Ramadhan Special Thread
Na malaika hao waandishi huwa wanapeana shifti au kubadilishana zamu ,na mda wao ni baada ya swala ya al asir na ndio maana tunaambiwa sana tusiache kuitikia adhana ya swalla ya al asir ile mida ya saa kumi,na ndio maana Allah amesema na swala zote mziswali na hasa ile swala ya kati na kati,ipo kati kwa kati kwasababu kuna asubuhi alfajir na adhuhur mbili hizo halafu jioni magharibi na isha mbili hizo,kwahiyo ya kati ni al asiri

Kwahiyo na mda huo wa al asir matendo yetu yanapandishwa mbinguni kwa Allah,yaani wanao zamu al asir ya leo wanapanda na matendo yetu ala asir ya kesho,na inasemwa wakati huo wa kubadilisha shift mbingu huwa wazi

Na Allah ingawa anajua kila kitu kinachoendelea,lkn huwa uliza hao Malaika je mmewaachaje waja wangu,malaika wanajibu tulipoingia tuliwakuta wanaswali na tumewaacha wanaswali pia
 
Kuna malaika wengj sana kazi zao,kuna huyo wa kifo malakuli mauti naye anawasaidizi wake wanaofanya kazi ya kutoa roho za waja,inasema huyo mkuu mwenyewe huiona dunia kama vile mtu anavyoliangalia draft,najua wengi tunalijua draft au bao,kwahiyo anaangalia kete ipi inatakiwa kuondoka leo anaiondoa kupitia wasaidizi wake

Kuna hao ambao munkar na nakir kama sijakosea mara tu baada ya kuzikwa huja kutuhoji pale makaburini

Kwa kifupi kuna mengi sana ya kuyaeleza kuhusu hawa viumbe wa Allah

Lakini la mwisho si kwa umuhimu tunaambiwa mwanadamu huwa na fukra mbili moyoni mwake,fikra moja ni kutoka kwa shetani na nyengine kutoka kwa malaika,ukiona moyo wako unakupa fikra za kufanya maovu basi jua unachochewa na shetani na ukiona unapata fikra za kufanya mambo mema basi jua fikra hizo zinatoka kwa malaika,na ndio zinatoka kwa Allah,basi msifu na mtukuze Allah kwa kukuongoza

Ngoja tuishie hapa kuhusiana na Malaika kwani tutakesha hapa,nitakuja na kipengele kingine inshallah

Tumche Allah ukweli wa kumcha
 
Na malaika hao waandishi huwa wanapeana shifti au kubadilishana zamu ,na mda wao ni baada ya swala ya al asir na ndio maana tunaambiwa sana tusiache kuitikia adhana ya swalla ya al asir ile mida ya saa kumi,na ndio maana Allah amesema na swala zote mziswali na hasa ile swala ya kati na kati,ipo kati kwa kati kwasababu kuna asubuhi alfajir na adhuhur mbili hizo halafu jioni magharibi na isha mbili hizo,kwahiyo ya kati ni al asiri

Kwahiyo na mda huo wa al asir matendo yetu yanapandishwa mbinguni kwa Allah,yaani wanao zamu al asir ya leo wanapanda na matendo yetu ala asir ya kesho,na inasemwa wakati huo wa kubadilisha shift mbingu huwa wazi

Na Allah ingawa anajua kila kitu kinachoendelea,lkn huwa uliza hao Malaika je mmewaachaje waja wangu,malaika wanajibu tulipoingia tuliwakuta wanaswali na tumewaacha wanaswali pia
Kumbusha kwani hakika ukumbusho huwafaa waumini ambao wamejitakasa basi hao ndio watakao faulu
Allah atufanyie wepesi Insha'Allah

جزاك الله خير
 
Tunakumbushana waislamu,ili funga zetu ziwe salama basi tunatakiwa kujiepusha na mambo yote ya kipuuzi,chunga sana thread unazosoma kipindi hiki cha ramadhani

Binafsi huwa nasoma nyuzi chache sana ambazo hazina viashiara vya maudhui ya hovyo,najua kabisa sitasoma komenti za matusi na kipuuzi

