Ramadhan Special Thread
001-Mlango Wa Ikhlaasw Na Kutia Niyyah Katika ‘Amali Zote,

Maneno, Hali Zilizodhihirika Na Zilizofichika.



Alhidaaya.com





قَالَ اللهُ تَعَالَى

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ حُنَفَاءَ وَيُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُؤْتُوا الزَّكَاةَۚ وَذَٰلِكَ دِينُ الْقَيِّمَةِ

Na hawakuamrishwa isipokuwa wamwabudu Allaah wenye kumtakasia niyyah Dini, wenye kujiengua na upotofu kuelemea Dini ya haki na wasimamishe Swalaah na watoe Zakaah; na hiyo ndiyo Dini iliyosimama imara.[Al-Bayyinah: 5]



لَن يَنَالَ اللَّـهَ لُحُومُهَا وَلَا دِمَاؤُهَا وَلَـٰكِن يَنَالُهُ التَّقْوَىٰ مِنكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ سَخَّرَهَا لَكُمْ لِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ ۗ وَبَشِّرِ الْمُحْسِنِينَ

Haimfikii Allaah nyama zake wala damu yake, lakini inamfikia taqwa kutoka kwenu. Hivyo ndivyo Tulivyowatiisha (hao wanyama) kwenu ili mpate kumtukuza Allaah (kusema: Allaahu Akbar) kwa yale Aliyokuongozeni; na wabashirie wafanyao ihsaan. [Al-Hajj: 37]



قُلْ إِن تُخْفُوا مَا فِي صُدُورِكُمْ أَوْ تُبْدُوهُ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ ۗ وَيَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ ۗ وَاللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ

Sema: “Mkificha yale yaliyomo katika vifua vyenu au mkiyafichua, Allaah Anayajua. Na Anajua yale yaliyomo katika mbingu na yale yaliyomo katika ardhi. Na Allaah juu ya kila kitu ni Muweza.” [Aal-‘Imraan: 29]





Hadiyth - 1

وعن أمير المؤمِنين أبي حَفْصٍ عمرَ بنِ الخطابِ بنِ نُفَيْلِ بنِ عبدِ العُزّى بن رياحِ بنِ عبدِ اللهِ بن قُرْطِ بن رَزاحِ بنِ عدِي بنِ كعب بنِ لُؤَيِّ بنِ غالبٍ القُرشِيِّ العَدويِّ رضي الله عنه قالَ: سَمِعتُ رَسُولَ اللهِ صلى الله عليه وسلم يقُولُ: ((إنّمَا الأَعْمَالُ بالنِّيّاتِ، وَإِنَّمَا لِكُلِّ امرِئٍ مَا نَوَى، فَمَنْ كَانَتْ هجرته إلى الله ورسوله، فهجرته إلى الله ورسوله، ومن كانت هِجْرَتُهُ لِدُنْيَا يُصيبُهَا، أَوْ امْرَأَةٍ يَنْكَحُهَا، فَهِجْرَتُهُ إِلى مَا هَاجَرَ إِلَيْه)). مُتَّفَقٌ عَلَى صِحَّتِهِ. رَوَاهُ إمَامَا الْمُحَدّثِينَ، أبُو عَبْدِ الله مُحَمَّدُ بْنُ إسْمَاعيلَ بْن إبراهِيمَ بْن المُغيرَةِ بنِ بَرْدِزْبهْ الجُعْفِيُّ البُخَارِيُّ، وَأَبُو الحُسَيْنِ مُسْلمُ بْنُ الحَجَّاجِ بْنِ مُسْلمٍ الْقُشَيريُّ النَّيْسَابُورِيُّ رضي اللهُ عنهما فِي صحيحيهما اللَّذَيْنِ هما أَصَحُّ الكُتبِ المصنفةِ.

Kutoka kwa Amiri wa Waumini, Abu Hafsw ‘Umar bin Al-Khatwaab bin Nufayl bin ‘Abdil ‘Uzza bin Riyaah bin ‘Abdillaah bin Qurt bin Razaah bin ‘Adiyyi bin Ka’ab bin Lua-yyi bin Ghaalib Al-Qurashiyyi Al-‘Adawiyyi (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia: “Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Hakika kusihi kwa ‘amali huzingatiwa na niyyah. Na hakika kila mtu atalipwa kwa kile alichokinuia. Ambaye hijrah yake itakuwa ni kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake, basi hijrah yake itakuwa ni kwa ajili ya Allaah na Rasuli Wake. Na ambaye hijrah yake ni kuiendea dunia ili aihodhi, au kumuendea mwanamke ili amuoe; basi hijrah yake itakuwa ni kwa aliloliendea.” [Hadiyth hii imepokelewa na Maimaam wawili ‘Ulamaa wa Hadiyth, Abuu ‘Abdillaah Muhammad bin Ismaa’iyl bin Ibraahiym bin Al-Mughiyrah bin Bar-dizbah Al-Ju’fiyy Al-Bukhaariy, na Abul-Husayn Muslim bin Al-Hajjaaj bin Muslim Al-Qushayriyy An-Naysaaburiyy (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) Wameipokea katika vitabu vyao ambavyo ndio Swahiyh katika vitabu vya Hadiyth vilivyosanifiwa]





Hadiyth - 2

وعن أمِّ المؤمِنينَ أمِّ عبدِ اللهِ عائشةَ رضي الله عنها قالت: قالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((يَغْزُو جَيْشٌ الْكَعْبَةَ فإِذَا كَانُوا بِبَيْدَاءَ مِنَ الأَرضِ يُخْسَفُ بِأَوَّلِهِمْ وآخِرِهِمْ)). قَالَتْ: قلتُ: يَا رَسُولَ اللهِ، كَيْفَ يُخْسَفُ بأوَّلِهِمْ وَآخِرِهِمْ وَفِيهمْ أسْوَاقُهُمْ وَمَنْ لَيْسَ مِنْهُمْ؟! قَالَ: ((يُخْسَفُ بِأَوَّلِهِمْ وَآخِرِهِمْ ثُمَّ يُبْعَثُونَ عَلَى نِيّاتِهمْ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ. هذَا لَفْظُ الْبُخَارِيِّ

Mama wa Waumini, Ummu ‘Abdillaah, ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa), amesimulia: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kuna jeshi litakalotaka kuivamia Al-Ka’bah, litakapofika katika ardhi ya jangwa, wote watadidimizwa.” Nikauliza: Eee Rasuli wa Allaah, vipi wote wadidimizwe na miongoni mwao kuna raia wa kawaida na hawakuwa miongoni mwao? Akajibu: “Wote watadidimizwa kisha watafufuliwa kulingana na niyyah zao.” [Hadiyth hii ni lafdh ya Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 3

وعن عائِشةَ رضيَ اللهُ عنها قَالَتْ: قَالَ النبي صلى الله عليه وسلم: ((لا هِجْرَةَ بَعْدَ الفَتْحِ، وَلَكِنْ جِهَادٌ وَنِيَّةٌ، وَإِذَا اسْتُنْفِرْتُمْ فانْفِرُوا)). مُتَّفَقٌ عَلَيْه

‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema: Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakuna hijrah baada ya Fat-hi (ukombozi wa Makkah), lakini kuna jihaad na niyyah. Na mnapohimizwa kutoka katika jihaad basi nendeni haraka.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 4

وعن أبي عبدِ اللهِ جابر بن عبدِ اللهِ الأنصاريِّ رَضي اللهُ عنهما قَالَ: كُنَّا مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم في غَزَاةٍ، فَقالَ: ((إِنَّ بالمدِينَةِ لَرِجَالًا ما سِرْتُمْ مَسِيرًا، وَلا قَطَعْتُمْ وَادِيًا، إلا كَانُوا مَعَكمْ حَبَسَهُمُ الْمَرَضُ)). وَفي روَايَة: ((إلا شَرَكُوكُمْ في الأجْرِ)). رواهُ مسلمٌ.
ورواهُ البخاريُّ عن أنسٍ رضي الله عنه قَالَ: رَجَعْنَا مِنْ غَزْوَةِ تَبُوكَ مَعَ النَّبيِّ صلى الله عليه وسلم فقال: ((إنَّ أقْوامًا خَلْفَنَا بالْمَدِينَةِ مَا سَلَكْنَا شِعْبًا وَلا وَاديًا، إلا وَهُمْ مَعَنَا؛ حَبَسَهُمُ العُذْرُ))

Abu ‘Abdillaah, Jaabir bin ‘Abdillaah Al-Answaary (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Tulikuwa pamoja na Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika vita fulani. Akasema: “Hakika Madiynah kuna watu ambao nyinyi hamkwenda mwendo wowote wala hamkupita jangwa lolote isipokuwa wao walikuwa nanyi, wamezuiliwa na ugonjwa.” Na katika simulizi nyingine imesema: “Isipokuwa wameshirikiana nanyi katika ujira.” [Muslim].





Hadiyth – 5

وعن أبي يَزيدَ مَعْنِ بنِ يَزيدَ بنِ الأخنسِ رضي الله عنهم وهو وأبوه وَجَدُّه صحابيُّون قَالَ: كَانَ أبي يَزيدُ أخْرَجَ دَنَانِيرَ يَتَصَدَّقُ بِهَا، فَوَضعَهَا عِنْدَ رَجُلٍ في الْمَسْجِدِ، فَجِئْتُ فأَخذْتُها فَأَتَيْتُهُ بِهَا. فقالَ: واللهِ، مَا إيَّاكَ أرَدْتُ، فَخَاصَمْتُهُ إِلى رسولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: ((لكَ مَا نَوَيْتَ يَا يزيدُ، ولَكَ ما أخَذْتَ يَا مَعْنُ)). رواهُ البخاريُّ.

Abu Yaziyd Ma’ni bin Yaziyd bin Al-Akhnas (Radhwiya Allaahu ‘anhum), yeye na baba yake na babu yake wote ni Maswahaba, amesema: Baba yangu Yaziyd alikuwa amezitoa dinaar akizitolea swadaqah. Akaziweka kwa mtu Msikitini. Nikaja nikazichukua na nikaja nazo. Akaniambia: Wa-Allaahi sikuwa nimekukusudia wewe! Nikashtakiana naye kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), akasema: “Ee Yaziyd, utapata ulilolinuia, na ee Ma’ni! Ulichokichukua ni chako”. [Al-Bukhaariy]





Hadiyth – 6

وعن أبي إسحاقَ سَعدِ بنِ أبي وَقَّاصٍ مالِكِ بنِ أُهَيْب بنِ عبدِ منافِ ابنِ زُهرَةَ بنِ كلابِ بنِ مُرَّةَ بنِ كعبِ بنِ لُؤيٍّ القُرشِيِّ الزُّهريِّ رضي الله عنه أَحَدِ العَشَرَةِ المشهودِ لهم بالجنةِ رضي الله عنهم قَالَ: جاءنِي رسولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم يَعُودُنِي عَامَ حَجَّةِ الوَدَاعِ مِنْ وَجَعٍ اشْتَدَّ بي، فقُلْتُ: يَا رَسُولَ اللهِ! إنِّي قَدْ بَلَغَ بي مِنَ الوَجَعِ مَا تَرَى، وَأَنَا ذُو مالٍ وَلا يَرِثُني إلا ابْنَةٌ لي، أفأَتَصَدَّقُ بِثُلُثَيْ مَالِي؟ قَالَ: ((لا))، قُلْتُ: فالشَّطْرُ يَا رَسُولَ اللهِ؟ فقَالَ: ((لا))، قُلْتُ: فالثُّلُثُ يَا رَسُولَ اللهِ؟ قَالَ: ((الثُّلُثُ، والثُّلُثُ كَثيرٌ- أَوْ كبيرٌ- إنَّكَ إنْ تَذَرْ وَرَثَتَكَ أغنِيَاءَ خيرٌ مِنْ أنْ تَذَرَهُمْ عَالَةً يتكفَّفُونَ النَّاسَ، وَإنَّكَ لَنْ تُنفِقَ نَفَقَةً تَبْتَغي بِهَا وَجهَ اللهِ إلا أُجِرْتَ عَلَيْهَا حَتَّى مَا تَجْعَلُ في فِيِّ امْرَأَتِكَ))، قَالَ: فَقُلتُ: يَا رسولَ اللهِ، أُخلَّفُ بعدَ أصْحَابي؟ قَالَ: ((إِنَّكَ لَنْ تُخَلَّفَ فَتَعملَ عَمَلًا تَبتَغي بِهِ وَجْهَ اللهِ إلا ازْدَدتَ بِهِ دَرَجةً ورِفعَةً، وَلَعلَّكَ أنْ تُخَلَّفَ حَتّى يَنتَفِعَ بِكَ أقْوَامٌ وَيُضَرَّ بِكَ آخرونَ. اللَّهُمَّ أَمْضِ لأصْحَابي هِجْرَتَهُمْ ولا تَرُدَّهُمْ عَلَى أعقَابهمْ، لكنِ البَائِسُ سَعدُ بْنُ خَوْلَةَ)). يَرْثي لَهُ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم أنْ ماتَ بمَكَّة. مُتَّفَقٌ عليهِ.

Abu Is-haaq Sa’d bin Abi Waqqaas Maalik bin Uhayb bin ‘Abdi-Manaaf bin Zuhrah bin Kilaab bin Murrah bin Ka’b bin Lu-ayyi Al-Qurashiyy Az-Zuhriyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu), ambaye ni mmojawapo kati ya waliobashiriwa Jannah, amesimulia: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alinitembelea mwaka wa Hajjatul-Wadaa’i kutokana na ugonjwa ambao uliokuwa umenishitadi. Nikamwambia: Ee Rasuli wa Allaah, ugonjwa umenifikisha kama unionavyo, nami ni mwenye mali nyingi, wala hakuna atakayenirithi isipokuwa bint yangu (mmoja tu). Je, nizitoe swadaqah thuluthi mbili za mali yangu? Akasema: “Hapana.” Nikasema: Basi nitoe nusu yake ee Rasuli wa Allaah? Akasema: “Hapana”. Nikasema: Je, thuluthi (moja)? Akasema: “Thuluthi (unaweza kutoa). Na hiyo thuluthi ni nyingi – kwa hakika uwaache wenye kukurithi ni wenye kujiweza, ni bora kulikoni kuwaacha wawe mafukara wakiomba watu. Na hakika hutatoa gharama ya matumizi ukawa unataka radhi za Allaah kwa matumizi hayo, isipokuwa utapewa ujira kwayo; hata unachokitia katika kinywa cha mkeo.” Nikamwambia: Eee Rasuli wa Allaah, nitaachwa (niishi muda mrefu) baada ya wenzangu?” Akasema: “Hakika hutoachwa ukafanya 'amali kwa ajili ya kutafuta radhi ya Allaah kwa 'amali hiyo, ispokuwa utazidi daraja na utukufu kwa 'amali hiyo. Na (huenda) ukaachwa (uishi) mpaka watu wanufaike kwa sababu yako, na wengine wadhuriwe kwa sababu yako. Ee Rabb! Wakamilishie Maswahaba wangu hijrah yao, wala usiwarejeshe nyuma kwa visigino vyao. Lakini masikini ni Sa’d bin Khawlah!” Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamsikitikia kwa kuwa amekufa Makkah. [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 7

وعنْ أبي هريرةَ عبدِ الرحمنِ بنِ صخرٍ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((إنَّ الله لا ينْظُرُ إِلَى أَجْسَامِكُمْ، ولا إِلى صُوَرِكمْ، وَلَكن ينْظُرُ إلى قُلُوبِكمْ)). رواه مسلم

Abuu Hurayrah, ‘Abdir-Rahmaan bin Swakhr (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kwa hakika Allaah hatazami viwiliwili vyenu wala sura zenu, lakini Anatazama nyoyo zenu na matendo yenu.” [Muslim]





Hadiyth – 8

وعن أبي موسى عبدِ اللهِ بنِ قيسٍ الأشعريِّ رضي الله عنه قَالَ: سُئِلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَنِ الرَّجُلِ يُقاتلُ شَجَاعَةً، ويُقَاتِلُ حَمِيَّةً، ويُقَاتِلُ رِيَاءً، أَيُّ ذلِكَ في سبيلِ الله؟ فقال رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((مَنْ قَاتَلَ لِتَكونَ كَلِمَةُ اللهِ هي العُلْيَا، فَهوَ في سبيلِ اللهِ)). مُتَّفَقٌ عَلَيهِ

