Lini Tanzania itapata kiongozi kama Hugo Chavez? Watanzania hatunufaiki na rasilimali zetu

Nyankurungu2020

JF-Expert Member
Oct 2, 2020
4,086
6,568
Marehemu Hugo Chavez alikuwa kiongozi anayefaa na kama hapa Tanzania tungekuwa na kiongozi kama Hugo Chavez tungefurahia kuwa Watanzania.

Leo hii hili taifa lina kila aina ya rasilimali ambazo kama tungekuwa na kiongozi makini basi tusingesikia wananchi wanapata tabu. Leo hii wananchi wanahangaika kupata huduma za afya, elimu,maji na huduma nyingi za msingi.

Kama tumejitahidi awamu hii kudhibiti rushwa na ubadhirifu na kisha fedha zilizokuwa zinapotea zinaenda mikononi mwa serikali. Mbona huduma za afya zipo duni? Mbona wananchi masikini wanahangaika kulipishwa kupata huduma za afya? Kwa nini shule hazina madarasa? Wanafunzi wanafunzi wanakaa chini!

Kwa nini tukomae kujenga madaraja kama Busisi na Oysterbay wakati huduma za msingi kwa wananchi masikini hazipo?

Mbona Hugo Chavez alihakikisha rasilimali za taifa lake zinawanufaisha wananchi wote maskini kwa matajiri. Sisi viongozi wetu mnakwama wapi?
 
Lazima tuwe na katiba mpya bila katiba hatuna muda mrefu tutaingia vitani maana kila Rais anapendelea kujenga kwake au kuwabeba kabila lake.
 
Akili yako nyembamba, huwezi kuona mafanikio kama nchi watanzania tuliyoyapata chini ya awamu ya tano! Na wala sintapoteza muda kujaribu kumuelewesha mpumbafu!
Mafanikio ya kulipia huduma za afya bila kupata dawa? Shule kukosa madarasa? Kuchangisha michango ya ujenzi wa shule huku mnajenga madaraja yasiyo na tija
 
Mafanikio ya kulipia huduma za afya bila kupata dawa? Shule kukosa madarasa? Kuchangisha michango ya ujenzi wa shule huku mnajenga madaraja yasiyo na tija
Nilishasema sina muda wa kupoteza kujaribu kumuelewesha !
 
Nini wewee. Mtaji wako ni nguvu zako mwenyewe
Korosho, mbaazi, ufuta, na mazao mengine ya biashara na kilimo ambayo ndio yanaajiri sehemu kubwa ya Watanzaia, hapa wanatumia nguvu zao za mwili na pesa. Serikali haichangii chochote, wakati wa kuuza bei wanapanga wao na kodi kibao. So, acheni dharau.
 
Akili yako nyembamba, huwezi kuona mafanikio kama nchi watanzania tuliyoyapata chini ya awamu ya tano! Na wala sintapoteza muda kujaribu kumuelewesha mpumbafu!
Acha porojo, taja hayo mafanikio!!! Au ule mradi kichaa wa ndege?! Kinyume na hapo, zaidi ya 85% ya miradi ya JPM ameikuta isipokuwa mazuzu wasiojua kinachoendelea serikalini ndo wanadhani ni miradi ya JPM!
 
Acha porojo, taja hayo mafanikio!!! Au ule mradi kichaa wa ndege?! Kinyume na hapo, zaidi ya 85% ya miradi ya JPM ameikuta isipokuwa mazuzu wasiojua kinachoendelea serikalini ndo wanadhani ni miradi ya JPM!
I don't reason with a fool! Case closed! Siwezi kumuelewesha mpumbafu!
 
Nichagueni mimi basi! Nitazirudisha milioni 50 kwenye kila kijiji, nitaurudisha mchakato wa katiba mpya, nitapunguza kiwango cha kodi kwa wafanyabiashara na wajasiriamali ili walipe bila shuruti, nitaanzisha shule za ufundi stadi kila kata ili wasanii na ma Iron boys/girls wote wakajifue huko, riba za mikopo zitashuka mpaka single digit, kilimo kitakuwqa ni cha umwagiliaji na serikali yangu itawatafutia wakulima masoko ndani na nje ya nchi!

nitaondoa ile 15% ya makato ya Bodi, nitaurejesha ule mchakato wa upandishaji madaraja ya wafanyakazi kwa wakati, umeme na maji vitakuwa ni bure!! Bima ya afya itaimarishwa kwa Watanzania wote, nitahakikisha napunguza mshahara wangu kwa 50% na posho zote za hovyo hovyo za Wabunge nitazifyekelea mbali! Ambaye hatoridhika, ataruhusiwa kuachia ngazi bila kinyongo na mshindi wa pili ataapishwa.

Nipeni kura ndugu zangu Watanzania hiyo 2025! Sitowaangusha.
 
I don't reason with a fool! Case closed! Siwezi kumuelewesha mpumbafu!
Angalia ulivyo mpumbavu! Umeshindwa kujibu hata swali jepesi kwa sababu huna unachojua! Very stupid! Utabaki kushangilia hivyo hivyo sawa na Kijakazi wa Mfalme Juha!!! No wonder post ya kwanza tu ukaanza kuji-defend kwa matusi kwa sababu unafahamu huna uwezo wa kujenga hoja!!!
 
Back
Top Bottom