Tumche Allah
 
Naam baada ya kuangalia baadhi ya sifa za muumini kuwa na imani ikiwemo kumwamini Allah,Siku ya Mwisho na kuwaamini Malaika

Sasa tuangalia sifa nyingine ya IMANI ni kuamini VITABU vya Allah

Hakika Allah ameshusha vitabu vinne hapa duniani kwa mujibu wa qur'an,navyo ni Zaburi chini ya Daud,Taurati chini ya Mussa,injili chini Issa bin Mariam na qur'an chini ya Muhammad swallallahu alaih wassallam

Basi hatuna budi kuamini vitabu vyote vya Allah,kwamba yeye ndio aliyeleta vitabu hivyo kwa waja wake kupitia Mitume wake

Na hakika ujumbe wa Allah ndani ya vitabu hivyo ni kwanza kumuabudu Mungu mmoja tu na kisha kufuata sheria zake, na sheria zake zilikuwa makhususi kutokana na zama na zama,kwa maana kila umma ulipewa sheria zake kutokana na wakati husika

Na katika vitabu hivyo kulitabiriwa kwa kuja mitume inayofuata mbeye yake,huyu Mtume Muhammad swallallahu alaih wassallamu alitabiriwa pia katika taurati na injili kama haya hii inavyosema na nyenginezo

7:157 - Ambao kwamba wanamfuata huyo Mtume, Nabii, asiye soma wala kuandika, wanaye mkuta kaandikwa kwao katika Taurati na Injili, anaye waamrisha mema na anawakanya maovu, na anawahalalishia vizuri, na ana waharimishia viovu, na anawaondolea mizigo yao na minyororo iliyo kuwa juu yao. Basi wale walio muamini yeye, na wakamhishimu, na wakamsaidia, na wakaifuata nuru iliyo teremshwa pamoja naye - hao ndio wenye kufanikiwa.

Kwahiyo Muislamu pamoja na kwamba hivyo vitabu vilitiwa mikono na wanadamu na kuondoa hili na kuweka lile,sisi kama waislamu hatuna budi kuamini kuwa hivyo viliteremshwa na Allah,sasa kuchafuliwa kwa vitabu hivyo ni jukumu lake Allah mwenyewe
 
Naam kwa siku ya leo tumalizie kipengele kingine cha imani nacho ni kuamini MITUME ya Allah

Ndugu zangu katika imani tunapaswa kuamini mitume yote ya Allah,na inasemwa kulikuwa kuna takribani Mitume laki moja na elfu ishirini na nne (124,000) kama nimekosea naomba nisahihishwe

Lakini Mitume wakubwa kabisa wapo kama watano au wanne,Mussa, Issa bin Mariam,Muhammad .........

Na ndani ya qur'an imetajwa kama Mitume 25 kama sikosei

Hawa wote ni Mitume ya Allah hatutakiwi kuwabagua hata mmoja na tunatakiwa wote tuwaamini kwamba wameletwa na Allah kufikisha ujumbe kwa watu wake

Huyu mmoja kwa bahati mbaya sana amepewa sifa ya kuwa Mungu na binadamu,na hivyo anaabudiwa na kukusudiwa na hao wanadamu angali wote ni viumbe wa Allah

Yeye mwenyewe anasema hivi;

Yohana 17:3-4
[3]Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.
And this is life eternal, that they might know thee the only true God, and Jesus Christ, whom thou hast sent.
[4]Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.
I have glorified thee on the earth: I have finished the work which thou gavest me to do.

Naam hapo tumemuona mhusika mwenyewe akijipambanua kuwa yeye ni nani?