Abuu Muwsaa, Abdillaah bin Qays Al-Ash’ariyy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa mtu aliyepigana kwa ajili ya kuambiwa shujaa, na anayepigana kwa taasubi (ukabila), na anayepigana kwa riyaa (kujionesha), ni yupo katika hao yupo katika njia ya Allaah? Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akajibu: “Anayepigana ili Dini ya Allaah iwe juu, basi huyo yupo katika njia ya Allaah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 9



وعن أبي بَكرَةَ نُفيع بنِ الحارثِ الثقفيِّ رضي الله عنه أَنَّ النَّبيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((إِذَا التَقَى المُسلِمَان بسَيْفَيهِمَا فالقَاتِلُ وَالمَقْتُولُ في النّارِ)). قُلتُ: يا رَسُولَ اللهِ، هذا القَاتِلُ فَمَا بَالُ المقْتُولِ؟ قَالَ: ((إنَّهُ كَانَ حَريصًا عَلَى قتلِ صَاحِبهِ)). مُتَّفَقٌ عليهِ

Abu Bakrah, Nufay’i bin Al-Haarith At-Thaqafiy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesimulia kuwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) amesema: “Waislamu wawili wakipigana kwa panga zao, basi muuaji na aliyeuliwa wataingia motoni.” Nikauliza: Ee Rasuli wa Allaah, huyu aliyeua (ni sawa kuingia motoni)! Je, aliyeuliwa? Akajibu: “Yeye aliyeuliwa alikuwa na hamu ya kumuua mwenzie.” [Al-Bukhaariy na Muslim]





Hadiyth – 10



وعن أبي هريرةَ رضي الله عنه قَالَ: قالَ رَسُول الله صلى الله عليه وسلم: ((صَلاةُ الرَّجلِ في جمَاعَةٍ تَزيدُ عَلَى صَلاتهِ في بيتهِ وصلاته فِي سُوقِهِ بضْعًا وعِشرِينَ دَرَجَةً، وَذَلِكَ أنَّ أَحدَهُمْ إِذَا تَوَضَّأَ فَأَحْسَنَ الوُضوءَ، ثُمَّ أَتَى المَسْجِدَ، لا يَنْهَزُهُ إِلا الصَلاةُ، لا يُرِيدُ إلا الصَّلاةَ: لَمْ يَخْطُ خُطْوَةً إِلا رُفِعَ لَهُ بِهَا دَرجَةٌ، وَحُطَّ عَنْهُ بها خَطِيئَةٌ حَتَّى يَدْخُلَ المَسْجِدَ، فإِذا دَخَلَ المَسْجِدَ كَانَ في الصَّلاةِ مَا كَانَتِ الصَّلاةُ هِي تَحْبِسُهُ، وَالمَلائِكَةُ يُصَلُّونَ عَلَى أَحَدِكُمْ مَا دَامَ في مَجْلِسِهِ الَّذِي صَلَّى فِيهِ، يَقُولُونَ: اللَّهُمَّ ارْحَمْهُ، اللَّهُمَّ اغْفِرْ لَهُ، اللَّهُمَّ تُبْ عَلَيهِ، مَا لَم يُؤْذِ فيه، مَا لَمْ يُحْدِثْ فِيهِ)). مُتَّفَقٌ عليهِ

Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema: “Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mtu kuswali kwa jamaa’ah (ujira wake) huzidi kuswali sokoni kwake na nyumbani kwake kwa daraja zaidi ya ishirini. Nako ni kuwa, mmoja wao anapotawadha vizuri kisha akaenda Msikitini, hakusudii isipokuwa Swalaah, hakuna lililomuinua isipokuwa ni Swalaah tu, basi (atakuwa) hakuinua hatua isipokuwa atainuliwa daraja kwa hatua hiyo na ataondolewa dhambi kwa hatua hiyo mpaka aingie Msikitini, atakuwa angali yupo katika Swalaah maadamu Swalaah ndiyo iliyomzuia. Na Malaika humuombea rahmah mmoja kati yenu maadamu yupo katika kikao chake alichoswalia, wanaomba: “Ee Rabb Mrehemu, Ee Rabb Mghufurie! Ee Rabb Mpokelee tawbah yake!” (Hali inaendelea namna hiyi) maadamu hajaudhi au kupatwa na hadathi.” [Al-Bukhaary na Muslim]





Hadiyth – 11



وعن أبي العبَّاسِ عبدِ اللهِ بنِ عباسِ بنِ عبد المطلب رضِيَ اللهُ عنهما، عن رَسُول الله صلى الله عليه وسلم فيما يروي عن ربهِ تباركَ وتعالى قَالَ: ((إنَّ اللهَ كَتَبَ الحَسَنَاتِ والسَّيِّئَاتِ ثُمَّ بَيَّنَ ذلِكَ، فَمَنْ هَمَّ بحَسَنَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا كَتَبَها اللهُ تَبَارَكَ وتَعَالى عِنْدَهُ حَسَنَةً كامِلَةً، وَإنْ هَمَّ بهَا فَعَمِلَهَا كَتَبَهَا اللهُ عَشْرَ حَسَناتٍ إِلى سَبْعمائةِ ضِعْفٍ إِلى ضعَافٍ كَثيرةٍ، وإنْ هَمَّ بِسَيِّئَةٍ فَلَمْ يَعْمَلْهَا كَتَبَهَا اللهُ عِنْدَهُ حَسَنَةً كَامِلةً، وَإنْ هَمَّ بِهَا فَعَمِلَهَا كَتَبَهَا اللهُ سَيِّئَةً وَاحِدَةً)). مُتَّفَقٌ عليهِ.

‘Abul-‘Abbaas, ‘Abdillaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amepokea kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika aliyopokea kutoka kwa Rabb wake Mtukufu. Amesema: “Kwa hakika Allaah Ameandika mema na mabaya, kisha akabainisha hayo: Atakayefanya hamu ya kutenda jema kisha asitende, Allaah Aliyetukuka Atamuandikia Kwake jema moja kamili. Na akilifanyia hamu na akalitenda, Allaah Atamuandikia mema kumi hadi nyongeza mia saba, hadi nyongeza nyingi zaidi (zaidi ya hizo). Na akifanya hamu ya kutenda jambo baya kisha asilitende, Allaah Atamuandikia Kwake jema kamili. Na akifanya hamu ya kulitenda na akalitenda, Allaah Atamuandikia baya moja.” [Al-Bukhaary na Muslim]





Hadiyth – 12

وعن أبي عبد الرحمن عبدِ الله بنِ عمرَ بن الخطابِ رضيَ اللهُ عنهما، قَالَ: سمعتُ رسولَ الله صلى الله عليه وسلم، يقول: ((انطَلَقَ ثَلاثَةُ نَفَرٍ مِمَّنْ كَانَ قَبْلَكُمْ حَتَّى آوَاهُمُ المَبيتُ إِلى غَارٍ فَدَخلُوهُ، فانْحَدرَتْ صَخْرَةٌ مِنَ الجَبَلِ فَسَدَّتْ عَلَيْهِمُ الغَارَ، فَقالُوا: إِنَّهُ لا يُنْجِيكُمْ مِنْ هذِهِ الصَّخْرَةِ إِلا أنْ تَدْعُوا اللهَ بصَالِحِ أعْمَالِكُمْ. قَالَ رجلٌ مِنْهُمْ: اللَّهُمَّ كَانَ لِي أَبَوانِ شَيْخَانِ كبيرانِ، وكُنْتُ لا أغْبِقُ قَبْلَهُمَا أهْلًا ولا مالًا، فَنَأَى بِي طَلَب الشَّجَرِ يَوْمًا فلم أَرِحْ عَلَيْهمَا حَتَّى نَامَا، فَحَلَبْتُ لَهُمَا غَبُوقَهُمَا فَوَجَدْتُهُما نَائِمَينِ، فَكَرِهْتُ أنْ أُوقِظَهُمَا وَأَنْ أغْبِقَ قَبْلَهُمَا أهْلًا أو مالًا، فَلَبَثْتُ- والْقَدَحُ عَلَى يَدِي- أنتَظِرُ اسْتِيقَاظَهُما حَتَّى بَرِقَ الفَجْرُ والصِّبْيَةُ يَتَضَاغَوْنَ عِنْدَ قَدَميَّ، فاسْتَيْقَظَا فَشَرِبا غَبُوقَهُما. اللَّهُمَّ إنْ كُنْتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابِتِغَاء وَجْهِكَ فَفَرِّجْ عَنّا مَا نَحْنُ فِيهِ مِنْ هذِهِ الصَّخْرَةِ، فانْفَرَجَتْ شَيْئًا لا يَسْتَطيعُونَ الخُروجَ مِنْهُ.

قَالَ الآخر: اللَّهُمَّ إنَّهُ كانَتْ لِيَ ابْنَةُ عَمّ، كَانَتْ أَحَبَّ النّاسِ إليَّ- وفي رواية: كُنْتُ أُحِبُّها كأَشَدِّ مَا يُحِبُّ الرِّجَالُ النساءَ- فأَرَدْتُهَا عَلَى نَفْسِهَا فامْتَنَعَتْ منِّي حَتَّى أَلَمَّتْ بها سَنَةٌ مِنَ السِّنِينَ فَجَاءتْنِي فَأَعْطَيْتُهَا عِشْرِينَ وَمائةَ دينَارٍ عَلَى أنْ تُخَلِّيَ بَيْني وَبَيْنَ نَفْسِهَا فَفعَلَتْ، حَتَّى إِذَا قَدَرْتُ عَلَيْهَا- وفي رواية: فَلَمَّا قَعَدْتُ بَينَ رِجْلَيْهَا، قالتْ: اتَّقِ اللهَ وَلا تَفُضَّ الخَاتَمَ إلا بِحَقِّهِ، فَانصَرَفْتُ عَنْهَا وَهيَ أَحَبُّ النَّاسِ إليَّ وَتَرَكْتُ الذَّهَبَ الَّذِي أعْطَيتُها. اللَّهُمَّ إنْ كُنْتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابْتِغاءَ وَجْهِكَ فافْرُجْ عَنَّا مَا نَحْنُ فيهِ، فانْفَرَجَتِ الصَّخْرَةُ، غَيْرَ أَنَّهُمْ لا يَسْتَطِيعُونَ الخُرُوجَ مِنْهَا.
وَقَالَ الثَّالِثُ: اللَّهُمَّ اسْتَأْجَرْتُ أُجَرَاءَ وأَعْطَيْتُهُمْ أجْرَهُمْ غيرَ رَجُل واحدٍ تَرَكَ الَّذِي لَهُ وَذَهبَ، فَثمَّرْتُ أجْرَهُ حَتَّى كَثُرَتْ مِنهُ الأمْوَالُ، فَجَاءنِي بَعدَ حِينٍ، فَقالَ: يَا عبدَ اللهِ، أَدِّ إِلَيَّ أجْرِي، فَقُلْتُ: كُلُّ مَا تَرَى مِنْ أجْرِكَ: مِنَ الإبلِ وَالبَقَرِ والْغَنَمِ والرَّقيقِ، فقالَ: يَا عبدَ اللهِ، لا تَسْتَهْزِئْ بي! فَقُلْتُ: لا أسْتَهْزِئ بِكَ، فَأَخَذَهُ كُلَّهُ فاسْتَاقَهُ فَلَمْ يتْرُكْ مِنهُ شَيئًا. الَّلهُمَّ إنْ كُنتُ فَعَلْتُ ذلِكَ ابِتِغَاءَ وَجْهِكَ فافْرُجْ عَنَّا مَا نَحنُ فِيهِ، فانْفَرَجَتِ الصَّخْرَةُ فَخَرَجُوا يَمْشُونَ)). مُتَّفَقٌ عليهِ.

Abu ‘Abdir-Rahmaan, ‘Abdillaah bin ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhwiya Allaahu ‘anhumaa) amesema: Nilimsikia Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Waliondoka watu watatu, miongoni mwa watu waliokuwa kabla yenu waliosafiri hadi wakaingia pangoni ili walale. Likaviringika jiwe kutoka juu ya jabali likawafungia pango. Wakasemezana: Hakuna kitakachowaokoa kutokana na jiwe hili isipokuwa mumuombe Allaah kwa ‘amali zenu njema. Mmoja miongoni mwao akaanza kuomba: Ee Rabb, nilikuwa nina wazazi wawili wazee wakongwe, nilikuwa sitangulizi (kabla yao kunywa maziwa) familia wala watumwa. Siku moja haja ya kutafuta kuni ikanipeleka mbali, sikuweza kuwarudia (mapema) mpaka wakalala. Nikawakamulia maziwa yao, nikawakuta wameshalala. Nikachukia kuwaamsha na (nikachukia pia) kuwapa maziwa familia na watumwa kabla yao. Nikawa na (bilauri) imo mikononi mwangu mpaka waamke, hadi alfajiri ikatokeza huku watoto wakipiga kelele kwa njaa miguuni mwangu; wakaamka na wakanywa maziwa yao. Ee Rabb, ikiwa nilifanya hivyo kwa kutaka radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo ya jiwe hili. Kukafunguka kidogo kidogo kwa namna ambayo hawawezi kutoka. Mwengine akasema: Ee Rabb, nilikuwa nina bint wa ‘ammi yangu, nilikuwa nikimpenda mno, (Riwaayah nyingine imesema): Nilikuwa nikimpenda kama vile wanaume wanavyopenda mno wanawake. Nikamtaka (kuzini nae), akanikatalia. Mpaka alipokuja mwaka wa ukame, akanijia nikampa dinaar 120 ili niwe nae faragha. Akakubali. Nilipokuwa nimeshamuweza, (Riwaayah nyingine inasema): Nilipoketi baina ya miguu yake akanambia: Mche Allaah, usiivunje pete ila kwa haki yake. Nikamuondokea nikiwa nampenda mno (wala sikumfanya chochote), na nikamuachia dhahabu niliyompa. Ee Rabb, ikiwa nilifanya hivyo kwa ajili ya kupata radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo. Jiwe likafunguka, lakini walikuwa hawawezi kutoka. Mtu wa tatu akasema: Ee Rabb, mimi niliwaajiri wafanyakazi, nikawapa ujira wao isipokuwa mtu mmoja, aliuacha ujira wake na akaenda. Nikauzalisha ujira wake mpaka ukawa ni mali nyingi. Baada ya muda akanijia na kuniambia: Ee mja wa Allaah, nipe ujira wangu! Nikamwambia: Kila unachokiona katika ngamia, ng’ombe, mbuzi na watumwa ni ujira wako! Akaniambia: Ee mja wa Allaah, usinifanyie istihzai (usinikebehi)! Nikamwambia: Sikufanyii istihzai. Akachukua mali yote na akayachunga na wala hakubakisha mali yoyote. Ee Rabb, ikiwa nilifanya hivyo kwa kutaka radhi Zako, basi tufariji katika dhiki tuliyonayo. Jiwe likafunguka wakatoka zao.” [Al-Bukhaariy na Muslim]
 
Naam katika hadith hii ya mwisho tunajifunza kwamba unaweza kumuomba Allah kupitia amali zako njema ikiwa tu ulizofanya kwa kutaka radhi za Allah

Kwahiyo unataja amali au kitendo ambacho unajua kabisa ulifanya kwa kutaka radhi za Allah,basi ndio iwe sababu ya Allah kukuondolea au kukutalia shida zako
 
Assalaam alaikum warahmatullah wabarakatuh

NASAHA ZA IJUMAA

Alhamdulillah imetufikia Ijumaa siku adhimu mno kwetu sisi waislamu,tutambue kwamba zile eid mbili Eid ya kufunga na Eid ya kuchinja pamoja na ukubwa wake lakini haziifikii siku ya Ijumaa kwa uzito wake

Tunakumbushana Tumche Allah popote pale tulipo,na kumcha Allah ni kufuata maamrisho yake na kuacha makatazo yake,hapo tutakuwa tumefikia lengo la uchaji Mungu, tumuombe Allah atuwezeshe kufikia daraja hilo

Naam nasaha zangu leo ningependa kuzungumzia kuhusiana na kuishi vizuri na majirani,ndugu zangu jirani ana nafasi kubwa sana katika maisha ya muislamu,ni eneo ambalo limepewa uzito mkubwa mno kutoka kwa Nabii swallallahu alaih wassalam

Na yeye kila mara alikuwa akikumbushwa na Jibril alayh salam juu ya umuhimu wa kujali sana jirani,kila malaika Jibril akimjia humkumbusha kuhusiana na kuwajali majirani,mpaka imepokelewa katika hadith kwamba mpaka Mtume swallallahu alaih wasallam alihisi huenda akifa jirani atamrithi

Chunga sana jirani yako asikose furaha kwa ajili yako,chunga sana jirani asihuzunike lwasababu yako,kuna kisa kimoja kinasema kuna mwanamke wa kiislamu,alikuwa anafunga,anaswali na kufanya ibaadati nyingine lakini upande wa pili jirani yake hakusalimika na maneno yake

Alikuwa anaongea maneno machafu kwa jirani na mwisho wa siku pamoja ibaadati zake alihukumiwa kwenda motoni,nadhani umepata picha jinsi jirani alivyopewa umuhimu

Nabii swallallahu alaih wasallam alikuwa anasema ukipika mchuzi basi ongeza maji kidogo na jirani yako apate,lakini leo hii kwako unapika pilau harufu inaenda kwa jirani,hata kumchotea kidogo nae afurahi hatufanyi hivyo

Umetoka shamba na matunda,mikungu ya ndizi,labda na nafaka mbali mbali hata kusema walau nitenge kidogo kwa ajili ya jirani hatufanyi hivyo

Jirani yako unamuona kabisa hali yake ya maisha ni mtihani nawe alhamdulillah uko vizuri,huwazi hata kumsaidia nae ajisikie mtu,ndio kwanza unasema kila mtu atapambana na hali yake

Hayo yanapaswa kufanywa na wasio na dini,maana dini ni muongozo wa maisha ya mwanadamu,na ndio maana dini ya kiislamu haijaacha chochote kuhakikisha mwanadamu anapata nuru na mwangaza wa kuyaendea maisha yake

Uislamu unasema hivi hata pale unapotaka kujenga ghorofa karibu na jirani yako basi unapaswa kushauriana nae,ukitaka kupiga fensi ushauriane nae au umpe taarifa,kuna hekima kubwa sana juu ya haya

Kwahiyo ndugu zangu naihusia nafsi yangu pamoja na yako juu ya kumcha Allah na kuishi vyema na majirani zetu

Subhaanaka allahumma wabihamdik ashahadu anlaa ilaha ila anta astaghfiruka waatubu ilaik

Ijumaa Mubaraka!
 
