hivyo, fahamu kuwa hakuna ulazima wa kugawa nyama hiyo ingawa inapendeza kufanya hivyo.



Ama kwa hali yako hapo ulipo, unatakiwa kuifanya ‘Aqiyqah hapo ulipo na ukala nyama yako hiyo na unaweza kumpatia na huyo jirani yako Muislamu.



Unaweza pia kumpatia huyo jirani yako asiye Muislamu, sababu ni kuwa hata yule jirani asiyekuwa Muislamu ana haki moja na anaweza kupatiwa nyama hiyo kwa kutengeneza ujirani mwema na pia ni njia ya kumfanyia Da’wah akapata kuujua Uislamu.



Kwa hiyo, si lazima upate maskini ndio uwapatie hiyo nyama, na isiwe hiyo ndio sababu ya kukuzuia wewe kufanya ‘Aqiyqah hapo ulipo kwa sababu hakuna maskini.



Na Allaah Anajua zaidi
 
'Aqiyqah Anayofanyiwa Mtoto Mchanga Katika Sunnah
Maswali: Uzazi - Malezi
'Aqiyqah Anayofanyiwa Mtoto Mchanga



www.alhidaaya.com





SWALI:





Assalam alyekum

Mimi naomba kuelimishwa kuhusu suala zima la hakiki kwa mtoto. je ni utaratibu upi ambao inatubidi kuufuata ili kufikia mafundisho kama alivyotufundisha bwana Mtume (s.a.w.)







JIBU:



AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.






Kwanza tunakunasihi kutokufupisha maamkizi ya Kiislaam na Thanaa au kuwatakia Radhi Swahaba na mengineyo ambayo watu wanakosea kama hivyo. Jambo hilo limekemewa na ‘Ulamaa wetu. Bonyea viungo vifuatavyo upate faida:



Hukmu Ya Kufupisha Thanaa (Kumtukuza Allaah) Na Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) Na Maamkizi Ya Kiislam
Al-Lajnah Ad-Daaimah: Haijuzu Kufupisha Kumswalia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Maandishi
Imaam Ibn Baaz: Kufupisha Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Kwa Mfumo Wowote Haijuzu


Ama kuhusu suala la kumfanyia mtoto 'Aqiyqah, kwanza tufahamu maana ya 'Aqyqah.



‘Aqiyqah maana yake ni kukata. Na katika sharia ni mbuzi anayechinjwa kwa ajili ya mtoto aliyezaliwa anapofika siku ya saba tokea kuzaliwa kwake.



‘Aqiyqah ni Sunnah iliyotiliwa mkazo kwa mwenye uwezo nayo.





Na hili ni jukumu la wazazi kumfanyia mtoto wao kwa kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)

“Kila mtoto amefungika na ‘Aqiyqah yake, itachinjwa kwa ajili yake siku ya saba na atapewa jina, na atanyolewa kichwa chake” (Ahmad na An-Nasaaiy).





Kwa ajili ya shughuli hiyo ni lazima achinjwe mnyama anayefaa kuchinjwa kwa ajili ya Udh-hiyah kwa kuzingatia kusalimika kwake na kasoro yoyote kama kuwa kilema au kukosa jicho na umri wake uwe zaidi ya mwaka.





Baada ya kuchinjwa mnyama huyo akiwa ni mbuzi au kondoo ni Sunnah kumgawa kama inavyogaiwa nyama ya Udh-hiyah. Baadhi ya nyama watakula watu wa nyumbani, na nyingine utatoa sadaka.





Ni vyema na ndio sahihi zaidi kuchinja siku ya 7 ama riwaya za siku ya 14 au 21 au 28 hazina uhakika sana. Kwa hiyo mtu ajihimu sana kuchinja siku hiyo ya saba. Ikiwa hakuweza kwa sababu fulani fulani, basi Maulamaa wanasema kuwa anaweza kufanya wakati wowote katika uhai wake.





‘Aqiyqah ya mtoto wa kiume ni mbuzi wawili na wa kike ni mbuzi mmoja kama alivyofanya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):

“Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alichinja mbuzi wawili alipozaliwa Hasan” (At-Tirmidhiy).





Japokuwa zipo riwaya nyingine ambazo zinaonyesha kuwa mtoto wa kiume na wa kike wanachinjiwa mbuzi mmoja mmoja.





Wanachuoni wamekanusha riwaya hizi kwa kusema ni vyema kwa mvulana kuchinjiwa mbuzi wawili lakini ikiwa mzazi hana uwezo basi atachinja mmoja.





Ikiwa mtoto atakufa kabla ya siku ya saba basi hatochinjiwa.





Pia ni Sunnah siku ya saba hiyo unayofanya 'Aqiyqah, kumpa mtoto jina, na jina liwe zuri na haswa bora kama alivyofundisha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama majina ya uja wa Allaah kama, 'Abdur-Rahmaan, 'Abdullaah n.k. au majina ya Mitume, Maswahaba na wema waliotangulia.





Na si vizuri kuwaita watoto majina mabaya au yasiyo na maana kama; Vita, Pondamali, Chausiku, Kufakulala n.k.





Na pia amfanyie tahniyk, tahniyk ni kumlambisha mtoto tende alizozitafuna au asali au kitamu chochote atakachokipata.





Kuna baadhi ya 'Ulamaa wamependekeza kumuadhinia mtoto anapozaliwa kwenye sikio lake la kuume ili liwe jambo la kwanza analosikia mtoto ni neno la Tawhiyd, lakini maelezo au Hadiyth zilizosimuliwa kuhusu kumuadhinia mtoto sikio la kulia na kumkimia sikio la kushoto, hakuna iliyo sahihi kwa mujibu wa Wanachuoni wabobezi wa elimu ya Hadiyth.





Hayo ni mambo muhimu ya kuzingatia kwa wazazi wanaporuzukiwa watoto.





Tunatumai ya kuwa tutakuwa tumejibu swali lako na kwa manufaa zaidi bonyeza viungo vifuatavyo:



Kufanya 'Aqiyqah Ni Lazima Au Sunnah?

'Aqiyqah Ni Lazima Au Sunnah? | Alhidaaya.com



‘Aqiyqah –Inafaa Kuwafanyia Watoto Wanapokuwa Wakubwa – Tofauti ‘Aqiyqah Ya Mtoto Wa Kiume Na Wa Kike




Anaweza Kujifanyia Mwenyewe 'Aqiyqah Ukubwani Ikiwa Hakufanyiwa Na Wazazi Wake?




Nani Mwenye Jukumu la Aqiyqah?




‘Aqiyqah; Je, Ni Lazima Wapatikane Mbuzi Weupe Tu?




Afanye ‘Aqiyqah Nchi Za Njei Anakoishi Ambako Hakuna Jirani Waislamu Au Afanye Nyumbani Walioko Masikini?






Na Allaah Anajua zaidi
 
'Aqiyqah: Je Ni Lazima Mnyama Achinjwe Nyumba Anayoishi Na Lazima Mtoto Anyolewe Nywele?
Maswali: Uzazi - Malezi
SWALI:

Assalam alaykum..: nina watoto wawili mapacha...wenye umri wa mwaka mmoja...nimewafanyia haqyika kwa kufuata yale yote nikiyopata kuyasoma humu katika toleo la 16 Rajab1435H..lakin nimeingiwa na wasiwasi huwenda sikufanya kama vile inavyo takiwa kwa maana..:
1:sikuweza ifanya hiyo haqyika katika nyumba ninayoishi mimi lakin ndani ya kijiji hichohicho..nilifanyia kwa rafiki yangu
2:siku hiyo sikuweza kuwanyoa nyele...je kwa kufanya hivi nitakuwa nimeharibu hiyo haqyika..!!? Na kama nimeharibu naweza kurejeza tena kuwafanyia...
wahadha salam a'laykum

JIBU:



AlhamduliLLaah - Sifa njema zote Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

Tunashukuru kwa utekelezaji wako wa Sunnah ya ‘Aqiyqah baada ya kupata mafunzo kutoka kwetu. Hakika hii inatuzidishia iymaan kwamba ndugu zetu mnafuata mafunzo haya na juhudi zetu si za bure. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Azidi kutuelimisha na kutuongoza.

Ama kuhusu ‘Aqiyqah uliyoifanya kwa kukosekana mambo mawili uliyoyataja, ni kwamba haikuharibu ‘Aqiyqah yako kwa sababu hakuna dalili kwamba ‘Aqiyqah lazima itekelezwe katika nyumba anayoishi mtu au lazima mtoto anyolewe nywele. Kwa hiyo huna haja kurejea kutekeleza tena bali inatosheleza na tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Akutakabalie na Awajaalie watoto wawe waja wema na wenye taqwa.

Itambulike kwamba kumnyoa nywele moto, ni katika Sunnah iliyopendekezwa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama ilivyokuja dalili katika Hadiyth ya Abu Rafi‘i (Radhiya Allaahu ‘anhu) kuwa al-Hasan bin ‘Aliy (Radhiya Allaahu ‘anhuma), mama yake, ambaye ni Faatwimah (Radhiya Allaahu ‘anha) alitaka kumfanyia ‘Aqiyqah ya kondoo wawili. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Usifanye ‘Aqiyqah, lakini mnyoe nywele zake, halafu utoe sadaka ya fedha yenye uzito wa nywele hizo”. Kisha akazaliwa al-Husayn (Radhiya Allaahu ‘anhuma), akafanya mithili ya hivyo” (Ahmad).

Ni dhahiri kwamba kuna hikma na faida ya kumnyoa mtoto nywele na anayeweza kutekeleza ni kheri kwake na kwa mtoto. Ama asiyejaaliwa kutekeleza hana ubaya bali atakuwa amekosa faida zake tu, na mtu hulipwa kwa niyyah yake.

Na Allaah Anajua zaidi
 
Adhabu Inayompata Baba kwa Kutowaangalia Watoto Wake
Maswali: Uzazi - Malezi


SWALI:



Adhabu gani inaompata baba anaye mtupa mwanawe au wanawe wa halali?



JIBU:


Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.


Shukrani zetu kwa swali lako kuhusu baba kutowaangalia watoto wake.

Hakika hakuna adhabu maalumu ambayo shari’ah imetoa kuhusiana na suala hilo. Katika shari’ah tofauti, baba anaadhibiwa kwa kutowaangalia watoto wake ambao ana jukumu juu yao kuhusu hilo. Na katika shari’ah ya Kiislamu pia, lau baba atashitakiwa kwa Qaadhi basi Qaadhi mwanzo atamlazimisha awatunze na kuwahudumikia. Kushindwa kufanya hivyo itabidi achukuliwe hatua na Qaadhi kutoa adhabu ya ta’ziyr kulingana na dhulma yenyewe.


Ama Kesho Akhera, adhabu yake itakuwa kubwa kwani hilo huingia katika dhulma.

Na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

“Ogopeni dhulma kwani dhulma ni kiza Siku ya Qiyaamah” (Muslim).



Na Allaah Anajua zaidi
 
Amemkatisha Mtoto Kunyonya Kwa Ajili Ya Kwenda Kutafuta Elimu - Je, Amlipe Mtoto?
Maswali: Uzazi - Malezi
SWALI:



Assalam Alaykum Warahmatullah Wabarakatuh.

Sifa zote njema anastahiki kushukuriwa Allah Subhanahu Wata'ala.

Mimi ni mama mwenye mtoto wa kiume ambae nilimkatisha kunyonya kwa ajili ya kuondoka ndani ya nchi na kwenda nchi nyengine kwa kwenda kutafuta Elimu.



Nilikuwa nina nia ya kumchukuwa mtoto wangu huyo lakini kutokana na mazingira ya nchi niendayo ikaniwia vigumu kumchukuwa, kwani sikuwa na mtu wa kuweza kukaa nae pindipo nitakapo ingia darasani. Nilimuacha akiwa na umri wa mwaka mmoja na mwezi mmoja, naomba kufahamishwa ni kweli utakapomkatisha maziwa mtoto unatakiwa umlipe na ni vipi naweza kumlipa?



InshaAllah nawatakia kila la kheri











JIBU:



Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.









Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kumuachisha mtoto wako kunyonya.

Ni jambo linalofahamika vyema kabisa sasa kuwa maziwa ya mama ndio mazuri sana kwa siha, afya na makuzi mazuri kwa mtoto. Kwa hiyo, Allaah Aliyetukuka Amewaagizia kinamama wawe ni wenye kuwanyonyesha watoto wao miaka miwili kamili. Hata hivyo, hilo ni kwa atakayetaka kukamilisha muda huo, (al-Baqarah [2]: 233).



Pia, wazazi (mama na baba) wanaweza kushauriana katika kumuachisha mtoto kunyonya kwa sababu moja au nyingine. Mashauriano hayo yawe ni yenye kutazama maslahi ya mama na mtoto. Kila mmoja asiwe ni mwenye kudhuriwa na mwengine kwa njia yoyote ile.



Ikiwa wazazi watashauriana kumuachisha mtoto kutakua hakuna kulipwa chochote mtoto. Kwa sababu ya mama kutokuwepo au kwa sababu nyingine yoyote ile ambayo itamfanya asiweze kumnyonyesha, jukumu la kumpatia mtoto mwangalizi au mnyonyeshaji mwengine litamuangukia baba. Baba atalazimika kumuajiri mwanamke wa kumnyonyesha mtoto au kumtazama.







Bonyeza viungo vifuatavyo upate maelezo zaidi:







Je Kuna Malipo Kama Hukumnyonyesha Mtoto?




Mama Hataki Kunyonyesha - Nini Hukmu Yake?




Mtoto Asiyenyonyeshwa Na Mama Yake Inapasa Alipwe?



Na Allaah Anajua zaidi
 
Amwache Mumewe Nchi Za Ki-Magharibi Ili Arudi Tanzania Kumsomesha Mwanawe Qur-aan?
Maswali: Uzazi - Malezi



SWALI:




ASSALAM ALAYKUM WARAHMATULLAHI TAALA WABARAKATU.MIMI NIKO UENGEREZA NA HUKU WATOO HAWASOMI QUR~ANI KWA JUHUDI KAMA NYUMBANI [ZANZIBAR] NA KUTOKANA NA MASOMO MAPYA YATAKAYOANZA MASKULINI TUNAOGOPA MBELE YA ALLAH KUHUSU UCHUNGAJI WA WATOO, KWA HIVYO NIMEAMUA NIENDE ZANZIBAR KWA AJILI YA MTOTO WANGU NAOMBA MUNIJULISHE ISLAMIC INTERNATIONAL SCHOOL ILIYOBORA. JEE NIKO SAWA MUME WANGU KUMUACHA HUKU IKIWA TUMEKUBALIANA HIVYO.










JIBU:




Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.










Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kumuacha Mume Uingereza nawe kwenda Zanzibar na mtoto. Na dada yangu mwanzo inatakiwa tufahamu kuwa katika kila nchi haswa za Uzunguni na Afrika Mashariki zina matatizo ikiwa umemtia mtoto wako shule kwani masomo yanayojaliwa huko ni kufuata mtaala wa serikali wa masomo.




Kisha, inatakiwa tufahamu kuwa malezi ya mtoto yanahitaji ushirikiano wa baba mzazi na mama. Bila ya hao wawili kutakuwa na kasoro nyingi katika ukuaji wa mtoto mwenyewe. Naona ushauri mwema ni nyinyi wazazi mfanye juhudi ya kumtafutia mtoto wenu shule ya Kiislamu ambayo imefanya indimaj (integration) kwa kusomesha mitaala yote miwili katika jingo moja. Na nadhani huko zipo. Lau si hivyo basi muhame nyote wewe na mumeo muende Zanzibar kwa ajili ya kuishi na kumsomesha kijana wenu.




Sijui kama kwa sasa Zanzibar imekuwa na Islamic International school au la kwani mara hapo miaka ya nyuma kulikuwa hakuna. Itabidi kama kuna jamaa zako huko uwasiliane nao kuhusu suala hilo la shule. Na mara nyingine shule zinaitwa kwa jina Islamic lakini hakuna Uislamu ndani yake bali ni kuwavutia Waislamu na kupata pesa zao mbali na kuwa waanzilishaji ni Waislamu.




Ikiwa mumeelewana kuwa wewe uende Zanzibar kwa lengo la mtoto kupata mafunzo ya Dini hakuna taabu kisheria lakini itabidi muwe wavumilivu kwani kuna changa moto nyingi. Kuna changa moto ya matamanio kwa mume na mke ndio Umar bin al-Khatwtwaab (Radhiya Allaahu ‘anhu) akaweka kuwa mujahidina wasikae zaidi ya miezi minne ila warudi wakutane na ahli zao, baadaye warudi tena vitani. Kuna changa moto ya maneno baina ya watu wa mke au mume kupeleka kwa wapili wako na hapo kutoka vurugu. Kuna pia changa moto ya upweke kwa nyote wawili.




Hata hivyo, uamuzi ni wenu lakini mnatakiwa mufikirie kwa kina suala hilo kabla kutoa uamuzi wa mwisho. Kwa hiyo, ni muhimu sana mutake ushauri kwa Allaah Aliyetukuka kwa kuswali Swalah ya Istikhaarah.




Na Allaah Anajua zaidi.
 
Skip to main cont

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب المجاهدة

011 – Mlango Wa Kufanya Juhudi



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى:



وَالَّذِينَ جَاهَدُوا فِينَا لَنَهْدِيَنَّهُمْ سُبُلَنَا ۚ وَإِنَّ اللَّـهَ لَمَعَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٦٩﴾

Na wale waliofanya juhudi kwa ajili Yetu, bila shaka Tutawaongoza njia Zetu. Na hakika Allaah Yu Pamoja na watendao ihsaan. [Al-‘Ankabuwt: 69]



وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ ﴿٩٩﴾

Na mwabudu Rabb wako mpaka ikufikie yakini (mauti). [Al-Hijr: 99]



وَاذْكُرِ اسْمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلْ إِلَيْهِ تَبْتِيلًا ﴿٨﴾

Na dhukuru Jina la Rabb wako, na jitolee Kwake kwa kujitolea (kikamilifu). [Al-Muzzammil: 8]



فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

Basi yule atakayetenda kheri (hata kama) uzito wa chembe ya atomu (au mdudu chungu) ataiona. [Zalzalah: 7]



وَمَا تُقَدِّمُوا لِأَنفُسِكُم مِّنْ خَيْرٍ تَجِدُوهُ عِندَ اللَّـهِ هُوَ خَيْرًا وَأَعْظَمَ أَجْرًا ۚ وَاسْتَغْفِرُوا اللَّـهَ ۖ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٢٠﴾

Na chochote kile cha kheri mnachokadimisha kwa ajili ya nafsi zenu, mtakikuta kwa Allaah. Ni bora, na ujira mkubwa zaidi. Na muombeni Allaah maghfirah, hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu). [Al-Muzzammil: 20]



وَمَا تُنفِقُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢٧٣﴾

Na chochote mtoacho katika khayr basi Allaah kwacho ni Mjuzi. [Al-Baqarah: 273]





Hadiyth – 1

عن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ الله تَعَالَى قَالَ: مَنْ عادى لي وَلِيًّا فَقَدْ آذَنْتُهُ بالحَرْبِ، وَمَا تَقَرَّبَ إِلَيَّ عَبْدي بشَيءٍ أَحَبَّ إلَيَّ مِمَّا افْتَرَضْتُ عَلَيهِ، وَمَا يَزَالُ عَبْدِي يَتَقرَّبُ إلَيَّ بالنَّوافِلِ حَتَّى أحِبَّهُ، فَإذَا أَحبَبتُهُ كُنْتُ سَمعَهُ الَّذِي يَسْمَعُ بِهِ، وَبَصَرَهُ الَّذِي يُبْصِرُ بِهِ، ويَدَهُ الَّتي يَبْطِشُ بِهَا، وَرِجْلَهُ الَّتِي يَمْشي بِهَا، وَإنْ سَأَلَني لأُعْطِيَنَّهُ، وَلَئِنِ اسْتَعَاذَنِي لأُعِيذَنَّهُ)). رواه البخاري

Imetoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiyah Allaahu ‘anhu) kwamba: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Allaah (Ta’aalaa) Anasema: “Mwenye kumfanyia uadui kipenzi Changu, basi Nimeshamtangazia vita. Mja Wangu hajikurubishi Kwangu ila kwa jambo linalonipendeza mno kulikoni kutenda fardhi nilizomfaradhishia; mja Wangu ataendelea kujikurubisha Kwangu kwa kujitolea mpaka Nimpende. Nitakapompenda, Nitakuwa ni masikilizio yake anayosikilizia, na ni macho yake anayoonea, na ni mkono wake anaoshikia, na ni mguu wake anaotembelea. Akiniomba Nitampa, na akiomba kinga Kwangu Nitamkinga.” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 2

عن أنس رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فيما يرويه عن ربّه عز وجل قَالَ: ((إِذَا تَقَربَ العَبْدُ إلَيَّ شِبْرًا تَقَربْتُ إِلَيْه ذِرَاعًا، وَإِذَا تَقَرَّبَ إلَيَّ ذِرَاعًا تَقَربْتُ مِنهُ بَاعًا، وِإذَا أتَانِي يَمشي أتَيْتُهُ هَرْوَلَةً)). رواه البخاري

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Nabiy(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu aliyopokea kutoka kwa Rabb Wake (‘Azza wa Jalla) Anasema: “Mja Wangu atakaponikaribia kwa shubiri, Nitamkaribia kwa dhiraa. Akinikaribia kwa dhiraa, Nitamkaribia kwa pima, na akinijia kwa kutembea nami Nitamkimbilia.” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 3

عن ابن عباس رضي الله عنهما قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((نِعْمَتَانِ مَغبونٌ فيهما كَثيرٌ مِنَ النَّاسِ: الصِّحَّةُ، وَالفَرَاغُ)). رواه البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Watu wengi wamepoteza neema mbili: afya na faragha [wakati].” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 4

عن عائشة رَضي الله عنها: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يقُومُ مِنَ اللَّيلِ حَتَّى تَتَفَطَّرَ قَدَمَاهُ فَقُلْتُ لَهُ: لِمَ تَصنَعُ هَذَا يَا رسولَ الله، وَقدْ غَفَرَ الله لَكَ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ؟ قَالَ: ((أَفَلا أُحِبُّ أنْ أكُونَ عَبْدًا شَكُورًا)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa): Kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akisimama usiku (kuswali) mpaka miguu yake ikivimba. Nikamuuliza: mbona unafanya hivi yaa Rasula-Allaah na hali ya kuwa Allaah Ameshakughufuria dhambi zako zilizotangulia na zitakazokuja? Akajibu: “Kwani sipendelei niwe ni mja mwenye kushukuru?” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 5

عن عائشة رضي الله عنها، أنَّها قَالَتْ: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا دَخَلَ العَشْرُ أَحْيَا اللَّيلَ، وَأيْقَظَ أهْلَهُ، وَجَدَّ وَشَدَّ المِئْزَر. مُتَّفَقٌ عَلَيه

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa): Alikuwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inapoingia kumi la mwisho (katika mwezi wa Ramadhwaan) hukesha usiku, akiwaamsha watu wa nyumbani kwake akijipinda na kukaza kikoi chake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 6

عن أبي هريرة رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((المُؤْمِنُ القَوِيُّ خَيرٌ وَأَحَبُّ إِلَى اللهِ مِنَ المُؤْمِنِ الضَّعيفِ، وَفي كُلٍّ خَيرٌ. احْرِصْ عَلَى مَا يَنْفَعُكَ، واسْتَعِنْ بِاللهِ وَلا تَعْجَزْ. وَإنْ أَصَابَكَ شَيءٌ فَلا تَقُلْ لَوْ أنّي فَعَلْتُ كَانَ كَذَا وَكَذَا، وَلَكِنْ قُلْ: قَدرُ اللهِ، وَمَا شَاءَ فَعلَ؛ فإنَّ لَوْ تَفْتَحُ عَمَلَ الشَّيطَانِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Amesema Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) “Muumin mwenye nguvu ni bora na anapendeza mno mbele ya Allaah kulikoni Muumin dhaifu, na katika wote (hao) kuna khayr, fanya bidii katika jambo linalokunufaisha, na uombe msaada kwa Allaah na wala usifanye uvivu. Utakaposibiwa na jambo usiseme; Lau ningalifanya kadhaa na kadhaa, lakini sema: "Qadaru Allaahi wa maa Shaa Fa'ala - Allaah Amejaaliya, na Atakalo Yeye huwa." Kwani kusema; lau, hufungua ‘amali ya shaytwaan.” [Muslim]





Hadiyth – 7

عن أبي هريرة رضي الله عنه أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((حُجِبَتِ النَّارُ بالشَّهَواتِ، وَحُجِبَتِ الجَنَّةُ بِالمَكَارِهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Moto umezunguka kwa matamanio, na Jannah imezungukwa kwa machukivu.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 8

عن أبي عبد الله حُذَيفَةَ بنِ اليمانِ رضي الله عنهما، قَالَ: صَلَّيْتُ مَعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم ذَاتَ لَيلَةٍ فَافْتَتَحَ البقَرَةَ، فَقُلْتُ: يَرْكَعُ عِنْدَ المائَةِ، ثُمَّ مَضَى. فَقُلْتُ: يُصَلِّي بِهَا في ركعَة فَمَضَى، فقُلْتُ: يَرْكَعُ بِهَا، ثُمَّ افْتَتَحَ النِّسَاءَ فَقَرَأَهَا، ثُمَّ افْتَتَحَ آلَ عِمْرَانَ فَقَرَأَهَا، يَقرَأُ مُتَرَسِّلًا: إِذَا مَرَّ بآية فِيهَا تَسبيحٌ سَبَّحَ، وَإذَا مَرَّ بسُؤَالٍ سَأَلَ، وَإذَا مَرَّ بتَعَوُّذٍ تَعَوَّذَ، ثُمَّ رَكَعَ، فَجَعَلَ يَقُولُ: ((سُبْحَانَ رَبِّيَ العَظِيمِ)) فَكَانَ رُكُوعُهُ نَحوًا مِنْ قِيَامِهِ، ثُمَّ قَالَ: ((سَمِعَ اللهُ لِمَنْ حَمِدَهُ ربَّنا ولك الحمد)) ثُمَّ قَامَ قِيامًا طَويلًا قَريبًا مِمَّا رَكَعَ، ثُمَّ سَجَدَ، فَقَالَ: ((سُبْحَانَ رَبِّيَ الأَعْلَى)) فَكَانَ سُجُودُهُ قَريبًا مِنْ قِيَامِهِ. رواه مسلم

Abuu ‘Abdillaah, Hudhayfah bin Al-Yamaani (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Usiku mmoja niliswali na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaanza kusoma Suwratu Al-Baqarah. Nikasema (moyoni) atarukuu katika Aayah ya mia. Lakini akaendelea, nikasema atamaliza Suwrah yote katika rakaah moja. Akaendelea. Nikasema: Atarukuu akimaliza Suwrah hii, halafu akaianza Suwratu An-Nisaa. Akaisoma yote, kisha akaianza Suwratu Aal-‘Imraan, akaisoma yote. Alikuwa akisoma taratibu, anapoisoma Aayah yenye kumsabih Allaah, yeye humsabbih, na anaposoma Aayah ya kuomba yeye huomba, na anaposoma Aayah ya kujikinga yeye hujikinda. Kisha akarukuu na akawa anasema: “Subhaana Rabbiyal-‘Adhwiym - Ametakasika Rabb wangu Adhimu.” Rukuu yake ikawa inafanana na kisimamo chake, kisha akasema: “Sami’a Allaahu liman Hamidah Rabbanaa walakal Hamd - Allaah Amemsikia mwenye kumuhimidi, Ee Rabb wetu, ni Zako Wewe tu sifa njema.” Kisha akasimama kisimamo kirefu kinachokaribiana na rukuu, kisha akasujudu, akasema: “Subhaana Rabbiyal-A’laa - Ametakasima Rabb Aliye juu.” Sijdah yake yake ikakaribiana na kisimamo chake. [Muslim]





Hadiyth – 9

عن ابن مسعود رضي الله عنه قَالَ: صَلَّيْتُ مَعَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم لَيلَةً، فَأَطَالَ القِيامَ حَتَّى هَمَمْتُ بأمْرِ سُوءٍ! قيل: وَمَا هَمَمْتَ بِهِ؟ قَالَ: هَمَمْتُ أنْ أجْلِسَ وَأَدَعَهُ. مُتَّفَقٌ عَلَيه

‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: “Usiku mmoja niliswali na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akarefusha kisimamo hata nikafikiria kutenda jambo baya. Akaulizwa: kwani ulifikiri kufanya nini? Akajibu: Nilifikiria nikae chini na nimuache Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 10

عن أنس رضي الله عنه عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((يَتْبَعُ المَيتَ ثَلاَثَةٌ: أهْلُهُ وَمَالُهُ وَعَملُهُ، فَيَرجِعُ اثنَانِ وَيَبْقَى وَاحِدٌ: يَرجِعُ أهْلُهُ وَمَالُهُ، وَيَبقَى عَملُهُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Mambo matatu humfuata maiti: Familia yake, mali yake na ‘amali zake. Mawili kati ya hayo hurejea nayo na kubakia na moja; familia na mali hurejea na ikabakia ‘amali yake.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 11

