Naam kwa siku ya leo tumalizie kipengele kingine cha imani nacho ni kuamini MITUME ya Allah
Ndugu zangu katika imani tunapaswa kuamini mitume yote ya Allah,na inasemwa kulikuwa kuna takribani Mitume laki moja na elfu ishirini na nne (124,000) kama nimekosea naomba nisahihishwe
Lakini Mitume wakubwa kabisa wapo kama watano au wanne,Mussa, Issa bin Mariam,Muhammad .........
Na ndani ya qur'an imetajwa kama Mitume 25 kama sikosei
Hawa wote ni Mitume ya Allah hatutakiwi kuwabagua hata mmoja na tunatakiwa wote tuwaamini kwamba wameletwa na Allah kufikisha ujumbe kwa watu wake
Huyu mmoja kwa bahati mbaya sana amepewa sifa ya kuwa Mungu na binadamu,na hivyo anaabudiwa na kukusudiwa na hao wanadamu angali wote ni viumbe wa Allah
Yeye mwenyewe anasema hivi;
Yohana 17:3-4
[3]Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
And this is life eternal, that they might know thee the only true God, and Jesus Christ, whom thou hast sent.
[4]Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
I have glorified thee on the earth: I have finished the work which thou gavest me to do.
Naam hapo tumemuona mhusika mwenyewe akijipambanua kuwa yeye ni nani?
Allah awaongoze kwakweli waione nuru ya kweli,na siku ya kiama Allah atamuuliza huyu Mtume je,uliwaambia watu wakuubudu wewe na mama yako?
Atajibu "hakika haipaswi kwa mimi kusema maneno hayo,kwani ulikuwa nami nilipo kuwa nao,hao ni waja wako ukitaka utawaadhibu au ukitaka utawasamehe"
Kila mtume alikuja kwa zama za watu wake,kwa maana baada ya daud na kuja Mussa,basi hakupaswa kufuatwa daud tena ila alipaswa kufuatwa Mussa,baada ya Mussa alipaswa kufuatwa Issa bin mariam ingawa pamoja na kuja na injili alisema yeye hakuja kutengua hata nukta moja ya taurati ila amekuja kuikamilisha
Na baada ya Issa akaja Muhammad swallallahu alaih wassallam, ambaye anapaswa kufuatwa yeye sasa katika zama zake na ishara zake
Ndio Mtume akasema lau nabii Mussa angekuwa hai hadi leo basi nabii Mussa angepaswa kumfuata Muhammad swallallahu alaih wassallamu
Hii ni shaka ambayo watu wanaweka juu ya Mtume Muhammad ambaye ndie mtume wa mwisho na hatotokea tena Mtume yeyote mpaka pale kitakapo tokea kiama
Inshallah hayo ni kwa uchache,panapo majaliwa kesho tutakuja kuangalia vipengele vingine
Subhanaka allahuma wabihamdik ashahadu anlaa ilaha ila anta astaghfiruka waatubu ilayk
Tumche Allah ukweli wa kumcha