Tunaendelea na darsa ya Swalaa ya Nabii swallallahu alaih wasallam


051-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Qunuut Katika Swalah Ya Witr


Qunuut Katika Swalah Ya Witr



"Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم)akifanya Qunuut katika Rak’ah za Witr kwenye Swalah ya Witr"([1]) mara nyingine([2]) na "alifanya kabla ya rukuu"([3])

Alimfundisha Al-Hasan Ibn 'Aliy (رضي الله عنه) kusema [baada ya kumaliza kisomo chake katika Witr]:




اللّهُـمَّ اهْـدِنـي فِـيمَنْ هَـدَيْـتَ، وَعـافِنـي فِـيمَنْ عافَـيْتَ، وَتَوَلَّـني فِـيمَنْ تَوَلَّـيْتَ، وَبارِكْ لـي فِـيمَا أَعْطَـيْتَ، وَقِـني شَرَّ ما قَضَـيْتَ، (فَ) إِنَّـكَ تَقْـضي وَلا يُقْـضى عَلَـيْك، (وَ) إِنَّـهُ لا يَـذِلُّ مَنْ والَـيْتَ، (وَلا يَعِـزُّ مَن عـادَيْتَ)، تَبـارَكْـتَ رَبَّـنا وَتَعـالَـيْتَ. (لاَ مَنْجَا مِنْكَ إِلاَّ إِلَيْكَ)




Allaahumma-Hdiniy fiyman Hadayta, wa 'Aafiniy fiyman 'Aafayta, wa Tawallaniy fiyman Tawwallayat, wa Baarik liy fiymaa A'twayta, wa Qiniy sharra maa Qadhwayta, [fa]Innaka Taqdhwi wa laa yuqdhwaa 'Alayka, [wa] innahu la yadhwillu man Walayta, (wa laa yai'izzu man 'Aadayta) Tabarakta Rabbanaa wa Ta'aalayta [La manjaa Minka illa Ilayka]




“Ee Allaah, Niongoze pamoja na Uliowaongoza, na Unipe afya njema pamoja na Uliowapa afya njema, na Nifanye kuwa ni mpenzi Wako pamoja na Uliowafanya wapenzi na Nibariki katika Ulichonipa na Nikinge na shari ya Ulilolihukumu kwani] Wewe Unahukumu wala Huhukumiwi. [Na] Hakika hadhaliliki Uliyemfanya mpenzi [wala hatukuki Uliyemfanya adui] Umetakasika Ee Mola wetu na Umetukuka [Hakuna mahali pa kuokoka isipokuwa Kwako]([4])







[1] Ibn Naswr na Ad-Daaraqutwniy ikiwa na isnaad Swahiyh.

[2] Tumesema, "…. Mara nyingine", kwa sababu Maswahaba waliosimulia

Swalah ya Witr, hawakutaja qunuut humo, kwani ingelikuwa Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) alifanya daima humo wangelitaja wote. Lakini 'Ubayy Ibn Ka'ab pekee amesimulia qunuut katika Witr, hivyo inaonyesha kwamba alikuwa akifanya mara nyingine. Kwa hiyo, ni dalili kwamba qunuut katika Witr sio wajibu, na hii ni rai ya Maulamaa wengi. Kwa sababu hii, Mwanachuoni mtafiti wa Hanafi Ibn Al-Humaam, ametambua katika Fat-h Al-Qadiyr (1/306/ 359, 360) kwamba rai ya kuwa ni wajibu haikuthibiti kwa dalili na ni dhaifu. Na hivi ni katika kusahilisha mambo na sio kufanya magumu, kwani rai hii aliyoipa nguvu ni kinyume na madhehebu yake.
[3] Ibn Abi Shaybah (12/41/1), Abu Daawuud, An-Nasaaiy katika Sunan Al-

Kubraa (218/1-2), Ahmad, At-Twabaraaniy, Al-Bayhaqiy na Ibn 'Aasakir (4/244/1) amesimulia hii pamoja na du'aa inayofuatia, ikiwa na isnaad Swahiyh. Ibn Mandah amesimulia du'aa katika Tawhiyd (70/2) pekee ikiwa na isnaad tofauti ya Hasan. Takhriyj yake imetolewa katika Al-Irwaa (426).
[4] Ibn Khuzaymah (1/119/2) na pia Ibn Abi Shayah n.k kwa Hadiyth ya mwisho.






TANBIHI:


An-Nasaaiy ameongeza katika mwisho wa qunuut: ‘Wa Swalla Allaahu ‘alaan-Nabiyyil-Ummiyy’ (Allaah Amswalie Mtume asiyejua kusoma na kuandika), imesimuliwa ikiwa na isnaad Dhwa’iyf. Miongoni mwa waliokiri ni dhaifu ni Ibn Hajar Al-‘Asqalaaniy na Az-Zurqaaniy. Hivyo hatukuitia katika muundo wetu wa kuunganisha usimulizi unaokubalika. Al-‘Izz bin ‘Abdus-Salaam amesema katika Al-Fataawa (66/1/19): “Kumswalia Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) katika qunuut sio sahihi, wala haifai kuongeza kitu katika Swalah ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa vyovyote. Rai hii inaonyehsa kwamba hakuipanua kwa hoja ya kuingiza fikra ya bid’ah hasanah (uzushi mzuri) kama Maulamaa wa mwishoni wanavyodai.Lakini, imethibitika katika Hadiyth kuhusu ‘Ubayy bin Ka’ab akiswalisha watu katika Swalah za masiku ya Ramadhan kwamba alikuwa akimswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) katika mwisho wa qunuut, na hii ilikuwa katika ukhalifa wa ‘Umar (رضي الله عنه), imesimuliwa na Ibn Khuzaymah katika Swahiyh yake (1097). Vile vile imethibitika kutoka kwa Abu Haliymah Mu’aadh Al-Answaariy ambaye alikuwa akiwaswalisha wakati wa ukhalifa wa ‘Umar – imesimuliwa na Ismaa’iyl Al-Qaadhwiy (Namba. 107) na wengineo, hivyo ziada hii imethibitika kutokana na desturi ya Salaf na hivyo haifai kuipa kauli kwamba ni bid’ah. Na Allaah Anajua zaidi.
 
052-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Tashahhud Ya Mwisho Na Uwajibu Wake


Tashahhud Ya Mwisho


Wajibu Wa Tashahhud Hii



Kisha baada ya kumaliza Rak’ah ya nne, alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akikaa kwa ajili ya Tashahhud ya mwisho. Aliwaamrisha kuhusu hii na akifanya kama alivyofanya katika Tashahhud ya kwanza isipokuwa “alikaa mutawarrikan”([1]) “paja lake la kushoto likiwa ardhini na miguu yake yote miwili ikitokeza kutoka upande mmoja (yaani upande wa kulia)”([2]) “Aliweka mguu wake wa kushoto chini ya paja (la kulia) na muundi”([3]) “mguu wake wa kulia akiuinua”([4]) au mara nyingine “akiulaza pamoja ardhini”([5]) “paja lake la kushoto lilifunika goti lake (kushoto) akiliegemeza”([6])




Ameweka mfano wa kumswalia yeye (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Tashahhud, kama Tashahhud ya kwanza. Njia za kumswalia (صلى الله عليه وآله وسلم) zimetajwa kabla katika sehemu yake.





[1] Al-Bukhaariy.

[2] Kifungu kile kile kilichotajwa hapo mbeleni. Ama katika Swalah ya rakaa mbili kama Alfajiri, Sunnah ni kukaa muftarishan. Tofauti hii imeelezewa kirefu kutoka kwa Imaam Ahmad katika Masaail ya Ibn Haaniy kutoka kwa Imaam Ahmad (Uk. 79)

[3] Abu Daawuud na Al-Bayhaqiy ikiwa na isnaad Swahiyh.

[4] Muslim na Abu ‘Awaanah.

[5] Kifungu kile kile kilichotajwa hapo mbeleni

[6] Kifungu kile kile kilichotajwa hapo mbeleni
 
053-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Wajibu Wa Kumswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم)






Wajibu Wa Kumswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم)



Alimsikia mtu (صلى الله عليه وآله وسلم) akiomba du’aa bila ya kumtukuza Allaahتعالى , wala kumswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) hivyo akasema: ((Huyu mtu ameharakiza)). Kisha akamwita na kumwambia yeye na wengineo: ((Anaposwali mmojawenu, aanze kwa kumsifu Mola wake, (عزرجل) na kumtukuza kisha amswalie [katika usimulizi mmoja: amswalie] Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) kisha aombe anayotaka)).([1])

Pia, “alimsikia mtu akimtukuza na kumsifu Allaah na kumswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Swalah, hivyo Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: ((Omba na utaitikiwa, uliza utapewa))([2])












[1]Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Khuzaymah (1/83/2) na Al-Al-Haakim ambaye amekiri ni Swahiyh na Adh-Dhahabiy amekubali.

[2] An-Nasaaiy ikiwa na isnaad Swahiyh.
 
054-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Wajibu Wa Kujikinga Kutokana Na Mambo Manne Kabla Ya Kuomba Du’aa


Wajibu Wa Kujikinga Kutokana Na Mambo Manne Kabla Ya Kuomba Du’aa


Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((Atakapomaliza mmoja wenu Tashahhud (ya mwisho) aombe kujikinga kwa Allaah kutokana na mambo manne, aseme:




اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِـنْ عَذابِ جَهَـنَّم، وَمِـنْ عَذابِ القَـبْرِ، وَمِـنْ فِتْـنَةِ المْحْـيا وَالمْمـاتِ، وَمِـنْ شَـرِّ (فِتْـنَةِ) المْْسِيحِ الدَّجَّال




“Allaahumma inniy a’uwdhu Bika min ‘adhaabi Jahannam, wamin ‘adhaabil qabri, wa min fitnatil mahyaa wal-mamaat, wamin sharri [fitnatil] Masiyhid-Dajjaal”




“Ee Allaah, mimi najikinga Kwako] na adhabu za moto (wa Jahannam) na adhabu za kaburi na fitna ya uhai, na ya kufa, na shari ya [fitna] ya Masiyhid-Dajjaal)) [Kisha ajiombee mwenyewe kinachompata]([1]) Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akiomba (du’aa) katika Tashahhud yake”([2])




Pia alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwafundisha Maswahaba (رضي الله عنهم) hivyo kama alivyowafundisha Surah za Qur-aan”([3])








[1] Muslim, Abu ‘Awaanah, An-Nasaaiy na Ibn Al-Jaruud katika Al-Muntaqaa (27). Imetolewa katika Al-Irwaa (350).

[2] Abu Daawuud na Ahmad ikiwa na isnaad Swahiyh.

[3] Muslim na Abu ‘Awaanah.

Share Email Telegram WhatsApp
‹ 053-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Wajibu Wa Kumswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم)up055-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kuomba (Du’aa) Kabla Ya Kutoa Salaam Na Aina
 
055-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kuomba (Du’aa) Kabla Ya Kutoa Salaam Na Aina Zake






Kuomba (Du’aa) Kabla Ya Kutoa Salaam Na Aina Zake



Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) katika Swalah yake akiomba aina mbali mbali za du’aa.”([1]) Akiomba wakati mwingine kwa du’aa hizi na wakati mwingine zile, na akazikubali du’aa nyingine na “akamuamrisha mwenye kuswali achague azipendazo”([2]) Nazo ni:







1- اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِـنْ عَذابِ القَـبْر، وَأَعـوذُ بِكَ مِـنْ فِتْـنَةِ المْسيحِ الدَّجّـال، وَأَعـوذُ بِكَ مِـنْ فِتْـنَةِ المْحْـيا وَالمْمـات. اللّهُـمَّ إِنِّـي أَعـوذُ بِكَ مِنَ المْأْثَـمِ وَالمْغْـرَم




Allaahumma inniy a’uwdhu Bika min ‘adhaabil qabri, wa a’uwdhu bika min fitnatil Masiyhid Dajaal wa a’uwdhu bika min fitnatil mahyaa wal- mamaat, Allaahumma inniy ‘a’uwdhu bika minal ma-athami wal-maghrami




“Ee Allaah! Hakika mimi najikinga Kwako kutokana na adhabu ya kaburi, na najikinga Kwako kutokana na fitna ya Masihid-dajjaal, na najikinda Kwako kutokana na fitna ya uhai na ya mauti, Ee Allaah, hakika mimi najikinda Kwako kutokana na dhambi([3]) na deni”([4]) ([5])







2- اللَّهُمَّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا عَمِلْتُ، وَمِنْ شَرِّ مَا لَمْ أَعْمَلْ (بَعْدُ)




Allaahumma inniy a’uwdhu Bika min sharri ma ‘amiltu wamin sharri ma lam a’amal (ba’ad)




“Ee Allaah, hakika mimi najikinga Kwako kutokanan na shari nilizozitenda na shari nisizozitenda([6]) [bado]([7])







3- أللَّهُمَّ حَاسِبْنِي حِسَاباً يَسِيراً




Allaahumma Haasibniy hisaaban yasiyran




“Ee Allaah, nihesabie hisabu nyepesi”([8])







4- اللّهُـمَّ بِعِلْـمِكَ الغَـيْبِ وَقُـدْرَتِـكَ عَلـى الْخَلقِ، أَحْـيِني ما عَلِـمْتَ الحـياةَ خَـيْراً لـي، وَتَوَفَّـني إِذا كَانَتِ الوَفـاةَ خَـيْراً لـي، اللّهُـمَّ وَأَسْـأَلُـكَ خَشْيَتَـكَ في الغَـيْبِ وَالشَّهـادَةِ، وَأَسْـأَلُـكَ كَلِمَـةَ الحَـقِّ (وفي رواية: الْحُكْم) وَالْعَدْلَ فِي الْغَضَبِ وَالرِّضَى، وَأَسْـأَلُـكَ القَصْدَ في الفَقْـرِ وَالغِنَـى، وَأَسْـأَلُـكَ نَعـيماً لاَيَبِيدُ، وَأَسْـأَلُـكَ قُـرَّةَ عَيْـنٍ (لاَ تَنْفَذَُ وَ) لا تَنْـقَطِعْ وَأَسْـأَلُـكَ الرِّضَـى بَعْـدَ القَضـاءِ، وَأَسْـأَلُـكَ بًـرْدَ الْعَـيْشِ بَعْـدَ الْمَـوْتِ، وَأَسْـأَلُـكَ لَـذَّةَ النَّظَـرِ إِلـى وَجْـهِكَ (وَأَسْأَلُكَ) الشَّـوْقَ إِلـى لِقـائِـكَ، في غَـيرِ ضَـرّاءٍ مُضِـرَّة، وَلا فِتْـنَةٍ مُضـلَّةٍ، اللّهُـمَّ زَيِّـنّا بِزينَـةِ الإيـمان، وَاجْـعَلنا هُـداةً مُهْـتَدين




Allaahumma bi ‘Ilmikal-ghaybi, wa Qudratika ala khalqi. Ahyiniy maa ‘alimtal-hayaata khayran liy wa Tawafaniy idhaa kaanatil wafaatu khayran liy. Allaahumma wa As-aluka Khashyataka fil ghaybi wash-shahaadah, wa As-aluka kalimatal haqqi, [al-hukmu], wal-‘adla fil ghadhwabi war-ridhwaa, wa As-alukal qaswda fil faqri wal-ghinaa, wa As-aluka na'iyman laa yabiydu, wa As-aluka quratan ‘aynin [laa tanfadhu wa] la tanqatwi’u, wa As-alukar-ridhwaa ba'dal-qadhwai, wa As-aluka bardal-‘aysha ba'dal mawti, wa As-aluka ladhatan nadhwari ilaa Wajhika, wa [As-aluka] ash-shawqa ilaa Liqaaika, fiy ghayri dhwaraain mudhwirratin, wa la fitnaatin mudhwillah. Allaahumma Zayinnaa bi ziynatil iymaani, wa Ja'alnaa hudaatan muhtadiyn.