عن ابن مسعود رضي الله عنه قَالَ: قَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((الجَنَّةُ أَقْرَبُ إِلَى أَحَدِكُمْ مِنْ شِرَاكِ نَعْلِهِ، وَالنَّارُ مِثلُ ذلِكَ)). رواه البخاري

‘Abdullaa bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Jannah ipo karibu zaidi kwa mmoja wenu kulikoni mkanda wa kiatu chake, na moto ni hivyo hivyo.” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 12

عن أبي فِراسٍ ربيعةَ بنِ كعبٍ الأسلميِّ خادِمِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، ومن أهلِ الصُّفَّةِ رضي الله عنه، قَالَ: كُنْتُ أبِيتُ مَعَ رسولِ الله صلى الله عليه وسلم فآتِيهِ بِوَضُوئِهِ وَحَاجَتِهِ، فَقَالَ: ((سَلْنِي)) فقُلْتُ: اسْأَلُكَ مُرَافَقَتَكَ في الجَنَّةِ. فَقَالَ: ((أَوَ غَيرَ ذلِكَ؟)) قُلْتُ: هُوَ ذَاكَ، قَالَ: ((فأَعِنِّي عَلَى نَفْسِكَ بِكَثْرَةِ السُّجُودِ)). رواه مسلم

Abuu Firaas, Rabi’ bin Ka’b Al-Aslamiy mtumishi wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na ni katika watu wa suffah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilikuwa nikilala kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikimpelekea maji ya kutawadhia na mahitajio yake mengineo. Akaniambia: “Niombe.” Nikamwambia: Nakuomba kuwa na wewe Jannah. Akaniuliza: “Una lingine?” Nikamjibu: Ni hilo tu. Akaniambia: “Nisaidie juu nafsi yako kusujudu kwa wingi.” [Muslim]





Hadiyth – 13

عن أبي عبد الله، ويقال: أَبُو عبد الرحمن ثوبان - مولى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم رضي الله عنه، قَالَ: سَمِعْتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: ((عَلَيْكَ بِكَثْرَةِ السُّجُودِ؛ فَإِنَّكَ لَنْ تَسْجُدَ للهِ سَجْدَةً إلا رَفَعَكَ اللهُ بِهَا دَرجَةً، وَحَطَّ عَنكَ بِهَا خَطِيئةً)). رواه مسلم

Abuu ‘Abdillaah, pia huitwa Abuu ‘Abdir-Rahmaan, Thawbaan muachwa huru wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Kithirisha kusujudu kwa wingi, kwani wewe hutosujudu sijdah (moja) isipokuwa Allaah Atakupandisha daraja kwa sijdah hiyo, na Atakuondoshea dhambi kwa sijdah hiyo.” [Muslim]





Hadiyth – 14

عن أَبي صَفوان عبد الله بنِ بُسْرٍ الأسلمي رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((خَيرُ النَّاسِ مَنْ طَالَ عُمُرهُ، وَحَسُنَ عَمَلُهُ)). رواه الترمذي، وَقالَ: ((حديث حسن))

Abuu Swafwaan, ‘Abdullaah bin Busri Al-Aslamiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mbora katika watu ni yule ambaye umri wake umerefuka na ‘amali zake zikatangamaa.” [At-Tirmidhiy, na amsema: Hadiyth hii ni Hasan]





Hadiyth -15

عن أنس رضي الله عنه، قَالَ: غَابَ عَمِّي أَنَسُ بْنُ النَّضْرِ رضي الله عنه عن قِتالِ بدرٍ، فَقَالَ: يَا رسولَ الله، غِبْتُ عَنْ أوّل قِتال قَاتَلْتَ المُشْرِكِينَ، لَئِن اللهُ أشْهَدَنِي قِتَالَ المُشركِينَ لَيُرِيَنَّ اللهُ مَا أصْنَعُ.

فَلَمَّا كَانَ يَومُ أُحُدٍ انْكَشَفَ المُسْلِمونَ، فَقَالَ: اللَّهُمَّ أعْتَذِرُ إلَيْكَ مِمَّا صَنَعَ هؤُلاءِ- يعني: أصْحَابهُ- وأبْرَأُ إلَيْكَ مِمَّا صَنَعَ هؤُلاءِ- يَعني: المُشركِينَ- ثُمَّ تَقَدَّمَ فَاسْتَقْبَلهُ سَعدُ بْنُ مُعاذٍ، فَقَالَ: يَا سعدَ بنَ معاذٍ، الجَنَّةُ وربِّ الكعْبَةِ إنِّي أجِدُ ريحَهَا منْ دُونِ أُحُدٍ. قَالَ سعدٌ: فَمَا اسْتَطَعتُ يَا رسولَ الله مَا صَنَعَ!

قَالَ أنسٌ: فَوَجَدْنَا بِهِ بِضْعًا وَثَمانينَ ضَربَةً بالسَّيفِ، أَوْ طَعْنةً بِرمْحٍ، أَوْ رَمْيَةً بسَهْمٍ، وَوَجَدْنَاهُ قَدْ قُتِلَ وَمَثَّلَ بِهِ المُشْرِكونَ فما عَرَفهُ أَحَدٌ إلا أُخْتُهُ بِبَنَانِهِ.

قَالَ أنس: كُنَّا نَرَى أَوْ نَظُنُّ أن هذِهِ الآية نزلت فِيهِ وفي أشباهه: {مِنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللهَ عَلَيْهِ} [الأحزاب: 23] إِلَى آخِرها. مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Ammiy yangu Anas bin Nadhwr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) hakuwepo katika Vita vya Badr. Akasema: Yaa Rasula-Allaah, nilighibu katika vita vya kwanza ulivyopigana na washirikina. Wa-Allaahi! Allaah Akinijaalia kuhudhuria katika kupigana na washirikina, Atawadhihirishia (washirikina) kile nitakachofanya. Siku ya Vita vya Uhud, Waislamu walikimbia akaomba: Ee Rabb, nakuomba msamaha kwa yale waliyoyafanya hawa (watu wake), na najitenga kwa yale waliyoyafanya washirikina. Halafu akaenda mbele, akakabiliwa na Sa’d bin Mu’aadh, akamwambia: Ee Sa’d bin Mu’aadh, Jannah! Naapa kwa Rabb wa Al-Ka’bah, naisikia harufu yake chini ya jabali la Uhud. Sa’d akasema: Sina uwezo wa kukueleza namna alivyofanya Anas bin An-Nadhwr yaa Rasula-Allaah. Anas bin Maalik anaelezea: Tukamkuta amepigwa zaidi ya mapigo themanini ya mapanga, au kudungwa mkuki au kurushia mshale. Tulimkuta ameshauliwa na washirikina na wamemkata pua na masikio yake. Basi hakuna aliyeweza kumtambua isipokuwa dada yake, alimtambua kwa ncha ya vidole vyake. Anas bin Maalik anaeleza: Tulikuwa tukiona au tukidhani Aayah hii Suwratu Al-Ahzaab: 23. Ilikuwa imeshuka kwa sababu yake na mfano wake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّـهَ عَلَيْهِ ۖ

Miongoni mwa Waumini, wapo wanaume wamesadikisha yale waliyomuahidi Allaah. [Al-Ahzaab: 23]





Hadiyth – 16

عن أبي مسعود عقبة بن عمرو الأنصاري البدري رضي الله عنه قَالَ: لَمَّا نَزَلَتْ آيةُ الصَّدَقَةِ كُنَّا نُحَامِلُ عَلَى ظُهُورِنَا، فَجَاءَ رَجُلٌ فَتَصَدَّقَ بِشَيءٍ كَثيرٍ، فقالوا: مُراءٍ، وَجَاءَ رَجُلٌ آخَرُ فَتَصَدَّقَ بِصَاعٍ، فقالُوا: إنَّ اللهَ لَغَنيٌّ عَنْ صَاعِ هَذَا! فَنَزَلَتْ: {الَّذِينَ يَلْمِزُونَ الْمُطَّوِّعِينَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ فِي الصَّدَقَاتِ وَالَّذِينَ لا يَجِدُونَ إِلا جُهْدَهُمْ} [التوبة: 79]. مُتَّفَقٌ عَلَي

Kutoka kwa Abuu Mas'uwd ‘Uqbah bin ‘Amruw bin Al-Answaariy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Ilipoteremka Aayah ya swadaqah tulikuwa tukibeba mizigo kwa migongo yetu (pato lake tukitolea swadaqah). Akaja mtu, akatoa swadaqah mali nyingi. Wanafiki wakasema: Anajionyesha. Akaja mtu mwingine akatoa swadaqah kiasi cha pishi. Wanafiki wakasema: Allaah hana haja ya pishi la huyu! Ikashuka Aayah hii katika Suwrat At-Tawbah: 79. [Al-Bukhaariy na Muslim]

الَّذِينَ يَلْمِزُونَ الْمُطَّوِّعِينَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ فِي الصَّدَقَاتِ وَالَّذِينَ لَا يَجِدُونَ إِلَّا جُهْدَهُمْ

Wale wanaowafedhehesha wenye kujitolea kwa hiari katika kutoa swadaqah miongoni mwa Waumini, na (pia) wale wasiopata (kitu cha kutoa) isipokuwa juhudi zao. [At-Tawbah: 79]





Hadiyth – 17

عن أبي ذر جندب بن جُنادة رضي الله عنه، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فيما يروي عن اللهِ تَبَاركَ وتعالى، أنَّهُ قَالَ: ((يَا عِبَادي، إنِّي حَرَّمْتُ الظُلْمَ عَلَى نَفْسي وَجَعَلْتُهُ بيْنَكم مُحَرَّمًا فَلا تَظَالَمُوا.

يَا عِبَادي، كُلُّكُمْ ضَالّ إلا مَنْ هَدَيْتُهُ فَاستَهدُوني أهْدِكُمْ.

يَا عِبَادي، كُلُّكُمْ جَائِعٌ إلا مَنْ أطْعَمْتُهُ فَاستَطعِمُوني أُطْعِمْكُمْ.

يَا عِبَادي، كُلُّكُمْ عَارٍ إلا مَنْ كَسَوْتُهُ فاسْتَكْسُونِي أكْسُكُمْ.

يَا عِبَادي، إنَّكُمْ تُخْطِئُونَ باللَّيلِ وَالنَّهارِ وَأَنَا أغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا، فَاسْتَغْفِرُوني أغْفِرْ لَكُمْ.

يَا عِبَادي، إنَّكُمْ لَنْ تَبْلُغوا ضُرِّي فَتَضُرُّوني، وَلَنْ تَبْلُغُوا نَفعِي فَتَنْفَعُوني.

يَا عِبَادي، لَوْ أنَّ أوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجنَّكُمْ كَانُوا عَلَى أتْقَى قَلْبِ رَجُلٍ وَاحِدٍ مِنْكُمْ مَا زَادَ ذلِكَ في مُلكي شيئًا.

يَا عِبَادي، لَوْ أنَّ أوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجنَّكُمْ كَانُوا عَلَى أفْجَرِ قَلْبِ رَجُلٍ وَاحِدٍ مَا نَقَصَ ذلِكَ من مُلكي شيئًا.

يَا عِبَادي، لَوْ أنَّ أوَّلَكُمْ وَآخِرَكُمْ وَإِنْسَكُمْ وَجنَّكُمْ قَامُوا في صَعِيدٍ وَاحِدٍ فَسَألُوني فَأعْطَيتُ كُلَّ إنْسَانٍ مَسْألَتَهُ مَا نَقَصَ ذلِكَ مِمَّا عِنْدِي إلا كما يَنْقصُ المِخْيَطُ إِذَا أُدْخِلَ البَحْرَ.

يَا عِبَادي، إِنَّمَا هِيَ أعْمَالُكُمْ أُحْصِيهَا لَكُمْ ثُمَّ أوَفِّيكُمْ إِيَّاهَا، فَمَنْ وَجَدَ خَيرًا فَلْيَحْمَدِ الله وَمَنْ وَجَدَ غَيْرَ ذلِكَ فَلا يَلُومَنَّ إلا نَفْسَهُ)).

قَالَ سعيد: كَانَ أَبُو إدريس إِذَا حَدَّثَ بهذا الحديث جَثا عَلَى رُكبتيه. رواه مسلم

Abuu Dharr, Jundub bin Junaadah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika aliyopokea kutoka kwa Rabb wake (Ta’aalaa) Anasema: “Enyi waja Wangu, hakika Nimeharamisha dhulma, na Nimeijaalia ni haramu miongoni mwenu; kwa hivyo msidhulumiane. Enyi waja Wangu, nyote mmepotea isipokuwa Niliyemuongoza, kwa hivyo Niombeni uongofu Nami Nitawaongoa. Enyi waja Wangu, nyote mna njaa isipokuwa niliyemlisha, kwa hivyo niombeni chakula Nami Nitawalisha. Enyi waja Wangu, nyote mpo uchi isipokuwa Niliyemvisha, kwa hivyo niombeni Niwavishe, Nami Nitawavisha. Enyi waja Wangu, nyinyi mnakosea usiku na mchana, Nami Naghufuria dhambi zote; kwa hivyo niombeni maghfirah Nami Nitawaghufuria. Enyi waja Wangu, nyinyi hamuwezi kunidhuru wala hamuwezi kuninufaisha. Enyi waja Wangu, lau wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, wana Aadam wenu na majini wenu wangalikuwa sawa na moyo wa mchaji Allaah mno miongoni mwenu, basi hilo lisingalipunguza chochote katika Ufalme Wangu. Enyi waja Wangu, lau wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, wana Aadam wenu na majini wenu wangalikuwa sawa na moyo wa mtu muovu mno miongoni mwenu, basi hilo lisingalipunguza chochote katika Ufalme Wangu. Enyi waja Wangu, lau wa mwanzo wenu na wa mwisho wenu, wana Aadam wenu na majini wenu wangesimama katika uwanja mmoja, wakaniomba; Nami Nikampa kila mmoja ombi lake, isingalipungua chochote katika Nilichowapa isipokuwa ni kama vile sindano iliyochovywa baharini inavyopunguza maji. Enyi waja Wangu, hakika Nimezidhibiti ‘amali zenu, kisha Nitawalipa; atakayekuta khayr amuhimidi Allaah, na atakayekuta kinyume chake basi asilaumu isipokuwa ailaumu nafsi yake.” Sa’d (ambaye ni mpokezi wa Hadiyth hii) amesema: Abuu Idriys alikuwa, anapohadithia Hadiyth hii, akikaa kwa kupiga magoti. [Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب الحث عَلَى الازدياد من الخير في أواخر العمر

012 – Mlango Wa Mahimizo Ya Kuzidisha Kutenda Khayr Mwisho Wa Umri



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:



أَوَلَمْ نُعَمِّرْكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن تَذَكَّرَ وَجَاءَكُمُ النَّذِيرُ ۖ

“Je, kwani Hatukukupeni umri wa kukumbuka mwenye kukumbuka humo? [Faatwir: 37]



قَالَ ابن عباس والمُحَقِّقُونَ: أَو لَمْ نُعَمِّرْكُمْ سِتِّينَ سَنَةً؟ وَيُؤَيِّدُهُ الحديث الَّذِي سنذْكُرُهُ إنْ شاء الله تَعَالَى، وقيل: معناه ثماني عَشْرَة سَنَةً، وقيل: أرْبَعينَ سَنَةً، قاله الحسن والكلبي ومسروق ونُقِلَ عن ابن عباس أيضًا. وَنَقَلُوا أنَّ أَهْلَ المدينَةِ كانوا إِذَا بَلَغَ أَحَدُهُمْ أربْعينَ سَنَةً تَفَرَّغَ للعِبادَةِ

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) na ‘Ulamaa wenye tahakiki wamesema: “Je, hatukuwapa umri wa miaka sitini?” Kauli hii inatiliwa nguvu na Hadiyth itakayokuja in shaa Allaah (Ta’aalaa). Na imesemekana kuwa, maana yake ni: Miaka kumi na nane, na pia imesemekana ni miaka arobaini. Kauli hii imesemwa na Al-Hasan, Al-Kalbiy na Masruwq. Vile vile imenukuliwa kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Abbaas wakaeleza kuwa: Watu wa Madiynah ilikuwa mtu akitimiza umri wa miaka arobaini, hujihusisha na ‘Ibaadah pekee.





