Habari,
Naomba ushauri kuhusiana na magodoro yanayobonyea kwa kati mana nimenunua godoro halijamaliza hata mwezi na sasa hivi linabonyea kwa sana hapa kati na ni kama nimelala kwenye mtumbwi.
Naomba ushauri jinsi ya kutatua hii hali kwa waliopitia hii hali.
Ahsante
Habari wana Jf,
Je kuna mtu anatoa huduma ya usafiri kutoka Bunju au Boko kila J3 mpaka Ijumaa kuelekea Posta au Upanga???
If yes then gharama ya usafiri ikoje?
Tusaidiane ili tuwahi makazini
Habarini,
Naomba ushauri kuhusiana na biashara ya kukodisha turubai, je ni size ipi ambayo inapendwa sana katika kukodishwa (4m kwa 10m au 6m kwa 10m au 8m kwa 10m)?
Material ipi ya turubai uwa inadumu, je ni pvc ikiwa na high strength polyster au pe tarps?
Nitashukuru kwa msaada wenu wataalam
Habari,
Naomba msaada wa kufahamishwa kampuni inayoweza kusafirisha mzigo kutoka China kwa uhakika na kwa gharama nafuu. Ni mashine mbili ambazo zinafit kwenye 1 CBM hivo ingependeza kufahamishwa bei per CBM.
Ahsante
Heshima Kwenu
Mwenye kujua lodges au gesti nzuri zilizopo Geita mjini na bei yake nitashukuru.
Pia nitashukuru msaada wa namba za hiyo lodge kama mnazo.
Ahsante
Habarini WanaJf,
Naomba ushauri wa kufahamishwa kuhusu tiles nzuri za kuweka kwenye nyumba ambazo hazipauki na zenye gharama reasonable.
Nimeona kuna tiles za kampuni ya Goodone, Goodwill na Twyford na nlitaka kufahamishwa kua ni kampuni ipi yenye tiles zisizopauka na nzuri
Habari,
Nahitaji fundi wa kurekebisha sofa seti moja kwa bei nafuu na material ni juu yangu. Kitambaa cha sofa kimechanika na nahitaji kubadilisha.
Napatikana Boko
Habari,
Nahitaji fundi wa kurekebisha sofa seti moja kwa bei nafuu na material ni juu yangu. Ni kitambaa cha sofa ndio kimechanika na nahitaji kubadilisha.
Napatikana Boko
Ahsante
Nahitaji mizani yenye uwezo wa kupima 0 mpaka 10 kg na iwe na mhuri na stika kutoka kwa wakala wa vipimo.
Budget yangu ni 40,000(maongezi yanakaribishwa)
Habari,
Husika na kichwa cha habari hapo juu.
Nahitaji Tub yenye uwezo wa kufit katika hizo dimension na nitashukuru ukiniwekea na bei.
Napatikana Tegeta.
Thanks
Habari Wajumbe,
Nlikua nahitaji msaada kuhusiana na kupata building permit mana nlikua najenga vibanda vyangu vya uhani nikaambiwa na Serikali ya Mtaa kua yabidi niwe na kibali.
Nahitaji msaada wakuu
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.