“Ee Allaah, Kwa ujuzi Wako wa mambo yaliyofichikana, na uwezo Wako wa kuumba, niweke hai iwapo Unajua kwamba uhai ni bora kwangu, na nifishe iwapo kufa ni bora kwangu, Ee Allaah, nakuomba pia khofu yako kwa siri na dhahiri na ninakuomba neno la haki [na katika riwaaya: hukmu], na uadilifu wakati nimefurahi na wakati nimekasirika, na ninakuomba matumizi ya wastani wakati wa utajiri na wakati wa umaskini, na ninakuomba neema isiyokwisha na ninakuomba kituliza jicho (moyo) [kisicho toweka na] kisichokatika, na ninakuomba kuridhia baada yakuwa umeshanipangia, na ninakuomba maisha ya utulivu baada ya kufa, na ninakuomba ladha ya kukutizama uso Wako, [na nakuomba] shauku ya kukutana Nawe, pasina madhara yanayodhuru, wala fitna yenye kupoteza. Ee Allaah, Tupambe kwa kipambo cha imani, na Tujaalie tuwe waongozi wenye kuongoka”([9])







5-Amemfundisha Abu Bakr As-Swiddiyq (رضي الله عنه) kusema:




اللّهُـمَّ إِنِّـي ظَلَـمْتُ نَفْسـي ظُلْمـاً كَثـيراً وَلا يَغْـفِرُ الذُّنـوبَ إِلاّ أَنْت، فَاغْـفِر لي مَغْـفِرَةً مِنْ عِنْـدِكَ وَارْحَمْـني، إِنَّكَ أَنْتَ الغَـفورُ الرَّحِـيمُ




Allaahumma Inniy dhwalamtu nafsiy dhwulman kathiyran walaa yaghfirudh-dhunuuba illa Anta, fa-Ghfirliy maghfiratan min ‘indika, wa-Rhamniy Innaka Antal-Ghafuurur-Rahiym




“Ee Allaah, hakika mimi nimejidhulumu nafsi yangu, dhulma nyingi, na hasamehe madhambi ila Wewe, basi Nisamehe msamaha kutoka Kwako, na Unirehemu, hakika Wewe ni mwingi wa kusamehe, mwingi wa kurehemu”([10])







6- Amemuamrisha ‘Aaishah (رضي الله عنها) aseme:




اللَّهُمَّ إِني أسْأَلُكَ مِنَ الْخَيْرِ كُلِّهِ (عَاجِلِهِ وَآجِلِه) مَا عَلِمْتُ مِنْهُ وَمَا لَمْ أعْلَمْ، وَأعُوذُ بِكَ مِنَ الشَّرِّ كُلِّهِ، (عَاجِلِهِ وَآجِلِهِ) مَا عَلِمْتُ مِنْهُ وَمَا لَمْ ‏‏ أعْلَمْ، وَأسْأَلُكَ (وَفي رواية: اللَّهُمَّ إِنِّي أسْأَلُكَ) الْجَنَّةَ وَمَا قَرَّبَ إلَيْهَا مِنْ قَوْلٍ أوْ عَمَلٍ، وَأعُوذُ بِكَ مِنَ النَّارِ وَمَا قَرَّبَ إِلَيْهَا مِنْ قَوْلٍ أوْ عَمَلٍ، وَأسْأَلُكَ (وَفي رواية: اللَّهُمَّ إِنِّي أسْأَلُكَ) مِنَ (الْ) خَيْرِ مَا سَألَكَ عَبْدُكَ وَرَسُولُكَ (مُحَمَّدٌ وَأعُوذُ بِكَ مِنْ شَرِّ مَا اسْتَعَاذَكَ مِنْهُ عَبْدُكَ وَرَسُولُكَ مُحَمَّدٌ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ) (وَ أسْأَلُكَ) مَا قَضَيْتَ لِي مِنْ أَمْرٍ أنْ تَجْعَلَ عَاقِبَتَهُ (لي) رُشْداً




Allaahumma inniy As-aluka minal-khayri kullihi ‘aajilihi wa aajilihi maa `alimtu minhu wa maa lam a`lam, wa a’uwdhu Bika mina-sharri kullihi `aajilihi wa aajilihi maa `alimtu minhu wa maa lam a`lam. Wa As-aluka




[Allaahumma inniy As-aluka] Al-Jannata wamaa qarraba ilayhaa bi qawlin au ‘amal. Wa a’uwdhu Bika minan-naari wamaa qarraba ilayhaa min qawlin au ‘amal. Wa As-aluka [Allaahumma inniy As-aluka] minal-khayri ma sa-alaka ‘Abduka wa Rasuuluka Muhammadun, wa a’uwdhu Bika min sharri ma sta’aadhaka minhu ‘Abduka wa Rasuuluka Muhammadun Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam. [Wa As-aluka] maa qadhwayta liy min amrin an Taj’ala ‘aqibatahu [liy] rushdaa.




“Ee Allaah hakika mimi nakuomba mema yote [karibu na mbali] ninayoyajua na nisiyoyajua, na najikinga Kwako na shari zote [karibu na mbali] ninazozijua na nisizozijua, na nakuomba [na katika riwaaya: Ee Allaah hakika mimi nakuomba] Pepo na kila kauli au kitendo kinachokaribisha nayo, na najikinga Kwako na moto na kila kauli na kitendo kinachokaribisha nao, na nakuomba [na katika riwaaya: Ee Allaah, hakika hakika mimi nakuomba] kutokana na kheri alizokuomba Mja Wako na Mjumbe Wako [Muhammad na najikinga Kwako na shari alizojikinga nazo Mja Wako na Mjumbe Wako Muhammad SwallaLlaahu ‘alayhi wa sallam], [na nakuomba] kwa mambo yote uliyonikidhia Ujaalie matokeo yake [kwa ajili yangu] yawe ya uongofu([11])







7- Alimuuliza mtu: ((Unasema nini katika Swalah?)) Akasema: “Nakiri kwamba (yaani nashuhudia) kisha nauomba Allaah Pepo, na najikinga Naye kutokana na moto. Lakini Naapa, hakuna dandana (mnong’ono)([12]) mzuri kama wako au wa Mu’aadh”. Hivyo akasema: ((Dandana [mnong’ono] wetu ni kama wako))([13])







8-Amemsikia mtu akisema katika Tashahhud yake:




اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ يا اللهُ (وَفِي رواية: بِاللّه) (الْواحِدُ) الأَحَـدُ ،الصَّـمَدُ الَّـذي لَـمْ يَلِـدْ وَلَمْ يولَدْ، وَلَمْ يَكـنْ لَهُ كُـفُواً أَحَـدٌ- أَنْ تَغْـفِرَ لي ذُنـوبي إِنَّـكَ أَنْـتَ الغَفـورُ الرَّحِّـيمُ

Allaahumma inniy As-aluka yaa Allaah [BiLlahi] [Al-Waahidu] Al-Ahad As-Swamadu Alladhiy lam Yalid walam Yuwlad walam Yakun Lahu kufuwan ahad-an Taghfira liy dhunubiy Innaka Antal-Ghafuwrur Rahiym.




“Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba Ee Allaah, [na katika riwaayah: Naapa kwa Allaah] [Wewe ni Mmoja] Uliye Pekee, Mwenye kutegemewa kwa haja zote, Ambaye Hakuzaa wala Hakuzaliwa, na wala hakuna mfano Wake na kitu chochote, Unisamehe makosa yangu, hakika Wewe ni Mwingi wa Kusamehe, Mwenye Kurehemu”.

Hii (صلى الله عليه وآله وسلم) alisema: ((Amesamehewa, Amesamehewa))([14])







9-Alimsikia mtu mwingine akisema katika Tashahhud yake:




اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْأَلُـكَ بِأَنَّ لَكَ الْحَـمْدُ لا إِلـهَ إِلاّ أَنْـتَ (وَحْـدَكَ لا شَـريكَ لَـكَ) (المَنّـانُ) (يا) بَديـعَ السَّمواتِ وَالأَرْضِ يا ذا الجَلالِ وَالإِكْـرام، يا حَـيُّ يا قَـيّومُ (إِنِّـي أَسْأَلُـكَ) (الجَـنَّةَ وَأَعـوذُ بِـكَ مِنَ الـنّار)

Allaahumma inniy As-aluka bianna Lakal-hamdu, laa ilaaha illa Anta [Wahdaka laa shariyka Lak], [Almannaan], [yaa] Badiy’a s-samawati wal-ardhwi, yaa Dhal-Jalaali wal-Ikraami, yaa Hayyu yaa Qayyuum, [inniy as-aluka] [al-Jannata, wa a’uwdhu Bika minan-Naari]




“Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba, kwa vile sifa njema zote ni Zako, hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, [Peke Yako Huna mshirika] [mwingi wa kuneemesha]. [Ee] Mwanzishi (muumbaji) wa mbingu na ardhi, Ee mwenye Utukufu na Ukarimu, Ee Uliye Hai Mwenye kusimama kwa dhati Yako, [hakika mimi nakuomba] [Pepo, na najilinda Kwako kutokana na moto”].




Hivyo Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) akawaambia Maswahaba: ((Mnajua kaomba nini?)) Wakasema: “Allaah na Mjumbe Wake wanajua zaidi”. Akasema: ((Naapa kwa Yule Ambaye nafsi yangu imo mikononi Mwake, amemuomba Allaah kwa Jina Lake tukufu)) [katika riwaaya nyingine: Tukufu kabisa]([15]) ambalo Anapoombwa Anajibu na Anapoombwa Hutoa)).([16])




10- Kitu cha mwisho alichokuwa akisema baina ya Tashahhud na tasliym ilikuwa ni:




اللّهُـمَّ اغْـفِرْ لي ما قَدَّمْـتُ وَما أَخَّرْت، وَما أَسْـرَرْتُ وَما أَعْلَـنْتُ، وَما أَسْـرَفْتُ، وَما أَنْتَ أَعْـلَمُ بِهِ مِنِّي. أَنْتَ المُقَـدِّمُ، وَأَنْتَ المُـؤَخِّـرُ لا إِلهَ إِلاّ أَنْـتَ




Allaahumma-Ghfirliy maa qaddamtu wamaa akhartu, wa maa asrartu, wamaa a’lantu, wamaa asraftu, wamaa Anta A’lamu bihi minniy, Antal Muqaddimu, wa Antal Muakhiru, laa ilaaha illa Anta.




“Ee Allaah! Nisamehe niliyoyatanguliza, na niliyoyachelewesha, na niliyoyafanya kisiri, na niliyoyafanya kwa dhahiri na niliyoruka mipaka, na ambayo Wewe Unayajua zaidi kuliko mimi, Wewe Ndiye Mwenye kutanguliza na Wewe Ndiye Mwenye kuchelewsha, hakuna apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe”.([17])












[1] Hatukusema “ ….katika Tashahhud yake”, kwa sababu matini ni “…katika

Swalah yake”, bila ya kuelezea kama Tashahhud au sehemu nyingine. Hivyo inajumuisha sehemu zote zifaazo kwa du’aa mfano katika Sujuud na Tashahhud. Amri ya kuomba du’aa katika vikao viwili zimetajwa kabla.

[2] Al-Bukhaariy na Muslim. Amesema Al-Athram: “Nilimuuliza Ahmad:

Niombe na nini baada ya Tashahhud? Akasema: Kama ilivyosimuliwa. Nikasema: Kwani Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakusema: ((Achague du’aa zozote azipendazo?)) Akasema: Achague katika zilizosimuliwa. Nikakariri swali, akasema: Kutoka zilizosimuliwa. Hii imenukuliwa na Ibn Taymiyyah (Majmuu’a Al-Fataawa 69/218/1), ambaye amenukuu akiongeza: ‘Hivyo, ‘du’aa zozote’ zinakusudiwa Anazozipenda Allaah, na sio du’aa yoyote…” Kisha akasema: ‘Hivyo ni bora kusema zile zilizokubaliwa, du’aa zilizothibiti, na hizi ndizo zilizosimuliwa na zenye manufaa”. Ndivyo hivyo, lakini kutambua du’aa gani hakika zenye manufaa inategemea na elimu Swahiyh, nayo ni nadra kupatikana kwa watu. Kwa hivyo ni bora kushikilia du’aa zilizonukuliwa khaswa zikiwa zinajumuisha zile anazopenda mwenye kuswali. Na Allaah Anajua zaidi








[3] "Ma-tham" ni yale yanayomsababisha mtu kutenda dhambi au dhambi yenyewe.

[4] "Maghram" ni mzigo. Hapa ina maana deni kama ilivyothibiti katika Hadiyth nyingine ambayo ‘Aaishaah amesema: “Mtu alimwambia: “Kwa nini kila mara unajikinga kutokana na maghram ewe Mjumbe wa Allaah?” Akajibu: ((Hakika mtu anapokuwa na deni, husema uongo na anaaahidi na kuvunja ahadi yake)).

[5] Al-Bukhaariy na Muslim.

[6] Yaani kutokana na shari ya vitendo viovu nilivyovitenda, na kutokana na shari ya maovu ya kutokutenda vitendo vyema.

[7] An-Nasaaiy ikiwa na isnaad Swahiyh na Ibn Abi ‘Aaswim katika kitabu

chake As-Sunnah (Namba. 370- ikiwa na utafiti wangu). Ziada ni kutoka kwake.

[8] Ahmad na Al-Haakim ambaye amekiri ni Swahiyh, na Adh-Dhahabiy amekubali.

[9] An-Nasaaiy na Al-Al-Haakim ambaye amekiri ni Swahiyh, na Adh-Dhahabiy amekubali.

[10] Al-Bukhaariy na Muslim.

[11] Ahmad, Atw-Twayaalisiy, Al-Bukhaariy katika Al-Adaab Al-Mufrad, Ibn

Maajah na Al-Haakim ambaye amekiri ni Swahiyh, na Adh-Dhahabiy amekubali. Nimetoa takhiryj yake katika Silsilatul-Ahaadiyth As-Swahiyhah (1542).

[12] "Dandanah" ni kusema kwa sauti ndogo isiyosikika, lakini maneno yasiyofahamika – katika hali hii ni maneno ya kimya ya du’aa. Kauli ya mwisho ina maana: “Maneno yetu ni kama yako”.

[13] Abu Daawuud, Ibn Maajah na Ibn Khuzaymah (1/87/1) ikiwa na isnaad Swahiyh.

[14] Abu Daawuud, An-Nasaaiy, Ahmad na Ibn Khuzaymah. Al-Haakim amekiri ni Swahiyh,na Adh-Dhahaby amekubali.

