Hahhahah sasa wewe mie mkali wa hizi kazi tokea nipo chuo kitamboo nimeivuruga sana hiyo k.koo hahah hadi leo nipo yaani na sibanduki ng'ooo inabidi tuwasaidie wenzetu bana maana haya maisha mtu akikuongezea jero kwenye product ni kubwa sanaaaa.Na hivi vyuma vimekaza acha tu na wenyewe wale.Ila si unajua mjini wasioujua bado wengi utawapata tu maana hawapo humu JF .

Ngoja niwape chimbo la pochi za bei rahisi zile ronya na za kati 6000,8000,12000 lipo maeneo ya nyamwezi karibu na soko la shimoni kale kamtaa cha kati uje utokee msimbazi kota,karibu wanapouza maturubali, lingine lipo mtaa wa congo na aggrey kwa juu ghorofani kama unataka kutoka congo kituo cha basi pale wanauza high quality PU zao 22k, 25k, 28k,3 0 nk ambazo ukikuta kwenye botique ni mwendo wa 50k,70k hadi 100k. Pia tena hiyohiyo congo/mchikichi pale katikati kwa ghorofani wanauza pochi eh bei chee tatizo lenu mnapita juu juu tu ingieni maduka ya ndani na chini yana mambo mazuri Wallet nazo mchikichi zipo za kumwaga za kiume na za kike bei chee hakikisha unaingia ndani kabisa kwenye vichochoro. Haya kwa wale wa mabegi ya kusafiria kuna mchina anazalisha mwenyewe maeneo ya Veta karibu na sofia house kule anakutengeneezea design unayotaka eh,pesa yako tu. Kuna kingine nimesahau? Danhappy
Nimekupanda bure, mimi naweza kupata wapi nguo za watoto wachanga, age 0-8yrs?
 
Ngoja nikupe machimbo best. Kizuri kula na mwenzio. Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule Mnazi Mmoja wengi wanaouza Kariakoo wanaenda kufuata huko. Viatu navyo vinapatikana huu Mtaa wa Narung'ombe na Congo pale nenda straight kwenye maduka ya Wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini, nop. Unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile vi-sandles wanauza 2500/pc. Cheni zama Mchikichi katikati kuna Mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki. Magauni nayo ingia ndanindani kule Congo na Aggrey, wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka ku-type ah!
Vp kuhusu nguo za ndani za kina mama
 
Mkuu katika kupambana na hali tunaomba chimbo LA hotbasic, manga na suruali za kiume
Machimbo ya kiume yapo mtaa wa Congo na Mchikichi na Aggrey but unatakiwa uingie kule ndani kabisa wanaita underground sio huku njenje pia Congo na narung'ombe kwa ndani kabisa underground utajionea maajabu ya viatu na pamba za ukweli..usiangalie maduka ya nje nje tu. Tena zipo nguo quality mwenyewe tu ushindwe kuchagua
Msaada kwa wenye uzoefu na vitu vya Stationary wanisaidie maana nmezoea kununua maduka ya mwanzoni mwa Mtaa wa Kongo.
Yanapatikana kule mitaa ya gerezani yanapakana na maduka ya dawa za binadam, nadhani ni Gerezani na Nyamwezi kama sijakosea mitaa vizur ukifika maeneo ya Gerezan ukimuuliza mtu anakuonyesha.
Na mwenye kujua chimbo la post cards, memory cards na frash .
Yapo Mchikichi ya Likoma karibia na Akiba Bank branch ya Kariakoo yaani memory card bei che na headphone nenda kajionee.
Nimekupanda bure, mm naweza kupata wapi nguo za watoto wachanga, age 0-8yrs?

Vp kuhusu nguo za ndani za kina mama
Yapo mtaa mmoja unaitwa Muhonda upande wa pili wa Msimbazi. Kule wanauza kila aina ya chupi ronya na quality bei zao zipo vizuri wanauza boxer soks hata hiz skintight tunazouziwa buku kumi moja zinauzwa kule kwa dz bei nzuri.
Pia mtaa wa mchikichi nao kuna wachina na wazawa wanaouza kwa bei ya jumla kwa quantity kubwa.
 
