Hii ni tahadhari kwa vijana kuhusu uhalisia wa biashara, si kuwakatisha tamaa wala kuwaambia waajiriwe. Biashara ni njia nzuri, imetajirisha watu lakini si hadithi ya kupendeza kama inavyochorwa mitandaoni. Biashara ni vita, inahitaji akili, mikakati madhubuti, uwezo wa kujifunza kila siku, uvumilivu wa hali ya juu na nidhamu isiyotetereka.
Wakati kijana anapofikiria kuingia kwenye biashara, mara nyingi picha anayojenga akilini ni hii:
Lakini kwa uhalisia wa Tanzania, Wafanyabiashara wanaoishi maisha hayo ni asilimia ndogo mno na hata ndani ya aina za biashara wanazofanya, wao ni kundi dogo (cartel)
Wafanyabiashara wakubwa katika maeneo mengi ni walafi wa kiwango cha juu, Hawatosheki kamwe ! kila siku ni mipango ya kuzoa wateja wengi hata wa yule mdogo asiye na uwezo wa kujitetea iwe rushwa, ushawishi wa connections, discounts, n.k. Kwao, mfanyabiashara mdogo anaewakaribia ni adui wa lazima kuangamizwa mapema lasivyo anaweza kuwaibia wateja wao. Kwa nchi zilizoendelea wafanyabiashara wakubwa wamedhibitiwa kucheza rafu kwa pesa na connections walizonazo.
Takribani 90% ya wafanyabiashara kwa kipindi cha miaka 20 wamepitia au wanapitia changamoto hizi:
Wakati kijana anapofikiria kuingia kwenye biashara, mara nyingi picha anayojenga akilini ni hii:
- Kwenda ofisini siku yoyote apendayo, muda anaoamua mwenyewe
- Kuwa bosi / ceo wa biashara yake.
- Kusafiri kwenda vacations
- Kuendesha gari la kifahari
- Kuishi kwenye nyumba nzuri ya ndoto
Lakini kwa uhalisia wa Tanzania, Wafanyabiashara wanaoishi maisha hayo ni asilimia ndogo mno na hata ndani ya aina za biashara wanazofanya, wao ni kundi dogo (cartel)
Wafanyabiashara wakubwa katika maeneo mengi ni walafi wa kiwango cha juu, Hawatosheki kamwe ! kila siku ni mipango ya kuzoa wateja wengi hata wa yule mdogo asiye na uwezo wa kujitetea iwe rushwa, ushawishi wa connections, discounts, n.k. Kwao, mfanyabiashara mdogo anaewakaribia ni adui wa lazima kuangamizwa mapema lasivyo anaweza kuwaibia wateja wao. Kwa nchi zilizoendelea wafanyabiashara wakubwa wamedhibitiwa kucheza rafu kwa pesa na connections walizonazo.
Takribani 90% ya wafanyabiashara kwa kipindi cha miaka 20 wamepitia au wanapitia changamoto hizi:
- Kuishi na msongo wa mawazo kutokana na madeni yasiyokwisha
- Kuamka kila siku alfajiri na kurudi usiku.
- Kufilisika na kufunga biashara
- kuambulia patupu siku nzima
- Kukimbizana na kodi na tozo zisizotabirika wala zenye miongozo ya kueleweka
- Kukosa uhakika wa mapato, faida au hata wateja wa kudumu
- Kukosa muda wa kupumzika, maisha ya familia au kujitunza kiafya
- Kwenda kwa waganga mambo yakiwa magumu (mtashangaa lakini ndio wateja wakubwa)
- Sheria
- Masoko
- Mikopo
- Uendeshaji
- Teknolojia
- Mauzo
- Uhasibu
- Ubora nk