[15] Tawassul hii (kujikurubisha) kwa Allaah kwa kutumia Majina Yake mazuri

na sifa Zake, ni amri ya Allaah تعالى ((وَلِلَّهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا)) [Al-A’raaf 7: 180]. Ama kumuomba Allaah kwa kukurubia vitu vingine mfano, ‘kwa kumtaja fulani na fulani’ au ‘kwa makarama ya fulani na fulani’ au ‘masharifu’ n.k – matini ya Imaam Abu Haniyfah (رحمه الله ) na Maswahaba zake, wametaja kuwa desturi hii ni makruuh (inachukiza). Kwa ujumla imeharamishwa. Hivyo inasikitisha kwamba watu wengi miongoni mwao MaShaykh, wamedharau tawassul zilizokubaliwa – hutowasikia wakijikurubisha kwa Allaah kwa tawassul hizo, bali wamebobea katika aina za tawassul za bid’ah ambazo angalau kwa uchache zinasemwa kuwa zimekhitilafiana – wanazidumisha kama kwamba nyinginezo hazifai. Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah ameandika makala ndefu kuhusu maudhui hii yenye kichwa cha habari: At-Tawassul Wal-Wasiylah (Kujikurubisha kwa Allaah na njia zake) ipasayo kufuatwa, kwani ni muhimu sana hakuna mfano wake katika maudhui hii. Pia kuna makala yangu "Tawassul Anwaa'uhaa wa Ahkaamuhaa" ambayo pia ni muhimu katika maudhui yake na mfumo wake, na pia inakanusha shubuhaat mpya kutoka kwa baadhi ya Madaktari wa kisasa wa dini. Allaah Atuongoze pamoja nao.
[16] Abu Daawuud, An-Nasaaiy, Ahmad, Al-Bukhaariy katika Al-Adaabu Al-

Mufrad, At-Twabaraaniy na Ibn Mandah katika Tawhiyd (44/2, 67/1, 70/1-2) ikiwa na isnaad Swahiyh.

[17] Muslim na Abu ‘Awaanah.
 
056-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Tasliym (Kutoka Salaam) Na Uwajibu Wake


Tasliym (Kutoka Salaam)


Kisha, “Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akitoa salaam upande wa kulia:

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ



Assalaamu ‘Alaykum wa RahmatuLlaah



“Amani na Rahma iwe juu yenu” (akigeuka hadi weupe wa shavu lake la kulia ukionekana)



Na upande wa kushoto:

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ



Assalaamu ‘Alaykum wa RahmatuLlaah



“Amani na Rahma iwe juu yenu”



(akigeuka hadi weupe wa shavu lake la kushoto ukionekana)”([1]) Mara nyingine aliongeza katika maamkizi upande wa kulia:

وَبَرَكَاتُهُ

Wa Barakaatuh



…Na Baraka Zake (zishuke kwenu)([2])



"Aliposema

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ وَرَحْمَةُ اللَّهِ



Assalaamu ‘Alaykum wa RahmatuLlaahi

“Amani na Rahma ya Allaah iwe juu yenu”

Upande wa kulia, alipunguza mara nyingine alipatoa salamu upande wa kushoto;

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ



Assalaamu ‘Alaykum

“Amani iwe juu yenu”([3])



Mara nyingine, "aliamkia mara moja tu:

السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ

Assalaamu ‘Alaykum



“Amani iwe juu yenu”

(mbele ya uso wake akigeuza upande wake wa kulia kidogo) [au kidogo tu]"([4])

"Walikuwa wakiashiria mikono yao walipotoa slaamu upande wa kulia na kushoto; Alipowaona Mjumbe wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alisema: ((Mna nini nyinyi? Mnaashiria mikono yenu kama kwamba ni mikia ya farasi mwitu?! Anapotoa salamu mmoja wenu, atazame mbele ya mwenziwe na sio kuashiria kwa mikono yake))



Hivyo waliposwali naye, hawakuashiria) [katika riwaaya nyingine: ((Inatosheleza kila mmoja wenu kuweka mkono wake pajani kisha kutoa slaamu kwa nduguye aliyoko upande wa kulia kwake au kushoto))([5])







Wajibu Wa Tasliym (Kutoa Salaam)



Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم) akisema: ((…na inamalizika (yaani Swalah) kwa tasliym))([6])







[1] Abu Daawuud, An-Nasaaiy na At-Tirmidhiy ambaye amekiri ni Swahiyh.

[2] Abu Daawuud na Ibn Khuzaymah (1/82/2) ikiwa na isnaad Swahiyh.

‘Abdul-Haqq pia amekiri kuwa ni Swahiyh katika Ahkaam (56/2) kama alivyokiri An-Nawawiy na Ibn Hajar. Pia imesimuliwa kupitia njia nyingine na ‘Abdur-Razzaaq katika Muswannaf (2/219). Abu Ya’ala katika Musnad yake (3/1253), At-Twabaraaniy katika Mu’jam Al-Kabiyr (3/67/2) na Mu’jam Al-Awswatw (Namba: 4476 – Nambari zangu) na Ad-Daaraqutwniy.

[3] An-Nasaaiy, Ahmad na Siraaj ikiwa na isnaad Swahiyh.

[4] Ibn Khuzaymah, Al-Bayhaqiy, Adh-Dhwiyaa katika Al-Mukhtaarah na 'Abdul-Ghaaniy Al-Maqdisiy katika Sunan yake (243/1) ikiwa na isnaad Swahiyh; Ahmad, At-Twabaraaniy katika Mu'jam Al-Awswatw (32/2), Al-Bayhaqi, Ibn Al-Mulaqqin (29/1) na Al-Al-Haakim ambaye amekiri ni Swahiyh, na Adh-Dhahabiy amekubali. Takhriyj yake imetolewa katika Al-Irwaa Al-Ghaliyl katika Hadiyth Namba 327.

[5] Muslim, Abu 'Awaanah, Siraaj, Ibn Khuzaymah na At-Twabaraaniy.





TANBIHI:



Maibaadhi wamegeuza Hadiyth hii. ‘Aalim wao Rabiy' amesimulia katika Musnad isiyotegemewa ikiwa na kauli mbali mbali kuthibitisha rai zao kwamba kunyanyua mikono pamoja na takbiyr inatengua Swalah! Kauli hiyo ni uongo, kama nilivyoelezea katika Adh-Dhwa'iyfah (6044).

[6] Al-Al-Haakim, na Adh-Dhahabiy amekiri Swahiyh. Imeshatolewa kikamilifu katika 'Takbiyr' ya kufungulia.
 
057-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Hitimisho




Hitimisho



Yote yaliyotangulizwa humu kuhusu sifa ya Swalah ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) yanawahusu wanamume na wanawake, na wala haikuthibiti katika Sunnah kwamba kuna baadhi ya mambo yanamtofautisha (inayomtenga) mwanamke, bali inahikisha kauli ya ujumla ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم):

((Swalini kama mlivyoniona nikiswali)).




Hivyo imejumuisha wanawake wote, na kauli ya Ibraahiym An-Nakha'iy amesema: "Mwanamke anafanya kama anavvyofanya mwanamume katika Swalah" [Imetoka kwa Ibn Abi Shaybah (1/75/2) ikiwa na isnaad Swahiyh kutoka kwake]




Al-Bukhaariy amesimulia katika At-Tariykh As-Swaghiyr (Uk. 95) ikiwa na isnaad Swahiyh kutoka kwa Umm Ad-Dardaa: "Alikuwa akikaa katika Swalah yake kikao cha wanaume na alikuwa ni Faqihi"




Ama Hadiyth inayosema mwanamke ajikunje katika Sujuud na kwamba yeye sio sawa na mwanamume, ni Hadiyth Mursal haina hoja. [Amesimulia Abu Daawuud katika Al-Maraasil] (117/87) kutoka kwa Yaziyd Ibn Abi Habiyb ambaye ametolewa katika Adh-Dwa'iyfah (2652).

Ama ile aliyosimulia Imaam Ahmad katika Masaail (ya mwanawe) Ibn 'Abdullaah kutoka kwake, (Uk.71) kutoka kwa Ibn 'Umar kwamba alikuwa akiwaamrisha wanawake waketi kimarufaa, (Hadiyth hii) haisihi isnaad yake kwa sababu yumo 'Abdullaah bin Al-'Amriy ambaye dhwa’iyf.




********







Haya ndiyo yaliyowezekana kukusanya pamoja katika kuelezea Sifa Ya Swalah ya Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم) Kutoka Takbiyr Hadi Tasliym. Natumai kwamba Allaah Ataijaalia iwe yenye ikhlaasw mbele ya Uso Wake Mkarimu na uongofu kwa Sunnah ya Mtume Wake Raufur-Rahiym (…Mpole)




سُبْحـانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ سُبْحَانكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمدِك، أَشْهَـدُ أَنْ لا إِلهَ إِلاّ أَنْتَ أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتوبُ إِلَـيْك. اللّهُـمَّ صَلِّ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى آلِ مُحمَّدٍ. وَبارِكْ عَلـى مُحمَّـدٍ وَعَلـى آلِ مُحمَّـد كَمـا صَلَّيْتَ وَبارَكْتَ عَلـى إبْراهيم وَآلِ إبْراهـيمَ إِنَّكَ حَمـيدٌ مَجـيد




Subhaana-Llaahi wa-Bihamdihi, Subhaanaka Llaahumma wa-Bihamdika, ash-hadu an laa ilaaha illa Anta, Astaghfiruka wa atuwbu Ilayka, Allaahumma swalliy ‘alaa Muhammad, wa ‘alaa aali Muhammad, wa Baarik ‘alaa Muhammad, wa ‘alaa aali Muhammad, kama Swallayta wa Baarakta ‘alaa Ibraahiyma, wa aali Ibraahiyma, Innaka Hamiydum-Majiyd.




“Ametakasika Allaah, na sifa njema zote ni zake. Kutakasika ni kwako Ee Allaah, na sifa njema zote ni Zako. Nakiri kwamba hakuna mola apasae kuabudiwa kwa haki ila Wewe, nakuomba msamaha na ninarejea Kwako.

Ee Allaah, Mswalie Muhammad na jamaa zake Muhammad, na Mbariki Muhammad na jamaa zake Muhammad kama Ulivyomswalia na Ukambariki Ibraahiym na jamaa zake Ibraahiym hakika Wewe ni mwenye kusifika Mtukufu”([1])

















[1] Du'aa ya mwanzo ni du'aa kamili inayojulikana kama Kaffaaratul-Majlis

(kafara ya kikao): ((Atakayeisema katika mkusanyiko wa kumkumbuka (Allaah) itakuwa kama ni mhuri wa kuchapia, na atakayesema katika mkusanyiko wa maneno ya kipuuzi, itakuwa kama ni kafara yake)) [Imeripotiwa na Al-Al-Haakim na Atw-Twabaaraniy ikiwa Swahiyh]. Du'aa ya pili ni Sunnah kumswalia Mtume (صلى الله عليه وآله وسلم). Du'aa hizi mbili hivyo ni njia bora kabisa katika kutekeleza miongozo ya Kiislamu. ((Hapana watu wowote wale wanaokaa kikao chochote bila ya kumtaja Allaah, wala kumswalia Mtume ila itakuwa dhambi kwao, Allaah Akipenda Atawaadhibu, au Akipenda Atawasamehe)) [Imesimuliwa na At-Tirmidhy, Al-Al-Haakim, Ahmad ikiwa Swahiyh] Taz. Silsilatu Al-Haadiyth As-Swahiyhah cha Shaykh Al-Albaaniy (74/81) kwa maelezo.
 
Alhamdulillah tumemaliza kusoma kitabu cha Sifa ya Swalaa ya Nabii swallallahu alaih wasallam

Kuna mengi tumejifunza na kupitia kwayo tumeona mapungufu yetu na kuyafanyia kazi

Binafsi nimejikuta na mapungufu kadhaa lakini alhamdulillah nimeyafanyia kazi na tayar yapo katika utekelezaji,natumaini nawe pia utafanya hivyo

Kumbuka kusoma kwa muislamu ni ibada,na kujua mlango mmoja wa ibada na kuifanya ibada yako vizuri ni bora kuliko kuswali swala za sunna 1000

Elimu imesogezwa karibu na wewe hapa jamii forums

Endelea kufuatilia uzi.........
 
Makosa Katika Ufahamu Wa Hukmu Za Wudhuu



Imetarjumiwa Na: Abu 'Abdir-Rahmaan Sulaymaan




Alhidaaya.com







1 – Wapo baadhi ya watu wanasema huwezi kutia Wudhuu huku ukiwa uko uchi.



Mwanachuoni 'Abdul-'Aziyz bin Baaz (Rahimahu Allaah) amesema:



"Kufunika tupu (uchi) wako si katika nguzo za Wudhuu [Kwa mfano kuchukua Wudhuu ukiwa bafuni unaoga]."

[Fatawa Ibn Baaz 10/101]





2 – Kuna wanaodhania kwamba kutanguliza kuosha kiungo cha mkono wa kushoto kwanza kabla ya kulia kwa kusahau ni makosa wakati unatia Wudhuu.



Imam An-Nawawiy (Rahimahu Allaah) amesema:



"Wamekubaliana Wanachuoni kuwa kuanza kutia Wudhuu viungo vya mkono wa kulia na kufuatia mkono wa kushoto ni Sunnah, lakini ukianza mkono wa kushoto kabla ya kulia pia Wudhuu huo unakubalika."

[Sharh Swahiyh Muslim 3/10]





3 – Watu wengi hunyanyua kidole wakati wakitamka shahaadah wakati wa kusoma du'aa ya kumaliza kuchukua Wudhuu.



‘Allaamah Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:

"Siijui asli yake kitendo hicho.

[Fataawa Nuwr 'Alaa Ad-Darb 8/117]





4 – Kuna baadhi ya watu wanasema ukigusa najisi itakubidi urudie kutia Wudhuu tena!



‘Allaamah Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:



‘Kukanyaga najisi wakati bado kibichi/kimajimaji hakitengui Wudhuu wako, Hata hivyo, mtu anatakiwa kusafisha, na hapa inakusudiwa ni kusafisha pale palipoingia najisi hiyo tu.’

[Fataawa Ibn 'Uthaymiyn 2/119]





6 – Watu wengi huona tabu kupangusa kwenye soksi zenye tundu wakati wanatia Wudhuu.



‘Allaamah Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:



"Inajuzu kufuta juu ya soksi hata kama ina matundu na pia kupangusa juu ya Khuff nyepesi (soksi za ngozi), kwa sababu Maswahaba wengi walikuwa maskini, na kwao ni kawaida kukuta wamevaa Khuff zenye matundu."

[Fataawa Ibn 'Uthaymiyn 11/116]





7 – Kuna baadhi ya watu wanapangusa soksi wakati wanachukua wudhuu, soksi hizo zina mapicha ya viumbe vyenye roho.



‘Allaamah Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema:



‘Haijuzu kupangusa soksi zenye picha ya mnyama, kwani kupangusa juu ya Khuff inajuzu lakini si katika kumuasi Allaah."

[Fataawa Ibn 'Uthaymiyn 11/116]



Na sifa zote Anastahiki Allaah, na Rahmah na amani za Allaah ziwe juu ya Mtume wetu wa mwisho Muhammad, familia yake, na Maswahaba zake na wote watakaomfuata.
 
Nguzo Za Swalaah, Vitendo Vya Waajib Na Sunnah Katika Swalaah





Alhidaaya.com





BismiLlaah ar-Ramaanir Rahiym



Nguzo za Swalah ni 14: Nguzo ni zile ambazo ukiswali na ukaziacha kwa makusudi Swalah yako inabatilika, na ikiwa umeacha kwa kusahau, Swalah yako pia itakuwa haikukamilika hadi urejee kitendo chenyewe au urejee rakaa na kisha mwishoni utoe Sajdatus-Sahw. Lakini ukiwa umesahau nguzo ya Takbiyratul-Ihraam, basi itakubidi uiswali Swalah upya tokea mwanzo.



Nguzo hizo 14 ni hizi zifuatazo:



1. Kusimama katika Swalah za Fardh kwa yule mwenye uwezo. (Wanachuoni wengine wamesema nguzo ya kwanza ni Niyah kabla ya Kusimama). Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema:

وَقُومُوا لِلَّـهِ قَانِتِينَ

"Na simameni mbele ya Allaah katika hali ya utiifu" [Al-Baqarah: 238].



Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Swali hali ya kuwa umesimama, usipoweza, basi kwa kukaa na usipoweza basi kwa kulala ubavu" (Al-Bukhaariy na Abu Daawuud).



2. Takbiyrah ya kuhirimia (Takbiyratul-Ihraam) kwa tamko la Allaahu Akbar kutokana na kauli ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Ufunguo wa Swalah ni kujitwaharisha, na kuifunga ni Takbiyrah, na kuifungua ni kutoa Salaam" (Abu Daawuud na At-Tirmidhiy).



3. Kusoma Suratul-Faatihah katika kila rakaa. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema: "Hapana Swalah kwa ambaye hakusoma Suratul Faatihah" (Al-Bukhaariy).



