Wenzetu maswahaba walipokuwa wanaagana baada ya mazungumzo yao,walikuwa wanapeana nasaha kwa kusomeana suratil al asir ndio kisha wanaagana
Sura hii inazungumzia kwamba hakika wanadamu wote haijalishi waislamu au wasio waislamu,kuanzia baba yetu Adamu mpaka Mtume wa mwisho Muhammad swalla lahhu alaihy wa salaam, wote wapo katika hasara
Isipokuwa wale waliomwamini Allah kwa maana Mungu mmoja, kisha wakafanya mambo mema kwa maana matendo mema,kisha wakahusiana kuhusu mambo ya haki,kwa maana haki ya kumjua Allah, kukijua kitabu cha Allah na kujua mafundisho sahihi ya mtume Muhammad
Kisha wakahusiana juu ya kusubiri,hakika subira ni ibada kubwa sana,maana uwe na subira ya kuacha maovu uliyoyazoea na uwe na subira na kudumu kufanya mambo mema,maana hakika kudumu kufanya ibada za Allah ni mtihani mkubwa sana
Hawa ndio ambao hawapo katika hasara yani wamesamilika
Je sisi tupo upande upi? Tujitathimini na kufanya yale yenye kutupa mwisho mwema