Nimemsamehe aliyekuwa Rais wa Tanzania John Magufuli lakini sitomsahau kwa yote aliyonifanyia

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Oct 31, 2014
5,360
11,505
Inawezekana ningekuwa na chuki kiasi kikubwa sana kutokana na mambo mbalimbali ambayo aliyatenda au nena Mh. Rais alipokuwa Madarakani.

Kwa njia moja au nyingine yalitesa na kuumiza watu wangu wa karibu na mimi mwenyewe pia. Lakini inapofikia mtu akawa mgonjwa mahututi akiwa kitandani hana msaada mwingine wowote au anapofariki ukimtizama na kugundua kila kitu kilikuwa ubatili. Unaingiwa na moyo wa kibinadamu. Unamsamehe.

Unaweza kumbuka mtu alivyokukana wakati wa dhiki ukiwa unahitaji msaada wake. Au alipokukanyaga na akaendelea kusimama juu yako ukiwa umelala chini. Unayaacha hayo yapite.

Ntampongeza Mh. Magufuli kwa kuwa vile ambavyo alikuwa. Aliishi vile ambavyo alikuwa. Ingawa naamini katika Utawala wake ndipo ambapo tulishuhudia Viongozi wanafiki ambao hawajawahi kutokea. Ukimtoa yeye ambaye aliishi kama alivyokuwa. Alikuwa amezungukwa na viongozi wanafiki, wachumia tumbo, wasiokuwa na msimamo.

Ntaendelea kujifunza kuwa Duniani tunapita. Kila kitu kitabaki. Hatuhitajj majivuno. Itakayobaki ni Milima, Mawe halisi na viumbe visivyo hai.

Roho ya Marehemu IWEKWE INAPOSTAHILI. AMINA
 
Mwenyezi Mungu amjalie busara na hekima mama yetu Samia Suluhu Hassan iki awezw kuurudisha umoja na mshikamano kati yetu, na pia ile hali ya kukata tamaa na kuombeana mabaya iliyoanza kutamalaki kwenye jamii.

Aponye majeraha yote kama itawezekana. Apumzike kwa amani Mr. Bulldozer. Alitunyoosha kweri kweri!!!!
 
mtoa mada umeongea kama mimi. kila mtu angekuwa akiamka tu anafikiria kwa sekunde siku moja ataiacha dunia hakika dunia ingekuwa mahala pazuri pa kuishi. pia wazaz tujitahidi kuwapa hekima hii watoto hata tamaa za kifisad zitapungua. kuna kabila linashawish watoto na vizaz vyao kuwa wezi, walafi na mafisadi. wanaaminishwa katika pesa kuwa ndo kila kitu, haijalishi imekujaje. mtu haangaikii legacy.
 
Mwenyezi Mungu amjalie busara na hekima mama yetu Samia Suluhu Hassan iki awezw kuurudisha umoja na mshikamano kati yetu, na pia ile hali ya kukata tamaa na kuombeana mabaya iliyoanza kutamalaki kwenye jamii.

Aponye majeraha yote kama itawezekana. Apumzike kwa amani Mr. Bulldozer. Alitunyoosha kweri kweri!!!!
Mama anatakiwa atumie hekima na busara aitishe maridhiano ya kitaifa ya husishe viongozi wa dini, vyama vya siasa na wazee wastaafu
 
Mwinyi junior kaweza ndani ya muda mfupi Zanzibar wanaongea lugha moja. Viongozi waislaam japo Wana kaupendeleo lakini hofu ya MUNGU IPO wanajua kuna Leo na kesho. Mama Samia ana Baraka zangu.
Mwenyezi Mungu amjalie busara na hekima mama yetu Samia Suluhu Hassan iki awezw kuurudisha umoja na mshikamano kati yetu, na pia ile hali ya kukata tamaa na kuombeana mabaya iliyoanza kutamalaki kwenye jamii.

Aponye majeraha yote kama itawezekana. Apumzike kwa amani Mr. Bulldozer. Alitunyoosha kweri kweri!!!!
 
Back
Top Bottom