Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,445
7,816
Naibu Spika akiongea katika hafla ya kuwaapisha mawaziri, manaibu na viongozi wengine, amewapongeza wote walioteuliwa na kuwashauri wameteuliwa kufanya kazi za Rais nao wao wanamsaidia hivyo wazifanye kama wasaidizi wa Rais wa Jamhuri wa Muungano na si vinginevyo. Kuhusu Bunge, amesema kuna watu wanahisi kazi ya Bunge kila wakati ni kukosoa pekee. Amesema uko wakati Bunge linaishauri Serikali, kuna wakati linatunga sheria pia uko wakati Bunge linaisimamia Serikali.

Tulia amesema katika kipindi cha awamu ya sita imekuwa ikiwasikiliza ushauri wa wabunge na imekuwa ikizifanyia kazi.

Kwa muktadha huo, Tulia amesema Bunge liko tayari kushirikiana na awamu ya sita kwa mambo yote ambayo itayaleta bungeni ili wasimamie Serikali.

Naibu Spika amesema pale ambapo wanahitaji kukosoa Serikali wataikosoa kwa heshma na kwa muktadha ambao katiba inaruhusu kufanya hivyo, kwenye kushauri watashauri na si lazima Serikali kufata ushauri wa Bunge lakini katiba imetoa nafasi ya Bunge kuisimamia Serikali na kupata fursa ya kuiuliza Serikali walifanyia ushauri gani.

''Mihimili yote ina kazi zake na hapo mheshimiwa Rais nisisitize jambo moja maana kunakuwa na upotoshaji, Rais ni mkuu wa nchi, wapo watu wanachukua hiyo sehemu inayosema Rais ni kiongozi wa Serikali lakini Rais ana mambo yote, ni mkuu wa nchi, ni kiongozi wa Serikali, ni amiri Jeshi mkuu wa nchi hii.

Naamini kwa ufafanuzi huu watu watafahamu kwamba Rais wa Jamhuri wa muungano wa Tanzania, mheshimiwa Samia Suluhu Hassan sio tu kiongozi wa Serikali lakini ni mkuu wa nchi kwa hiyo yeye uongozi wake hauko sawasawa yeyote wa mhimili wowote ulioko hapa nchini"


Alisema Naibu spika, Tulia Ackson
 
Hata mimi nimemsikia. Kwa kifupi, huyu hata Ndugai atakuwa na nafuu.

Kaongea alichongea ili kumfurahisha Mama ampe uspika, na akiupata, atakuwa ni bora Ndugai.

Wabunge kama mko makini, huyu msimpe uspika ingawa sioni uwezekano wa nyinyi kupinga chaguo la Raisi(Mwenyekiti wa CCM) ni nani awe spika.

Kwa sasa Mama anaweka Spika wake (atakaeilinda serikali yake Bungeni) na baadae ataweka Waziri Mkuu wake.

Tukio la Ndugai kushinikizwa kujiuzulu ni ushahidi tosha wa hii katiba mbovu tulioanayo(Mungu ana makusudi kwa kila jambo).

Hata hivyo, nafurahi Ndugai kaonja machungu ya hii katiba mbovu, na ipo siku CCM kama chaka watakuja kujutia hii katiba.
 
Kumbukeni Huyu mama ni mwanasheria kabisa, pale Leo anapokuja na kusema kuwa Rais wa Tanzania ndo Muhimili mkubwa wa mihimili yote iliyoopo, hiyo ipo kwenye ibara gani ya katiba yetu au ni kujipendekeza kumezidi? Hebu wanasheria twambieni kama kuna Kifungu kama hicho kwenye katiba yetu
 
Naibu Spika akiongea katika hafla ya kuwaapisha mawaziri, manaibu na viongozi wengine, amewapongeza wote walioteuliwa na kuwashauri kuwa ni kazi za Rais nao wanamsaidia hivyo wazifanye kama kazi zake na si vinginevyo. Kuhusu Bunge, amesema kuna watu wanahisi kazi ya Bunge ni kukosoa pekee.

Tulia amesema Bunge liko tayari kushirikia na Serikali katika kutimiza majukumu yake, ikifika sehemu ya kushauri watashauri na si lazma Serikali kufata ushauri lakini wataisimamia.

Tulia amesema Rais ni mkuu wa nchi, ana mambo yote.
Mkuu umeniwahi Kuweka Uzi na Mimi imenishangaza
 
Kumbukeni Huyu mama ni mwanasheria kabisa, pale Leo anapokuja na kusema kuwa Rais wa Tanzania ndo Muhimili mkubwa wa mihimili yote iliyoopo, hiyo ipo kwenye ibara gani ya katiba yetu au ni kujipendekeza kumezidi? Hebu wanasheria twambieni kama kuna Kifungu kama hicho kwenye katiba yetu
Faida za elimu ya jalalani hio.
 
Back
Top Bottom