ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,600
- 21,653
Baadhi ya post zangu za Zamani....
JE QUR'AN NI NAKALA YA BIBLIA?
MFUMO WA UZAZI / HUMAN PRODUCTION
Kwanza nianze na mambo machache au utaratibu ambao unahusika moja Kwa moja na uzazi wa binadamu.
Mwanzo ni kurutubishwa Kwa Yai kwenye sehemu inaitwa fallopian tube,kinachotumika kurutubisha ni mbegu ya kiume (sperm) au kitalaam spermatozoon,kwahiyo kinachotakiwa ni tone dogo la manii ambalo Lina mbegu kama million 10. Na maji haya au tone hili la manii hutengenezwa na testicles (makende) na kuhifadhiwa hapo,halafu kuna glands ambazo zipo karibu na maeneo hayo ambazo huongeza au kutengeneza maji maji katika sperm.
Kwahiyo upandikizaji wa Yai ambalo tayar limepevuka hufanyika katika system ya uzazi ya mwanamke,na kupitia katika follopiana tube na kuelekea katika uterus na huko hujishikiza na hatimaye placenta inatengenezwa au inajitengeneza, na Kwa mfano kama upandikizaji wa Yai ukifanyika katika follopian tube badala ya uterus basi huo ujauzito utaharibika.
Na baada ya embryo kuweza kuonekana na jicho la kawaida basi huonekana kama muunganiko WA kanyama kadogo ambako si rahisi kujua kama binadamu,na inaendelea kukua katika hatua mbali mbali ambazo hujulikana Leo,na kuwa umbile la mifupa,misuli (muscles), mifumo ya ufahamu na kadhalika.
Sasa tuje katika mkabala au maelezo ya qura'n :
Qur'an katika mfumo mzima wa uzazi inazungumzia katika maeneo yafuatayo;
1) Utungwaji WA mimba unafanywa na kiasi kidogo cha manii/shahawa
2) kuna maji maji ya uzazi
3) kuna Utungwaji WA Yai lililo pevuka
4) mabadiliko ya embryo
1) Utungwaji WA mimba unafanywa na kiasi kidogo cha manii/shahawa
Hapa quran inazungumzia swala hili mara Kumi na moja,nitaandika baadhi ya Aya Tu:
((Amemuumba mtu kwa tone la manii. Naye mara amekuwa mshindani dhaahiri.))
16:4
((Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?))
75:37
((Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.))
23:13
2) Maji maji ya Uzazi
Qur'an inazungumzia maji maji ya Uzazi ambayo inafurahisha kuyafanyia uchambuzi hapa;
((Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.))
76:2
((Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,))
86:6
Sasa ebu tuangalie haya maji ambayo huambatana na sperm Yana mchanganyiko upi?
a) secretion of male genital gland contains spermatozoons
b) seminal vesicles - hizi organs zina hifadhi spermatozoons zipo karibu na prostate gland,zinatoa maji maji yake ingawa hazina fertilizing agent
c) prostate gland - maji maji yake inaipa sperm creamy texture and characteristic odour
d) glands annexed to the urinary tract
Na hizi ni Aina za maji maji ambazo Qur'an imezigusia na kudhibitishwa na modern science.
3) Utungwaji WA Yai lililo pevuka
Baada ya Yai kuwa fertilized katika fallopian tube inakwenda kwenye uterus na hapo inasemwa implantation of the egg.
Na Qur'an inasema hivi katika tukio Hilo;
((Nasi tunakiweka katika matumbo ya uzazi tunacho kitaka mpaka muda ulio wekwa))
22:5
Na Ile Hali ya Yai kuwa katika uterus na kujishikiza katika ukuta mwembamba Kwa AJILI ya kukua, na huo ndio ugunduzi wa modern time.
Na Hali hii pia imeelezwa katika Qur'an tangu zamani huko;
((Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.))
23:14
((Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.))