Machimbo ya kiume yapo mtaa wa Congo na mchikichi..na aggrey but unatakiwa uingie kule ndani kabisa wanaita underground sio huku njenje pia Congo na narung'ombe kwa ndani kabisa underground utajionea maajabu ya viatu na pamba za ukweli..usiangalie maduka ya nje nje tu.Tena zipo nguo quality mwenyewe tu ushindwe kuchagua

Yanapatikana kule mitaa ya gerezani yanapakana na maduka ya dawa za binadam..nadhani ni gerezani na nyamwezi kama sijakosea mitaa vizur ukifika maeneo ya gerezan ukimuuliza mtu anakuonyesha

Yapo mchikichi ya likoma karibia na Akiba Bank branch ya k.koo yaani memory card bei che na headphone nenda kajionee



Yapo mtaa mmoja unaitwa Muhonda upande wa pili wa msimbazi.kule wanauza kila aina ya chupi ronya na quality bei zao zipo vizuri wanauza boxer soks hata hiz skintight tunazouziwa buku kumi moja zinauzwa kule kwa dz bei nzuri.
Pia mtaa wa mchikichi nao kuna wachina na wazawa wanaouza kwa bei ya jumla kwa quantity kubwa.
Big up sana umekuwa msaada mkubwa sana hasa kwetu wa mikoani.
 
Msaada dada wa huko nairobi. nina mtaji wa 1000000
Inatosha inategemea style yako ya uuzaji....
Na Wale wote mliouliza kuhusu nairobi
Mzigo wa nai na k/koo ni almost the same na wanatoa copy ya nguo aina zote na bei ni ndogo kuanzia gauni jeans, skirt, mabazee na vitenge...
Hapo ukienda nai na kukusanya hizo copy kuja kuuza kwa jumla inalipa Sana hata hao wanaouza jumla k/koo wengi wao wanatoa nai
 
Mi ninachokifanya naenda nai nafunga Mzigo wangu nikifika dukani nauza jumla na reja reja bei sawa na dar nahakikisha kila pc1 inatoa efu 4 na nasafari kila wiki kwa sehemu niliyopo nategemewa na wenye maduka na wanaouza kwa kutembeza muhimu fanya utafiti wa eneo ulilopo na kujua aina ya nguo zenye mzunguko mkubwa maana biashara si kupamba duka bali bidhaa zitoke.

K/koo siku izi wanamix copy na og na wanakuuzia bei moja.. @honort hope nimekupa idea
 
Inatosha inategemea style yako ya uuzaji....
Na Wale wote mliouliza kuhusu nairobi
Mzigo wa nai na k/koo ni almost the same na wanatoa copy ya nguo aina zote na bei ni ndogo kuanzia gauni jeans, skirt, mabazee na vitenge...
Hapo ukienda nai na kukusanya hizo copy kuja kuuza kwa jumla inalipa Sana hata hao wanaouza jumla k/koo wengi wao wanatoa nai
Asante, nitakutafuta nimfungulie mama watoto duka la nguo.
 
Ngoja nikupe machimbo eh best kizuri kula na mwenzio...Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule mnazi mmoja wengi wanaouza k.koo wanaenda kufata huko, Viatu navyo vinapatikana huu mtaa wa Narung'ombe na congo pale nenda straight kwenye maduka ya wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini nop unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile visandles wanauza 2500/pc. Cheni zama mchikichi katikati kuna mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki.Magauni nayo ingia ndanindani kule congo na aggrey wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka kutype ah.

zamani nilikuwa nafata vitu kariakoo ila siku hizi ukiingia huko kweupo kabisa

asante kwa feedback
 
Ngoja nikupe machimbo eh best kizuri kula na mwenzio...Vitenge mara nyingi machimbo yake yapo NIDA kule mnazi mmoja wengi wanaouza k.koo wanaenda kufata huko, Viatu navyo vinapatikana huu mtaa wa Narung'ombe na congo pale nenda straight kwenye maduka ya wachina yaani sio wale machinga wanaomwaga chini nop unazama dukani utakuta zile simple wanauza 4000/pc na vile visandles wanauza 2500/pc. Cheni zama mchikichi katikati kuna mchina anauza mpaka 2000-3000/dz na hazipauki.Magauni nayo ingia ndanindani kule congo na aggrey wanauza nayo bei chee 6000-8000-1000-16000/pc. Vingine siku ingine nitakwambia nimechoka kutype ah.
Madera VP mkuu?
 
Naona umeamua kumwaga UPUPU wote, maana yake kila mmoja aelekee straight kwa Mchina (muuzaji)...!!

Unataka/unategemea sisi Madalali tukale wapi..! anyway, najua tumefanya makosa sisi wenyewe kukupeleka kwenye Machimbo...

Naahidi atutarudia tena kufanya Makosa..!!
Ehhhh una roho mbaya riziki haizuiwi usiwe mchoyo Wa hivi
 
Back
Top Bottom