Rais Samia azindua ugawaji wa vitendea kazi kwa maafisa ugani kilimo. Asema Serikali imeongeza bajeti ya utafiti kutoka Tsh 7.35bn hadi 11bn

Rais Samia Suluhu Hassan anazindua Ugawaji wa Vitendea kazi kwa Maafisa Ugani nchini ikiwemo Pikipiki 2,000, Vifaa vya Kupima afya ya Udongo (Soil agro scanner) 143, simu janja 384 na visanduku vya ufundi vya Maafisa Ugani 3,400.

#TunaImaninaSamia
#Hakunakinachosimama
#KaziInaendelea.

------

HOTUBA YA RAIS SAMIA SULUHU HASSAN (KWA UFUPI)
Tuliyoyapata mwaka huu ni mafanikio yaliyopatikana baada ya kuweka nguvu katika maeneo mbalimbali kwenye kilimo.

Tumeongeza bajeti ya utafiti kutoka shilingi bilioni 7.35 hadi bilioni 11, nimeyafanya haya kama muumini wa kilimo na nikiamini kitatusaidia kupiga hatua.

Tumefanikisha kufungua masoko ya mazao mbalimbali ikiwemo zao la Parachichi katika nchi za India na Afrika Kusini na hii ni baada ya kukidhi viwango vya ubora.

Mchele wetu sasa unaliwa Ulaya, leo ukienda katika supermarket za Ubelgiji na Ufaransa utaukuta mchele kutoka Tanzania, wameanza kidogo kidogo na wamewezeshwa na benki zetu.

Tumeweza kufanikisha kupatikana kwa ithibati ya ubora yenye viwango vya kimataifa kwa maabara zetu za mimea na viuatilifu.

Kiwanda cha kuchakata tumbaku mjini Morogoro tunakwenda kukifungua, na hii inatokana na uzalishaji wa tumbaku kuongezeka.

Serikali inaendelea kuimarisha huduma za ugani, tunakwenda kugawa pikipiki 6700 leo, na pikipiki 300 tulishagawa hapo kabla na kufanya jumla ya pikipiki tutakazogawa kuwa 7000.

Nimeridhia ombi la maafisa ugani la kumilikishwa moja kwa moja pikipiki watakazopewa baada ya kuzitumia kwa miaka miwili na hii itaenda sambamba na masharti tutakayoyaweka.

Leo tutagawa pia vipima afya ya udongo katika halmshauri 143, tunafahamu kuwa ukiwa na afya njema utazalisha zaidi, hivyo hivyo na kwenye udongo.


Janga la Uviko-19 limebadilisha mwelekeo wa uchumi duniani na kufanya hata mazao ya biashara na yasiyo ya biashara yote kuwa ni mazao ya biashara.

Niwaombe sana vijana wa Tanzania kuingia katika sekta ya kilimo, hamtajuta. Mtatengeneza fedha nyingi za halali.

Wizara ya Kilimo ihakikishe huduma ya upimaji wa udongo inakua, kwa muda mrefu udongo wetu umetumika kwa muda mrefu sasa ipatikane tiba.

Tuanzishe mifuko ya mzunguko (Revolving Fund) ya pembejeo na maendeleo ya kilimo, pale tunapopata shida katika kupata pembejeo na pembejeo kupanda bei mfuko huu ukashushe bei ili wakulima wetu wasiumie.

Nitoe wito kwa maafisa ugani, vifaa mlivyokabidhiwa ikiwemo pikipiki mvitunze na mkavitumie kwa kazi zilizokusudiwa.

Nawaombeni sana wabunge, tuibebeni sana sekta ya kilimo, kwa kauli moja muipitishe ili yale tuliyoyapanga yaende kutekelezwa.

Tunakoelekea sasa ni kwenye kilimo cha kisasa, kuongeza uzalishaji wa mazao yetu, kufanya kilimo biashara na ndio maana tunajielekeza kujenga maghala na kufungua masoko mapya.

