Sasa hii ndio inadhihirisha wazi kuwa wameona dhahiri JPM anaenda kuanguka uchaguzi huu!

Wasichojua wala hawataki kujifunza; ni kwamba hapo ndio wanamuongezea kura na maarufu Lissu.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemuandikia barua mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu ya kumuita katika kikao cha kamati ya maadili ya Taifa.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dkt. Charles Mahera amesema hilo leo jijini Arusha wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo ameeleza kuwa mgombea huyo atafika mbele ya kamati Septemba 29 mwaka huu.

Akizungumzia uratibu na usimamizi wa kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu amesema tume imekumbana na changamoto kwa baadhi ya wagombea wa kiti cha Rais kutoheshimu sheria, taratibu na maadili ya uchaguzi.

Ameongeza kuwa baadhi ya wagombea wamekuwa wakitumia maneno ya kukashifu wagombea wenzao, tume, pamoja na kutoa taarifa zisizo za kweli zenye lengo la kuleta taharuki na uzushi miongoni mwa Watanzania.

Chanzo: TBC Online
Naomba wamuite na Magufuli kwa sababu amekua akiwatishia wananchi kwamba wakichagua upinzani hawatapata maendeleao
 
Hivi msemaji wa Chama anaongea kwa niaba ya nani?
Hapa tume wanaongelea maadili ya mgombea Mimi CCM sio mgombea naweza mporomoshea mitusi yote ya nguoni Lisu na CCM wala tume haiwezi nifanya chochote .Polepole sio mgombea NEC hawamjui hata akimporomoshea mitusi ya Nguoni Lisu
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemuandikia barua mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu ya kumuita katika kikao cha kamati ya maadili ya Taifa.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dkt. Charles Mahera amesema hilo leo jijini Arusha wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo ameeleza kuwa mgombea huyo atafika mbele ya kamati Septemba 29 mwaka huu.

Akizungumzia uratibu na usimamizi wa kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu amesema tume imekumbana na changamoto kwa baadhi ya wagombea wa kiti cha Rais kutoheshimu sheria, taratibu na maadili ya uchaguzi.

Ameongeza kuwa baadhi ya wagombea wamekuwa wakitumia maneno ya kukashifu wagombea wenzao, tume, pamoja na kutoa taarifa zisizo za kweli zenye lengo la kuleta taharuki na uzushi miongoni mwa Watanzania.

Chanzo: TBC Online
NEC inaanza kuburuzwa na CCM iokoe jahazi linazama.
 
Nasikitika sana kuona tume inachezewa na huyu kibaraka wa mabeberu, wamuondoe tu,au wampotezee watanzania tutafanya yetu Oct.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imemtaka mgombea urais (CHADEMA), Tundu Lissu afike katika kikao cha kamati ya maadili ya Taifa Septemba 29. NEC imesema baadhi ya wagombea wamekuwa wakitumia maneno ya kukashifu wagombea wenzao, tume, pamoja na kutoa taarifa zisizo za kweli.

Source:

Acha Mahera ajiunge na Jiwe the Hague anajua Sirro amegoma kupelekeshwa anataka amalize kwa amani hataki the Hague ....sasa Mahera yumo mtegoni !! Muda staafu umefika ana 61 yrs asubiri ....
 
Tume hii iliyoengua wagombea wa CHADEMA na kuwaacha CCM kupita bila kupingwa ina uhalali gani wa kumbyooshea mtu kidole?

Hawana akili tu, wangegundua kuwa kwa sasa ukimwekea mizengwe Lissu unachukiwa na watu wengi...sijui kwanini hawajifunzi?
 
Hapa tume wanaongelea maadili ya mgombea Mimi CCM sio mgombea naweza mporomoshea mitusi yote ya nguoni Lisu na CCM wala tume haiwezi nifanya chochote .Polepole sio mgombea NEC hawamjui
Kwa hiyo Tumani Makene akitukana ni sahihi?
 
Halafu wanakanusha eti hawajawaita wakati mpaka ushahidi tunao, hao ma DED ni wanafamilia wetu na wanatupatia taarifa

Kama ushahidi mnao basi mtaweka mezani.

NEC wataweka ushahidi wao na Tundu Lissu ataweka ushahidi wenu.

Ila ni muhimu kuhudhuria hiki kikao cha maadili ya Taifa.
 
Anapashwa kushughulikiwa huyu naona tume imechoka kumlealea!
Wewe unaamini kuwa chini ya Mahera kuna Tume ya Uchaguzi au kakitengo ka CCM kanakofanyia kazi kwenye ofisi za NEC?

Hawa ndio watu ambao hata siku watakapoondoka Duniani hakuna kitu cha maana watakachokiacha cha kukumbukwa kwa mema. Hata watoto wao watashindwa kutumia majina ya wazazi wao kutokana na aibu iliyoachwa na wazazi wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom