Ramadhan Special Thread
Tupo mlango wa kuamini yasiyoonekana kuhusiana na hadith


Screenshot_20250429_193201_CamScanner.jpg
 
Screenshot_20250429_193507_CamScanner.jpg


Hapo kuhusu kiumbe kuandikwa muovu au mwema,ni kwakuwa Allah anajua yaliyo mbele yetu,anajua jinsi tutakavyo ishi kama tutakuwa wema au waovu,kwahiyo anajua mwisho wetu
 
08-Nini maana ya Tawhiyd katika Sifa za Allaah?



Tawhiyd katika Sifa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kuthibitisha vile vile Alivyojiwekea Sifa Mwenyewe Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) au Rasuli Wake.

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ﴿١١﴾

Hakuna chochote kinachofanana Naye, Naye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote. [Ash-Shuwraa: 11]



((ينزِلُ ربُّنا تبارك وتعالى فِي كلّ ليلةٍ إِلَى السّمَاء الدُّنْيَا)) متّفق عليه

نزولاً يليق بجلاله

((Rabb wetu Huteremka kila usiku katika mbingu ya dunia)) [Al-Bukhaariy, Muslim]



Kuteremka kunakolaikiana na Ujalali Wake.
 
09-Nini faida ya Tawhiyd kwa Muislamu?



Faida ya Tawhiyd kwa Muislamu ni kupata Hidaaya duniani na kuwa katika amani Aakhirah.

الَّذِينَ آمَنُوا وَلَمْ يَلْبِسُوا إِيمَانَهُم بِظُلْمٍ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ الْأَمْنُ وَهُم مُّهْتَدُونَ ﴿٨٢﴾

Wale walioamini na hawakuchanganya iymaan zao na dhulma; hao ndio watakaopata amani nao ndio walioongoka. [Al-An’aam: 82]



((وَحَقُّ الْعِبَادِ عَلى اللهِ أَنْ لاَ يُعَذِّبَ مَنْ لاَ يُشْرِكُ بِهِ شَيْئًا)) متّفق عَلَيهِ

((Haki ya waja kwa Allaah ni kwamba Hatomwadhibu yeyote ambaye hamshirikishi na chochote kile)) [Al-Bukhaariy, Muslim]
 
10-Je, Allaah Yuko wapi?



Allaah Yuko mbinguni juu ya ‘Arsh.

الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ ﴿٥﴾

Ar-Rahmaan juu ya ‘Arshi Istawaa [Twaahaa: 5]



Maana ya Istawaa: Yuko juu kwa namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah.



((إِنَّ اللَّهَ كَتَبَ كِتَابًا : إِنَّ رَحْمَتِي سَبَقَتْ غَضَبِي، فَهُوَمكتوبٌ عِنْدَهُ فَوْقَ الْعَرْشِ)) البخاري

((Hakika Allaah Ameandika maandishi kwamba: “Rahmah yangu imeshinda ghadhabu yangu, nayo yameandikwa kumhusu Yeye juu ya 'Arsh)) [Al-Bukhaariy]
 
Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com









11-Je, Allaah Yuko na sisi kwa dhati Yake au kwa ujuzi Wake?



Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Yuko na sisi kwa ujuzi Wake Anatuona na Anatusikia. Hayuko na sisi kwa dhati Yake.



قَالَ لَا تَخَافَا ۖ إِنَّنِي مَعَكُمَا أَسْمَعُ وَأَرَىٰ ﴿٤٦﴾

(Allaah) Akasema: “Msikhofu; hakika Mimi Niko pamoja nanyi, Nasikia na Naona. [Twaahaa: 46]



((إنَّكُمْ تَدْعونَ سَميعاً قَريباً وَهُوَ مَعَكُم)) رواه مسلم.

((Hakika nyinyi mnamuomba Mwenye kusikia, Aliye karibu, na Yeye Yuko pamoja nanyi)) [Muslim]
 
13-Shirki gani iliyokuwa kubwa?



Shirkii kubwa ni kufanya ‘ibaadah kwa kumuelekea asiye Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kama du'aa.



قُلْ إِنَّمَا أَدْعُو رَبِّي وَلَا أُشْرِكُ بِهِ أَحَدًا﴿٢٠﴾

Sema: (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم): “Hakika mimi namuomba Rabb wangu na wala simshirikishi na yeyote.” [Al-Jinn: 20]



((أَكْبرَرُ الْكَبآئِر الإشراكُ باللهِ)) رواه البخاري

((Dhambi kubwa ni kumshirikisha Allaah)) [Al-Bukhaariy]
 
14-Ni yapi madhara ya kumshirikisha Allaah?



Madhara ya kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) husababisha kudumu milele motoni.



إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللَّـهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ ۖ

Hakika mwenye kumshirikisha Allaah bila shaka Allaah Atamharamishia Jannah, na makazi yake yatakuwa ni motoni. [Al-Maaidah: 72]



((من ماتَ يُشرِك باللهِ شيئاً دخل النّار)) رواه مسلم

((Atakayekufa na huku amemshirikisha Allaah kwa chochote, ataingia motoni)) [Muslim]
 
Inshaallah tutaendelea na darsa ya aqydah kesho.... na darsa ya Swalaa ya Nabii

Endelea kuwa nami kheri kubwa itapatikana

................................................................................................
 
