Ramadhan Special Thread
Ndugu zangu waislamu naomba tuulizane hapa,hivi kuna Allah wa ramadhani na Allah wa nje ya Ramadhani?

Kama wapo tofauti ni sahihi sana kufuata maamrisho na makatazo ya huyu wa ramadhani ambaye tuna muheshimu sana

Ila kama Allah ni mmoja sasa inakuwaje hofu yetu na utii wetu ni kipindi cha ramadhani tu?

Je siku nyingine Allah hulala na kujisahau kutufuatilia ndio maana huwa hatumuogopi?

Ndugu zangu maisha ya dunia mwenye dunia yake anasema "maisha ya dunia ni starehe ya mda mfupi sana lkn maisha ya akhera ni yenye kuendelea na ya milele"

Inakuwaje haya maisha ya miaka 60 mpaka 7o tena hapa kwa walio jaaliwa maana si wote ni wenye kufika huko,tunayaona bora kuliko maisha ya milele,ambayo ni starehe kwa watendao mema na mateso kwa watendao maovu na wasio fuata amri ya Allah


Haya maisha ya hapa duniani mfano wake ni kama msafiri ambaye anasafiri kwenda sehemu fulani,akiwa njiani anakuta mti wenye kivuli na anaamua kumpumzika hapo kidogo kisha huyo huendelea na safar yake

Hapa duniani ni kama tupo kivulini tu kwa mda mchache kisha hao tunaelekea kwa Allah,je iweje kivuli cha mda mfupi tu kitusahau lishe safari yetu?


Huu uzima wetu na kuwa kwetu hai tusione tuna miaka mingi sana ya kuishi,hakika kifo ni fumbo kubwa sana,kwani hatujui siku wala saa,juzi tu ijumaa kabla ya swala ya ijumaa tulimswalia jirani yetu na kumkimbiza haraka makaburini kumzika ili tuwahi kuswali swala ya ijumaa

Tukiwa makaburini nikawa natafakari hapa huyu marehemu kitacho msaidia ni amali zake njema/vitendo vyake vyema,sijui alijiandaaje katika uhai wake?

Wakati tunaondoka nikawaza hapa sasa anatusikia tukiondoka na kumwacha peke yake na wakati huo malaika wawili mda si mrefu watamtembelea na kumuhoji maswala mbali mbali,je ana yapi ya kuwaeleza? Maana majibu yake yatategemeana na jinsi gani aliishi hapa duniani

Nilikuwa mnyonge sana,nikasema ipo siku moja watu watasema katika kaburi langu "leta dongo,lete majani na kuanza kufukia kaburi langu na hao wataondoka zao nibaki na malaika wawili,je nitasema nini ikiwa maisha yangu hayakuwa ya ucha mungu?

Allah atunusuru

Tumche Allah ukweli wa kumcha
🙏🙏🙏🙏
 
Mwalimu wa Muhammad swalla llahu alaih wasallam Malaika Mkuu Jibril ambaye kazi yake miongoni mwa kazi zake ni kupeleka wahyi,ufunuo kwa mitume wote wa Allah

Alimjia mwanafunzi wake na kumuuliza ni nini IMANI

Muhammad swallallahu alaih wassallam akajibu 'imani ni kumuamini Allah na Siku ya mwisho,kuamini Malaika,Vitabu,Mitume,kadari yake kwa maana kher na shari yake vyote vinatoka kwa Allah,kuamini Hesabu na Mizani

Baada ya hapo Jibril akamwambia Mtume je,mtu akiamini hayo atakuwa na imani, Muhammad akajibu naam
 
Ili mtu awe na imani lazima amuamini Allah ukweli wa kumuamini,kwamba hakuna yeyote anayepaswa kuabudiwa kwa haki au kususudiwa kwa lolote isipokuwa Allah,na kwamba wala hana mshirika katika ufalme wake na uumbaji

Haifai kwa mtu yoyote kufanya ibada kinyume na kumuabudu Allah,haifai kuombwa na kutakwa msaada kwa yeyote isipokuwa Allah

Kufanya ibada na kukusudiwa kiumbe kingine tofauti na Allah,hio ni shiriki au ushirikina ambao ni dhambi kubwa sana mbele ya Allah,na lau mtu akafa na itikadi hii basi huyo ni wa motoni Milele

Lakini kwa masikitiko makubwa kuna waislamu ambao ama kwa kujua au kutokujua wanaingia katika mkumbo wa kushawishiwa na marafiki na majirani zao kwenda kuombewa na hawa manabii na mitume wenye majina yao hapa mjini,pasina kujua kwamba wanamshirikisha Allah

Kule wanaombewa kwa kuegemeza nguvu zao kwa kiumbe ambacho kimeumbwa na Allah,yaani kiumbe cha Allah kimepewa sifa ya uungu ambacho hakina

Katika qur'an inaelezwa siku ya kiama,Issa bin Mariam ataulizwa,je uliwaambiwa watu wakuabudu wewe na mama yako?

