Rais Samia azindua ugawaji wa vitendea kazi kwa maafisa ugani kilimo. Asema Serikali imeongeza bajeti ya utafiti kutoka Tsh 7.35bn hadi 11bn

Ni utaratibu mzuri kwa wakulima watakao kuwa serious, hii itasaidia commercial farms nyingi kuanzishwa maana capital is everything kwenye hizi farms, lakini sheria za ardhi na serikali kuingilia ingilia wakulima especially kwenye bei na mauzo ya mavuno yao inaweza kuwa issue, kazi bado anayo kama anataka mapinduzi ya kweli lakini mwanzo mzuri
 
Msoga wasipomzonga naona ni mmoja wa vijana wenye nia njema na nchi hii...anajua anachokifanya... hongera kwa JPM kuibua kipaji.
Bashe hajaibuliwa na marehemu wenu tafuteni sehemu nyingine ya kujiliwaza.

Bashe anajurikana kitambo kama yuko vizuri upstairs, labda umtaje Rostam Aziz ndiye aliyemuibuwa unaweza kueleweka, lakini kwakuwa upo kundi lile la washamba huwezi kulijuwa hili.
 
Bashe yuko vizuri.
qRI8Gs7.gif
 
Nani kama Mama
Hongera Mama na Bashe

Mkirudisha na ruzuku na kujazia nguvu umwagiliaji throughout the year tutashinda

Masoko pia yatafutwe
 
Kuijali kwa maneno tu.
Mara zote amekua akiambia kuwa Bei ya pembejeo imepanda Mara 3 wanaomba ashughulikie, lakini kimya. Leo anakuja na hili. Alipaswa aanze na pembejeo.
Sasa uniform za afisa ugani kwa sasa za nn? Kama mkulima kashindwa kununua pembejeo sababu ya Bei kubwa hizo uniform kazi yake inakua nn?
Tatizo mfumo wa ruzuku unahujumiwa kwa viwango vya kutisha
 
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

View attachment 2175655
Bashe is good.Ila nashauri kwa mara nyingine tena yafuatayo:
1.Maafisa Ugani wawe na weledi unaotakiwa.Wengi wanaogopa kwenda kwa wakulima because they are incompetent.
2.Ihakikishwe kwamba vyombo vyao vya usafiri vipo up and running wakati wote.Kwa hiyo wapewe posho ya mafuta na service inayo tosheleza haja.
3.Hela ya kutosha kwa ajili ya mashamba darasa ijumlishe pia vifaa kama pesticides,sprayers,mbolea nk.
4.Hizo pikipiki baada ya miaka miwili,wapewe ziwe zao,ila waendelee kupata posho ya mafuta na service,in that way watazitunza.Wasainishwe mkataba unaoainisha hili.
5.Nashauri mishahara yao iongezwe,ili kushawizi brains kuingia huko.
6.Mwisho nashauri pia vijana waliofaulu vizuri ndio wachaguliwe ku-pursue course ya Kilimo.

Otherwise hongera sana Bashe,viatu vimekutosha.
 
Daa, haki ya nani, sasa mkuu samia anahusikaje hapo wakati hata huyo bashe ni zao la Magu?
Weee Magu alimzaa Bashe au sio? Kwa hiyo Bashe alikuwa minister wa kilimo enzi za mwendazake au sio?

Kwa akili yako mbovu,Baraza la Mawaziri la Samia na Mwendazake lipi unaona linakuja na majibu ya kero za Wananchi?

Mtwana akifanya vizuri sifa ni za mfalme.

Ukweli unaujua ila chuki zinakuhangaisha.

Hakunaga Rais mtaalamu wa kilimo,injinia,mwanasheria, IGP nk kama yule mjinga alivyowaaminisha wapuuzi kama wewe.
 
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

View attachment 2175655
Labda mapinduzi ya Kilimo CHUMBANI KWAKE
 
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

View attachment 2175655
Labda mapinduzi ya Kilimo CHUMBANI KWAKE huko.

Hakuna nchi yoyote ile Duniani iliyowahi kufanya Mapinduzi ya Kilimo kwa Bajeti ya $ 40M. Hizo fedha ni Sawa na Bajeti ya Shule ya Msingi hapo SOUTH AFRICA TU.
 
Back
Top Bottom