Hadiyth – 1



عن أبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((أعْذَرَ الله إِلَى امْرِئٍ أَخَّرَ أجَلَهُ حَتَّى بَلَغَ سِتِّينَ سَنَةً)). رواه البخاري

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Hakumbakishia udhuru mtu Aliyemuakhirishia mauti yake hata akafikia umri wa miaka sitini.” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 2



عن ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: كَانَ عمر رضي الله عنه يُدْخِلُنِي مَعَ أشْيَاخِ بَدرٍ فكأنَّ بَعْضَهُمْ وَجَدَ في نفسِهِ، فَقَالَ: لِمَ يَدْخُلُ هَذَا معنا ولَنَا أبْنَاءٌ مِثلُهُ؟! فَقَالَ عُمَرُ: إنَّهُ منْ حَيثُ عَلِمْتُمْ! فَدعانِي ذاتَ يَومٍ فَأدْخَلَنِي مَعَهُمْ فما رَأيتُ أَنَّهُ دعاني يَومَئذٍ إلا لِيُرِيَهُمْ، قَالَ: مَا تقُولُون في قولِ الله تعالى: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} [النصر: 1].

فَقَالَ بعضهم: أُمِرْنَا نَحْمَدُ اللهَ وَنَسْتَغْفِرُهُ إِذَا نَصَرنَا وَفَتحَ عَلَيْنَا، وَسَكتَ بَعْضُهُمْ فَلَمْ يَقُلْ شَيئًا. فَقَالَ لي: أَكَذلِكَ تقُول يَا ابنَ عباسٍ؟ فقلت: لا. قَالَ: فما تقول؟ قُلْتُ: هُوَ أجَلُ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم أعلَمَهُ لَهُ، قَالَ: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} وذلك علامةُ أجَلِكَ {فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا} [النصر: 3].

فَقَالَ عمر رضي الله عنه: مَا أعلم مِنْهَا إلا مَا تقول. رواه البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikuwa akiniingiza katika mashauri pamoja na wazee waliopigana katika Vita vya Badr, basi kana kwamba mmoja wao alikasirika moyoni mwake, akauliza: Mbona huyu anaingia pamoja na sisi na wakati sisi tunao watoto kama yeye? ‘Umar akamwambia: Huyu ni kama mnavyomjua! Siku moja akaniita na kuniingiza pamoja nao. Sikuona siku hiyo kuwa ameniita ila ni kwa ajili ya kutaka kuwaonesha wao. Akawauliza: Mnasemaje kuhusu kauli ya Allaah “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi?” Baadhi yao walisema: Tumeamriwa tumuhimidi Allaah na tumuombe maghfirah Allaah Atakapotunusuru na Kutupa ushindi. Baadhi yao walinyamaza wala hawakusema kitu. Akaniuliza: Nawe unasema hivyo hivyo ee Ibn ‘Abbaas? Nikamjibu: Hapana. Akasema: Unasemaje? Nikamwambia: Hayo ni mauti ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Allaah Alimjulisha Akamwambia: “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi.” Hiyo ndiyo alama ya mauti yako, “Basi sabbih kwa Himidi za Rabb wako na muombe maghfirah; hakika Yeye daima ni Tawwaabaa (Mwingi mno wa kupokea tawbah).” [An-Naswr]

‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: Hivyo ulivyosema ndivyo ninavyojua. [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 3



عن عائشة رضي الله عنها، قَالَتْ: مَا صلّى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم صلاةً بَعْدَ أنْ نَزَلتْ عَلَيهِ: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} إلا يقول فِيهَا: ((سُبحَانَكَ رَبَّنَا وَبِحَمْدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لي)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

وفي رواية في الصحيحين عنها: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُكْثِرُ أنْ يقُولَ في ركُوعِه وسُجُودهِ: ((سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ رَبَّنَا وبِحَمدِكَ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لِي)).

وفي رواية لمسلم: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُكثِرُ أنْ يَقُولَ قَبلَ أنْ يَمُوتَ: {إذا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} … إِلَى آخِرِ السورة.

وفي رواية لَهُ: كَانَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم يُكثِرُ مِنْ قَولِ: ((سبْحَانَ اللهِ وَبِحَمدِهِ أسْتَغفِرُ اللهَ وأتُوبُ إِلَيْهِ)). قَالَتْ: قُلْتُ: يَا رسولَ اللهِ، أَراكَ تُكثِرُ مِنْ قَولِ سُبحَانَ اللهِ وَبِحَمدهِ أسْتَغْفِرُ اللهَ وأتُوبُ إِلَيْه؟ فَقَالَ: ((أخبَرَني رَبِّي أنِّي سَأرَى عَلامَةً في أُمَّتي فإذا رَأيْتُها أكْثَرْتُ مِنْ قَولِ: سُبْحَانَ اللهِ وبِحَمدهِ أسْتَغْفرُ اللهَ وَأَتُوبُ إِلَيْه فَقَدْ رَأَيْتُهَا: {إِذَا جَاءَ نَصْرُ اللهِ وَالْفَتْحُ} فتح مكّة، {وَرَأَيْتَ النَّاسَ يَدْخُلُونَ فِي دِينِ اللهِ أَفْوَاجًا * فَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ وَاسْتَغْفِرْهُ إِنَّهُ كَانَ تَوَّابًا}))

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hakuswali Swalaah yoyote baada ya kuteremka Suwrah hii “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi.” Isipokuwa alikuwa akisema: “Kutakasika ni Kwako Rabb wetu, Ee Rabb nisamehe.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Swahiyh Al-Bukhaariy na Swahiyh Muslim; Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema katika rukuu yake na sujuwd yake: “Kutakasika ni Kwako Rabb wetu, Ee Rabb nisamehe.”

Riwaayah nyingine ya Muslim imesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema kabla ya kuondoka kwake duniani. “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi.” Mpaka mwisho wa Aayah. [An-Naswr]

Riwaayah nyingine tena ya Muslim imesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikithirisha kusema: “Kutakasika ni kwa Allaah na shukurani zote ni Zake, namuomba Allaah msamaha na ninatubia Kwake.” Nikamuuliza Ee Rasuli wa Allaah, nakuona unakithirisha kusema: Kutakasika ni kwa Allaah na shukurani zote ni Zake, namuomba Allaah msamaha na ninatubia Kwake. Akajibu: Rabb wangu Ameniambiwa kuwa mimi nitaona alama katika Ummah wangu, nitakapoiona nikithirishe kusema: “Kutakasika ni kwa Allaah na shukurani zote ni Zake, namuomba Allaah msamaha na ninatubia Kwake.” Nami nimeshaiona: “Pindi itakapokuja Nusura ya Allaah na ushindi, na utawaona watu wanaingia katika Dini ya Allaah makundi makundi, basi sabbih kwa Himidi za Rabb (Mola) wako na muombe maghfirah; hakika Yeye daima ni Tawwaabaa (Mwingi mno wa kupokea tawbah).” [An-Naswr]





Hadiyth – 4



عن أنس رضي الله عنه قَالَ: إنَّ اللهَ عز وجل تَابَعَ الوَحيَ عَلَى رسولِ الله صلى الله عليه وسلم قَبلَ وَفَاتهِ حَتَّى تُوُفِّيَ أكْثَرَ مَا كَانَ الوَحْيَ عَلَيِّه. مُتَّفَقٌ عَلَيه

Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Allaah Alimteremshia Wahyi Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa wingi kabla ya kufariki kwake, alipofariki Wahyi ulikuwa umeshateremka mwingi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 5



عن جابر رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((يُبْعَثُ كُلُّ عَبْدٍ عَلَى مَا مَاتَ عَلَيهِ)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila mja atafufuliwa katika hali aliyokufa nayo.” [Muslim]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب في بيان كثرة طرق الخير

13 – Mlango Wa Ubainifu Wa Njia Nyingi Za Khayr



Alhidaaya.com





قَالَ الله تَعَالَى:



وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ فَإِنَّ اللَّـهَ بِهِ عَلِيمٌ ﴿٢١٥﴾

Na lolote mlifanyalo katika khayr basi hakika Allaah kwa hilo ni Mjuzi.[Al-Baqarah: 215]



وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ﴿١٩٧﴾

Na lolote mlifanyalo katika ya khayr Allaah Analijua. [Al-Baqarah: 197]



فَمَن يَعْمَلْ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ خَيْرًا يَرَهُ ﴿٧﴾

Basi yule atakayetenda kheri uzito wa chembe ya atomu (au mdudu chungu) ataiona. [Az-Zalzalah: 7]



مَنْ عَمِلَ صَالِحًا فَلِنَفْسِهِ ۖ ﴿١٥﴾

Yeyote atendaye jema, basi ni kwa ajili ya nafsi yake. [Al-Jaathiyah: 15]





Hadiyh – 1



عن أبي ذر جُنْدبِ بنِ جُنَادَةَ رضي الله عنه قَالَ: قُلْتُ: يَا رسولَ الله، أيُّ الأعمالِ أفْضَلُ؟ قَالَ: ((الإيمانُ باللهِ وَالجِهادُ في سَبيلِهِ)). قُلْتُ: أيُّ الرِّقَابِ أفْضَلُ؟ قَالَ: ((أنْفَسُهَا عِنْدَ أهلِهَا وَأكثَرهَا ثَمَنًا)). قُلْتُ: فإنْ لَمْ أفْعَلْ؟ قَالَ: ((تُعِينُ صَانِعًا أَوْ تَصْنَعُ لأَخْرَقَ)). قُلْتُ: يَا رَسُول الله، أرأيْتَ إنْ ضَعُفْتُ عَنْ بَعْضِ العَمَلِ؟ قَالَ: ((تَكُفُّ شَرَّكَ عَنِ النَّاسِ؛ فإنَّهَا صَدَقَةٌ مِنْكَ عَلَى نَفْسِكَ)). مُتَّفَقٌ عليه

Abuu Dharr, Jundub bin Junaadah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimuuliza Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Ni ‘amali gani bora zaidi? Akajibu: “Ni kumuamini Allaah na kupigana Jihaad katika njia Yake.” Nikamuuliza: Ni kupi kuacha huru mtumwa kuliko bora zaidi? Akajibu: “Ni yule aliye mbora na mzuri kwa watu wake na mwenye thamani kubwa.” Nikamuuliza: Nisipoweza? Akajibu: “Umsaidie mwenye kuhitaji au umsaidie kazi yule ambaye hana ujuzi nayo.” Nikamuuliza: Ee Rasuli wa Allaah, nieleze iwapo sitoweza kufanya baadhi ya ‘amali? Akajibu: “Utaizuia shari yako isiwafikie watu; kufanya hivyo ni swadaqah juu ya nafsi yako.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2



عن أبي ذر أيضًا رضي الله عنه: أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((يُصْبحُ عَلَى كُلِّ سُلامَى منْ أَحَدِكُمْ صَدَقةٌ: فَكُلُّ تَسبيحَةٍ صَدَقَةٌ، وَكُلُّ تَحمِيدةٍ صَدَقَة، وَكُلُّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةٌ، وَكُلُّ تَكبيرَةٍ صَدَقَةٌ، وَأمْرٌ بِالمعرُوفِ صَدَقةٌ، ونَهيٌ عَنِ المُنْكَرِ صَدَقةٌ، وَيُجزئُ مِنْ ذلِكَ رَكْعَتَانِ يَركَعُهُما مِنَ الضُّحَى)). رواه مسلم

Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hupambaukiwa kila kiungo cha mmoja wenu kulazimika kutoa swadaqah. Kila Tasbiyh (Subhaana Allaah) ni swadaqah, kila Tahmiyd (AlhamduliLLaah) ni swadaqah, kila Tahliyl (Laa ilaaha illa-Allaah) ni swadaqah, na kila Takbiyr (Allaahu Akbar) ni swadaqah. Kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza maovu ni swadaqah. Yote haya hutosheleza na rakaa mbili za Dhwuhaa mtu anapoziswali.” [Muslim]





Hadiyth – 3



عَنْهُ، قَالَ: قَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((عُرِضَتْ عَلَيَّ أعْمَالُ أُمَّتِي حَسَنُهَا وَسَيِّئُهَا فَوَجَدْتُ في مَحَاسِنِ أعْمَالِهَا الأذَى يُمَاطُ عَنِ الطَّريقِ، وَوَجَدْتُ في مَسَاوِئِ أعمَالِهَا النُّخَاعَةُ تَكُونُ في المَسْجِدِ لا تُدْفَنُ)). رواه مسلم

Abuu Dharr (RadhwiyaAllaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Nilionyeshwa ‘amali nzuri na mbaya za Ummah wangu. Nikaona katika jumla ya mema yao ni kuondoshwa takataka njiani, na nikaona katika jumla ya mabaya yao ni kutema mate Masjid na wala yasifunikwe.” [Muslim]