4. Kurukuu.



5. Utulivu (Twumaaniynah) katika Rukuu.



6. I'itidaal (hapa inaingia na kunyanyuka kutoka katika Rukuu hadi anaponyooka mtu).



7. Utulivu katika I'Itidaal.



8. Kusujudu.



9. Utulivu katika kusujudu. Kutulia wakati wa kurukuu, kusujudu, kusimama, kukaa baina ya Sijdah mbili kwa msemo wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Kisha rukuu mpaka utulizane hali ya kurukuu, kisha nyanyuka mpaka ulingane sawa hali ya kusimama, kisha sujudu mpaka utulizane na hali umesujudu, kisha nyanyuka mpaka utulizane hali ya kuwa umekaa" (Al-Bukhaariy).



10. Kikao baina ya Sijdah mbili.



11. Utulivu katika kikao baina ya Sijdah mbili.



12. Tashahhud ya mwisho.



13. Kikao katika Tashahhud ya mwisho.



14. Salaam (Kutoa Salaam) ya kwanza.



Utahakikisha unafuatanisha yote hayo kama utaratibu ulivyopangika.



Waajib Katika Swalah:



Ni lile ambalo ni wajibu kulifanya au kusema, inaondoka kwa kusahau na kulazimisha mwenye kuswali kusujudu sijdah mbili za kusahau. Yeyote mwenye kuacha kwa kusudi Swalah yake inabatilika ikiwa anajua uwajibu wake.



Istilahi hii inatumika kwa madhehebu ya Hanafi na Hanbali ila ma-Hanafi hawaoni kuwa mwenye kuacha wajibu kwa kusudi inabatilisha Swalah yake bali yeye amefanya madhambi anayostahiki adhabu. Ama ma-Maaliki na ma-Shaafi'y hawana kigawanyo hichi cha Waajib kwao ila wao wana nguzo na Sunnah kwa ujumla wake.



Ama hapa tutaweka yale yaliyotajwa ambayo yanaelekea kuwa na nguvu zaidi.



Kwanza kabla hatujataja mambo yenyewe, tunapaswa kujua kuwa mambo ya Waajib ni yale ambayo vilevile atakapoacha mtu kwa makusudi hubatilika Swalah yake, na atakapoacha kwa kusahau inamtosheleza yeye kusujudu Sijda mbili za kusahau 'Sujuudus-Sahw'.



Ama mambo ya Waajib ambayo yametajwa katika kitabu cha 'Swahiyhu Fiqhus-Sunnah' kwa dalili mbalimbali za Aayah na Hadiyth ni 9 kama yafuatayo:



1. Du'aa ya ufunguzi wa Swalah 'Du'aa al-Istiftaah'.



2. Kusema 'A'udhu biLlaahi Minash-Shaytwaan ar-Rajiym' kabla ya kusoma 'BismiLlaah ar-Ramaanir Rahiym' na 'Suratul-Faatihah'.



3. Kusema 'Aamiyn' baada ya Suratul-Faatihah.



3. Takbiyrah za kuhama baina ya kitendo na kitendo.



4. Kusema 'Sami'a Allaahu liman hamidah'



5. Kusema 'Rabbana Lakal Hamdu' katika I'itidaal.



6. Kusema 'Subhaana Rabbiyal 'Adhwiym' wakati wa kurukuu na kusema 'Subhaana Rabbiyal A'ala' wakati wa kusujudu.



7. Tashahhud ya kwanza.



8. Kikao cha Tashahhud ya kwanza.



Wanachuoni wengine wametaja mambo ya Waajib ni 8 kama yafuatayo:



1. Takbiyrah nyingine zote isiyo ile ya Ihraam.



2. Kusema 'Sami'a Allaahu liman hamidah' kwa Imaam na mwenye kuswali peke.



3. Kusema 'Rabbana Lakal Hamdu'.



4. Kusema 'Subhaana Rabbiyal 'Adhwiym’ mara moja kwenye kurukuu.



5. Kusema 'Subhaana Rabbiyal A'ala' kwenye kusujudu.



6. Kusema 'Rabbi-Ghfir liy' kwenye kikao baina ta Sijda mbili.



7. Tashahhud ya mwanzo.



8. Kikao katika Tashahhud ya mwanzo.



Hizi ndizo maarufu zaidi kwa Wanachuoni wengine.



Sunnah Za Swalah



Hizi ni kauli na vitendo zinazopendeza kuletwa katika Swalah. Mwenye kufanya hayo hupata thawabu wala Swalah haibatiliki kwa kuachwa hata kwa kusudi. Wala sijdah ya kusahau hailetwi. Hapa tuna vigawanyo viwili vya Sunnah katika Swalah; Sunnah za kauli na Sunnah za vitendo.



Sunnah Za Kauli



1. Kisomo baada ya al-Faatihah.



2. Dhikr nyinginezo katika Rukuu.



3. Dhikr baada ya kusimama kutoka katika Rukuu na baada ya kusema ‘Rabbana Lakal Hamd’.



4. Dhikr nyinginezo katika Sujuud.



5. Du’aa baina ya Sijdah mbili.



6. Kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika Tashahhud ya kwanza na ya pili.



7. Du’aa baada ya Tashahhud ya kwanza na ya pili.



8. Salaam ya pili.



9. Dhikr na du’aa mbalimbali baada ya Swalah.



Sunnah Za Vitendo



1. Kuweka Sutrah (kizuizi mbele ya sehemu unayoswalia) katika Swalah.



2. Kunyanyua mikono wakati wa Takbiyratul Ihraam, na wakati wa kurukuu na na wakayi wa kunyanyuka kwayo na wakati wa kuinuka kutoka katika Tashahhud ya kwanza. Na kadhalika wakati unapoinama na kuinuka.



3. Kuweka mkono wa kuume juu ya mkono wa kushoto juu ya kifua unaposimama kuswali.



4. Kutazama mahali pa kusujudu.



5. Kulingana sawa mgongo unaporukuu na kutonyanyua kichwa au kukiinamisha sana, na kuweka viganja kwenye magoti mawili na huku umeviachanisha vidole vya mikono na kuachanisha viwiko visiguse mbavu au tumbo lako.



6. Kuteremka katika Sijdah kwa mikono miwili kabla ya magoti (Wengine huona kushuka kwa magoti kabla ya mikono).



7. Kuimakinisha paji la uso, pua na mikono (viganja viwili) kwenye ardhi pamoja na kupanua mikono isiguse mbavu zako; kuwe na uwazi wa kuweza kupita kinyama kidogo. Na viganja vyako viwe usawa wa mabega au masikio wakati uko katika kusujudu na viwiko vikiwa vimenyanyuliwa juu na vidole vya mikono vikiwa vinaelekea Qiblah. Matumbo ya vidole vya miguu yakiwa ardhini visigino vikielekea juu na hali vidole vya miguu vikielekea Qiblah.



8. Kulilalisha guu la kushoto na kulisimamisha la kulia wakati wa kikao baina Sijdah mbili.



9. Kurefusha kikao baina ya Sijdah mbili.



10. Kikao cha mapumziko baada ya kukamilisha rakaa ya kwanza na ya tatu.



11. Kutegemea ardhi kwa mikono wakati mtu anaponyanyuka kutoka kusujudu na kwenda kwenye rakaa nyingine.



12. Kukaa kikao cha Iftiraash (Kusimamisha mguu wa kulia na kukalia mguu wa kushoto) katika Tashahhud ya mwanzo. Na kukaa kikao cha Tawarruk (kusimamisha mguu wa kulia na kuipitisha mguu wa kushoto chini ya muundi wa mguu wa kulia na huku kikalio chako kimekaa juu ya ardhi).



13. Kuashiria kwa kidole cha shahada katika Tashahhud kuanzia mwanzo hadi mwisho bila kukishusha na huku unasoma na ukikitazama. (Abu Maalik Kamaal Saalim, Swahiyh Fiqhus Sunnah, Mj. 1).



Ingawa kuna ikhtiliaaf baina ya Wanachuoni katika mas-alah hayo, tunapenda kuwakumbushia Hadiyth ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliyesema: "Swalini kama mlivyoniona nikiswali" (Al-Bukhaariy).



Kwa hivyo, ni juu yetu kufanya juhudi kufuata yote aliyofanya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ili Swalah zetu zitimize daraja zote za ujra na ili tuchume thawabu nyingi zaidi.
 
Hawajafanya Jimai Bali Wamefanya Matendo Mengine Wanahesabiwa Wamezini? Nini Hukmu Yao?
Maswali: Zinaa-Liwati



SWALI:



ASSALAMU ALAYKUM, NINATAKA UFAFANUZI KUZINI NI KULE KWA MWANAMME KUUINGIZA UTUPU WAKE KWA MWANAMKE AU HATA KAMA HAJAUINGIZA TAYARI WANAKUWA WAMESHAZINI. NA JEE KAMA WATATUBIA KWA KOSA LA KUFANYA HILO TENDO BILA YA TUPU YA MWANAMME KUINGIA KWENYE TUPU YA MWANAMKE NI LAZIMA IPITISHWE ILE HUKUMU YA ALLAH SUBHANAHU WATAALA YA KUPIGWA MAWE AU MIKWAJU MIA?









JIBU:



Sifa zote njema Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu kwa mwanamme na mwanamke kufanya starehe bila ya kuzini hasa.

Hakika ni kuwa katika Uislamu zinaa inayochukuliwa kuwa ni ile halisi ni kule kujamiiana mwanamme na mwanamke ambao si wanandoa kishari’ah. Hao ndio wenye kupata adhabu ya kishari’ah – ikiwa hajaoa au kuolewa basi adhabu yake ni kupigwa mikwaju mia na ikiwa ameoa au kuolewa, yuko katika ndoa au ametalikiwa basi adhabu ni kupigwa mawe hadi kufa. Kwa ufupi zinaa ni kuingia utupu wa mwanamme kwenye utupu wa mwanamke.



Mbali na kitendo hicho cha kuthibitisha jimai vitendo vingine vinahesabiwa kuwa ni zinaa lakini hakuna adhabu kwa mwenye kufanya ila tu anapata madhambi na anahitajika kuomba tawbah kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala).



Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) huku Anawakataza waja Wake wasizini na kuikaribia na kuchanganyika na sababu zitakazo kupelekea katika uzinzi. Anasema Aliyetukuka:

“Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu” (al-Israa’ [17]: 32), yaani ni dhambi kubwa.

Na pia, “Na ni njia mbaya”, yaani ni njia mbaya sana kwa mtu kuifuata. Kila kiungo katika mwili wa mwanaadamu kinazini kama alivyotuelezea Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam), mikono, miguu, mdomo, macho na viungo vinginevyo.




Bonyeza viungo vifuatavyo upate maelezo zaidi:




Kufanya Mapenzi Bila Ya Kitendo Cha Ndoa Kwa Ambaye Hajaolewa?







Kulala Pamoja Bila Ya Kufunga Ndoa




Nakaribia Kuzini na Mke wa Ndugu Yangu Vipi Nijiokoe?




Nakaribia Kuzini Na Shemeji, Je, Nifanyeje Kujiepusha Na Vipi Nitahukumiwa Na Allaah?






Ikiwa mtu amefanya mambo mengine bila ya kujimai kabisa inatakiwa afuate na kutekeleza masharti yafuatayo ili aweze kusamehewa na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):



1. Asirudie tena kosa hilo.

2. Ajute kwa kufanya kosa hilo.

3. Aweke azma ya kutorudia tena.



Ukiwa mtu atatekeleza masharti hayo basi Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Atamsamehe.



Na Allaah Anajua zaidi
 
Kufanya Mapenzi Bila Ya Kitendo Cha Ndoa Kwa Ambaye Hajaolewa?
Maswali: Zinaa-Liwati





SWALI:




Asalaam alykum, hukumu ya kufanya zinaa kwa asiekua katika ndoa ni kuchapwa fimbo 100 hadharani. Je nini hukumu ya afanyae 'romance' kwa asiekua katika ndoa. Ahsante









JIBU:




Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.




Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kufanya mapenzi tu bila ya kujamiiana. Awali ya yote sijui kwa nini Muislamu atakwenda kufanya mapenzi kabla ya ndoa baada ya Allaah Aliyetukuka kutuambia tusikaribie hata zinaa:




“Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya” (17: 32).




Hii inaonyesha wazi kuwa jambo la kukaribia zina ni maasi makubwa na Muislamu anapaswa kujiepusha nayo kabisa. Vile vile haya ni mambo ya uchafu wa Makafiri, sisi Waislamu tuna sheria zetu zilizowekwa katika mas-ala mapenzi na ndoa, na kuzifuata ndio usalama wetu kutokana adhabu ya Allaah na pia usalama wetu binafsi.




Pia Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amehimiza pale aliposema:




“Ni bora kwa mwanamme kupigwa sindano ya chuma katika kichwa chake kuliko kuushika mkono wa mwanamke ambaye si halali yake” [At-Twabaraaniy na Silsilat Al-Ahaadiyth As-Swahiyhah - Shaykh Al-Albaaniy].




Hata hivyo, kufanya kitendo hicho hakina adhabu maalumu katika sheria ya Kiislamu. Kwa kufanya lile ni funzo kwa wenye kufanya vitendo kama hivyo ambavyo vitawakaribisha na zinaa, sheria imemuachia mtawala wa Kiislamu au Qaadhi atoe adhabu. Hata hivyo, adhabu kama ambazo huitwa Ta’ziyr katika sheria itakuwa duni kuliko ile ya viboko mia moja. Inawezekana ikawa ni viboko kumi au adhabu nyengine yoyote anayohukumu Qaadhi.




Na Allaah Anajua zaidi
 
Nakaribia Kuzini na Mke wa Ndugu Yangu Vipi Nijiokoe?



Alhidaaya.com







SWALI:



Assalaam aleykum. Mimi nikijana,ila nina tatizo kubwa ambalo linalo nifanya huwa nakosa raha kwa ajili ya Mwenyezi Mungu wangu.mimi naishi na kaka yangu.ambaye ananisaidia kwa sasa, kutoka na nina matatizo katika hiyo nchi tunayo ishi.ila ndugu yangu yeye ameowa,na anawatoto. Ila kuna jambo ambalo limekuwa,limenifanya kuwa karibu sana na mkewe kutokana huwa na msaidia sana kazi zake.mpaka ikawa ananieleza matatizo yake na ndugu yangu.na kwa mujibu ya maelezo yake,ndugu yangu alikuwa anamakosa,ya kuwa ya kumuuzi mkewe. kama kwenda nje ya ndoa,ilifikia mpaka mkewe alitaka kuachika.ila nilijitahidi kuongea na shemeji yangu alinisikiliza na kuacha hizo fikira mbaya.ila baadae mambo ya kabadilika tukajikuta mimi na shemeji yangu, tumeingia kwenye mtihani wa kupendana.na kufikia mpaka tukaanza kupigana mabusu,ila hatujawahi kuzini hata siku moja kwa kumuogopa Mola wetu.kwani mimi na shemeji yangu tunaswali.je unaweza kutusaidiaje kuliacha hili tatizo?na tofauti gani ya kukurubia zinaa na kuzini?











JIBU:



AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na Salaam zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho





Shukrani ndugu yetu kwa swali lako zuri kuhusu mas-ala nyeti kama hiyo. Pia shukrani zetu kwako ni kuwa umeliona lipo tatizo na hivyo kutaka usaidizi wa kuweza kutatua tatizo hilo kabla hujapitiwa na wakati na kuingia katika madhambi ambayo huenda ikawa vigumu kujitoa kwayo.



Ujana ni wakati ambapo damu inakuwa moto na matamanio yanampelekea mja kujaribu mambo mengi pamoja na kuingia katika mambo ya maasi. Lakini inatakiwa kwetu sisi tuchukue vielelezo vya vijana walioelezwa na Allaah Aliyetukuka waliokataa kuingia katika madhambi aina yoyote. Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Anatueleza kuhusu vijana wa pangoni:





“Hakika wao walikuwa ni vijana waliomuamini Rabb wao. Nasi Tukawazidishia uongofu. Na Tukazitia nguvu nyoyo zao pale waliposimama mbele ya mfalme wakasema: Rabb wao ni Rabb wa mbingu na ardhi. Hatutamuabudu mungu mwingine badala Yake” (18: 13 – 14).





Utaona hapa vijana walisimama imara na kwa sababu hiyo Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Akawaongezea uongofu. Hilo halikutosha, hivyo wakaona ni afadhali waondoke katika sehemu yenye maasiya pamoja na kuomba usaidizi wa Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) katika hilo. Anatuelezea Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) hilo pale Aliposema:



“Ee Rabb! Tupe rehema zinazotoka kwako na Tutengezee uongofu katika kila jambo letu” (18: 10).



Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Anatueleza kuhusu Nabii Yuusuf (‘Alayhis Salaam) na mitihani aliyopata kutoka kwa mke wa waziri alipokuwa kijana barobaro. Ikafika hadi ya kwamba mwanamke huyo anamtaka kwa nguvu lakini akakataa katakata jambo hilo la kuzini. Hapo Nabii Yusuf (‘Alayhis Salaam) kutaka kujiokoa na dhambi hilo alimuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala):





“Ee Rabb! Napendelea zaidi gereza kuliko haya wanayoniitia; na usiponiondolea hila zao nitawaelekea na nitakuwa miongoni mwa wajinga (wafanyao maasi)” (12: 33).





Maombi hayo yake ya ikhlaasw yakapokewa na Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) na hivyo kuondoka katika mazingira hayo mabaya.





Kosa lako ulilofanya ambalo ni aina mojawapo ya zinaa ni kukaa faragha na shemeji yako. Hilo ni jambo ambalo limekatazwa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwani watatu wenu ni shetani. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:





“Tahadharini na kuingia kwa wanawake”. Akaulizwa: “Je, ham-wa (ndugu ya mume [shemeji])”. Akasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Huyo ni mauti” (al-Bukhaariy na Muslim).





Na katika Hadiyth nyengine, akasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Hakai faragha mwanamke na mwanamume isipokuwa watatu wao ni shetani. Hakika shetani hutembea kama damu mwilini mwa mwanadamu”.





Amesema tena (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Mwenye kumuamini Allaah na Siku ya Mwisho, basi asikae peke yake na mwanamke asiyekuwa maharimu yake pamoja naye, kwani watatu wao ni shetani” (Ahmad).





Tunafahamu kuwa shetani ni adui wetu wa jadi na hatutakii mema na mazuri.





Kuwa kwako karibu na shemeji yako ndiyo kutakuletea matatizo zaidi kuliko kutatua baina ya hao wanandoa. Hiyo ni kwamba lau kakako atakuja jua ukaribu wenu wa namna hiyo sijui anaweza kukufanya nini? Je, ataanza kukuchukia na kuondoa usaidizi wake au vipi? Ikiwa uhasama unaweza kuwa namna hiyo je, hamujaogopa basi kumuasi Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala)? Kisha kusikiliza mashtaka ya upande mmoja sio sawa kwani unapata shida anazokumbana nazo mmoja wao peke yake kati ya wawili hao. Inatakiwa kwako baada ya kuelezwa na kuyasikia ya shemeji yako umuite nduguyo naye akueleze ili upate toa uamuzi. Au uwalete wote pamoja umsikilize mmoja baada ya mwengine kabla ya kuwa unao uwezo ima ya kuwapatia nasiha au kutatua shida kutoka shinani mwake katika matatizo hayo. Ikiwa kumkalisha chini nduguyo ni vigumu usiwe ni mwenye kusikiliza malalamishi ya shemeji yako kwani itakuwa nadharia kama sasa kuwa nduguyo ni mkosa bila hata kufanya mengi yanayotakiwa katika kusikiliza kesi za watesi. Yatakiwa tuelewe kuwa msingi mkuu wa Uislamu ni: “Mtu anakuwa hana hatia mpaka ithibitishwe kinyume chake”.





Kuhusu kaka yako kwenda kuzini, je, upo ushuhuda wowote kuhusu hilo? Ikiwa hamna, hayo katika sheria yanachukuliwa ni masingizio na anayehusika kufanya hayo masingizio anapewa adhabu ya kupigwa mijeledi 80.







Hali hiyo ya zinaa baina yenu ni lazima itafika ikiwa tumeacha maagizo ya Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) na Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na ukitojichunga utajikuta umezini kikweli na pengine shemejiyo abebe mimba yako. Ikifika hali hiyo, mnategemea nini na mtakuwa katika hali gain wakati huo? Je, mumefikiria yote hayo? Au ni vishawishi vya shetani vya muda mfupi vyenye kuwapumbaza?





Ni masikitiko makubwa kuwa mke anasema kuwa mumewe anazini na sasa nyinyi mnataka kutumbukia huko huko kwenye kitanda chake ndani ya nyumba yake!! Hili sijui mnalionaje nyinyi?





Hakika ni kuwa japokuwa hamjazini kwa kujamiiana lakini mmezini kwa njia nyingi. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametueleza kuwa jicho kwa kuangalia linazini, masikio, midomo, mikono, miguu na viungo vyengine vyote vinazini. Na kwa kuwa mmefika hata kupigana mabusu mmekaribiwa zaidi na zinaa yenyewe.





Inawezekana kuwa Imani ipo lakini ikiwa mngekuwa mnamuogopa Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) kihakika hamgefika katika kupigana mabusu. Kuswali peke yake si hoja, kwani yapo madhambi ambayo yanafuta thawabu za Swalah. Swalah inatakiwa imuepushe mtu na machafu ambayo nyinyi mnayaendea polepole. Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Anasema:





“Bila shaka, Swalah humzuiliya mtu mwenye kuiswali mambo machafu na maovu, na kwa yakini kumdhukuru Allaah ni jambo kubwa kabisa. Na Allaah Anajua mnayoyatenda” (29: 45).





Je, Swalah mnayoswali imewaepusha na machafu na maovu ikiwa mnapigana busu? Nadhani jawabu ya swali hili litatoka kwako.





Kwa hakika zifuatazo ni nasiha zetu ambazo zinaweza kuwasaidia sana:





(a) Kuwa na niya nzuri na ikhlaasw katika matendo yako.







(b) Tambua kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Anakuona wakati wote. Katika hilo Atakupatia thawabu kwa mema unayoyafanya hata yakiwa ni wizani wa atomu na unapofanya maovu unaandikiwa madhambi. Ufahamu kuwa baadaye utahesabiwa na Aliye muadilifu na wala hutodhulumiwa.





(c) Kukumbuka mauti, kwani maisha ya hapa duniani ni mafupi. Je, umejitayarisha vipi kukutana na Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala)? Pia kujikumbusha Akhera kwa kuzuru makaburi.





(d) Kutekeleza ‘Ibaadah kama inavyotakiwa kwa kufuata Sunnah za Bwana Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).





(e) Kusoma Qur-aan kwa mazingatio na kujaribu kuyafuata maagizo yake katika maisha yako. Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Anatueleza: “Na wanaposomewa Aayah Zetu huwazidishia Imani, na wakamtegemea Mola wao Mlezi tu” (8: 2).





(f) Kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) kwa wingi kwa kumtakasa kwa kusema (SubhaanAllaah), kumtukuza na kumsifu (AlhamduliLlaah), kumpwekesha (Laa ilaaha illa Allaah), Allaahu Akbar (Allaah ni Mkubwa). Pia kuleta nyiradi za asubuhi na jioni. Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Anaesema: “Wale walioamini na zukatulia nyoyo zao kwa kumkumbuka Allaah. Sikilizeni! Kwa kumkumbuka Allaah nyoyo hutulia” (13: 27). Pia: “Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allaah nyoyo zao hujawa hofu” (8: 2).





(g) Kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Akuletee la kheri ili usiwe pale nyumbani wakati mwingi. Hilo ni ima kupata nafasi ya masomo ikiwa bado wewe unataka kuendelea na masomo, kibarua, kazi ya kudumu na kadhalika. Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Akusaidie katika hilo.





(h) Kuhama mazingira ya madhambi. Hapo ulipo unakaribia kila siku katika kuyaendea madhambi kwa njia moja au nyingine japokuwa huzini kwa kukutana kimwili na shemeji yako. Tumetoa mfano wa vijana wa pango, na pia Nabii Yuusuf (‘Alayhis Salaam) ambao walihama katika sehemu zao au kuomba kufungwa jela ili wapate kuepukana na madhambi. Nawe huna budi kutafuta njia yoyote ile ya kuwa anapotoka kakako hutakuwa nyumbani na utarudi tu anapokuwa amerudi. Hilo linaweza kufanyika ikiwa utajiunga na masomo au utapata kazi au utakuwa unatoka asubuhi na hurudi mpaka jioni. Ikiwa hutoweza kufanya hivyo, basi unapaswa uhame hapo haraka sana, maana huruhusiwi kuwa faragha na mke wa kaka yako ambaye si maharimu wako.





Soma makala hii muhimu sana inayohusiana na masuala hayo:





Ikhtilaatw (Kuchanganyika Wanaume Na Wanawake)







Ama kuhusu kuzini na kukurubia zinaa tunaweza kuelewa hilo kutokana na Aayah ifuatayo:





“Wala msikaribie zinaa. Hakika hiyo zinaa ni uchafu mkubwa na ni njia mbaya sana” (17: 32).





Zinaa ni kitendo ambacho tupu mbili, ya mwanamme na mwanamke ambao hawajaoana kisheria zinaingiliana katika tendo la ndoa. Ama mkiwa mmevua nguo, kulala kwenye kitanda kimoja na mkawa mmejifunika shuka moja haihesabiwi kisheria kuwa ni zinaa. Kukaribia zinaa ni mambo yote yanayofanywa na vishawishi vyake ambavyo vinaweza kukupeleka katika zinaa yenyewe. Mfano wake ni kukaa faragha na mwanamke unayeweza kumuoa, kumuangalia mwanamke kwa matamanio, kutembea kwenda katika maagano na mwanamke, kumshika, kumbusu na kadhalika. Kwa ufupi ni kuwa kila kinachokupelekea katika zinaa ni kuikaribia.







Mshairi mmoja wa wakati huu amesema: “Mtizamo, kisha kutabasamu, kisha salamu, kisha mazungumzo, kisha ahadi na mwisho uharara wa kitandani (kujamiiana)”.







Ndugu zetu tutahadhari sana kwani hii dunia ina ghururi. Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) Akutoe katika janga hilo baya pia Atuepushe sisi na hayo.







Na Allaah Anajua zaidi
 
Katembea Na Mume Wa Rafiki Yake, Kaomba Msamaha
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:




Salaam aleykum, nimelala na mme wa mtu nikaona vibaya nikaomba samahani kwa mkewe akanisamehe yakaisha, baadae mme wa yule dada akanifata tena na mimi na mapenzi nae tukaendelea kufanya hivyo vitendo tena sio mara moja nimemwambia tuoane anababaisha lakini kuzini na mimi ndo kazi yake, ni aibu wala sioni sifa kwa sababu namuogopa mwenyezi mungu nasali sala tano ila hapo tu kwenye zinaa na huyo mme wa mtu ndo nashindwa ila Alhamdulillah nimeamua kuacha sema tatizo lipo hapa natamani kumuomba mkewe samahani lakini nashindwa kwa sababu mwanzo aliumia sasa wenyewe wanapatana naogopa kuwagombanisha tena sielewi tamuomba vp samahani, NIMEPATA MCHUMBA NAOGOPA ASIJE AKAONA NAMUACHISHA YY ME LABDA TAOLEWA, nifanyeje? Nijibu haraka jamani nipo kwenye wakati mgumu sitaki kuolewa bila kumuomba samahani nikisubiri je huyo atakaekua mume wangu akisikia, naombeni ushauri jamani.










JIBU:










Sifa zote njema Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema Siku ya Mwisho.




Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kutembea na mume wa mtu.

Hakika ni kuwa zinaa ni katika madhambi makubwa ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Ameliwekea adhabu kali sana kwa mwenye kuiendea. Pia inatakiwa utahadhari sana na hata ‘Ibaadah yako ya Swalah, kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anatufahamisha kinaganaga kazi ya Swalah pale Aliposema: “Soma uliyofunuliwa katika Kitabu, na usimamishe Swalah. Hakika Swalah inazuilia mambo machafu na maovu” (al-‘Ankaabuut 29: 45).

Kazi ya Swalah ni kukuzuilia wewe ‘Faahishah’ ambayo ni zinaa na maovu yote. Vipi utakuwa unaswali kisha unatembea na mume wa watu na unazini naye.




Kama Muislamu, Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anatulezea kuwa,

“Muislamu haumwi na nyoka kwenye tundu moja mara mbili”. Itakuaje wewe uwe utazini mara ya kwanza na usamehewe mbali na kuwa jambo hilo ni gumu sana kwa mume au mke pia kulikubali. Kukubali kwa mkewe ni kuonyesha kuwa anakutakia wewe kheri lakini wewe ukaenda nyuma yake ukarudia tena kosa hilo.




Tufahamu kuwa masharti ya kukubaliwa toba ni manne inapoingia haki ya mwanadamu katika suala lako hilo. Nayo ni kama yafuatayo:




1. Kujiondoa katika maasiya.

2. Kujuta kwa kufanya dhambi hilo.

3. Kuazimia kutorudia tena kosa hilo.

4. Kuomba msamaha kwa uliyemkosea.




Katika kosa hilo inaonyesha hujatekeleza sharti namba nne. Hivyo, inatakiwa wewe ufanye bidii kutekeleza hilo sharti, kwani unapokufa huenda akakudai haki siku ya Qiyaamah siku ambayo utamlipa thawabu zako na ikiwa huna basi madhambi yake utapatiwa wewe. Fanya bidii uombe msamaha kabla hujaaga dunia. Na ni ajabu ya kuwa mwanaume ambaye anadai anakupenda kisha akakataa kukuoa lakini anataka kustarehe nawe, nawe ukawa ni mwenye kukubali bila ya kusita kabisa. Je, kwa ishara hukufahamu kuwa huyo mwanaume anataka kukuchezea na kukupeleka motoni pamoja naye. Fanya bidii ukaombe msamaha kabla ya kuaga dunia na hatujui kila mmoja wetu ataondoka lini hapa duniani.




Ufahamu kuwa malipo mara nyingine ni hapahapa ulimwenguni, kama ulivyomfanyia mwenzio mke wa mtu ukalipwa kwa mumeo kufanywa anazurura na wanawake wengine usipate raha ya ndoa. Kisha jambo ambalo ni muhimu ni kuweza kutazama kama una mimba ya yule mwanamme uliyezini naye. Ikiwa utakuwa umebeba mimba itakuwa kwako haifai kuolewa mpaka uzae na uwe tayari umetubu na kuonekana mabadiliko yako ya kimaadili ndio utapata idhini kishari’ah ya kuolewa. Pia ufahamu kuwa ikiwa mume anayetaka kukuoa anataka mwanamke bikra utakuja adhirika usiku wa mwanzo kwani akiona si bikira basi kutakuwa na ugomvi na pengine kuachana. Kwa hivyo, ikiwa atauliza kama wewe ni bikira ni lazima useme ukweli kwani kusema uongo ni dhulma nyingine mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala).




Ushauri wetu nenda tena ukaombe msamaha kwa mke wa mume kama inawezekana na hakutotokea madhara yoyote yale kwa kufanya hivyo, basi ni bora kufanya. Lakini ukiwa atahofia kutokea matatizo au shari kwa kufanya hivyo, ni bora uepuke na uombe Istighfaar sana na umuombee du'aa njema huyo aliyemfanyia ubaya na kumfanyia wema ukiweza.




Na Allaah Anajua zaidi
 
Hizi ni Baadhi Ya Nyuzi Zangu Za Zamani


Tunajifunza Nini Kwenye Kisa Cha Yusufu


Hakika katika matukio ambayo tumesimuliwa katika vitabu vitakatifu yapo mambo mengi ya kujifunza. Usisahau popcorn au korosho pembeni yako huku unapata madini!

Jambo la Kwanza ni Usiri katika mambo yako binadamu sio watu hata kidogo ingawa machoni ni kama watu lkn katika nyoyo zao hakuna utu...na hasa ndugu zetu WA karibu hawa bwana ndio wabaya sana kwakuwa wanajua nyendo zetu na mipango yetu. Wanasema kikulacho kipo kinguoni kwako hakika wahenga hawakukosea kabisa...kuna watu wetu WA karibu hawapendi mafanikio yetu. Hawapendi kuona tunatoka sehemu moja na kwenda level nyingine kimaisha na furaha Yao ni kutuona daima tunataabika na kupata shida...kwahiyo sio kila Jambo la kuongea nao...mambo mengine weka Chini ya kapeti wayaone Tu yakiwa yameshakamilika.

Rejea katika kisa cha Yusuphu...alimwambia Baba yake hakika Mimi nimeona ndotoni Nyota Kumi na moja pamoja na Jua na Mwezi vikinisujudia...mara baada ya kumwambia Baba yake hiyo ndoto yake...Nabii Yakubu alimwambia mwanae...usiwasimulie hiyo ndoto yako hao ndugu zako kwani hakika shetani ni adui dhahiri Kwa binadamu....hapo tunaona kabisa kwamba Nabii Yakubu aliogopa wasije ndugu zake wakaingiwa na fitina na kumdhuru ndugu Yao....nitanukuu Aya ya Qur'an :

Suratul Yusuphu
إِذْ قَالَ يُوسُفُ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ إِنِّي رَأَيْتُ أَحَدَ عَشَرَ كَوْكَبًا وَالشَّمْسَ وَالْقَمَرَ رَأَيْتُهُمْ لِي سَاجِدِينَ

Yusuf alipo mwambia baba yake: Ewe babaangu! Hakika mimi nimeota nyota kumi na moja, na jua, na mwezi. Nimeota zikinisujudia.