75:37-38
4) Mabadiliko ya Embryo ndani ya Uterus;
Qur'an imezungumzia mabadiliko ya kiumbe ndani ya uterus kama ambavyo modern science imedhibitisha hivyo, na yanashahabiana Sawa Sawa.
((Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.))
23:14
Modern sayansi inasema Kwanza kunakuwa na umbile kama big g/nyama iliyotafunwa ( chewing gum/chewing fresh) ,katika udogo wake kabisa ambao unaweza kuonekana na jicho la kawaida inakuwa kama nyama iliyotafunwa,halafu umbile la mifupa hujitokeza ( mesenchyma) ,halafu mifupa iliyoundwa hufunikwa na misuli ( muscle), halafu baadae organ za fahamu na kufuatiwa na jinsia za kiumbe.
((Kisha akamtengeneza, na akampulizia roho yake, na akakujaalieni kusikia na kuona, na nyoyo za kufahamu. Ni uchache mnavyo shukuru.))
32:9
((Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa))
53:45-46
Huyo ndio Mwenyezi Mungu,,hakika tukiacha ushabiki wa Imani zatu na kuziweka pembeni,unaona kabisa elimu hii ni ufunuo wa Mwenyezi Mungu Kwa mja wake Muhammad ( s.a.w).
Na kumbuka katika Karne Ile hakukuwa na maendeleo ya kufahamu nini kinaendelea ndani ya tumbo la mwanadamu kuhusiana na uzazi na kubwa zaidi kila hatua ambayo Qur'an imeeleza hakika haikutofautiana na tafiti zilizo fanywa na wavumbuzi wa Karne ya 20.
Na Mwenyezi Mungu alimchagua Mtume ambaye hajui kusoma wala kuandika ili adhibitishe maneno yake kuwa Ni ufunuo usio na Shaka ndani yake na unatoka Kwa Yule ambaye ni mjuzi WA mambo yote,yawe na Siri na yasiyo ya Siri na mambo ya ghaibu.
Mambo ni mengi na Mda ni mchache,next time panapo majaliwa INSHAALLAH
JE QUR'AN NI NAKALA YA BIBLIA?
MFUMO WA UZAZI / HUMAN PRODUCTION
Kwanza nianze na mambo machache au utaratibu ambao unahusika moja Kwa moja na uzazi wa binadamu.
Mwanzo ni kurutubishwa Kwa Yai kwenye sehemu inaitwa fallopian tube,kinachotumika kurutubisha ni mbegu ya kiume (sperm) au kitalaam spermatozoon,kwahiyo kinachotakiwa ni tone dogo la manii ambalo Lina mbegu kama million 10. Na maji haya au tone hili la manii hutengenezwa na testicles (makende) na kuhifadhiwa hapo,halafu kuna glands ambazo zipo karibu na maeneo hayo ambazo huongeza au kutengeneza maji maji katika sperm.
Kwahiyo upandikizaji wa Yai ambalo tayar limepevuka hufanyika katika system ya uzazi ya mwanamke,na kupitia katika follopiana tube na kuelekea katika uterus na huko hujishikiza na hatimaye placenta inatengenezwa au inajitengeneza, na Kwa mfano kama upandikizaji wa Yai ukifanyika katika follopian tube badala ya uterus basi huo ujauzito utaharibika.
Na baada ya embryo kuweza kuonekana na jicho la kawaida basi huonekana kama muunganiko WA kanyama kadogo ambako si rahisi kujua kama binadamu,na inaendelea kukua katika hatua mbali mbali ambazo hujulikana Leo,na kuwa umbile la mifupa,misuli (muscles), mifumo ya ufahamu na kadhalika.
Sasa tuje katika mkabala au maelezo ya qura'n :
Qur'an katika mfumo mzima wa uzazi inazungumzia katika maeneo yafuatayo;
1) Utungwaji WA mimba unafanywa na kiasi kidogo cha manii/shahawa
2) kuna maji maji ya uzazi
3) kuna Utungwaji WA Yai lililo pevuka
4) mabadiliko ya embryo
1) Utungwaji WA mimba unafanywa na kiasi kidogo cha manii/shahawa
Hapa quran inazungumzia swala hili mara Kumi na moja,nitaandika baadhi ya Aya Tu:
((Amemuumba mtu kwa tone la manii. Naye mara amekuwa mshindani dhaahiri.))