Hadiyth – 4



عَنْهُ: أنَّ ناسًا قالوا: يَا رَسُولَ الله، ذَهَبَ أهلُ الدُّثُور بالأُجُورِ، يُصَلُّونَ كَمَا نُصَلِّي، وَيَصُومُونَ كَمَا نَصُومُ، وَيَتَصَدَّقُونَ بِفُضُولِ أمْوَالِهِمْ، قَالَ: ((أَوَلَيسَ قَدْ جَعَلَ اللهُ لَكُمْ مَا تَصَدَّقُونَ بِهِ: إنَّ بِكُلِّ تَسْبِيحَةٍ صَدَقةً، وَكُلِّ تَكبيرَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَحمِيدَةٍ صَدَقَةً، وَكُلِّ تَهْلِيلَةٍ صَدَقَةً، وَأمْرٌ بالمَعْرُوفِ صَدَقَةٌ، وَنَهيٌ عَنِ المُنْكَرِ صَدَقَةٌ، وفي بُضْعِ أَحَدِكُمْ صَدَقَةٌ)) قالوا: يَا رسولَ اللهِ، أيَأتِي أَحَدُنَا شَهْوَتَهُ وَيَكُونُ لَهُ فِيهَا أجْرٌ؟ قَالَ: ((أرَأيتُمْ لَوْ وَضَعَهَا في حَرامٍ أَكَانَ عَلَيهِ فِيهَا وِزرٌ؟ فكذَلِكَ إِذَا وَضَعَهَا في الحَلالِ كَانَ لَهُ أَجْرٌ)). رواه مسلم

Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Baadhi ya watu walimuendea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, matajiri wamechukua thawabu zote. Wao wanaswali kama tunavyoswali, wanafunga kama tunavyofunga na wanatoa swadaqah katika mali yao iliyobaki. Akawaambia: “Nanyi pia Allaah Amewajaalia cha kutolea swadaqah; kila Tasbiyh (Subhaana Allaah) ni swadaqah, na kila Takbiyr (Allaahu Akbar) ni swadaqah, na kila Tahliyl (Laa ilaaha illa-Allaah) ni swadaqah, na kila Tahmiyd (AlhamduliLLaah) ni swadaqah. Kuamrisha mema ni swadaqah na kukataza maovu ni swadaqah, na mmoja wenu kujimai na mke wake ni swadaqah.” Wakauliza: Ee Rasuli wa Allaah, mmoja wetu anaenda kufanya matamanio yake na awe amepata swadaqah? Akawaambia: “Nielezeni lau kitendo kile atakifanya kwa njia ya haraam, si atapata dhambi? Vile vile atakapokitenda kwa njia ya halaal atakuwa na ujira.” [Muslim]





Hadiyth – 5



عَنْهُ، قَالَ: قَالَ لي النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((لاَ تَحْقِرنَّ مِنَ المَعرُوفِ شَيئًا وَلَوْ أنْ تَلقَى أخَاكَ بِوَجْهٍ طَليقٍ)). رواه مسلم

Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alinambia: “Usidharau chochote katika wema hata kama ni kumtazama ndugu yako (Muislamu) kwa uso wenye bashasha.” [Muslim]





Hadiyth – 6



عن أبي هريرةَ رضي الله عنه، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((كُلُّ سُلامَى مِنَ النَّاسِ عَلَيهِ صَدَقَةٌ، كُلَّ يَومٍ تَطلُعُ فِيهِ الشَّمْسُ: تَعْدِلُ بَينَ الاثْنَينِ صَدَقةٌ، وتُعِينُ الرَّجُلَ في دَابَّتِهِ، فَتَحْمِلُهُ عَلَيْهَا أَوْ تَرفَعُ لَهُ عَلَيْهَا مَتَاعَهُ صَدَقَةٌ، وَالكَلِمَةُ الطَيِّبَةُ صَدَقَةٌ، وبكلِّ خَطْوَةٍ تَمشيهَا إِلَى الصَّلاةِ صَدَقَةٌ، وتُميطُ الأذَى عَنِ الطَّريقِ صَدَقَةٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

ورواه مسلم أيضًا من رواية عائشة رَضي الله عنها، قَالَتْ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّهُ خُلِقَ كُلُّ إنْسان مِنْ بَنِي آدَمَ عَلَى سِتِّينَ وثلاثمائة مفْصَل، فَمَنْ كَبَّرَ اللهَ، وحَمِدَ الله، وَهَلَّلَ اللهَ، وَسَبَّحَ الله، وَاسْتَغْفَرَ الله، وَعَزَلَ حَجَرًا عَنْ طَريقِ النَّاسِ، أَوْ شَوْكَةً، أَوْ عَظمًا عَن طَريقِ النَّاسِ، أَوْ أمَرَ بمَعْرُوف، أَوْ نَهَى عَنْ منكَر، عَدَدَ السِّتِّينَ والثَّلاثِمائَة فَإنَّهُ يُمْسِي يَومَئِذٍ وقَدْ زَحْزَحَ نَفسَهُ عَنِ النَّارِ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Viungo vyote vya wana Aadam vinawajibia kutoa swadaqah kwa kila siku inapochomozewa na jua. Kusuluhisha kwa uadilifu baina ya watu wawili ni swadaqah. Kumsaidia mtu juu ya mnyama wake ukampandisha au ukamnyanyulia mzigo wake ni swadaqah, kuongea neno zuri ni swadaqah, kila hatua unayoipiga kwenda Masjid ni swadaqah na kuondoa takataka njani ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Vile vile Muslim ameipokea Hadiyth hii kutoka katika riwaayah ya; ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika kila mwana Aadam ameumbwa kwa viungo (vilivyotengana) mia tatu na sitini, atakayemtukuza Allaah (kwa Allaahu Akbar), akamhimidi Allaah (AlhamduliLLaah), akampwekesha Allaah (laa ilaaha illa-Allaah) akamsabih Allaah (Subhaana Allaah), akamuomba Allaah maghfirah (Astaghfiru-Allaah), akaondoa jiwe katika njia wanayopita watu, au akaamrisha mema na kukataza maovu kwa hiyo idadi ya mia tatu na sitini, hakika siku hiyo atafikwa na jioni haliyakuwa ameepushwa na moto.”





Hadiyth – 7



عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((مَنْ غَدَا إِلَى المسْجِد أَوْ رَاحَ، أَعَدَّ اللهُ لَهُ في الجَنَّةِ نُزُلًا كُلَّمَا غَدَا أَوْ رَاحَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Anayekwenda Masjid asubuhi au jioni, Allaah Humuandalia takrima (mapokelewo bora) Jannah kila anapokwenda, (iwe ni) asubuhi au jioni.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 8



عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا نِسَاءَ المُسْلِمَاتِ، لا تَحْقِرنَّ جَارَةٌ لِجَارَتِهَا وَلَوْ فِرْسِنَ شاةٍ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه



Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwaambia wanawake: “Enyi wanawake wa Kiislamu, jirani asidharau kamwe kumpa zawadi jirani yake japo ni kwato ya mbuzi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 9



عَنْهُ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((الإيمانُ بِضْعٌ وَسَبعُونَ أَوْ بِضعٌ وسِتُونَ شُعْبَةً: فَأفْضَلُهَا قَولُ: لا إلهَ إلا اللهُ، وَأَدْنَاهَا إمَاطَةُ الأذَى عَنِ الطَّريقِ، والحياءُ شُعبَةٌ مِنَ الإيمان)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Iymaan ni tanzu (matawi) sabini na kitu” au alisema: “ni tanzu (matawi) sitini na kitu, iliyo bora zaidi ni kusema: Laa Ilaaha illa-Allaah. Na ya chini ni kuondoa takataka njiani; na hayaa ni tawi katika matawi ya iymaan.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 10



عَنْهُ: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((بَينَما رَجُلٌ يَمشي بِطَريقٍ اشْتَدَّ عَلَيهِ العَطَشُ، فَوَجَدَ بِئرًا فَنَزَلَ فِيهَا فَشربَ، ثُمَّ خَرَجَ فإذَا كَلْبٌ يَلْهَثُ يأكُلُ الثَّرَى مِنَ العَطَشِ، فَقَالَ الرَّجُلُ: لَقَدْ بَلَغَ هَذَا الكَلْبُ مِنَ العَطَشِ مِثلُ الَّذِي كَانَ قَدْ بَلَغَ مِنِّي فَنَزَلَ البِئْرَ فَمَلأَ خُفَّهُ مَاءً ثُمَّ أمْسَكَهُ بفيهِ حَتَّى رَقِيَ، فَسَقَى الكَلْبَ، فَشَكَرَ الله لَهُ، فَغَفَرَ لَهُ)) قالوا: يَا رَسُول اللهِ، إنَّ لَنَا في البَهَائِمِ أَجْرًا؟ فقَالَ: ((في كُلِّ كَبِدٍ رَطْبَةٍ أجْرٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ.

وفي رواية للبخاري: ((فَشَكَرَ اللهُ لَهُ، فَغَفَرَ لَهُ، فأدْخَلَهُ الجَنَّةَ))

وفي رواية لهما: ((بَيْنَما كَلْبٌ يُطِيفُ بِرَكِيَّةٍ قَدْ كَادَ يقتلُهُ العَطَشُ إِذْ رَأَتْهُ بَغِيٌّ مِنْ بَغَايَا بَنِي إسْرَائِيل، فَنَزَعَتْ مُوقَها فَاسْتَقَتْ لَهُ بِهِ فَسَقَتْهُ فَغُفِرَ لَهَا بِهِ))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kulikuwa na mtu aliyekuwa akitembea njiani, akashikwa na kiu, akaona kisima. Akateremka ndani na akanywa maji, kisha akatoka, mara akamuona mbwa ana hema anakula mchanga kwa sababu ya kiu. Yule mtu akasema: Mbwa huyu amepatwa na kiu kama kile kilichonipata. Akateremka kisimani, akaijaza maji khuffu yake halafu akaizuia kwenye mdomo wake, akapanda hata akafika juu, akamnywesha mbwa yule. Allaah Akamlipa na Akamghufuria.” Maswahaba wakauliza: Kwani sisi tuna ujira katika Wanyama? Akawajibu: “Kunywesha kila kilicho hai ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema: “Allaah Akamlipa, Akamghufuria na Akamuingiza Jannah.”

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy na Muslim zimesema: “Mbwa aliokuwa akizunguka kando ya kisima, alikaribia kufa kwa kiu, ghafla akaonekana na mwanamke mmoja wa kikahaba katika wana wa Israiyl, akaivua khuffu yake, akachotea maji na akamnywesha, akaghufuriwa kwa kitendo hicho.”





Hadiyth – 11



عَنْهُ، عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((لَقدْ رَأيْتُ رَجُلًا يَتَقَلَّبُ في الجَنَّةِ في شَجَرَةٍ قَطَعَهَا مِنْ ظَهْرِ الطَرِيقِ كَانَتْ تُؤذِي المُسْلِمِينَ)). رواه مسلم.

وفي رواية: ((مَرَّ رَجُلٌ بِغُصْنِ شَجَرَةٍ عَلَى ظَهرِ طَرِيقٍ، فَقَالَ: وَاللهِ لأُنْحِيَنَّ هَذَا عَنِ المُسْلِمينَ لا يُؤذِيهِمْ، فَأُدخِلَ الجَنَّةَ)).

وفي رواية لهما: ((بَيْنَمَا رَجُلٌ يَمْشي بِطَريقٍ وَجَدَ غُصْنَ شَوكٍ عَلَى الطريقِ فأخَّرَه فَشَكَرَ اللهُ لَهُ، فَغَفَرَ لَهُ))



Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kwa hakika nilimuona mtu akitembea Jannah kwa sababu ya mti alioukata katikati ya njia uliokuwa ukiwaudhi Waislaamu.” [Muslim]

Riwaayah nyingine inasema: “Mtu mmoja alipita katikati ya tawi la mti uliokuwa katikati ya njia, akasema: Wa-Allaahi nitaliondoa tawi hili lisiwaudhi Waislaamu. Akaingizwa Jannah.”

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy na Muslim imesema: “Mtu mmoja alipokuwa akitembea njiani, akakuta tawi la mtu wenye miba njiani, akaliweka nyuma. Allaah Akamjazi na Akamghufuria.”





Hadiyth – 12



عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الوُضُوءَ، ثُمَّ أَتَى الجُمعَةَ فَاسْتَمَعَ وَأنْصَتَ غُفِرَ لَهُ مَا بَيْنَهُ وَبَيْن الجُمُعَةِ وَزِيادَةُ ثَلاثَةِ أيَّامٍ، وَمَنْ مَسَّ الحَصَا فَقَدْ لَغَا)). رواه مسلم



Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayetawadha vizuri kisha akaenda katika Swalaah ya Ijumaa, akasikiliza Khutbah na akanyamaza; ataghufuriwa baina ya Ijumaa hiyo na Ijumaa nyingine na ziada ya siku tatu, na atakayepangusa kwa vijiwe ameshafanya upuuzi.” [Muslim]





Hadiyh – 13



: عَنْهُ: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا تَوَضَّأ العَبْدُ المُسْلِمُ، أَو المُؤمِنُ فَغَسَلَ وَجْهَهُ خَرَجَ مِنْ وَجْهِهِ كُلُّ خَطِيئَةٍ نَظَرَ إِلَيْهَا بِعَينهِ مَعَ المَاءِ، أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ، فَإِذا غَسَلَ يَدَيْهِ خَرَجَ مِنْ يَدَيهِ كُلُّ خَطِيئَة كَانَ بَطَشَتْهَا يَدَاهُ مَعَ المَاءِ، أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ، فَإِذَا غَسَلَ رِجْلَيهِ خَرَجَتْ كُلُّ خَطِيئَةٍ مشتها رِجْلاَهُ مَعَ المَاء أَوْ مَعَ آخِرِ قَطْرِ المَاءِ حَتَّى يَخْرُجَ نَقِيًّا مِنَ الذُّنُوبِ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mja Muislaam au Muumin anapotawadha akaosha uso wake, litatoka katika uso wake kila dhambi alilolitazama kwa jicho lake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji. Atakapoosha mikono yake, litatoka kila dhambi alilolishika kwa mikono yake pamoja na maji au pamoja na tone la mwisho la maji. Atakapoiosha miguu yake, itatoka kila dhambi aliyoiendea kwa miguu yake pamoja na maji au tone la mwisho la maji, mpaka atoke hali ya kuwa ni msafi na hana dhambi.” [Muslim]





Hadiyth - 14



عَنْهُ، عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((الصَّلَوَاتُ الخَمْسُ، وَالجُمُعَةُ إِلَى الجُمُعَةِ، وَرَمَضَانُ إِلَى رَمَضَانَ مُكَفِّراتٌ لِمَا بَيْنَهُنَّ إِذَا اجْتُنِبَتِ الكَبَائِرُ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Swalaah tano. Ijumaa mpaka Ijumaa, na Ramadhwaan mpaka Ramadhwaan ni yenye kufuta (madhambi) yaliyo baina yake pindi yatakapoepukwa al-kabaair (madhambi makubwa).” [Muslim]