قَالَ يَا بُنَيَّ لَا تَقْصُصْ رُؤْيَاكَ عَلَىٰ إِخْوَتِكَ فَيَكِيدُوا لَكَ كَيْدًا ۖ إِنَّ الشَّيْطَانَ لِلْإِنسَانِ عَدُوٌّ مُّبِينٌ

(Baba) akasema: Ewe mwanangu! Usiwasimulie nduguzo ndoto yako, wasije wakakufanyia vitimbi. Hakika Shet'ani ni adui aliye dhaahiri kwa mwanaadamu.

Jambo la pili...Tusionyeshe upendeleo katika kuwapenda watoto wetu....hakika Nabii Yakubu alionyesha mapenzi yake makubwa Kwa Yusuphu na Kaka yake mpaka ikawapelekea wale ndugu wengine kuona wivu na hivyo kutaka kumdhuru Yusuphu au kumuua ili mapenzi ya Baba Yao yawaelekee kwao.

Hata Sisi huenda tukawapenda baadhi ya watoto wetu kuliko wengine,au mtoto mmoja badala ya mwingine...hii huweza kutokea huenda kutokana na Tabia ya mtoto husika ikakupendeza na hivyo ukajikuta unampenda zaidi ya mwingine.

Lakini pamoja na yote hayo basi tujitahidi kubalance upendo ili huyo mwingine au hao wengine wasione kabisa wazi wazi kuwa tunabaguliwa....kwani hiyo Hali yaweza pelekea kuleta uhasama miongoni mwao:

Rejea tena ktk Suratul Yusuphu

إِذْ قَالُوا لَيُوسُفُ وَأَخُوهُ أَحَبُّ إِلَىٰ أَبِينَا مِنَّا وَنَحْنُ عُصْبَةٌ إِنَّ أَبَانَا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ

Pale walipo sema: Hakika Yusuf na nduguye wanapendwa zaidi na baba yetu kuliko sisi, hali sisi ni kikundi chenye nguvu. Hakika baba yetu yumo katika upotofu wa dhaahiri.

اقْتُلُوا يُوسُفَ أَوِ اطْرَحُوهُ أَرْضًا يَخْلُ لَكُمْ وَجْهُ أَبِيكُمْ وَتَكُونُوا مِن بَعْدِهِ قَوْمًا صَالِحِينَ

Muuweni Yusuf, au mtupeni nchi mbali ili uso wa baba yenu ukuelekeeni nyinyi. Na baada ya haya mtakuwa watu wema.

Jambo la tatu....Hakika Mwenyezi Mungu ndio mwenye mipango Bora kabisa.....tunaona kuwa baada ya ndugu zake Yusuphu kutaka kupanga mpango wa kumuua...lkn bahati nzuri miongoni mwao akasema msimuue Ila mtupeni katika kisima baadae watakuja wasafiri na kumchukua na kuondoka nae na kweli walimuingiza kisimani...lkn Nabii Yusuphu akapewa maono na Mwenyezi Mungu IPO siku utawasimulia hii habari nao hawatambui:

فَلَمَّا ذَهَبُوا بِهِ وَأَجْمَعُوا أَن يَجْعَلُوهُ فِي غَيَابَتِ الْجُبِّ ۚ وَأَوْحَيْن إِلَيْهِ لَتُنَبِّئَنَّهُم بِأَمْرِهِمْ هَٰذَا وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ

Basi walipo mchukua na wakakubaliana wamtumbukize ndani ya kisima, tulimfunulia Yusuf: Hapana shaka yoyote utakuja waambia kwa jambo lao hili, na wala wao hawatambui.

Na kweli walikuja watu kuchota maji kisimani wakamtoa kisimani na kwenda kuumuza huko mbele ya safari...kwahiyo huenda wewe umetumbukizwa kwenye majanga mbali mbali,huenda umedhulumiwa,unamnyanyaswa na mapitio yote magumu unayopitia lkn kumbuka Mwenyezi Mungu atakutafutia njia ya kutokea kama Yusuph alipotoka ndani ya kisima kile.

Jambo la nne...Mwenyezi Mungu pekee ndo awezaye kutuepusha na machafu na maovu..Nabii Yusuph baada ya kuuzwa huko Misri..alinunuliwa na bwana mkubwa mmoja kiongozi ktk hiyo serikali...akamwambia mkewe naona tumchukue huyu kijana huenda akatufaa huko baadae au tukamfanya kuwa mwenzetu.

Sasa Yusuph inasemekana alikuwa handsome Sana yaani hakuna binadamu wa kiume mzuri kama yeye. Kwahiyo alipofikia ukubwani mke wa Waziri alimtamani Yusuph Bila ridhaa yake. Lakini tunaambiwa Yusuph nae angelimtamani pia Lau kuwa Mwenyezi Mungu hakumuonesha ishara na Mwenyezi Mungu anasema hakika Yusuph alisafishwa nafsi yake na mambo maovu:
Rejea ktk Suratul Yusuph tena...

وَلَقَدْ هَمَّتْ بِهِ ۖ وَهَمَّ بِهَا لَوْلَا أَن رَّأَىٰ بُرْهَانَ رَبِّهِ ۚ كَذَٰلِكَ لِنَصْرِفَ عَنْهُ السُّوءَ وَالْفَحْشَاءَ ۚ إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُخْلَصِينَ

Na hakika yule mwanamke alimtamani, na Yusuf angeli mtamani lau kuwa hakuona ishara ya Mola wake Mlezi. Hayo hivyo ni kwa ajili tumuepushe na uovu na uchafu. Hakika yeye alikuwa katika waja wetu walio safishwa

Kwahiyo hapa tunaona Bila rehma ya Mwenyezi Mungu ni vigumu Sana kwetu Sisi kuepukana na maovu na machafu, kubwa turejee Kwa Mola wetu tutubu na kumuomba atuongoze katika njia iliyonyooka ili tupate radhi zake na muongozo wake.

Jambo la Tano, Mwenye kufanya dhuluma hatengenekewi.....baada ya mke wa wazir kumtaka Yusuph kinguvu. Ilibidi Yusuph akatae kwakuwa aliona amekirimiwa vizuri na mume wa Yule bwana pale na kumpa makazi mazuri iweje amdhulumu Kwa kutembea na mke wake.


وَرَاوَدَتْهُ الَّتِي هُوَ فِي بَيْتِهَا عَن نَّفْسِهِ وَغَلَّقَتِ الْأَبْوَابَ وَقَالَتْ هَيْتَ لَكَ ۚ قَالَ مَعَاذَ اللَّهِ ۖ إِنَّهُ رَبِّي أَحْسَنَ مَثْوَايَ ۖ إِنَّهُ لَا يُفْلِحُ الظَّالِمُونَ

Na yule bibi wa nyumba aliyo kuwamo Yusuf alimtamani kinyume cha nafsi yake, na akafunga milango. Akamwambia: Njoo! Yusuf akasema: Audhubillahi! Najikinga na Mwenyezi Mungu. Huyu bwana wangu kaniweka maskani nzuri, na hakika wenye kudhulumu hawatengenekewi.

Hapo tunaona kuwa hata kutembea na wake za watu ni dhuluma.....je ni wangapi wanatembea na wake za watu? Na kibaya Zaidi mpaka wengine mnazaa nao kabisa...je hamuoni kuwa mnawadhulumu hao waume zao? Hakika anayedhulumu hafanikiwi...huenda sio kimaisha lkn Mola wako anajua zaidi.

La Tano ni....Umuhimu WA kuwa na Subira....hakika ktk habar ya Yusuph kuna mambo mengi Sana ya kujifunza...Mimi Kwa muktadha wa Uzi huu nimechambua machache....baadae Yusuph alipelekwa gerezani na kukaa Miaka kadhaa..baadae alitoka baada ya mfalme kumuhitaji kutafsiri Ile ndoto aliyoota mfalme...ambapo mfalme aliota kuwa...ng'ombe Saba wanene wanaliwa na ng'ombe Saba waliokonda na mashuke Saba mabichi na mengine makavu....sio lengo langu kuelezea hii ndoto.

Lakini kwakuwa Yusuph alifundishwa na Mola wake kutafsir mambo basi aliitwa na kuitafsir Ile ndoto...na baadae likasafishwa Jina lake kutokana na Ile kashfa ya kusingiziwa kumtaka mke wa wazir kinguvu,kumbuka baada ya mke wa waziri kumkimbiza Yusuph wote walikimbilia mlangoni na kukutwa pale mlangoni na Waziri, ndo mkewe akamsingizia Yusuph kuwa alitaka kumfanyia maovu.

Kwahiyo akaonekana hakuwa na hatia na baadae akaja kuwa mmiliki wa hazina zote pale Misri...hapa tunajifunza hakika Maisha Yana mapito mengi...kuna milima na mabonde lkn mwisho mwema huwa Kwa wenye Subira..
 
Hizi ni Baadhi Ya Nyuzi Zangu Za Zamani....

Ningependa Leo nizungumzie maswala ya kiroho na walengwa ambao Nataka niwakumbushe neno la Mungu ni Wale wanao mwamini Mwenyezi Mungu. Kama wewe humwamini Mwenyezi Mungu au unaamini Mungu hayupo basi huu Uzi haukufai.

Mwenyezi Mungu anasema katika Kitabu chake katika Suratul Ibrahim Aya ya 31:
''Waambie waja wangu walio amini, washike Sala, na watoe katika tulivyo waruzuku, kwa siri na dhaahiri, kabla haijafika Siku isiyo kuwa na biashara wala urafiki.''

Mwenyezi Mungu katika Kitabu chake amekuwa na kawaida ya kuongea na watu Kwa daraja zao, ndio maana kuna Aya anazungumza Kwa kusema Enyi watu na Aya nyingine anasema Enyi mlioamini. Anapozungumzia Enyi watu mara nyingi huzungumza na viumbe wake wote wanao mwamini yeye na wasio mwamini yeye na wanaomini Mungu zaidi ya mmoja. Na mara nyingi huwapa hoja mbali mbali za kufikirisha akili zao na bongo zao juu ya kuumbwa Kwa ulimwengu na viumbe wake pamoja na yaliyomo ndani yake, je hayo wanayo yaona hayatoshi kuwafanya wao kutafakari na kuona kuwa hayo hayakutokea bure Tu Ila kuna Mwenyezi Mungu aliyeumba mambo yote hayo? Huo ni mfano mmoja Tu nilio ugusa hapo.

Na anapo ongea na walioamini, anaongea na watu ambao tayar wamemwamini Mungu Mmoja na hawa ndio wamesalimika,kwasababu Mwenyezi Mungu hana ushirika wala usaidizi toka Kwa kiumbe kingine chochote kile, yeye ndio mkuu na ndiye aliye juu, sifa zake amezieleza vizuri katika Suratul Bakara Aya ya 255:

''Mwenyezi Mungu - hapana mungu ila Yeye Aliye hai, Msimamia mambo yote milele. Hashikwi na usingizi wala kulala. Ni vyake pekee vyote viliomo mbinguni na duniani. Ni nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao; wala wao hawajui chochote katika vilio katika ujuzi wake, ila kwa atakalo mwenyewe. Enzi yake imetanda mbinguni na duniani; na wala haemewi na kuvilinda hivyo. Na Yeye ndiye aliye juu, na ndiye Mkuu.''

Baada ya kuona sifa zake..turudi kwenye lengo kuu la Aya ambayo nimeshaitaja awali. Kwanza Mwenyezi Mungu anasema Waambie waja wangu walioamini wasimamishe Sala, ndugu zangu katika Imani, Sala au Swala ndio amali au kitendo cha Kwanza kuhesabiwa siku ya hukumu,hapo unaona ni jinsi gani Swala ilivyo na umuhimu mkubwa mbele ya Allah, na katika nguzo tano ambazo Uislamu umejengwa juu yake basi Swala ndio Nguzo ya pili kusimikwa mara baada Tu ya kukiri kuwa Hapana Mola apasae KUABUDIWA Kwa haki isipokuwa Allah/Mwenyezi Mungu. Na anayesimamisha au anayedumu na ibada hii basi hakika amesimamisha Dini,na ikasemwa pia tofauti ya walioamini na waliokufuru ni Swala.

Na Mtume (rehma na Amani iwe juu yake) akasema '' mfano wa swala tano ni kama mtu ambaye nyumba yake ipo karibu na mto, na anaoga mara tano Kwa siku. Je, mtu kama huyo atakuwa na uchafu mwilini mwake?'' Hapo inaonyesha hakika kila kipindi kimoja cha swala kinafuta madhambi ya mja wa Allah,hakika amali hii ni muhimu hivyo hatuna budi kujitahidi kuifanya kwa uwezo wetu wote Mjumbe wa Allah alisema ukimuona mtu anapenda kwenda msikitini basi yatosha kusema huyu mtu ana Imani.

Pili Mwenyezi Mungu anasema tutoe katika vile alivyoturuzuku Kwa Siri na dhahiri...ni mtu asiye mwamini Mwenyezi Mungu Tu ndio anaamini kuwa mafanikio aliyonayo kayapata Kwa ujanja wake au Kwa maarifa yake,lakini mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu hakika anajua vyote alivyonavyo amepewa na Mola wake mlezi,na hivyo Hana budi kutoa sadaka,zaka na kuwasaidia wenye uhitaji kwakuwa anajua ndani ya nafsi yake kuwa IPO siku ataulizwa juu ya neema aliyopewa.

Na sadaka waeza Toa Kwa Siri au Kwa dhahiri lakini kitu kibaya ni kutoa Kwa kutaka Sifa mbele za watu uonekane kuwa wewe ni mtoaji mzuri,hapo hautapata malipo toka Kwa Mwenyezi Mungu kwakuwa ulikusudia ktk moyo wako usifiwe na watu,lkn kama ulitoa mbele za watu Kwa Nia ya kutaka radhi za Mwenyezi Mungu basi hakika utapata malipo toka Kwa Mola wako.

Lakini tunaambiwa kutoa sadaka Kwa Siri ndio Bora zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu,na hapo unakuja ule msemo kuwa ukitoa sadaka Kwa mkono wa Kulia basi mkono WA kushoto usijue,maana halisi ndiyo utoe Kwa Siri sadaka yako...ingawa baadhi ya watu unakuta wakitoa hela zao msikitini basi daah wanazikunja hizo hela mpaka zinakosa hewa! Yaani kama zingekuwa zinapumua basi zingekosa pumzi na kufa hahah! Kutokutoa Kwa Siri ni kama vile unatoa huku unatangaza Kwa watu,Mimi bwana nimetoa shilingi kadhaa au unamuona Fulani alikuwa hana hela ya kula ujue Mimi ndio nimemsaidia,hakika sadaka za namna hiyo hazina malipo mbele ya Mwenyezi Mungu hata kidogo.

Mwisho Mwenyezi Mungu anawaonya waumini kuwa washike sala na kutoa katika vile walivyoruzukiwa kabla haijaja siku isiyo na biashara wala Urafiki, tunajua hapa duniani huwa tunanufaishana na kusaidiana Kwa kuwa ni marafiki,kuna watu hawafungwi jela kwasababu ya Urafiki,hawalipi Kodi stahiki kwasababu ya Urafiki, wanafanya dhuluma mbali mbali kisa Tu Wana Urafiki na polisi hivyo huwezi kuwagusa,yote hayo siku ya hukumu hakuna habari hizo....

Ukija upande WA biashara nako hivyo hivyo,hapa duniani ndio sehemu nzur ya kufanya biashara na Mwenyezi Mungu,ukitenda mema utalipwa mema zaidi ya hayo uliyotenda,ni sehemu ya kuchuma thawabu zitakazo kufaa huko mbele ya safari,lakini kama hakufanya biashara hiyo wakati huko hai basi siku hiyo ya hukumu hakutakuwa na nafasi nyingine ya kuchuma mema.

Namalizia na dua ya Nabii Ibrahim pale alipo muomba Mola wake Mlezi amsaidie kusimamisha Sala pamoja na familia yake:

"Mola wangu Mlezi! Nijaalie niwe mwenye kushika Sala, na katika dhuriya zangu pia. Ewe Mola wetu Mlezi, na ipokee dua yangu."
Surah Ibrahim :40
 
Back
Top Bottom