Sekta ya Kilimo imeendelea kuwa muhimili muhimu katika taifa letu na kuchangia maendeleo. Sekta ya Kilimo imetoa ajira kwa asilimia 61 ya watu wote na pia asilimia 65 ya malighafi lakini pia ni sekta inayofanya tujitosheleze kwa chakula.


HOTUBA YA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA (KWA UFUPI)
Wakati wote Rais anaposimama mbele ya jukwaa na kuwahutubia Watanzania, msisitizo wake ni kuhakikisha tunajikita katika kuboresha uchumi wetu wa ndani na katika sekta mbalimbali, sekta ya kilimo ikiwemo.

Nataka niwape siri, Rais wetu Samia Suluhu alitoa maelekezo kwa Serikali. Na mimi ndiye ninababe maelekezo yote ya serikali na kuhakikisha kuwa wakulima wanalima kilimo chenye ticha ili kiwasaidie Watanzania.


HOTUBA YA WAZIRI BASHE(KWA UFUPI)
Sekta ya kilimo haiwezi kubadilika bila kuchukua mabadiliko kwenye mambo ya msingi, kilimo ni biashara. Sekta hii inachangia wastani wa 25% hadi 27% ya pato la Taifa.

Kwa muda mrefu Mhe. Rais sekta hii imekuwa haikui kwa muda mrefu, biashara ya kilimo katika soko la Afrika inatarajiwa kuwa na dola trilioni moja ikifika mwaka 2030. Sisi kama Tanzania tunatakiwa kunufaika na biashara hii.

Mhe. Rais, tija ina fomula yake. Tija inahitaji mbegu bora, ticha inahitaji viwatilifu. Na leo utafanya zoezi moja, la kugawa pikipiki kwa maafisa ugani 7000 wa nchi nzima kama vitendea kazi.

"Sasa Mhe. Rais, Afisa ugani kwenye pikipiki yake atakuwa na Soil Scanner, atakuwa na uniform maalum ya kumtambulisha kama ilivyo kwa daktari. Na Wizara tutatenga bajeti ya uniform mbili kwa kila afisa ugani kwa mwaka.
Mhe. Rais sasa ninakuomba kama ikikupendeza, ninaomba baada ya maafisa ugani kuzitunza na kutumia pikipiki hizi kwa muda wa miaka miwili, basi ziwe za kwao. Hii itakuwa ni motisha kwao.

Lazima tuwe na kanda za kilimo kwenye nchi yetu, haiwezekani korosho inalimwa kuanzia Tandahimba hadi Uvinza. Hailipi, lazima tutengeneze kanda za uzalishaji.

Lakini Mhe. Rais na mimi nataka niseme bila unafiki, kabisa. Nimekuwa mbunge tangu 2015, nimesikiliza hotuba tatu za Marais, wewe ni Rais pekee uliyeipatia nafasi sekta ya kilimo.

Rais, mahitaji ya mafuta ya kula nchini ni wastani wa tani laki sita na nusu kwa mwaka, uzalishaji wetu wa ndani hauzidi laki mbili na arobaini kwa mwaka, tuna tofauti ya karibu laki nne.

Mama nasisitiza, maugani hawa wakiupiga mwingi baada ya miaka miwili pikipiki hizi tuwaachie ziwe mali yao.
Hotuba haijanoga kabisa. Hajamuongelea Simba wa Yuda?
 
Kila kitu nyuma yake kuna kutafuta kura
Kama isingekuwa hivyo hizo mbinu zinsingetumika kabisa maana zilishatumika now and then na hakuna matokeo...Hiyo ni kulambisha watoto pipi huku njaa ikiwamaliza; ni mbaya, ni hasara kwa taifa...Tuweke katiba mpya ili haya maamuzi yawe kwenye level ya kijiji na siyo watu wachache kuamua kwaajili ya wengi
 
