Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,816
- 4,566
===
Greatest of all time
Leo ni Sikukuu ya Soka.
Mnyama Mkubwa Mwituni. Simba SC itakuwa ikishuka dimbani kuwakabili Singida FG FC katika dimba la Mkwakwani pale jijini Tanga.
Simba ambayo imesheheni wachezaji mafundi kama vile Onana, Baleke, Kramo, Mwalimu Fabrice Ngoma na wengineo wanatarajiwa kutoa burudani kubwa sana kwa wapenda kandanda nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla mara baada ya butua butua na piga nikupige ya jana.
Singida ambayo imefuzu kucheza kimataifa nayo imesajili wachezaji kadhaa akiwemo Kiyombo, Babu Onyango, Yahaya Mbegu na wengineo wanatarajiwa kuleta ushindani.
Ewe mwana Simba uliyepo Kasulu, Jinja, Makambako, Kisumu, Uyui, Ndola, na mahala popote tegemea mpira mkubwa leo na mechi yenye mvuto.
Mechi itapigwa Saa 1:00 Usiku na itakuwa mubashara kupitia Azam Sports 1HD.
---
Kikosi cha Simba kinachoanza
Kikosi cha Singida FG kilichoanza
---
Mpira umeanza
04' Bado milango ni migumu bado hawajafungana
05' Singida wanapata goli lakini linakataliwa
40' Bado milango migumu kwa timu zote mbli huku zikishambuliana kwa zamu
45' Mapumziko timu bado hazijafungana
46' Anaingia Ngoma na Bocco wanatoka Kanoute na Baleke
55' Milango bado migumu kwa timu zote mbili
75' Bado hakuna goli
80' Bado timu hazijafungana
90' Zimekamilika na sasa matuta yanafuata.
Wapigaji Singida FG
Andabwile ❌
Tchakei ✅
Kagoma ❌
Abuya ✅
Wapigaji Simba SC
Luis ✅
Saido ✅
Mzamiru ✅
Phiri ✅
Mpira umekwisha Simba ameshinda kwa Penati 4 kwa 2