Mja huyu wa Allah atasema "hakika haipaswi kwa mimi kusema maneno hayo,hakika ulikuwa na mimi nilipokuwa nao,na hao ni viumbe wako,ama ukiamua utawahukumu au utawasamehe"

Hayo ni maneno ya mja wa Allah,hakika aliondoka duniani na itikadi moja tu kwamba hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah,na hii ilikuwa ndio desturi ya mitume wote wa Allah

Changamoto zako za maisha zisikufanye ukafanya shiriki na baadae ukaja kuangamia

Ntakuja kuendelea na kipengele kingine inshallah

Tumche Allah ukweli wa kumcha
 
IMG-20250317-WA0003.jpg
 
Naam tuendelee katika moja wapo ya kipengele cha imani

Kuamini SIKU YA MWISHO,,muumini wa kweli basi ni lazima aamini kwamba kuna siku ya mwisho au siku ya kisimamo ambacho hapo matendo ya waja yata angaliwa na kila mtu kulipwa haki yake

Aliofanya uovu atalipwa kwa uovu wake na kwa aliefanya wema atalipwa pia kwa wema wake

Inasemwa kisimamo kitakuwa na urefu wa miaka 50,000 naam miaka 50,000,hapo kila mwanadamu atahojiwa na Allah

Ndio hapo mwanadamu atasema nilitoa sadaka na kuswali kwa ajili yako,ataambiwa hapana ulitoa sadaka ili watu wakuone kwamba wewe ni mtoaji mzuri wa sadaka,atasema niliswali kwa ajili yako,ataambiwa na Allah hapana uliswali ili uonekane mbele za watu kwamba unaswali lkn hukuswali kwa ajili yangu

Ndio maana huwa tunakumbushana kwa lolote unalofanya lenye kheri basi fanya kwa kutaka radhi za Allah

Lakini kuna watu wema watasimama kisimamo cha mda mchache kama mtu anayeswali rakaa mbili tu za sunna,yaani kuna watu kisimamo kitakuwa kifupi mno kutokana na matendo yao

Jua litashushwa na kuna watu kutokana na matendo yao majasho yao yatakuwa katika visigino vyao,wengine magotini na wengine karibia na midomo yao

Kuna watu ambao watapata kivuli kutokana na matendo yao,kwahiyo hiyo siku siyo nyepesi kama tunavyodhani bali hakika ni nzito mno,katika suratul fatiha Allah anasema yeye ni mfalme wa siku ya malipo

Kwahiyo kama Allah amasema yeye ni mfalme wa siku hiyo basi jua hiyo ni siku kubwa mno

Je kama kweli unaamini kuna Siku ya Mwisho je umejiandaa vipi ikiwa wewe ni mtu mwenye imani?

Tumche Allah ukweli wa kumcha
 
Amiin amiin amiin ukhty,wallah kwa jinsi ambavyo nakuona imani yako waeza sema utadhani ulizaliwa ndani ya uislamu,kumbe ulikuwa upande wa pili na Allah akakuongoza katika nuru yake

Allah azidi kukuzidishia imani pamoja na kizazi chako pia

Nakupenda kwa ajili Allah
Rabbana la tuzigh quloobana baAAda ith hadaytana wahab lana min ladunka rahmatan innaka anta alwahhabu
رَبَّنَا لَا تُزِغْ قُلُوْبَنَا بَعْدَ اِذْ هَدَيْتَنَا وَهَبْ لَنَا مِنْ لَّدُنْكَ رَحْمَةً ۚاِنَّكَ اَنْتَ الْوَهَّابُ
Mola wetu Mlezi! Usizipotoe nyoyo zetu baada ya kwisha tuongoa, na utupe rehema itokayo kwako. Hakika Wewe ndiye Mpaji. (Imran verse 8) ndio nguzo yangu, alhamdulillah sote tu tuombe dua hii maana ikiwa bado tupo chini ya jua salama yetu ni kuomba nafsi zetu zisipotee baada ya kuamini
 
Naam tuendelee katika moja wapo ya kipengele cha imani

Kuamini SIKU YA MWISHO,,muumini wa kweli basi ni lazima aamini kwamba kuna siku ya mwisho au siku ya kisimamo ambacho hapo matendo ya waja yata angaliwa na kila mtu kulipwa haki yake

