- Thread starter
- #1,701
Vionjo vya Arsis 4 Kumwokoa Msukule Unguja 1 .
kama nilivyoahidi. Hiki kisa ni cha kusikitisha sana. Hii dunia ina hatari, kisa hiki kimetokea kama miaka 16 iliopita.
Siku hio mamangu mzazi alikwenda Zanzibar na wenzake kundi zima, waliletewa habari usiku, kua kuna binti kigori kafa ghafla baad ya kuumwa kuchqa kwa muda mfupi.
Kuna rafiki ya mamangu mzazi kaolewa kwenye ukoo huo na mjomba wa huyo binti, alipopata habari usiku huohuo akawajulisha habari ya kifo watu wa karibu, ikabidi mamangu na rafiki zake wengine wandoke nae alfajiri kuwahi maziko, waliondoka wao na ndege ndogo ya kukodisha, wengine kundi kubwa walienda na boti za asubuhi.
Walipofika Unguja wakaenda moja kwa moja wakaenda mpaka nyumba ya msiba wakawa ni kama wametokea palepale Unguja tu, watu wanajazana na wao wapo hapo. Kikatokea kitu cha ajabu sana, lakini Mwenyezi Mungu akitaka jambo lake liwe hakuna wakulizuwia. Kuna mama mmoja mtu mzima aliyekuja masibani akamwita mama mzazi wa yule binti aliyefariki pembeni. Akamwambia.
Mtu mzima; Mama pole sana, lakini nakuomba msihimize kumuosha huyu mtoto, mimi naona kama kuna mchezo umefanyika hapa, mbona hio sio maiti hapo? Usimwambie mtu, fanya hima na mimi kuna mazee namjua nakwenda kumwambia yupo ng'ambo. Yule bibi akatoka. Yule mama akabaki analia kwa kwikwi. Watu wanafanya maandalizi aoshwe, yule mama akamwita yule wifi yake amabae ni rafiki wa mamangu pia akamweleza alivyoambiwa na yule bibi, akamsisitiza asiseme kwa mtu yeyote wa pale, lakini maiti isioshwe mpaka yule bibi arudi.
Yule rafiki wa mamangu akmatonya mamangu, mamangu, unajua mambo ya wanawake tena, akatoka nje akampigia simu babu yangu tanga, saa hio hio. Babu yangu akmwabia nipe nusu saa nitakupigia. Babu akafanya mamboi yake akanipigia simu, kama saa tano hivi akanieleza alivyopigiwa simu, akanambia fanya hima uende Unguja lakinimwite Arsis uongee nae hili jambo.
Mimi kwa msisitizo wa babu na mamangu yuko kule nikamwita Arsis, ikaja sauti yake tu kama kawaida, akanambia usiwe na waiwasi, sisi na majeshi yapo kule. Wewe nenda kesho mpema usiende leo. Leo usiku tuonane pale mlangoni. Sehemu yetu ya kukutania Arsis alikua aniita mlangoni.
Mimi: Nikamwambia sawa lakini roho hainipi. Nikarudi nyumbani nikaingia ofisini kwangu, nikamwita Jini 1. Hakuchelewa akaja, live, tukasalimiana pale.
Jini1; Mbona una wasiwasi, mambo yapo vizuri.
Mimi; Najua mpaka sasa unafahamu kinachoendelea. Arsis kanambia nisiende leo kwanini?
Jini1; Tena babu yako kishaongea nao Unguja huko, kawaambia waoshe wazike tu leo hii, kama kawaida, wafanye kama hawajui kitu.Yule mama kazuiliwa hukohuko kwa mganahga wake asirudi mazikoni na mganga wake. Kwa hio huko mambo yanaendelea kama kawaoida na leo saa 10 wanazika, mpaka kaburi limeshachimbwa maiti imeshaoshwa watu wapo kama kawaida.
Mimi: Na huyo binti vipi?
Binti: Yupo palepalee kwao kafichw kichawi, hakuna anaemuona lakini yeye anaona kila kitu, leo watakuja kumchukua usiku sana kabla ya alfajiri, ndio watafatwa washikwe wpoyte ili huo ufisadi ukomeshwe, si unajua mambo ya Arsis?
Mimi; Sasa mi si niende leo?
Jini1; Wewe ukienda leo unaweza ukapatwa na hasira utaona kinachoendelea, tuwachie sisi tupo huko, hivi mama yupo huko, Bakora yupo huko na mimi nilikua huko msibani. Niwache niende, wewe mapema sana nenda usiwe na shaka kazi zitakungoja wewe, hakuna wa kuifanya hii kazi kabla wewqe hujafika, kunamajeshi huko si mchezo. Arsis anasisitiza usiku ukaonane nae.
Ikabidi nitulizane, nikawa na mawazo mengi na nanona muda haufiki, nikampoigia mama, akanambia huki maiti imeshaoshwa na watu ni wengi sana wanawake kwa wanaume, wanangoja muda ufike wakazike.
Mimi: Sikuonge mengi, ikabidi nikubali matokeo.
usiku kama kawaida nikaenda mlangoni nikamwita Arsis. Siku nyingi ilikua sijaenda. Nikakuta kuna mabadiliko ya majengo, ujenzi unaendelea, uwanja umejifinya kidogo.
Arsis: Vipi hali simba?