Hadiyth – 15



عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((ألا أَدُلُّكُمْ عَلَى مَا يَمْحُو اللهُ بِهِ الخَطَايَا وَيَرْفَعُ بِهِ الدَّرَجَاتِ؟)) قَالُوا: بَلَى، يَا رسولَ اللهِ، قَالَ: ((إِسْبَاغُ الوُضُوءِ عَلَى المَكَارِهِ، وَكَثْرَةُ الخُطَا إِلَى المَسَاجِدِ، وَانْتِظَارُ الصَّلاةِ بَعْدَ الصَّلاةِ فَذلِكُمُ الرِّبَاطُ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Jee, niwajulishe jambo ambalo Allaah Hufuta dhambi kwa sababu yake na Hupandisha daraja kwa sababu yake?” Wakasema: Tujulishe Ee Rasuli wa Allaah. Akawaambia: “Kutawadha vizuri wakati wa kuona karaha, kwenda hatua nyingi Masjid na kuingojea Swalaah baada ya Swalaah. Basi kufanya hayo ndio ar-ribaatwh (kujifunga katika njia ya Allaah).” [Muslim]





Hadiyth – 16



عن أبي موسى الأشعرِيِّ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ صَلَّى البَرْدَيْنِ دَخَلَ الجَنَّةَ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Abuu Muwsaa Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayeswali al-bardayni (Swalaah ya Al-Fajr na Al-‘Aswr) ataingia Jannah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 17



عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا مَرِضَ العَبْدُ أَوْ سَافَرَ كُتِبَ لَهُ مِثْلُ مَا كَانَ يَعْمَلُ مُقِيمًا صَحِيحًا)). رواه البخاري

Abuu Muwsaa Al- Ash’ariy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mja atakapougua au akasafiri, ataandikiwa mfano wa aliyokuwa akiyatenda alipokuwa nyumbani na alipokuwa mzima.” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 18



عن جَابرٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((كُلُّ مَعْرُوفٍ صَدَقَةٌ)) رواه البخاري، ورواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahhu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila kitendo chema ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 19



عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَا مِنْ مُسْلِمٍ يَغْرِسُ غَرْسًا إلا كَانَ مَا أُكِلَ مِنْهُ لَهُ صَدَقَةً، وَمَا سُرِقَ مِنهُ لَهُ صَدَقَةً، وَلا يَرْزَؤُهُ أَحَدٌ إلا كَانَ لَهُ صَدَقَةً)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Muislamu yeyote atakayepandikiza mti basi chochote kitakacholiwa katika mti huo ni swadaqah yake, na kitakachoibiwa ni swadaqah yake, na chochote kitakachopunguza itakuwa ni swadaqah yake.” [Muslim]





Hadiyth – 20



عَنْهُ، قَالَ: أراد بنو سَلِمَةَ أَن يَنتقِلوا قرب المسجِدِ فبلغ ذلِكَ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ لهم: ((إنَّهُ قَدْ بَلَغَني أنَّكُمْ تُرِيدُونَ أنْ تَنتَقِلُوا قُربَ المَسجِد؟)) فقالُوا: نَعَمْ، يَا رَسُول اللهِ قَدْ أَرَدْنَا ذلِكَ. فَقَالَ: ((بَنِي سَلِمَةَ، دِيَارَكُمْ تُكْتَبْ آثَارُكُمْ، ديَارَكُمْ تُكْتَبْ آثَارُكُمْ)). رواه مسلم

وفي روايةٍ: ((إنَّ بِكُلِّ خَطوَةٍ دَرَجَةً)). رواه مسلم

Jaabir (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Watu wa kabila la Banu Salamah walitaka kuhamia karibu na Masjid. Habari hiyo ilimfikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Akawauliza: “Nimesikia kuwa mnataka kuhamia karibu na Masjid.” Wakajibu: Ndio Ee Rasuli wa Allaah, tumetaka kufanya hivyo. Akawaambia: “Enyi Banu Salamah, kaeni huko huko majumbani mwenu (msihame), hatua zenu zinaandikwa, kaeni huko huko hatua zenu zinaandikwa.” [Muslim]

Riwaayah nyingine imesema: “Hakika katika kila hatua kuna daraja.” [Muslim]





Hadiyth – 21



عن أبي المنذِر أُبيِّ بنِ كَعْب رضي الله عنه، قَالَ: كَانَ رَجُلٌ لا أعْلَمُ رَجلًا أبْعَدَ مِنَ المَسْجِدِ مِنْهُ، وَكَانَ لا تُخْطِئُهُ صَلاةٌ، فَقيلَ لَهُ أَوْ فَقُلْتُ لَهُ: لَوِ اشْتَرَيْتَ حِمَارًا تَرْكَبُهُ في الظَلْمَاء وفي الرَّمْضَاء؟ فَقَالَ: مَا يَسُرُّنِي أنَّ مَنْزِلي إِلَى جَنْبِ المَسْجِدِ إنِّي أريدُ أنْ يُكْتَبَ لِي مَمشَايَ إِلَى المَسْجِدِ وَرُجُوعِي إِذَا رَجَعْتُ إِلَى أهْلِي فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((قَدْ جَمَعَ اللهُ لَكَ ذلِكَ كُلَّهُ)). رواه مسلم

وفي رواية: ((إنَّ لَكَ مَا احْتَسَبْتَ))

Abuu Al-Mundhir, Ubayy bin Ka’b (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Alikuwepo mtu mmoja, sijui kama kuna mwengine aliyekuwa anaishi mbali zaidi na Masjid kulikoni mtu huyo, alikuwa hapitwi na Swalaah yoyote. Akaulizwa au nikamuuliza: Waonaje lau ungalinunua punda wakati wa giza na wakati mchanga ukiwa umepata joto? Akajibu: Sipendelei nyumba yangu iwepo karibu na Masjid, mimi nataka niandikiwe hatua zangu za kwenda Masjid na kurejea kwangu kwa familia yangu.” Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Allaah Ameshakujumuishia yote.” [Muslim]

Riwaayah nyingine imesema: “Umeshapata ulilotarajia.”





Hadiyth – 22



عن أبي محمد عبدِ اللهِ بنِ عمرو بن العاصِ- رَضي الله عنهما، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((أرْبَعُونَ خَصْلَةً: أعْلاَهَا مَنيحَةُ العَنْزِ، مَا مِنْ عَامِلٍ يَعْمَلُ بِخَصْلَة مِنْهَا؛ رَجَاءَ ثَوَابِهَا وتَصْدِيقَ مَوْعُودِهَا، إلا أدْخَلَهُ اللهُ بِهَا الجَنَّةَ)). رواه البخاري

Abuu Muhammad, ‘Abdullaah bin ‘Amruw bin ‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna mambo arubaini ya wema, la juu kabisa ni mtu akopeshe mbuzi wake. Hakuna yeyote atakayetenda mojawapo katika hayo kwa kutarajia thawabu zake na kusadikisha miadi yake, isipokuwa Allaah Atamuingiza Jannah.” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 23



عن عَدِي بنِ حَاتمٍ رضي الله عنه قَالَ: سمعت النَّبيّ صلى الله عليه وسلم يقول: ((اتَّقُوا النَّارَ وَلَوْ بشقِّ تَمْرَةٍ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

وفي رواية لهما عَنْهُ، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَا مِنْكُمْ مِنْ أَحَدٍ إلا سَيُكَلِّمُهُ رَبُّهُ لَيْسَ بَينَهُ وَبَيْنَهُ تَرْجُمَانٌ، فَيَنْظُرُ أَيْمَنَ مِنْهُ فَلا يَرَى إلا مَا قَدَّمَ، وَيَنْظُرُ أَشْأَمَ مِنْهُ فَلا يَرى إلا مَا قَدَّمَ، وَيَنظُرُ بَيْنَ يَدَيهِ فَلا يَرَى إلا النَّار تِلقَاءَ وَجْهِهِ، فَاتَّقُوا النَّارَ وَلَو بِشِقِّ تَمْرَةٍ، فَمَنْ لَمْ يَجِدْ فَبِكَلِمَةٍ طَيِّبَةٍ))

Abuu ‘Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Jikingeni na moto japo kwa kutoa kipande cha tende.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy na Muslim kutoka kwake (‘Adiyy) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila mmoja wenu atazungumza na Rabb wake wala hakuna mwenye kutarjam baina yake na Rabb wake. Atatazama kuliani mwake, hataona ila alichotenda, atatazama kushotoni mwake, hataona ila alichotenda, atatazama mbele yake, hataona ila moto mbele yake. Basi ogopeni moto japo kwa kutoa kipande cha tende. Asiepata, azungumze neno jema.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 24



عن أنس رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ اللهَ لَيَرْضَى عَنِ العَبْدِ أنْ يَأكُلَ الأَكْلَةَ، فَيَحمَدَهُ عَلَيْهَا، أَوْ يَشْرَبَ الشَّرْبَةَ، فَيَحْمَدَهُ عَلَيْهَا)). رواه مسلم

Anas (Radhwiya Allaahu ‘amhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Allaah Humridhia mja anapokula chakula kimoja, Humhimidi Allaah kwa kukila, au anapokunya funda moja la maji Humhimidi Allaah kwa kunywa hicho kinywaji.” [Muslim]





Hadiyth – 25



عن أَبي موسى رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((عَلَى كلّ مُسْلِمٍ صَدَقَةٌ)) قَالَ: أرأيتَ إنْ لَمْ يَجِدْ؟ قَالَ: ((يَعْمَلُ بِيَدَيْهِ فَيَنْفَعُ نَفْسَهُ وَيَتَصَدَّقُ)) قَالَ: أرأيتَ إن لَمْ يَسْتَطِعْ؟ قَالَ: ((يُعِينُ ذَا الحَاجَةِ المَلْهُوفَ)) قَالَ: أرأيتَ إنْ لَمْ يَسْتَطِعْ، قَالَ: ((يَأمُرُ بِالمعْرُوفِ أوِ الخَيْرِ)) قَالَ: أرَأيْتَ إنْ لَمْ يَفْعَلْ؟ قَالَ: ((يُمْسِكُ عَنِ الشَّرِّ، فَإِنَّهَا صَدَقَةٌ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Muwsaa (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amepokea Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Kila Muislamu inampasa kutoa swadaqah.” Maswahaba wakamuuliza: Je itakuwaje asipopata cha kutoa? Akajibu: “Afanye kazi kwa mikono yake ajinufaishe na atoe swadaqah.” Akauliza: Jee, asipoweza? Akamwambia: “Atamsaidia mwenye haja anayesononeka.” Akamuuliza: Jee, asipoweza? Akajibu: “Ataamrisha wema.” Akauliza: Jee, asipofanya? Akamjibu: “Atajizuia kutenda shari, kwani huko pia ni kutoa swadaqah.” [Al-Bukhaariy na
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب الاقتصاد في الطَّاعَة

14 - Mlango Wa Iktisadi Katika Twaa-ah (‘Ibaadah)



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:



مَا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ لِتَشْقَىٰ ﴿٢﴾

Hatukukuteremshia Qur-aan ili upate mashaka. [Twaahaa: 2]



يُرِيدُ اللَّـهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ ﴿١٨٥﴾

Allaah Anakutakieni mepesi na wala Hakutakieni magumu. [Al-Baqarah: 185]





Hadiyth – 1

عن عائشة رضي الله عنها: أنَّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم دخل عَلَيْهَا وعِندها امرأةٌ، قَالَ: ((مَنْ هذِهِ؟)) قَالَتْ: هذِهِ فُلاَنَةٌ تَذْكُرُ مِنْ صَلاتِهَا. قَالَ: ((مهْ، عَلَيْكُمْ بِمَا تُطِيقُونَ، فَواللهِ لا يَمَلُّ اللهُ حَتَّى تَمَلُّوا، وكَانَ أَحَبُّ الدِّينِ إِلَيْهِ مَا دَاوَمَ صَاحِبُهُ عَلَيهِ)) مُتَّفَقٌ عَلَيه

Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliingia kwake wakati alikuweko mwanamke. Akauliza: “Ni nani huyu?” Akamwambia: Huyu ni mtu fulani anayetajwa kusifiwa kwa Swalaah zake. Akasema: “Wacheni hayo! Fanyeni mnayoweza, wa-Allaahi, Allaah Hachoki kuwaandikia thawabu zenu mpaka mtakapochoka nyinyi wenyewe (kufanya ‘ibaadah). Na ‘amali bora kabisa mbele ya Allaah ni ile anayodumu nayo mwenye kuifanya.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 2

وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: جَاءَ ثَلاثَةُ رَهْطٍ إِلَى بُيُوتِ أزْوَاجِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، يَسْأَلُونَ عَنْ عِبَادَةِ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا أُخْبِروا كَأَنَّهُمْ تَقَالُّوهَا وَقَالُوا: أَيْنَ نَحْنُ مِنَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم قدْ غُفِرَ لَهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِهِ وَمَا تَأخَّرَ. قَالَ أحدُهُم: أمَّا أنا فَأُصَلِّي اللَّيلَ أبدًا. وَقالَ الآخَرُ: وَأَنَا أصُومُ الدَّهْرَ وَلا أُفْطِرُ. وَقالَ الآخر: وَأَنا أعْتَزِلُ النِّسَاءَ فَلا أتَزَوَّجُ أبَدًا. فجاء رسولُ الله صلى الله عليه وسلم إليهم، فَقَالَ: ((أنْتُمُ الَّذِينَ قُلْتُمْ كَذَا وَكَذَا؟ أَمَا واللهِ إنِّي لأخْشَاكُمْ للهِ، وَأَتْقَاكُمْ لَهُ، لَكِنِّي أصُومُ وَأُفْطِرُ، وأُصَلِّي وَأَرْقُدُ، وَأَتَزَوَّجُ النِّساءَ، فَمَنْ رَغِبَ عَنْ سُنَّتِي فَلَيْسَ مِنِّي)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Imepokelewa na Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba kundi la watu watatu lilikuja katika nyumba za wake wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakiuliza kuhusu ‘ibaadah za Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Walipoelezwa waliziona kama ni kidogo, wakasema: Sisi hatuko sawa na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), yeye ameshaghufuriwa madhambi yake yaliyotangulia na yatakayokuja. Mmoja wao akasema: Ama mimi, nitaswali daima usiku wote. Mwengine akasema: mimi nitafunga Swawm mwaka mzima. Mwengine akasema: Mimi nitawaepuka wanawake, sitaoa kamwe. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawaendea na kuwauliza: “Ninyi ndio mliosema kadhaa na kadhaa? Ama wa-Allaahi mimi ninamkhofu Allaah zaidi ya nina taqwa zaidi kulikoni ninyi; lakini mimi ninafunga swawm na kufungua, ninaswali na ninalala, na pia ninaoa wake. Atakayekengeuka na Sunnah zangu basi si katika mimi.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 3

وعن ابن مسعود رضي الله عنه: أنّ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم، قَالَ: ((هَلَكَ المُتَنَطِّعُونَ)). قالها ثَلاثًا. رواه مسلم

Imepokewa kutoka ‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Wameangamia wenye kushadidia mambo.” Amesema hivyo mara tatu. [Muslim]





Hadiyth – 4



عن أَبي هريرةَ رضي الله عنه عن النَّبيّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إنَّ الدِّينَ يُسْرٌ، وَلَنْ يُشَادَّ الدِّيْنُ إلا غَلَبَهُ، فَسَدِّدُوا وَقَارِبُوا وَأبْشِرُوا، وَاسْتَعِينُوا بِالغَدْوَةِ وَالرَّوْحَةِ وَشَيءٍ مِنَ الدُّلْجَةِ)). رواه البخاري

وفي رواية لَهُ: ((سَدِّدُوا وَقَارِبُوا، وَاغْدُوا وَرُوحُوا، وَشَيءٌ مِنَ الدُّلْجَةِ، القَصْدَ القَصْدَ تَبْلُغُوا))

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika Dini ni nyepesi, wala hakuna atakayetia uzito katika Dini ispokuwa itamshinda, basi fanyeni kwa wastani, na karibieni katika ukamilifu na toeni bishara njema na ombeni msaada katika nyakati za asubuhi na jioni na baadhi katika nyakati za usiku.” [Al-Bukhaariy]

Riwaayah nyingine ya Al-Bukhaariy imesema: “Karibieni katika ukamilifu, fanyeni wastani, na wahini nyakati za asubuhi, jioni na baadhi ya nyakati za usiku kwa wastani wastani, mtafikia (malengo).”