Aliofanya uovu atalipwa kwa uovu wake na kwa aliefanya wema atalipwa pia kwa wema wake

Inasemwa kisimamo kitakuwa na urefu wa miaka 50,000 naam miaka 50,000,hapo kila mwanadamu atahojiwa na Allah

Ndio hapo mwanadamu atasema nilitoa sadaka na kuswali kwa ajili yako,ataambiwa hapana ulitoa sadaka ili watu wakuone kwamba wewe ni mtoaji mzuri wa sadaka,atasema niliswali kwa ajili yako,ataambiwa na Allah hapana uliswali ili uonekane mbele za watu kwamba unaswali lkn hukuswali kwa ajili yangu

Ndio maana huwa tunakumbushana kwa lolote unalofanya lenye kheri basi fanya kwa kutaka radhi za Allah

Lakini kuna watu wema watasimama kisimamo cha mda mchache kama mtu anayeswali rakaa mbili tu za sunna,yaani kuna watu kisimamo kitakuwa kifupi mno kutokana na matendo yao

Jua litashushwa na kuna watu kutokana na matendo yao majasho yao yatakuwa katika visigino vyao,wengine magotini na wengine karibia na midomo yao

Kuna watu ambao watapata kivuli kutokana na matendo yao,kwahiyo hiyo siku siyo nyepesi kama tunavyodhani bali hakika ni nzito mno,katika suratul fatiha Allah anasema yeye ni mfalme wa siku ya malipo

Kwahiyo kama Allah amasema yeye ni mfalme wa siku hiyo basi jua hiyo ni siku kubwa mno

Je kama kweli unaamini kuna Siku ya Mwisho je umejiandaa vipi ikiwa wewe ni mtu mwenye imani?

Tumche Allah ukweli wa kumcha
Allah atujalie tupate kivuli chake siku hii ya hesabu na zaidi atujalie tuwe miongoni mwa watakaopita bila ya hesabu

(Naomba kujua hizi rakaa mbili za sunna ni zipi? Dhuha?, baadia na kablia ama zipi?
 
Ili mtu awe na imani lazima amuamini Allah ukweli wa kumuamini,kwamba hakuna yeyote anayepaswa kuabudiwa kwa haki au kususudiwa kwa lolote isipokuwa Allah,na kwamba wala hana mshirika katika ufalme wake na uumbaji

Haifai kwa mtu yoyote kufanya ibada kinyume na kumuabudu Allah,haifai kuombwa na kutakwa msaada kwa yeyote isipokuwa Allah

Kufanya ibada na kukusudiwa kiumbe kingine tofauti na Allah,hio ni shiriki au ushirikina ambao ni dhambi kubwa sana mbele ya Allah,na lau mtu akafa na itikadi hii basi huyo ni wa motoni Milele

Lakini kwa masikitiko makubwa kuna waislamu ambao ama kwa kujua au kutokujua wanaingia katika mkumbo wa kushawishiwa na marafiki na majirani zao kwenda kuombewa na hawa manabii na mitume wenye majina yao hapa mjini,pasina kujua kwamba wanamshirikisha Allah

Kule wanaombewa kwa kuegemeza nguvu zao kwa kiumbe ambacho kimeumbwa na Allah,yaani kiumbe cha Allah kimepewa sifa ya uungu ambacho hakina

Katika qur'an inaelezwa siku ya kiama,Issa bin Mariam ataulizwa,je uliwaambiwa watu wakuabudu wewe na mama yako?

Mja huyu wa Allah atasema "hakika haipaswi kwa mimi kusema maneno hayo,hakika ulikuwa na mimi nilipokuwa nao,na hao ni viumbe wako,ama ukiamua utawahukumu au utawasamehe"

Hayo ni maneno ya mja wa Allah,hakika aliondoka duniani na itikadi moja tu kwamba hapana mola apasae kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah,na hii ilikuwa ndio desturi ya mitume wote wa Allah

Changamoto zako za maisha zisikufanye ukafanya shiriki na baadae ukaja kuangamia

Ntakuja kuendelea na kipengele kingine inshallah

Tumche Allah ukweli wa kumcha
Allah akulipe ramadhani hii sikua na mpango kabisa wa kuingia jf lkn baada ya kufungua siku moja nikakuta notification yako ktk uzi huu kila baada ya ftari nalazimika kupita ktk uzi huu kupata darsa, allah akuhifadhi kaka
 
