YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,907


Baada ya Ibada ya kuuombea na kuuaga mwili wa aliyekuwa Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli kufanyika katika kanisa la St Peters Jiji Dar es Salaam sasa ni muda wa uwanja wa Uhuru Dar Es Salaam. Wananchi wamekusanyika kwa wingi kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania

WAKAZI WA DAR WAJITOKEZA KUAGA MWILI WA RAIS MAGUFULI

Wakazi wa Dar wamejitokeza barabarani kumuaga aliyekuwa Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli

Wameonekana kutandika Khanga barabarani, wengine walibeba mashada na mabango yenye ujumbe

====

Wakazi wa Dar wamejitokeza barabarani kumuaga aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli.

Wakazi wa Dar walionekana kutandika Khanga barabarani ili magari yaliyobeba mwili wa Hayati Magufuli yapite juu yake kuonesha heshima.

Wananchi wengine walikuwa wamebeba mashada ambayo walikuwa wakiyapunga mwili wa Marehemu ukiwa Unapita kuelekea Uwanja wa Uhuru.

=====

SIKU YA PILI 21 MACHI 2021

Watu wanaendelea kuaga mwili uwanja wa Uhuru.





1.jpg
2.jpg


3.jpg


1.jpg
2.jpg
3.jpeg
4.jpg
5.jpg
6.jpeg
7.jpg
8.jpg
 
Ageni mpendwa wenu. Tulioumizwa nae tuna hangover tunaenda kuzimua mapema maana mama katoa mapumzika jumatatu.

Kubwa zaidi tarehe 25 nayo tumepewa ni siku ya bia.

Tumenyanyaswa sana yaani.

Waachieni wanaoshikiliwa magerezani haraka wakazione familia zao
Kwakweli, me namuomba madam president abadilishe DPP pia, huyu aliepo ni chanzo cha mrundikano wa cases nyingi mahakamani na pia akipenda amteue Prof. Mussa Asad kuwa Prime minister au Vice President.
 
Namtakia safari njema huko aendako, mengi aliyafanya hapa duniani mwisho wa siku aijuaye siri yake ya mwisho ni yeye na Mungu wake, sijui muda mchache kabla hajakata roho alisema nini na Mungu wake akiwa kitandani.

Vile alivyokuwa anapenda kulitaja jina la Mungu kila wakati ndio sitaki kabisa kumyooshea kidole, mimi sio Mungu nimuhukumu, zaidi maandiko yananitaka nisihukumu nisije kuhukumiwa, au kama yupo asie na dhambi kati yetu na awe wa kwanza kumpiga jiwe.

Narudia kusema tena; uwe na safari njema huko uendako, The late, John Joseph Pombe Magufuli.

#No one is born perfect.
 
Ageni mpendwa wenu. Tulioumizwa nae tuna hangover tunaenda kuzimua mapema maana mama katoa mapumzika jumatatu.

Kubwa zaidi tarehe 25 nayo tumepewa ni siku ya bia.

Tumenyanyaswa sana yaani.

Waachieni wanaoshikiliwa magerezani haraka wakazione familia zao
Si kwasababu ya wizi wa mali za umma.
 
kwakweli,me namuomba madam president abadilishe DPP pia, uyu aliepo ni chanzo cha mlundikano wa cases nying mahakaman ,,, na pia akipenda amteue Pro Mussa Asad kuwa Prime minister au Vice President
Vyovyote iwavyo mama aachane na group za mtangulizi wake.

Wasiojulikana wameua sana. Alikuwa na wapambe wa kumpa mizuka walikuwa wanasingizia na kuwabambikia watu kesi ili awape vyeo maana ilifikia kipindi ukisingiziwa kumtukana Rais ulikuwa ni uhaini. Na hii imefanya watu wako mahabusu mbalimbali kwa kuonewa.
 
Ageni mpendwa wenu. Tulioumizwa nae tuna hangover tunaenda kuzimua mapema maana mama katoa mapumzika jumatatu.

Kubwa zaidi tarehe 25 nayo tumepewa ni siku ya bia.

Tumenyanyaswa sana yaani.

Waachieni wanaoshikiliwa magerezani haraka wakazione familia zao
Kwa akili hizi sidhani kama taifa tutatoboa. Tutabaki wa kujilinganisha kila siku.
 
Back
Top Bottom