JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Mwanasiasa Lengai Ole Sabaya ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, amewaomba msamaha wote aliwakosea na kusema amewasamehe wale wote waliomkosea.
Amesema hayo katika Kanisa la Ebenezer Restoration Ministry For All Nations Jijini Arusha katika ibada ya shukrani, leo Jumapili Februari 4, 2024.
Sabaya amesema hataendeleza vita na maadui zake, bali anawaachia Mungu. Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mifumo ya haki na usawa nchini.
Ikumbukwe Aprili 5, 2023 Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi ilimwachia huru Sabaya baada ya kukiri kosa la kula njama pamoja na makosa mbalimbali yaliyokuwa yakimkabili.
Pia Sabaya aliachiwa huru kwa kesi nyingine mbili za matumizi mabaya ya madaraka na uhujumu uchumi, zilizoendeshwa jijini Arusha.
Chanzo: Mwananchi
Amesema hayo katika Kanisa la Ebenezer Restoration Ministry For All Nations Jijini Arusha katika ibada ya shukrani, leo Jumapili Februari 4, 2024.
Sabaya amesema hataendeleza vita na maadui zake, bali anawaachia Mungu. Pia amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweka mifumo ya haki na usawa nchini.
Ikumbukwe Aprili 5, 2023 Mahakama ya Hakimu Mkazi Moshi ilimwachia huru Sabaya baada ya kukiri kosa la kula njama pamoja na makosa mbalimbali yaliyokuwa yakimkabili.
Pia Sabaya aliachiwa huru kwa kesi nyingine mbili za matumizi mabaya ya madaraka na uhujumu uchumi, zilizoendeshwa jijini Arusha.
Chanzo: Mwananchi