Allah awaongoze kwakweli waione nuru ya kweli,na siku ya kiama Allah atamuuliza huyu Mtume je,uliwaambia watu wakuubudu wewe na mama yako?
Atajibu "hakika haipaswi kwa mimi kusema maneno hayo,kwani ulikuwa nami nilipo kuwa nao,hao ni waja wako ukitaka utawaadhibu au ukitaka utawasamehe"

Kila mtume alikuja kwa zama za watu wake,kwa maana baada ya daud na kuja Mussa,basi hakupaswa kufuatwa daud tena ila alipaswa kufuatwa Mussa,baada ya Mussa alipaswa kufuatwa Issa bin mariam ingawa pamoja na kuja na injili alisema yeye hakuja kutengua hata nukta moja ya taurati ila amekuja kuikamilisha

Na baada ya Issa akaja Muhammad swallallahu alaih wassallam, ambaye anapaswa kufuatwa yeye sasa katika zama zake na ishara zake

Ndio Mtume akasema lau nabii Mussa angekuwa hai hadi leo basi nabii Mussa angepaswa kumfuata Muhammad swallallahu alaih wassallamu

Hii ni shaka ambayo watu wanaweka juu ya Mtume Muhammad ambaye ndie mtume wa mwisho na hatotokea tena Mtume yeyote mpaka pale kitakapo tokea kiama

Inshallah hayo ni kwa uchache,panapo majaliwa kesho tutakuja kuangalia vipengele vingine

Subhanaka allahuma wabihamdik ashahadu anlaa ilaha ila anta astaghfiruka waatubu ilayk

Tumche Allah ukweli wa kumcha
 
Screenshot_2025_0318_211403.jpg
 
Naam leo tunaendelea na darsa yetu, tutaangalia kipengele cha kuamini kwamba Kadari ya Kher na Shari zote zinatoka kwa Allah

Kipengele hiki hakika wengi wetu huwa kinayumbisha sana imani zetu,yan hapa mtihani ni mkubwa sana

Kwahiyo itanibidi nikiongelee kwa mapana sana huenda kwa baraka za mwezi huu mtukufu baadhi yetu tukapata mwanga na kuamini juu ya kadari ya kheri na shari

Wengi wetu tukipata mitihani kidogo tu basi hao kwa waganga na kwenda kuombewa kwa asiyekuwa Allah,kwa kutaraji kwamba hao ndio watatupa ufumbuzi wa shida na changamoto zetu

Allah anasema hivi,yeye akikugusisha dhara basi hakuna wa kuiondoa isipokuwa yeye mwenyewe,na si vinginevyo,kwahiyo ukipata mtihani wowote mkusudie Allah peke yake

Kwanza tutambue kitu kimoja Allah wakati mwingine hutupa mitihani ili kutujaribu au ili turejee kwake

Pili tutambue kwamba hakuna jambo lolote ambalo linaweza kukupata au kukusibu pasina idhini ya Allah,yaani mpaka apitishe yeye ndio wewe udhurike

Hata mchawi hatokudhuru wewe isipokuwa atake Allah,kwahiyo ukijua nadharia hii itakusaidia sana kujua kwamba wa kukusudiwa pekee ni Allah

Na tujue kwamba Allah hufanya mambo yake pasina kujali matokeo yake,yani Allah hufanya alitakalo

Ebu chukulia wana israel walipokuwa wanateswa kule misri na firauni,kwa kuuliwa watoto wao wa kiume na kuachwa wa kike,Allah anasema hakika ule ulikuwa ni mtihani mkubwa sana kwa jamii ile,kwahiyo ni Allah ambaye amewapa mtihani ule,na aliwapa mtihani bila kujali matokeo yake

Nabii Ayubu huyu mja wa Allah alipewa mtihani wa maradhi kwa takribani miaka 18 mpaka mwili wake kuisha kabisa lkn aliomba abakie na ulimi ili amtaje Allah kwa wingi
 
Na mitihani ya Allah hupewa Mitume,Manabii na watu wa kawaida,lkn jinsi imani yako inavyokuwa kubwa ndivyo mitihani yako inakuwa mikubwa,na ndio maana Mitume walipewa Mitihani mikubwa sana kuliko watu wengine

Mtume swallallahu alaih wassallam anasema kutokubaliana na kadari ya Allah ni kufungua milango ya shetani,naam umefiwa na ndugu yako katika mazingira ya kutatanisha basi huyo kwa mganga kujua imekuwaje,umepata ajali huyo kwa mganga kujua je hii ajali ya kawaida au laa,hayo ni makosa makubwa sana

Hakika kheri na shari zote zinatoka kwa Allah,Allah hakushindwa kumzuia Mtume asipigwe kule Taifu na kuloa damu mwili mzima,lkn ulikuwa ni mtihani kwa waja wake

Allah hakushindwa kumzuia nabii Ibrahim asitupwe katika moto na washirikina lkn aliruhusu lifanyike hilo ili atimize lengo lake,lkn kwa kwa hekima yake baada ya nabii Ibrahim kutupwa katika moto,Allah akauambia ewe Moto kuwa baridi kwa Ibrahim,na matokeo yake Ibrahim alitoka salama kabisa
 
Issa bin mariam,alipotakiwa kuuwawa au kusurubiwa,Allah alimbadilisha mtu mwingine kwa kupewa sura yake na hivyo akaepuka kusurubiwa,matokeo yake akasurubiwa mtu mwingine,na hata ushahidi unaonyesha pale msalabani kuwa huyo mtu alikuwa analia kwa kusema "bwana wangu mbona umeniacha?"

Angekuwa ni Issa bin mariam asingelia kwakuwa alijua kabisa alikuja ili asulubiwe ili kuokoa wanadamu dhidi ya dhambi,je angeanzaje kulia wakati anajua kusudio lake?
 
Allah anasema katika suratil fajir "mwanadamu akineemeshwa kwa kuongezewa kipato hufurahia lakini akipunguziwa hulalamika na kuona anaonewa"

Allah anasema hiyo ni mitihani kutoka kwa Allah ili kupima imani za waja wake,huenda umepata ajali au maradhi basi wewe subir na kumtegemea Allah,kwa maana jitibie lkn huku unafanya subira na kumuomba Allah akufanyie wepesi kama alivyofanya nabii Ayubu

Nabii Yusufu alipewa mituhani ya kutupwa kisimani,kuuzwa kama mtumwa na mwishoe akafungwa gerezani,lkn yote hiyo ni mitihani ya Allah,katika kufikia makusudio fulani,kwahiyo hauko peke yako na wala hukuanza wewe,hiyo ni kadari ya Allah kikubwa subiri,na Allah anasema yupo pamoja na wanaosubiri
 
Ndio maana waislamu tumefundishwa kukubalina na hali zote zenye kuhuzunisha na kuumiza kama misiba kwakusema INNA LILAH WAINA ILAIH RAJIUU kwa maana SOTE NI WA ALLAH NA KWAKE TUTAREJEA mja huyu akisema hivi na kuwa na subira basi hulipwa ujira mkubwa sana kwasababu amekubaliana na kadari ya Allah

Kwahiyo siku zote tambua mwenye sifa ya kunufaisha na kudhuru ni Allah peke yake na si mwingine,maadamu upo hapa duniani basi kubali kadari ya Allah

Na kheri nayo inatoka kwa Allah,wala si ujanja wa mwanadamu kujiona yeye ana akili sana kwa kupata kwake,na tambua alichokupa Allah hakuna awezaye kukichukua labda atake mwenyewe

Anasema Allah mtukufu kwamba, "hata watu wote dunia nzima wakusanyike wa mwanzo na wa mwisho watake kukudhuru wewe basi hawataweza na hata wakusanyike wanadamu wote wa mwanzo na wa mwisho watake kukunufaisha wewe hawataweza labda atake yeye"

Kwahiyo mwenye uwezo ama wa kukupa kheri au shari ni Allah pekee na si mwingine
 
Kuna ufahamu mbaya wa kadari kwa baadhi yetu,utakuta mtu anasema kila kitu Allah ametupangia,kwahiyo uzinifu wangu nimeshaandikiwa au kupangiwa na Allah, au ulevi wangu ni kadari ya Allah

Hakika Allah anasema yeye haamrishi mambo machafu kwa waja wake,kwahiyo hayo mambo ya dhambi ni ubaya wa nafsi za wanadamu tu na si vinginevyo


KADARI NI KWA AJILI YA KHERI NA SHARI (MITIHANI)

Inshallah katika darsa hii ya IMANI nimebakiwa na vipengele viwili kuamini HESABU na MIZANI

inshallah ni hapo baadae

Subuhanaka allahuma wabihamdik ashahadu anlaa ilaha ila anta astaghafiruka waatubu ilayk
 
Back
Top Bottom