MAGUFULI, DAIMA TUTAKUKUMBUKA
Kifo hakina rufani, pia hakina huruma,
Kimempoka kundini, Rais mwenye heshima,
bado ali ujanani, mudawe umesimama,
Daima tutakuenzi, Tangulia Magufuli
Kifo hakina rufani, kwa kila mja lazima,
Kwa uchungu na huzuni, natakabari Karima,
Mjao yu mikononi, Dunia...