Hadiyth – 5



وعن أنس رضي الله عنه قَالَ: دَخَلَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم المَسْجِدَ فَإِذَا حَبْلٌ مَمْدُودٌ بَيْنَ السَّارِيَتَيْنِ، فَقَالَ: ((مَا هَذَا الحَبْلُ؟)) قالُوا: هَذَا حَبْلٌ لِزَيْنَبَ، فَإِذَا فَتَرَتْ تَعَلَّقَتْ بِهِ. فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((حُلُّوهُ، لِيُصلِّ أَحَدُكُمْ نَشَاطَهُ فَإِذَا فَتَرَ فَلْيَرْقُدْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Na amepokea Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliingia Masjid, akaona kamba imefungwa baina ya nguzo mbili. Akauliza: “Kamba hii ni ya nini?” Wakasema: Hii ni kamba ya Zaynab, anapochoka hujiegemeza kwayo. Basi Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Ifungueni na kila mmoja wenu aswali kwa nguvu zake, atakapochoka alale.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 6



وعن عائشة رضي الله عنها: أنَّ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا نَعَسَ أَحَدُكُمْ وَهُوَ يُصَلِّي فَلْيَرْقُدْ حَتَّى يَذْهَبَ عَنْهُ النَّومُ، فإِنَّ أحدكم إِذَا صَلَّى وَهُوَ نَاعِسٌ لا يَدْرِي لَعَلَّهُ يَذْهَبُ يَسْتَغْفِرُ فَيَسُبُّ نَفْسَهُ)). مُتَّفَقٌ عَلَيه

Na kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Anaposinzia mmoja wenu huku akiwa anaswali, basi alale mpaka usingizi utakapommalizikia kwani mmoja wenu atakaposwali na hali anasinzia, hatofahamu anayoyasema, hivyo huenda akawa anakusudia kuomba maghfirah kumbe anaitukana nafsi yake.” [Al-Bukhariy na Muslim]





Hadiyth – 7



وعن أَبي عبد الله جابر بن سمرة رضي الله عنهما، قَالَ: كُنْتُ أصَلِّي مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم الصَّلَوَاتِ، فَكَانتْ صَلاتُهُ قَصْدًا وَخُطْبَتُهُ قَصْدًا. رواه مسلم

Abuu ‘Abdillaah, Jaabir bin Samurah (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilikuwa nikiswali pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) baadhi ya Swalaah na ilikuwa Swalaah yake ni ya wastani na khutbah yake ilikuwa ni wastani.” [Muslim]





Hadiyth – 8



وعن أبي جُحَيْفَة وَهْب بنِ عبد اللهِ رضي الله عنه قَالَ: آخَى النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم بَيْنَ سَلْمَانَ وَأَبي الدَّرْداءِ، فَزارَ سَلْمَانُ أَبَا الدَّرداءِ فَرَأى أُمَّ الدَّرداءِ مُتَبَذِّلَةً، فَقَالَ: مَا شَأنُكِ؟ قَالَتْ: أخُوكَ أَبُو الدَّردَاءِ لَيْسَ لَهُ حَاجَةٌ في الدُّنْيَا، فَجاءَ أَبُو الدَّرْدَاءِ فَصَنَعَ لَهُ طَعَامًا، فَقَالَ لَهُ: كُلْ فَإِنِّي صَائِمٌ، قَالَ: مَا أنا بِآكِلٍ حَتَّى تَأكُلَ فأكل، فَلَمَّا كَانَ اللَّيلُ ذَهَبَ أَبُو الدَّردَاءِ يَقُومُ فَقَالَ لَهُ: نَمْ، فنام، ثُمَّ ذَهَبَ يَقُومُ فَقَالَ لَهُ: نَمْ. فَلَمَّا كَانَ من آخِر اللَّيلِ قَالَ سَلْمَانُ: قُم الآن، فَصَلَّيَا جَمِيعًا فَقَالَ لَهُ سَلْمَانُ: إنَّ لِرَبِّكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِنَفْسِكَ عَلَيكَ حَقًّا، وَلأَهْلِكَ عَلَيكَ حَقًّا، فَأعْطِ كُلَّ ذِي حَقٍّ حَقَّهُ، فَأَتَى النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم فَذَكَرَ ذلِكَ لَهُ فَقَالَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم: ((صَدَقَ سَلْمَانُ)). رواه البخاري

Abuu Juhayfah, Wahb bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alifunga undugu baina ya Salmaan na Abuu Dardaa. Salmaan akaenda kumtembelea Abuu Dardaa, akamuona mama Dardaa amevaa nguo iliyochakaa. Akamuuliza: Mbona upo hivyo? Akasema: Nduguyo Abuu Dardaa hana haja ya dunia (hataki wanawake). Abuu Dardaa akaja, akamtengenezea chakula nduguye (Salmaan) kisha akamwambia: Kula mimi nimefunga swawm. Salmaan akamwambia: Sitokula mpaka uanze wewe kula. Akala. Ulipofika usiku Abuu Dardaa akataka kuanza kuswali (Swalaah ya usiku). Salmaan akamwambia: Lala. Akalala. Ulipofika mwisho wa usiku Salmaan akamwambia sasa amka (uswali). Wakaswali wote. Kisha Salmaan akamwambia: Hakika Rabb wako Ana haki juu yako, na nafsi yako ina haki juu yako, na mkeo na familia yako wana haki juu yako. Kwa hiyo kila mmoja mpe haki yake. Abuu Dardaa akamuendea Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akatajiwa hayo, hapo Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Salmaan amepatia” [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 9



وعن أَبي محمد عبدِ اللهِ بنِ عَمْرو بن العاصِ رضي الله عنهما، قَالَ: أُخْبرَ النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم أنِّي أقُولُ: وَاللهِ لأَصُومَنَّ النَّهَارَ، وَلأَقُومَنَّ اللَّيلَ مَا عِشْتُ. فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((أنتَ الَّذِي تَقُولُ ذلِكَ؟)) فَقُلْتُ لَهُ: قَدْ قُلْتُهُ بأبي أنْتَ وأمِّي يَا رسولَ الله. قَالَ: ((فَإِنَّكَ لا تَسْتَطِيعُ ذلِكَ فَصُمْ وَأَفْطِرْ، وَنَمْ وَقُمْ، وَصُمْ مِنَ الشَّهْرِ ثَلاثةَ أيَّامٍ، فإنَّ الحَسَنَةَ بِعَشْرِ أمْثَالِهَا وَذَلكَ مِثلُ صِيامِ الدَّهْرِ)) قُلْتُ: فَإِنِّي أُطيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذلِكَ، قَالَ: ((فَصُمْ يَومًا وَأَفْطِرْ يَوْمَيْنِ)) قُلْتُ: فَإنِّي أُطِيقُ أفضَلَ مِنْ ذلِكَ، قَالَ: ((فَصُمْ يَومًا وَأفْطِرْ يَومًا فَذلِكَ صِيَامُ دَاوُد صلى الله عليه وسلم، وَهُوَ أعْدَلُ الصيامِ))

وفي رواية: ((هُوَ أفْضَلُ الصِّيامِ)) فَقُلْتُ: فَإِنِّي أُطيقُ أفْضَلَ مِنْ ذلِكَ، فَقَالَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((لا أفضَلَ مِنْ ذلِكَ))، قال: وَلأنْ أكُونَ قَبِلْتُ الثَّلاثَةَ الأَيّامِ الَّتي قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم أحَبُّ إليَّ مِنْ أهْلي وَمَالي

وفي رواية: ((أَلَمْ أُخْبَرْ أنَّكَ تَصُومُ النَّهَارَ وتَقُومُ اللَّيلَ؟)) قُلْتُ: بَلَى، يَا رَسُول الله، قَالَ: ((فَلا تَفْعَلْ: صُمْ وَأَفْطِرْ، وَنَمْ وَقُمْ؛ فإنَّ لِجَسَدِكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِعَيْنَيكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِزَوْجِكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإِنَّ لِزَوْرِكَ عَلَيْكَ حَقًّا، وَإنَّ بِحَسْبِكَ أنْ تَصُومَ في كُلِّ شَهْرٍ ثَلاثَةَ أيَّامٍ، فإنَّ لَكَ بِكُلِّ حَسَنَةٍ عَشْرَ أمْثَالِهَا، فَإِنَّ ذلِكَ صِيَامُ الدَّهْر)) فَشَدَّدْتُ فَشُدِّدَ عَلَيَّ، قُلْتُ: يَا رَسُول الله، إنِّي أجِدُ قُوَّةً، قَالَ: ((صُمْ صِيَامَ نَبيِّ الله دَاوُد وَلا تَزد عَلَيهِ)) قُلْتُ: وَمَا كَانَ صِيَامُ دَاوُد؟ قَالَ: ((نِصْفُ الدَّهْرِ)) فَكَانَ عَبدُ الله يقول بَعدَمَا كَبِرَ: يَا لَيتَنِي قَبِلْتُ رُخْصَة رَسُول الله صلى الله عليه وسلم.

وفي رواية: ((أَلَمْ أُخْبَرْ أَنَّكَ تَصُومُ الدَّهرَ، وَتَقْرَأُ القُرآنَ كُلَّ لَيْلَة؟)) فقلت: بَلَى، يَا رَسُول الله، وَلَمْ أُرِدْ بذلِكَ إلا الخَيرَ، قَالَ: ((فَصُمْ صَومَ نَبيِّ اللهِ دَاوُد، فَإنَّهُ كَانَ أعْبَدَ النَّاسِ، وَاقْرَأ القُرْآنَ في كُلِّ شَهْر)) قُلْتُ: يَا نَبيَّ اللهِ، إنِّي أُطِيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذلِكَ؟ قَالَ: ((فاقرأه في كل عشرين)) قُلْتُ: يَا نبي الله، إني أطيق أفضل من ذلِكَ؟ قَالَ: ((فَاقْرَأهُ في كُلِّ عَشْر)) قُلْتُ: يَا نبي اللهِ، إنِّي أُطيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذلِكَ؟ قَالَ: ((فاقْرَأهُ في كُلِّ سَبْعٍ وَلا تَزِدْ عَلَى ذلِكَ)) فشدَّدْتُ فَشُدِّدَ عَلَيَّ وَقالَ لي النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((إنَّكَ لا تَدرِي لَعَلَّكَ يَطُولُ بِكَ عُمُرٌ)) قَالَ: فَصِرْتُ إِلَى الَّذِي قَالَ لي النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم. فَلَمَّا كَبِرْتُ وَدِدْتُ أنِّي كُنْتُ قَبِلتُ رُخْصَةَ نَبيِّ الله صلى الله عليه وسلم.

وفي رواية: ((وَإِنَّ لِوَلَدِكَ عَلَيْكَ حَقًّا))

وفي رواية: ((لا صَامَ مَنْ صَامَ الأَبَدَ)) ثلاثً

: وفي رواية: ((أَحَبُّ الصِيَامِ إِلَى اللهِ تَعَالَى صِيَامُ دَاوُد، وَأَحَبُّ الصَّلاةِ إِلَى اللهِ تَعَالَى صَلاةُ دَاوُدَ: كَانَ ينام نصف الليل، ويقوم ثلثه، وينام سدسه، وكان يصوم يومًا ويفطر يومًا، وَلا يَفِرُّ إِذَا لاقَى))

وفي رواية قال: أنْكَحَني أَبي امرَأةً ذَاتَ حَسَبٍ وَكَانَ يَتَعَاهَدُ كنَّتَهُ-- أي: امْرَأَةَ وَلَدِهِ- فَيَسْأَلُهَا عَنْ بَعْلِهَا. فَتقُولُ لَهُ: نِعْمَ الرَّجُلُ مِنْ رَجُلٍ لَمْ يَطَأْ لَنَا فِرَاشًا، وَلَمْ يُفَتِّشْ لَنَا كَنَفًا مُنْذُ أتَيْنَاهُ. فَلَمَّا طَالَ ذلِكَ عَلَيهِ ذَكَرَ ذلك للنَّبيِّ صلى الله عليه وسلم، فَقَالَ: ((القِنِي بِهِ)) فَلَقيتُهُ بَعد ذلك، فَقَالَ: ((كَيْفَ تَصُومُ؟)) قُلْتُ: كُلَّ يَومٍ، قَالَ: ((وَكَيْفَ تَخْتِمُ؟)) قُلْتُ: كُلَّ لَيْلَةٍ، وَذَكَرَ نَحْوَ مَا سَبَقَ، وَكَانَ يَقْرَأُ عَلَى بَعْضِ أهْلِهِ السُّبُعَ الَّذِي يَقْرَؤُهُ، يَعْرِضُهُ مِنَ النَّهَارِ ليَكُونَ أخفّ عَلَيهِ باللَّيلِ، وَإِذَا أَرَادَ أنْ يَتَقَوَّى أفْطَرَ أيَّامًا وَأحْصَى وَصَامَ مِثْلَهُنَّ كرَاهِيَةَ أنْ يَترُكَ شَيئًا فَارَقَ عَلَيهِ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم



Abuu Muhammad, ‘Abdillaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliaambiwa kuwa mimi nasema: Wa-Allaahi nitafunga swawm mchana na nitaswali usiku maisha yangu yote. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniuliza: “Wewe ndiye uliyesema hivyo?” Nikamjibu: Ndiyo, hakika nimesema, nakutolee fidia baba yangu na mama yangu ee Rasuli wa Allaah. Akaniambia: “Wewe hutaweza kufanya hivyo, kwa hivyo funga swawm na ule, lala na uswali, na ufunge swawm siku tatu kila mwezi; kwani jema moja hulipwa kwa mema kumi mfano wake, na hiyo ni kama swiyaam ya dahari!” Nikamwambia: Mimi naweza kufanya zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Basi funga swawm siku moja na ule siku mbili.” Nikamwambia: Mimi naweza zaidi ya hivyo. Akanambia: “Basi funga swawm siku moja na ule siku moja, hivyo ni swiyaam ya Nabiy Daawuwd (‘Alayhis Salaam) nayo ndio Swawm ya wastani zaidi.”

