FT: Mlandege 1 - 0 Simba SC | Mapinduzi Cup | New Amaan Complex | Fainali | 13.01.2024. Kombe limebaki Mlandege

uran

JF-Expert Member
Nov 11, 2013
7,525
10,758
Match Day.
Updates...
Screenshot_20240113-190314~2.png

20240113_070016.jpg


Mlandege FC ambao ni mabingwa watetezi, watamenyana na Simba Leo Januari 13, 2024 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex mjini Zanzibar, ambapo mchezo wa fainali utaanza kutimua vumbi saa 2:15Usiku.

Fainali iliyopita;
Mlandege ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Singida Fountain Gate FC.

Ikumbukwe Mlandege walipewa Ofa ya Pikipiki kwa kila Mchezaji. Sijui this time wapewa nini, endapo watashinda.

Rekodi inaonyesha michuano hiyo inatawaliwa zaidi na timu za Tanzania Bara ikiwamo Azam FC iliyotwaa taji hilo mara tano,
Simba SC (mara tatu) huku Yanga na Mtibwa Sugar FC mara mbili kila moja.

Timu za Zanzibar ambazo ni Jamhuri ya Pemba, Polisi, KMKM, Mafunzo, Malindi na Miembeni zilitwaa ubingwa huo mara moja kila moja. Pia, Mamlaka ya Halmashauri ya Jiji la Kampala ya Uganda (KCCA) na Mamlaka ya Mapato ya Uganda (URA) zilishinda taji hilo mara moja kila moja.

Tukutane Saa 2:15Usiku kwa updates zaidi ya Mechi na Vikosi vitakavyoanza.

KIKOSI CHA MLANDEGE KINACHOANZA.
PSX_20240113_193116.png


KIKOSI CHA SIMBA KINACHOANZA.
20240113_192132.jpg

All the Best Mnyama.
#nguvumoja#

Updates...
Mpira Unaendelea hadi sasa Simba anafanya mashambulizi yakushtukiza kwenye lango la Mlandege.

Dakika ya 06'
Kapombe anakosa goli hapa.
Ah! ni faulu.

DK 08'
Mlandege wanafanya shambulizi kwenye lango la Simba inaondolewa na mtaalamu sana Sarr.

DK 12'
Phiri yuko chini baada ya kuchezewa rafu mbaya sana.
Mchezaji wa Mlandege anapata yellow card.
Mpira unaendelea....

DK 18'
Simba wanafanya shambulizi kali langoni mwa Mlandege.
Inapigwa nje na Onana, inakuwa Goal kick

DK 27'
Mpira Unaendelea bado Simba wanaishambulia Mlandege.
Mlandege 0- 0 Simba.

DK 35'
Mchezaji wa Mlandege yuko chini baada ya kugongana na Saidoo.
Amenyanyuka mpira Unaendelea

DK 40'
Simba wanapata kona, inapigwa haileti impact yoyote kwenye goli na Mlandege

DK 41'
Simba wanapata free kick.
Saido anapiga haileti shida.
inauwa goal kick.

DK 44'
Simba wanapata free kick nje kidogo ya box la 18.
Anaipiga Saidoo inapaa juu inakuwa goal kick..

DK 45'
Nyongeza ni Dakika 2.
Kuna mchezaji wa Mlandege yuko chini pale anafanyiwa matibabu.
Game bado ni 0 kwa 0.

Half Time.
Mlandege 0-0 Simba.

Kipindi Cha Pili Kimeanza sasa
Simba wanafanya Sub.
Baleke Inn
Phiri Out

Mlandege pia wanafanya Sub 2.
Arafat Inn
Joseph Out.

DK 46'
Simba wanafanya Shambulizi kali sana inakuwa kona.
Inapigwa haizai.

DK 50'
Onana anafanya juhudi binafsi hapa uwanjani.
lakini inaishia kuwa Goli kiki.

DK 54'
Mlandege wanapata goli hapa.
Baada ya Joseph kuwapiga chenga mabeki wa Simba.
Mlandege 1 - 0 Simba.
Game On.

DK 62'
Sub kwa Simba.
Sarr Out
Hamis Inn.

DK 63'
Simba wanakosa goli la wazi kabisa hapa.

DK 67'
Simba wanapiga kona haileti madhara.
Kipa wa Mlandege anaanza kupoteza muda.

DK 70'
Simba wanapata faulu nje kidogo ya 18.
Anapiga Saidoo, kipa anaicheza goli kipa.

DK 72'
Mlandege wanapata Free Kick nje kidogo ya 18.
Anapiga Benet, inakuwa kona.
Anapiga Yusufu Haji.
Haileti madhara kwa Simba.

DK 78'
Sub
Louis Miquisonne Out.
Chasambi Inn

DK 80'
Simba wanapata kona,
haileti madhara, kuna mchezaji mmoja wa Mlandege yuko chini pale anafanyiwa huduma ya kwanza.

DK 82'
Sub
Karabaka Inn
Onana Out.

DK 84'
Simba wanapiga free kick haileti madhara.

DK 86'
Ngoma anapiga akiwa na kipa.
Inadakwa na Kipa.

DK 90'
Nyongeza ni 5'
Game On...

DK 92'
Mchezaji wa Mlandege anatolewa nje kwa machela inawezekana amepata majeraha.

DK 90+4'
kuna shabiki wa Simba ameingia Uwanjani hapa.

Full Time.
Mlandege 1- 0 Simba.

Mpira Umemalizika.

Mlandege wamebeba tena Kombe kwa mara Mbili Mfululizo.
 
Tangaza kabisa wanayanga wasikanyage hapa maana hii mechi haiwahusu.

Kila la heri mnyama ukatafune ndege wako salama.
leo hakuna rangi mtaacha kuiona, walichofanyiwa singida ndio mtafanyiwa ninyi leo, mbaya zaidi hata hamna habari ni suala la muda tu kufikia saa4 utaona nyuzi za malalamiko zitakavyofurika mkilalamika msishiriki mapinduzi cup msimu ujao ni suala la muda tu nikuhakikishie tu kuwa YANGA sio wajinga, labda muingie na mbinu za kimafia za kuwapiga goli nyingi nyingi tofauti na hapo mtaambulia aibu
 
leo hakuna rangi mtaacha kuiona, walichofanyiwa singida ndio mtafanyiwa ninyi leo, mbaya zaidi hata hamna habari ni suala la muda tu kufikia saa4 utaona nyuzi za malalamiko zitakavyofurika mkilalamika msishiriki mapinduzi cup msimu ujao ni suala la muda tu nikuhakikishie tu kuwa YANGA sio wajinga, labda muingie na mbinu za kimafia za kuwapiga goli nyingi nyingi tofauti na hapo mtaambulia aibu
wee em teseka taratibuu, woiiih
 
Back
Top Bottom