16:4
((Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?))
75:37
((Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.))
23:13
2) Maji maji ya Uzazi
Qur'an inazungumzia maji maji ya Uzazi ambayo inafurahisha kuyafanyia uchambuzi hapa;
((Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.))
76:2
((Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,))
86:6
Sasa ebu tuangalie haya maji ambayo huambatana na sperm Yana mchanganyiko upi?
a) secretion of male genital gland contains spermatozoons
b) seminal vesicles - hizi organs zina hifadhi spermatozoons zipo karibu na prostate gland,zinatoa maji maji yake ingawa hazina fertilizing agent
c) prostate gland - maji maji yake inaipa sperm creamy texture and characteristic odour
d) glands annexed to the urinary tract
Na hizi ni Aina za maji maji ambazo Qur'an imezigusia na kudhibitishwa na modern science.
3) Utungwaji WA Yai lililo pevuka
Baada ya Yai kuwa fertilized katika fallopian tube inakwenda kwenye uterus na hapo inasemwa implantation of the egg.
Na Qur'an inasema hivi katika tukio Hilo;
((Nasi tunakiweka katika matumbo ya uzazi tunacho kitaka mpaka muda ulio wekwa))
22:5
Na Ile Hali ya Yai kuwa katika uterus na kujishikiza katika ukuta mwembamba Kwa AJILI ya kukua, na huo ndio ugunduzi wa modern time.
Na Hali hii pia imeelezwa katika Qur'an tangu zamani huko;
((Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.))
23:14
((Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.))
75:37-38
4) Mabadiliko ya Embryo ndani ya Uterus;
Qur'an imezungumzia mabadiliko ya kiumbe ndani ya uterus kama ambavyo modern science imedhibitisha hivyo, na yanashahabiana Sawa Sawa.
((Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.))
23:14
Modern sayansi inasema Kwanza kunakuwa na umbile kama big g/nyama iliyotafunwa ( chewing gum/chewing fresh) ,katika udogo wake kabisa ambao unaweza kuonekana na jicho la kawaida inakuwa kama nyama iliyotafunwa,halafu umbile la mifupa hujitokeza ( mesenchyma) ,halafu mifupa iliyoundwa hufunikwa na misuli ( muscle), halafu baadae organ za fahamu na kufuatiwa na jinsia za kiumbe.
((Kisha akamtengeneza, na akampulizia roho yake, na akakujaalieni kusikia na kuona, na nyoyo za kufahamu. Ni uchache mnavyo shukuru.))
32:9
((Na kwamba Yeye ndiye aliye umba jozi, dume na jike
Kutokana na mbegu ya uzazi inapo miminwa))
53:45-46
Huyo ndio Mwenyezi Mungu,,hakika tukiacha ushabiki wa Imani zatu na kuziweka pembeni,unaona kabisa elimu hii ni ufunuo wa Mwenyezi Mungu Kwa mja wake Muhammad ( s.a.w).
Na kumbuka katika Karne Ile hakukuwa na maendeleo ya kufahamu nini kinaendelea ndani ya tumbo la mwanadamu kuhusiana na uzazi na kubwa zaidi kila hatua ambayo Qur'an imeeleza hakika haikutofautiana na tafiti zilizo fanywa na wavumbuzi wa Karne ya 20.
Na Mwenyezi Mungu alimchagua Mtume ambaye hajui kusoma wala kuandika ili adhibitishe maneno yake kuwa Ni ufunuo usio na Shaka ndani yake na unatoka Kwa Yule ambaye ni mjuzi WA mambo yote,yawe na Siri na yasiyo ya Siri na mambo ya ghaibu.
Mambo ni mengi na Mda ni mchache,next time panapo majaliwa INSHAALLAH