Umesema sawa na mm nilivyosema/nilichotaka kusema
Sababu ya wafanyabiashara wakubwa mojawapo kushindwa ni operations cost, Kama alihitaji kutumia bil 1 kununua pembejeo, Sasa hivi atahitaji bil 3.
Hawa wafanyabiashara wakubwa waliowekeza kwenye kilimo Wana maafisa ugani wao, serikali ilipaswa kwa Sasa kuwapunguzia Bei ya pembejeo tu. Hayo mengine ndio yangefuata
Lakini pia yeye ana invest sana wakati wakuliman wadogo ambao wako wengi wanalima bila kutumia cash na investiments zao ni labour tu kisha wanauza soko lile lile analouza huyo mkulima aliye invest unadhani ata break even? Unless awe na political position auze ghala la taifa na hapo ndipo tunapodanganyana eti tunasaidia wakulima, how wakati vitu vipo obvious na watu hawataki kubadili chochote?
 
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

FPgfM9bX0AE0tfC.jpg
 
Kijana anajituma sana, aendelee kuchapa kazi aachane na akili za siasa chafu zilizozagaa kila mahala Tanzania.... Taifa bado lina hadhina ya watu Bashe yuko vizuri, kuna yule kijana Bashungwa yuko vizuri, Biteko akiacha yale mambo yake akafocus kazi yuko vizuri, Makamba junior yuko vizuri, Riz 1 yuko vizuri, yule kijana kutoka CDM wa Tunduma yuko vizuri, ...Taifa lina hazina ya vijana SHIDA SIASA CHAFU..

Jafo hatufai Mama piga chini yule Mzaramo..
 
S
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

Shamba darasa lilishashindwa kabisa. Nafurahi ubunifu wake lakini aachane na shamba darasa. Nashangaa sana watalaam wa wizara ya kilimo kupendekeza mkakati wa shamba darasa. Na declare interest, Mimi ni mtalaamu wa kilimo na mtafiti.
 
Dodoma.
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kumpatia Sh150 bilioni ili aziweke katika benki za biashara kama dhamana (security), hatua itakayowezesha wakulima nchini kuanza kupata ruzuku ya mbolea katika msimu wa kilimo ujayo.

Bashe ameomba fedha hizo leo Jumatatu Aprili 4, 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa ugawaji wa vitendea kazi kwa maofisa ugani nchini.

Bashe amesema bei ya mbolea katika soko la dunia imepanda kwa zaidi asilimia 300.

Amesema Rais Samia aliielekeza Benki Kuu (BoT) kutenga Sh1 trilioni kwa ajili ya sekta ya kilimo na kumuomba Sh150 bilioni kwa ajili ya kuweka katika benki za biashara kama security.

Amesema hatua hiyo itawezesha kuaanza kutoa ruzuku ya mbolea katika msimu ujao wa kilimo.

“Nakuhakikishia mheshimiwa Rais fedha hii haitapotea. Tumeshafanya hivi katika korosho kwa kugawa ruzuku ya pembeje na tumeongeza uzalishaji tani 40,000,”amesema.


Aidha, Bashe amesema jumla ya maofisa ugani 7,000 watagawiwa pikipiki na vifaa vya kupimia udongo.

“Tumeanza kuwapa elimu maofisa ugani kulingana ekolojia ya maeneo na mazao yanayozalishwa na tutawapa ekari moja kwa kila ofisa ugani, atapewa mbegu bora na mbolea ili akiwafundisha awapeleke shambani,”amesema.

Amesema kuwa majaribio yameanza katika mikoa mitatu ya Dodoma, Singida na Simiyu kwa kutenga mashamba 600 ambapo kila kijiji kitakuwa na shamba darasa ili wakulima wapate elimu stahiki.

Pia amesema maofisa ugani hao watapatiwa vifaa vya kupimia udongo na kwamba hapo mwanzo taarifa za udongo zilikuwa zinapatikana kama za uganga wa kienyeji.

Bashe amesema lengo hadi kufikia mwaka 2025 kila kata iwe na kipimia udongo chake ambapo mkulima atapimiwa udongo na kupewa cheti ambacho kitakuwa na taarifa zote za afya ya udongo wake na aina ya virutubisho vinavyotakiwa.

View attachment 2175655
Watakubali tuu kwamba Samia ni akili hadi kufikia 2025
 
Back
Top Bottom