Naam tuendelee katika moja wapo ya kipengele cha imani

Kuamini SIKU YA MWISHO,,muumini wa kweli basi ni lazima aamini kwamba kuna siku ya mwisho au siku ya kisimamo ambacho hapo matendo ya waja yata angaliwa na kila mtu kulipwa haki yake

Aliofanya uovu atalipwa kwa uovu wake na kwa aliefanya wema atalipwa pia kwa wema wake

Inasemwa kisimamo kitakuwa na urefu wa miaka 50,000 naam miaka 50,000,hapo kila mwanadamu atahojiwa na Allah

Ndio hapo mwanadamu atasema nilitoa sadaka na kuswali kwa ajili yako,ataambiwa hapana ulitoa sadaka ili watu wakuone kwamba wewe ni mtoaji mzuri wa sadaka,atasema niliswali kwa ajili yako,ataambiwa na Allah hapana uliswali ili uonekane mbele za watu kwamba unaswali lkn hukuswali kwa ajili yangu

Ndio maana huwa tunakumbushana kwa lolote unalofanya lenye kheri basi fanya kwa kutaka radhi za Allah

Lakini kuna watu wema watasimama kisimamo cha mda mchache kama mtu anayeswali rakaa mbili tu za sunna,yaani kuna watu kisimamo kitakuwa kifupi mno kutokana na matendo yao

Jua litashushwa na kuna watu kutokana na matendo yao majasho yao yatakuwa katika visigino vyao,wengine magotini na wengine karibia na midomo yao

Kuna watu ambao watapata kivuli kutokana na matendo yao,kwahiyo hiyo siku siyo nyepesi kama tunavyodhani bali hakika ni nzito mno,katika suratul fatiha Allah anasema yeye ni mfalme wa siku ya malipo

Kwahiyo kama Allah amasema yeye ni mfalme wa siku hiyo basi jua hiyo ni siku kubwa mno

Je kama kweli unaamini kuna Siku ya Mwisho je umejiandaa vipi ikiwa wewe ni mtu mwenye imani?

Tumche Allah ukweli wa kumcha
Hii siku ya malipo jaman Allah atupe tu pepo yake kwa rehema zake, nimejikuta nawaza ktk surah al haqqa kuanzia pale anaposema faama man uutiya kitabahu pindi mja atakapopewa kitabua chake huwa naweka hisia kabisa sijui nitapewa kwa mkono wa kulia ama laa subhanallah kisha kitabu kimehifadhi dogo na kubwa tena hakuna kitakachokuokoa isipokua matendo yako. Cheo na mali hazitatufaa kisha pasemwe mshikeni mfunge pingu kisha atupwe motoni la ilaha illa lah, naona bila rehema za Allah kutoboa ngumu lkn najipa moyo kuwa kuna njia mbili either kushukuru ama kukufuru na Allah atatufanyia wepesi ktk njia tutayoichagua, ya rabb tujalie mwisho uliokuwa mwema na usituache tukapotea baada ya kuamini
 
Hii siku ya malipo jaman Allah atupe tu pepo yake kwa rehema zake, nimejikuta nawaza ktk surah al haqqa kuanzia pale anaposema faama man uutiya kitabahu pindi mja atakapopewa kitabua chake huwa naweka hisia kabisa sijui nitapewa kwa mkono wa kulia ama laa subhanallah kisha kitabu kimehifadhi dogo na kubwa tena hakuna kitakachokuokoa isipokua matendo yako. Cheo na mali hazitatufaa kisha pasemwe mshikeni mfunge pingu kisha atupwe motoni la ilaha illa lah, naona bila rehema za Allah kutoboa ngumu lkn najipa moyo kuwa kuna njia mbili either kushukuru ama kukufuru na Allah atatufanyia wepesi ktk njia tutayoichagua, ya rabb tujalie mwisho uliokuwa mwema na usituache tukapotea baada ya kuamini
Amiini,naam ni kweli kabisa hakuna kiumbe ambacho kitaingia peponi kwa amali zake bali kwa rehma ya Allah tu kwani hakika mkamilifu ni Allah pekee

Kwahiyo kikubwa ni kufanya jitihada kadri ya uwezo wetu ili mradi Allah aone juhudi zetu na kwa mapenzi yake atupe fadhila na rehma zake
 
Allah akulipe ramadhani hii sikua na mpango kabisa wa kuingia jf lkn baada ya kufungua siku moja nikakuta notification yako ktk uzi huu kila baada ya ftari nalazimika kupita ktk uzi huu kupata darsa, allah akuhifadhi kaka
Mashaallah nafurahi kusikia hivyo,Allah atufanyie wepesi sote
 