Riwaayah nyingine imesema: “Hiyo ndiyo Swawm bora zaidi.” Nikamwambia: Mimi naweza zaidi ya hivyo. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: “Hakuna bora zaidi ya hivyo.” Kwa kweli lau ningelikubali zile siku tatu alizonipa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ingelipendeza kwangu zaidi kulikoni familia yangu na mali yangu.

Riwaayah nyingine imesema: “Si niliambiwa kuwa wewe unafunga swawm mchana na usiku wote unaswali?” Nikamjibu: Ndiyo ee Rasuli wa Allaah. Akaniambia: “Usifanye hivyo, funga swawm na ule, lala na uswali, hakika mwili wako una haki juu yako, na macho yako yana haki juu yako, na mkeo ana haki juu yako na mgeni wako ana haki juu yako, na hakika inakutosha ufunge swawm siku tatu kila mwezi; kwani katika kila jambo jema moja unapata mema kumi mfano wake; huko ndiyo swiyaam ya dahari!” Nikamkazania, nami nikakaziwa. Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, nina nguvu zaidi. Akanambia: “Funga Swawm ya Nabiy Daawuwd wala usizidishe juu ya hapo.” Nikamuuliza: Swawm ya Nabiy Daawuwd ilikuwaje? Akaniambia: “Nusu ya dahari.”

‘Abdullaah alipozeeka alikuwa akisema: Laiti kama ningelikubali ruhusa ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

Riwaayah nyingine imesema: “Si niliambiwa kuwa unafunga swawm dahari na unasoma Qur-aan yote kila usiku?” Nikamjibu: Ndiyo ee Rasuli wa Allaah, wala sijakusudia kufanya hivyo ila ni khayr tu. Akaniambia: “Funga Swawm ya Nabiy Daawuwd; kwani yeye aliwashinda watu kwa ‘ibaadah, na soma (ukhitimishe) Qur-aan kila mwezi.” Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, mimi naweza zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Soma kwa siku ishirini.” Nikamwambia: Ee Nabiy wa Allaah, mimi naweza zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Soma kwa siku kumi.” Nikamwambia: Ee Nabiy wa Allaah, mimi naweza zaidi ya hivyo. Akaniambia: “Soma umalize kila baada ya siku saba, wala usizidishe uchache wa hapo.” Nikatia mkazo nami nikakaziwa. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: “Huwezi kujua pengine unaweza kuwa na umri mrefu.” Na kweli nikawa kama alivyoniambia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).

Riwaayah nyingine imesema: “Na hakika mwanao ana haki juu yako.”

Na Riwaayah nyengine: “Hana Swawm mwenye kufunga daima.” Alikariri mara tatu.

Riwaayah nyingine imesema: “Swawm ipendezayo zaidi kwa Allaah ni Swawm ya Nabiy Daawuwd. Na Swalaah ipendezayo zaidi kwa Allaah ni Swalaah ya Nabiy Daawuwd; alikuwa akilala nusu ya usiku, akiswali thuluthi yake, akilala sudusi yake, na alikuwa akifunga swawm siku moja na akila siku moja, wala hakimbii anapokutana na adaui (vitani).”

Riwaayah nyingine imesema: Baba yangu alinioza mke mwenye nasaba nzuri, na alikuwa akimjulia hali mkwewe, akamuuliza hali ya mumewe, naye akimwambia: Mtu mzuri miongoni mwa watu. Kuanzia anioe, hakuja kulala na mimi wala kujamiiana nami. Hali hii ilipoendelea kwa muda mrefu, alitajiwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Akasema: “Nileteeni kwangu”. Nami nikamuendea. Akaniuliza: “Unafunga swawm vipi?” Nikamjibu: Kila siku. Akaniuliza: “Unahitimisha vipi Qur-aan?” Nikamjibu: Kila usiku. Akataja Hadiyth ambayo imetangulia kuelezwa.

‘Abdullaah alikuwa akisoma kwa baadhi ya familia yake subu’ anayoisoma (yaani alikuwa akihitimisha kwa siku saba), akiisoma mchana ili apate tahfifu wakati wa usiku. Na anapotaka tahfifu kwa kufunga swawm kila siku alikuwa anaacha kufunga swawm baadhi ya siku na baadaye kuzilipa. Anafanya hivyo kwa kuchelea asije kuacha mazoea aliyokuwa nayo mpaka wakati Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anafariki.





Hadiyth – 10



وعن أبي رِبعِي حنظلة بنِ الربيعِ الأُسَيِّدِيِّ الكاتب أحدِ كتّاب رَسُول الله صلى الله عليه وسلم، قَالَ: لَقِيَنِي أَبُو بَكر رضي الله عنه فَقَالَ: كَيْفَ أنْتَ يَا حنْظَلَةُ؟ قُلْتُ: نَافَقَ حَنْظَلَةُ! قَالَ: سُبْحَانَ الله مَا تَقُولُ؟! قُلْتُ: نَكُونُ عِنْدَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم يُذَكِّرُنَا بالجَنَّةِ وَالنَّارِ كأنَّا رَأيَ عَيْنٍ فإِذَا خَرَجْنَا مِنْ عِنْدِ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم عَافَسْنَا الأَزْواجَ وَالأَوْلاَدَ وَالضَّيْعَاتِ نَسينَا كَثِيرًا، قَالَ أَبُو بكر رضي الله عنه: فَوَالله إنَّا لَنَلْقَى مِثْلَ هَذَا، فانْطَلَقْتُ أَنَا وأبُو بَكْر حَتَّى دَخَلْنَا عَلَى رَسُول الله صلى الله عليه وسلم. فقُلْتُ: نَافَقَ حَنْظَلَةُ يَا رَسُول اللهِ! فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((وَمَا ذَاكَ؟)) قُلْتُ: يَا رَسُول اللهِ، نَكُونُ عِنْدَكَ تُذَكِّرُنَا بِالنَّارِ والجَنَّةِ كأنَّا رَأيَ العَيْن فإِذَا خَرَجْنَا مِنْ عِنْدِكَ عَافَسْنَا الأَزْواجَ وَالأَوْلاَدَ وَالضَّيْعَاتِ نَسينَا كَثِيرًا. فَقَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((وَالَّذِي نَفْسي بِيَدِهِ، لَوْ تَدُومُونَ عَلَى مَا تَكُونونَ عِنْدِي، وَفي الذِّكْر، لصَافَحَتْكُمُ الملائِكَةُ عَلَى فُرُشِكُمْ وَفي طُرُقِكُمْ، وَلَكِنْ يَا حَنْظَلَةُ سَاعَةً وسَاعَةً)) ثَلاَثَ مَرَات. رواه مسلم

Abuu Rabi’y, Handhwalah bin Ar-Rabiy’ Al-Usayyidiy ambaye ni mmoja katika waandishi wa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesimulia: “Siku moja Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alikutana nami, akaniuliza: Vipi hali ee Handhwalah? Nikamwambia: “Handhwalah anajikhofia unafiki! Akasema: Subhaana Allaah! Umesema nini? Nikamwambia: Sisi huwa tupo mbele ya Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akitukumbusha Jannah na moto kana kwamba huwa tukiziona. Lakini tunapoondoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hushughulika na wake zetu na watoto wetu na shughuli za kuendesha maisha yetu, hivyo hutufanya tusahau mengi. Abuu Bakr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: Wa-Allaahi nasi pia hukutana na hali kama hii. Mimi na Abuu Bakr tukaenda kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) nikamwambia: Handhwalah anajikhofia unafiki ee Rasuli wa Allaah, tunapokuwa kwako unatukumbusha moto na Jannah kana kwamba tunaziona kwa macho, tunapoondoka kwako, hushughulika na wake zetu na watoto wetu na shughuli za kuendesha maisha yetu, hivyo hutufanya tusahau mengi. Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Naapa kwa Ambaye nasfi yangu ipo mikononi Mwake, lau mnadumu katika hali mnayokuwa nayo kwangu na katika kumdhukuru Allaah, basi Malaika wangewasalimia nyinyi mnapokuwa vitandani mwenu na njiani. Lakini ee Handhwalah, kuna wakati wa kutekeleza ‘ibaadah na kuna wakati wa kuangalia mambo ya maisha.” Alikariri hivyo mara tatu. [Muslim]





Hadiyth – 11



وعنِ ابن عباس رضي الله عنهما، قَالَ: بينما النَّبيُّ صلى الله عليه وسلم يخطب إِذَا هُوَ برجلٍ قائم فسأل عَنْهُ، فقالوا: أَبُو إسْرَائيلَ نَذَرَ أنْ يَقُومَ في الشَّمْسِ وَلا يَقْعُدَ، وَلا يَسْتَظِل، وَلا يَتَكَلَّمَ، وَيَصُومَ، فَقَالَ النَّبيّ صلى الله عليه وسلم: ((مُرُوهُ، فَلْيَتَكَلَّمْ، وَلْيَسْتَظِلَّ، وَلْيَقْعُدْ، وَلْيُتِمَّ صَوْمَهُ)). رواه البخاري

‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alipokuwa ana khutubia, mara akamuona mtu amesimama. Akauliza kuhusu mtu huyo. Akaambiwa kuwa huyo ni Abuu Israaiyl ambaye ameweka nadhiri atasimama katika jua wala hatoki, wala hatajikinga na kivuli, wala hatazungumza na atafunga swawm. Basi Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Mwambieni azungumze, akae kivulini, akae chini na atimize Swawm yake.” [Al-Bukhaariy]
 
Riyaadhw Asw-Swaalihiyn



باب المحافظة عَلَى الأعمال

15 - Mlango Wa Kuhifadhi ‘Amali



Alhidaaya.com



قَالَ الله تَعَالَى:



أَلَمْ يَأْنِ لِلَّذِينَ آمَنُوا أَن تَخْشَعَ قُلُوبُهُمْ لِذِكْرِ اللَّـهِ وَمَا نَزَلَ مِنَ الْحَقِّ وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ﴿١٦﴾

Je, haujafika wakati kwa walioamini kwamba zinyenyekee nyoyo zao kwa ukumbusho wa Allaah na yale yaliyoteremka ya haki, na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? [Al-Hadiyd: 16]



وَقَفَّيْنَا بِعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ وَآتَيْنَاهُ الْإِنجِيلَ وَجَعَلْنَا فِي قُلُوبِ الَّذِينَ اتَّبَعُوهُ رَأْفَةً وَرَحْمَةً وَرَهْبَانِيَّةً ابْتَدَعُوهَا مَا كَتَبْنَاهَا عَلَيْهِمْ إِلَّا ابْتِغَاءَ رِضْوَانِ اللَّـهِ فَمَا رَعَوْهَا حَقَّ رِعَايَتِهَا ﴿٢٧﴾

Na Tukamfuatisha ‘Iysaa mwana wa Maryam, na Tukampa Injiyl. Na Tukaweka katika nyoyo za wale waliomfuata upole na rahmah na uruhubani (maisha ya utawa); wameyaanzisha wao wenyewe Hatukuwaandikia hayo juu yao isipokuwa ni kutafuta radhi za Allaah. Lakini hawakuuchunga ipasavyo kuchungwa. [Al-Hadiyd: 27]



وَلَا تَكُونُوا كَالَّتِي نَقَضَتْ غَزْلَهَا مِن بَعْدِ قُوَّةٍ أَنكَاثًا ﴿٩٢﴾

Na wala msiwe kama yule mwanamke aliyezongoa uzi wake vipande vipande baada ya (kuusokota na) kuwa mgumu. [An-Nahl: 92]



وَاعْبُدْ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأْتِيَكَ الْيَقِينُ ﴿٩٩﴾

Na mwabudu Rabb wako mpaka ikufikie yakini (mauti). [Al-Hajr: 99]





Hadiyth – 1

وعن عمر بن الخطاب رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ نَامَ عَنْ حِزْبهِ مِنَ اللَّيلِ، أَوْ عَنْ شَيءٍ مِنْهُ، فَقَرَأَهُ مَا بَيْنَ صَلاةِ الفَجْرِ وَصَلاةِ الظُّهْرِ، كُتِبَ لَهُ كَأَنَّمَا قَرَأَهُ مِنَ اللَّيلِ)). رواه مسلم

‘Umar bin Khatwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Atakayelala asisome hizbu (nyiradi) yake ya usiku au chochote katika hizbu yake ya usiku au chochote katika hizbu hiyo, halafu akaisoma baina ya Swalaah ya alfajiri na Swalaah ya adhuhuri, ataandikiwa kana kwamba ameisoma usiku.” [Muslim]





Hadiyth – 2

وعن عبد الله بن عَمْرو بن العاص رَضِيَ الله عنهما، قَالَ: قَالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَا عبدَ اللهِ، لا تَكُنْ مِثْلَ فُلان، كَانَ يَقُومُ اللَّيلَ فَتَرَكَ قِيَامَ اللَّيلِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

‘Abdullaah bin ‘Amruw bin Al-‘Aasw (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: Aliniambia: “Ee ‘Abdullaah, usiwe kama fulani, alikuwa akiswali usiku na kuacha kuswali usiku.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 3

وعن عائشة رضي الله عنها، قَالَتْ: كَانَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم إِذَا فَاتَتْهُ الصَّلاةُ مِنَ اللَّيلِ مِنْ وَجَعٍ أَوْ غَيرِهِ، صَلَّى مِنَ النَّهارِ ثنْتَيْ عَشرَةَ رَكْعَةً. رواه مسلم

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapopitwa na Swalaah ya usiku kwa sababu ya maradhi au jambo lingine, huswali wakati wa mchana, rakaa kumi na mbili.” [Muslim]
 
Malaika Jibril au wasio waislamu wanamuita Roho ( roho mtakatifu)

Alimwambia Nabii swallallahu alaih wasallam

'" ewe Muhammad mpende umpendaye lakini ipo siku utatengana naye na ishi utakavyoishi lakini jua ipo siku utakufa"

TUISHI NAYO HII
 
Back
Top Bottom