OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,249
- 103,956
Aliyekua DC wa Hai Lengai Ole Sabaya pamoja na wenzake leo wamefikishwa tena kwenye Mahakama ya Wilaya iliyopo Sekei Arusha, ili kujibu tuhuma zinazowakabili, Sabaya na wenzake wanakabiliwa na mashtaka matano.
Itakumbukwa June 04,2021 Sabaya na wenzake walifikishwa Mahakamani hapo ambapo baadaye Tumaini Kweka, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka anayeshughulika na usimamizi wa kesi alisema“uchunguzi katika baadhi ya makosa yanayomkabili Lengai na wenzake umefikia kwenye kiwango ambacho tunasema ni tamati ya kuweza kuwafikisha Mahakamani”.
“Mkurugenzi wa Mashtaka baada ya kujiridhisha kwamba kweli tuhuma zilizokua zinamkabiki Lengai na wenzake kisheria zinatengeneza kosa akaamua leo wafikishwe Mahakamani, kama mlivyoona alikua akituhumiwa kuongoza magenge ya kihalifu, vitendo vya rushwa, kutakatisha fedha haramu ambayo ni matokeo ya vitendo vya rushwa”.
“Vilevile Mkurugenzi alijiridhisha kwamba kuna unyang'anyi wa kutumia silaha, ndio maana amefikishwa Mahakamani leo kwa hayo makosa matano lakini kwa unyang'anyi wa kutumia silaha ni makosa mawili aliyatenda katika wakati mmoja lakini kwa wakati tofautitofauti, na kama tuhuma nyingine zitathibitika basi Mkurugenzi wa Mashtaka ataamua vinginevyo"
Zaidi, soma: Arusha: Lengai Ole Sabaya afikishwa Mahakamani kwa Uhujumu Uchumi, Utakatishaji Fedha
My Take: Mahakama na DPP huu ndiyo wa kutuaminisha umahiri wenu. Chapa ilale
======
PICHA: Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake, wakiwasili mahakamani mkoani Arusha kwenye kesi yao, leo Juni 18,2021 Ijumaa
Itakumbukwa June 04,2021 Sabaya na wenzake walifikishwa Mahakamani hapo ambapo baadaye Tumaini Kweka, Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Taifa ya Mashtaka anayeshughulika na usimamizi wa kesi alisema“uchunguzi katika baadhi ya makosa yanayomkabili Lengai na wenzake umefikia kwenye kiwango ambacho tunasema ni tamati ya kuweza kuwafikisha Mahakamani”.
“Mkurugenzi wa Mashtaka baada ya kujiridhisha kwamba kweli tuhuma zilizokua zinamkabiki Lengai na wenzake kisheria zinatengeneza kosa akaamua leo wafikishwe Mahakamani, kama mlivyoona alikua akituhumiwa kuongoza magenge ya kihalifu, vitendo vya rushwa, kutakatisha fedha haramu ambayo ni matokeo ya vitendo vya rushwa”.
“Vilevile Mkurugenzi alijiridhisha kwamba kuna unyang'anyi wa kutumia silaha, ndio maana amefikishwa Mahakamani leo kwa hayo makosa matano lakini kwa unyang'anyi wa kutumia silaha ni makosa mawili aliyatenda katika wakati mmoja lakini kwa wakati tofautitofauti, na kama tuhuma nyingine zitathibitika basi Mkurugenzi wa Mashtaka ataamua vinginevyo"
Zaidi, soma: Arusha: Lengai Ole Sabaya afikishwa Mahakamani kwa Uhujumu Uchumi, Utakatishaji Fedha
My Take: Mahakama na DPP huu ndiyo wa kutuaminisha umahiri wenu. Chapa ilale
======
PICHA: Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, Lengai Ole Sabaya na wenzake, wakiwasili mahakamani mkoani Arusha kwenye kesi yao, leo Juni 18,2021 Ijumaa