Allah atujalie tupate kivuli chake siku hii ya hesabu na zaidi atujalie tuwe miongoni mwa watakaopita bila ya hesabu

(Naomba kujua hizi rakaa mbili za sunna ni zipi? Dhuha?, baadia na kablia ama zipi?
Hapa ilimaanisha kwamba hao waja wema watakaa kisimamo cha mda mchache kama kitambo cha mtu kuswali rakaa mbili za suna,yani watachukua mda mdogo sana kuhojiwa wastani kuswali rakaa mbili hazizidi dakika tano
 
Hapa ilimaanisha kwamba hao waja wema watakaa kisimamo cha mda mchache kama kitambo cha mtu kuswali rakaa mbili za suna,yani watachukua mda mdogo sana kuhojiwa wastani kuswali rakaa mbili hazizidi dakika tano
Nilisoma vibaya nimerejea nimeeelewa shukran, nilidhani kuna fursa ya sunna ya rakaa mbili kwa ajili ya wepesi wa siku hii
 
Tumeangalia kumwamini Allah na Siku ya Mwisho katika yale mambo ambayo yana mfanya mtu awe na imani

Tuangalie kipengele kingine juu ya kuwaamini MALAIKA wa Allah

Hawa ni viumbe wa Allah ambao wameumbwa kwa nuru,na hawana jinsia ya kike wala ya kiume,hawana sifa ya kula,na wameumbwa wengine wana mbawa mbili,wengine tatu na wengine zaidi ya hizo,mfano Malaika Jibril inasemekana ana mbawa mia sita (600) akizikunjua zote basi anafunika upeo wa anga

Hawana sifa ya kumuasi Allah na watiifu sana,na Allah anasema hao walioko mbinguni hawajivuni kumwabudu yeye kwani wanamsifu na kumsujudia,kinyume chache sisi wanadamu na majini tunajivuna na kukataa kumwamudu Allah

Hayo ni kwa uchache,hawa ndio wanafanya majukumu mbali mbali ambayo wamepewa na mola wao,kuna wanao dili na mvua,wanadili na milima,mfano pale kipenzi cha umma Muhammad swallallahu alaih wassallam alipoenda kule Taif kuwalingania watu

Walikataa ujumbe wake,na wakubwa wao wakawaagiza wahuni wa barabarani wampige na kumrushia mawe,alipigwa sana mpaka mwili wake wote ukaloa damu,akiwa nje ya mji huo aliomba dua nzito haikuchukua mda,Malaika Jibril alitumwa na Allah aje kwa Muhammad na kumwambia Allah amesikia kilio chako,huyu hapa Malaika wa milima msikilize mahitaji yako yupo tayar kukutii

Mda kidogo akatokea Malaika huyo na kumsalimia Mtume,kisha akamwambia mimi nasimamia milima,niamuru nitaikusanya hii milima kisha niigonganishe na kisha kuwa ponda ponda wakazi wote wa mji huu wa Taif,lkn kwakuwa Mtume amejawa sana huruma akasema hapana,huenda katika migongo yao kikatoka kizazi ambacho kitakuja kumwamini na kumwabudu Allah
 
Lakini kuna malaika waandishi maalumu ambao ndio wanaandika matendo yetu ya kila siku,kila mwanadamu ana malaika wawili,mmoja kulia kwako na mwingine kushoto kwako,huyo wa kulia huandika matendo yako mema na huyo wa kushoto huandika maovu yako

Hao hawaachi hata jambo moja yani kila kitu unachofanya wanaandika,umesimama,umekaa,umeingia jf umekomenti ujinga au umekomenti zuri wanaandika,ila kuhusu nia ya kile ulichoandika ni jukumu la Allah mwenyewe

Yani Allah anamwambia Mtume na ndio anatuambia sisi kwamba,haufanyi jambo lolote lile ila wapo malaika mahususi wanaandika kila jambo unalofanya,hausomi qur'an ila wapo waandishi wanaandika,yani chochote kile kipo katika daftari lako

Ndio maana siku ya kiama tunaambiwa na Allah,wale watu waovu watakapopewa madaftari yao watastaajabu sana na kusema,daftar hili lina nini haliachi kubwa wala jambo dogo

Allah anaendelea kueleza katika qur'an kwamba wala halianguki jani la mti wowote ule bali hesabu yake anaijua ipo katika daftar maalumu imewekewa hesabu yake

Wala haianguki punje ndogo ya hadari katika giza la baharini au barani ila anaijua ipo katik daftar maalumu,kwahiyo hakuna ambacho Allah hana taarifa nacho
 
Back
Top Bottom