Assalaam alaikum ndugu zangu katika imani

Napenda kuweka jambo moja sawa,hakika Allah husamehe dhambi zote ikiwemo shirki lakini sharti uwe umetubu kabla hujafa

Yani kama umekufa na hujatubu basi wewe huta pata msamaha,tofauti na madhambi.mengine Allah anaweza kukusamehe kwa rehma zake au akakuadhibu na kisha akakusamehe

Lakini

Endapo umeaga dunia bila kutubu hiyo hain msamaha abadani
 
Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com







15-Je, Kitendo chema kinafaa kikiwa kimemshirikisha Allaah?



Hapana! Kitendo chema ambacho kina kumshirikisha Allaah hakifai kitu mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).

وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٨٨﴾

Na kama wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda. [Al-An’aam: 88]



((من عمِلَ عملاً أشرك معيَ فِيهِ غيري تركتُه وشِرْكَه)) حديث قدسي رواه مسلم.

((Atakayefanya kitendo na huku kanishirikisha Mimi na mwengine, namwacha yeye na mshirika wake)) [Hadiyth Qudsiy ameipokea Muslim]
 
16-Je, Shirki ipo kwa Waislamu?



Naam! Shirki ipo kwa Waislamuna masikitiko kuwa ipo tena wanamshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa wingi!



وَمَا يُؤْمِنُ أَكْثَرُهُم بِاللَّـهِ إِلَّا وَهُم مُّشْرِكُونَ ﴿١٠٦﴾

106. Na wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa wao ni wenye kufanya shirki. [Yuwsuf: 106]



((لاَ تقوم السّاعة حتّى تلحق قبائل مِن أُمّتي بالمشركين وحتى تُعبَد الأوثان)) صحيح رواه الترمذي.

((Qiyaamah hakitosimama mpaka kutafika wakati watu wa baadhi ya makabila katika ummah wangu wataungana na washirikina na hadi watakapoabudu asiye Allaah! [Swahiyh ameipokea At-Tirmidhiy]
 
16-Je, Shirki ipo kwa Waislamu?



Naam! Shirki ipo kwa Waislamuna masikitiko kuwa ipo tena wanamshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa wingi!



وَمَا يُؤْمِنُ أَكْثَرُهُم بِاللَّـهِ إِلَّا وَهُم مُّشْرِكُونَ ﴿١٠٦﴾

106. Na wengi kati yao hawamwamini Allaah isipokuwa wao ni wenye kufanya shirki. [Yuwsuf: 106]



((لاَ تقوم السّاعة حتّى تلحق قبائل مِن أُمّتي بالمشركين وحتى تُعبَد الأوثان)) صحيح رواه الترمذي.

((Qiyaamah hakitosimama mpaka kutafika wakati watu wa baadhi ya makabila katika ummah wangu wataungana na washirikina na hadi watakapoabudu asiye Allaah! [Swahiyh ameipokea At-Tirmidhiy]
Je hawa leo hawapo?

Je hatuoni waislamu wakienda kuombewa na mitume na manabii wa zama hizi kwa jina la Issa bin Mariam
 
17-Nini hukumu ya kumuomba asiye Allaah kama Mawalii?





Hukmu ya kuwaomba ‘Mawalii’ ni shirki yenye kumpeleka mtu motoni.



فَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَكُونَ مِنَ الْمُعَذَّبِينَ ﴿٢١٣﴾

Basi usiombe pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine ukaja kuwa miongoni mwa watakaoadhibiwa. [Ash-Shu’araa: 213]



((من ماتَ وَهُوَ يدعو مِن دون الله نِدّاً دخل النّار)) رواه البخاري

((Atakayefariki katika hali ya kumuomba asiye Allaah ataingia motoni)) [Al-Bukhaariy]





Mawalii: Waliokusudiwa hapa ni watu wema waliofariki wakaombwa wao makubirini badala ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) au wakatumiliwa kama ni tawassul ya kujikurubisha kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).
 
18-Je, Kuomba du'aa ni ‘ibaadah ya Allaah?





Naam! Kuomba du'aa ni ‘ibaadah ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).



وَقَالَ رَبُّكُمُ ادْعُونِي أَسْتَجِبْ لَكُمْ ۚ

Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni. [Ghaafir: 60]



((الدّعاء هُوَ العبادة)) رواه الترمذي وقال حديث صحيح

((Du’aa ndio ‘ibaadah)) [At-Tirmidhiy na amesema: Hadiyth Swahiyh]
 
19- Je, waliokufa wanasikia wito?



Hapana! Waliokufa hawasikii wito.



إِنَّكَ لَا تُسْمِعُ الْمَوْتَىٰ

Hakika wewe huwezi kusikilizisha wafu [An-Naml: 80].



وَمَا أَنتَ بِمُسْمِعٍ مَّن فِي الْقُبُورِ ﴿٢٢﴾

Nawe huwezi kuwasikilizisha walioko kaburini. [Faatwir: 22]



((إنَّ لِلَّهِ ملائكةً سَيّاحِين فِي الأرْضِ يُبَلّغوني عَنْ أُمّتي السَّلام)) رواه أحمد

((Hakika Allaah Anao Malaika wanaozunguka katika ardhi wakinifikishia salaam kutoka kwa ummah wangu)) [Ahmad]
 
Back
Top Bottom