Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358

Rais Samia akihutubia wakati wa uapisho wa viongozi, akizungumzia kuhusu Wizara mpya ya Mipango na Uwekezaji ameonesha namna ya kuweza kuzitambua fursa mbalimbali na kuzifanyia kazi kama nchi ili zisipotee.

Akitolea mfano sakata la sasa la fursa ya uwekezaji kwenye bandari zetu amesema haya, nanukuu

Nataka niseme vizuri hili suala la fursa na watu wanavyozitumia. Ndugu zangu wakati sisi tunalumbana bandari yetu apewe nani, iende isiende, ikae, ivue, isivue, wenzetu kwa kuona malumbano yetu mmeona wame-jump wamekwenda kulekule, na lile jumba lililowekwa bendera ya Tanzania, limewekwa bendera ya jirani.

Sasa Tanzania tumeuza, wale jirani wamekimbilia kule kufanya nini?

Na siku ambayo Bunge letu hapa lilisema kwamba ni ruhusa bandari yetu iendeshwe na Serikali na sekta binafsi, siku ya pili wenzetu wakasema ninyi moja? Sisi zote zilizoko huku ziende private sector na wakakimbilia kwenda kule kwenda kuwahi nafasi. Kama wale wanalumbana, njooni huku.

Sasa muone jinsi fursa zinavyokuja na kukimbia haraka haraka na jinsi wengine wanavyoweza kuzitumia haraka haraka.


Nimesema tu nitoe mfano huo kuona changamoto na jinsi ya kupata fursa kuzitumia na kuzifanya zisiponyoke.
 
Kwa hiyo tunatoa bandari zetu kwa bendera yetu kupata nafasi ya kupeperushwa kwenye jumba refu tu? Au kwa vile tunakimbizana na jirani badala ya maslahi mapana kwa vizazi vijavyo?

Nasema vizazi vijana maana kwa upande wa maslahi ya taifa tayari viongozi wetu mmetufelisha sana tangu kitambo, tazama leo ni zaidi ya miaka 60 ya uhuru lakin bado tunakimbizana na ukosefu wa maji salama hadi katika makao makuu ya nchi mbali na huko vijijini ambako bado tunakunywa maji pamoja na mifugo
 
Mungu wa Mbinguni asaidie Taifa letu na Viongozi wake. Kwamba Tanzania imefikia mahali tunatishiwa kwa bendera ya nchi jirani kupeperushwa kwenye jengo refu kuliko yote duniani.

Hii ni Tanzania iliyo na historia ya kuongoza mapambano ya ukombozi wa nchi za Afrika kusini mwa jangwa la Sahara ama?

Tanzania tunatakiwa Bandari yetu iwe mshindani wa Bandari ya Dubai na hizi za nchi za jirani wala si vinginevyo.

Hatuwezi kuwa wa shindani wa bandari ya Dubai kama watatuendesha wao tutaishia kubemendwa.

Huo ndio ukweli mchungu na mkataba wa makubaliano ya awali unaonesha hivyo.
 
Mombasa, Kenya

Advocate Murshid Abdallah Mohammed wa Mvita, Kenya, Wafanyabiashara, makuli wapinga uwekezaji wa DP World nchini Kenya kwa sababu zifuatazo:

PRESS RELEASE OBJECTING TO GIVING KENYA´S PORTS TO UAE DP WORLD



Jirani hapo Kenya wadau wa pwani na Kenya nzima waitisha press conference kupinga hatua za serikali kutaka kubinafsisha bandari ambazo ni mali ya umma, usalama wa taifa, sababu wananchi hawajashirikishwa, uchumi wa buluu kuathiriwa, bandari kavu kuhamishwa .....

Mr. Murshid Abdallah Mohamed. Biography : NPSC (National Police Service commission) Commissioner. Advocate of the High Court, former Commissioner, Boundaries IEBC Kenya ...


More info :
Nairobi, Kenya
Serikali ya Kenya yaruka kimanga, ahadi ilizotoa kwa Dubai kuhusu bandari

Kenya disowns port deal promises made to Dubai​

Friday July 22 2022​


DP World said the Kenyan government had promised to issue a request for a commercial proposal for the port deals before the election.

66884454-5477-40E7-9985-C0653ED10125.jpeg

Kenya had agreed to offer preference to DP World, owned by the government of Dubai and one of the world’s largest port operators, in a deal inked between the two States.

DP World said the Kenyan government had promised to issue a request for a commercial proposal for the port deals before the August 9 General Election.

Under the deal, DP World was to deploy its money to build three berths at the Mombasa port, develop cold storage supply chains in Kisumu and Naivasha and to build a special economic zone in Lamu.

The Dubai firm was to submit a commercial proposal to equip and operate the three completed berths in Lamu.

Kenya has however disowned promises of the tender made to Dubai Port (DP) World that would have allowed the UAE-based firm to offer a bid for development, operation and management of the country’s four ports.The Treasury has disowned the existence of such a deal and denied ever mentioning plans to issue a tender by July.

It was a ‘government-to-government’ agreement signed proposing to DP world to take part in the process. It was an agreement to explore how DP World can provide gateways into the country and the hinterland. Kenya Treasury CS Ukur Yatani has denied the deal.

When requested comments on whether the request for proposal (RFP) will be issued this month, Treasury Cabinet Secretary Ukur Yatani replied “No,” via text without offering any explanations.

Typically once an RFP is issued bidders are given weeks to fill and submit bids outlining the amount of investment required, financing options and a feasibility study which could take months.

DP World first entered the fray in Kenya in 2014 when the government floated an international competitive tender to concession the second container terminal in Mombasa. Port operators from China, Japan, Singapore, Netherlands and several other countries participated in the tender.

The Chinese group, PSA International, which had partnered with a local firm, Multiple Hauliers, had the highest marks, with DP World emerging second but was to secure the tender through backdoor like it had done in other countries before.

The process was then cancelled amid political undercurrents. The Treasury Cabinet Secretary previously confirmed that DP World were among many port operators being explored by the government as potential private partners to run the new Lamu Port
 
Rais Samia akihutubia wakati wa uapisho wa viongozi, akizungumzia kuhusu Wizara mpya ya Mipango na Uwekezaji ameonesha namna ya kuweza kuzitambua fursa mbalimbali na kuzifanyia kazi kama nchi ili zisipotee.

Akitolea mfano sakata la sasa la fursa ya uwekezaji kwenye bandari zetu amesema haya, nanukuu

Ndugu zangu wakati sisi tunalumbana bandari yetu apewe nani, wenzetu kwa kuona malumbano yetu wame-jump wameenda kulekule, na lile jumba lililowekwa bendera ya Tanzania, limewekwa bendera ya jirani.

Sasa Tanzania tumeuza, sasa wale majirani wamekimbilia kule kufanya nini?

Na siku ambayo Bunge letu hapa lilisema kwamba ni ruhusa bandari yetu iendeshwe na Serikali na sekta binafsi, siku ya pili wenzetu wakasema ninyi moja? Sisi zote zilizoko huku ziende private sector na wakakimbilia kwenda kule kwenda kuwahi nafasi. Kama wale wanalumbana, njooni huku.

Sasa muone jinsi fursa zinavyokuja na kukimbia harakaharaka na jinsi wengine wanavyoweza kuzitumia haraka haraka.


Nimesema tu nitoe mfano huo kuona changamoto na jinsi ya kupata fursa kuzitumia na kuzifanya zisipotee.

Huyu mama uyu, why unasaini mkataba kimia kimia, ajipange hii ngoma nzito sana
 
Back
Top Bottom