Mimi: Kama ujavyo, mimi niko poa.
Arsis: Usiwe na wasiwasi. SAema.
Mimi; Niseme nini Arsis na wewe ndio umeniita nije hapa?
Arsis: naona una maswali mengi na una hofu.
Mimi; Kawaida tu, hayo mambo ya Unguja vipi?
Arsis: kwanza leo nimekuita kuna viumbe nataka kukujulisha nao, au unaogopa?
Mimi; Niogope nini?
Arsis: Unaona ile miti mwili ipo nyuma yako?
Mimi; Ndiyo.
Arsis; Ile miti ya zamani sana usiione midogo, ile mbegu waliipanda Wajerumani ya kwao huko, ile miti ni shida sana kufa, ikishashika ardhi, inakaa miaka mingi sana na inakua kidogokidogo sana, jhaikatwi na mtu ile kabisa, hata wakijenga hapa, ipo pale na ipo humo ndani Ikulu. Unaijua kazi yake nini?
Nikawa najiuliza huyu Arsis kaniita kunieleza habari ya miti?
Mimi; Siijui kazi yake.
Arsis; kwanza kacheka, kazi yake hio ni alama, alama ya miaka mingi sana ijayo, wamaoijua wanajua alama ipi. Usiwe na wasiwasi, nataka uelewe hilo. sasa tazama kwenye ile miti, unaona nini?
Mimi kutazama nikaona kuna watu wawili, mmoja mrafu kiasi ana mwili mpana mpna sio mnene lakini, na mmoja kavaa tshirt ya mikono mirefu na jeans, nikamweleza Arsis ninachoona.
Arsis; sawasawa, huyo mmoja ni binadam kama wewe na mmoja ni jinni. Nebda kawasalimie ujuane nao. Usiogope.
Mimi: Siogopi kitu.
Arsis; Haya nenda halafu urudi.
Nikaenda nikapeana nao mikono, yule aliyevaa kanzu alikua ana mikono mipana sio kawaida. Yule mewingine alikua kama mimi tu, sema anainesha kazisi umri. Tukasalimiana, yule binge la mtu akasema sisi tunakujua siku nyingi, wewe ndio hujatuona kabla.
Mimi: Nyie kina nani?
Binadam: Sisi wanafunzi wa Arsis kama wewe.
Mimi nikashangaa , kwa sababu Arsis hajawahi kunambia kama ana wanafunzi.
Mimi; Mnaishi wapi?
Jini mubwa; Sisis tunaishi inapotupeleka kazi, sisi wote wanafunzi wa Arsis lakini mimi ni mwanajeshi, huyu mwenzangu ni mwanafunzi w udaktari, sasa hivi anachukua shahada ya juu.
Mimi; Mmesema mnanijua, mona siwajui wala sijawahi kuwasikia?
Jini Mkubwa; Tulikua hatukutakiwa utujue, tulijulishwa tu kua na wewe ni mwanafunzi wa kipekee wa Arsis.
Jini Mkubwa; twende tukatembee, hutaki kwenda Ikulu ndani ukapaone pakoje?
Arsis: Njoo Simba usiende mahali, haya nyie kwaherini, mtakua nae pamoja leo.
Itaendelea.
kama nilivyoahidi. Hiki kisa ni cha kusikitisha sana. Hii dunia ina hatari, kisa hiki kimetokea kama miaka 16 iliopita.
Siku hio mamangu mzazi alikwenda Zanzibar na wenzake kundi zima, waliletewa habari usiku, kua kuna binti kigori kafa ghafla baad ya kuumwa kuchqa kwa muda mfupi.
Kuna rafiki ya mamangu mzazi kaolewa kwenye ukoo huo na mjomba wa huyo binti, alipopata habari usiku huohuo akawajulisha habari ya kifo watu wa karibu, ikabidi mamangu na rafiki zake wengine wandoke nae alfajiri kuwahi maziko, waliondoka wao na ndege ndogo ya kukodisha, wengine kundi kubwa walienda na boti za asubuhi.
Walipofika Unguja wakaenda moja kwa moja wakaenda mpaka nyumba ya msiba wakawa ni kama wametokea palepale Unguja tu, watu wanajazana na wao wapo hapo. Kikatokea kitu cha ajabu sana, lakini Mwenyezi Mungu akitaka jambo lake liwe hakuna wakulizuwia. Kuna mama mmoja mtu mzima aliyekuja masibani akamwita mama mzazi wa yule binti aliyefariki pembeni. Akamwambia.
Mtu mzima; Mama pole sana, lakini nakuomba msihimize kumuosha huyu mtoto, mimi naona kama kuna mchezo umefanyika hapa, mbona hio sio maiti hapo? Usimwambie mtu, fanya hima na mimi kuna mazee namjua nakwenda kumwambia yupo ng'ambo. Yule bibi akatoka. Yule mama akabaki analia kwa kwikwi. Watu wanafanya maandalizi aoshwe, yule mama akamwita yule wifi yake amabae ni rafiki wa mamangu pia akamweleza alivyoambiwa na yule bibi, akamsisitiza asiseme kwa mtu yeyote wa pale, lakini maiti isioshwe mpaka yule bibi arudi.
Yule rafiki wa mamangu akmatonya mamangu, mamangu, unajua mambo ya wanawake tena, akatoka nje akampigia simu babu yangu tanga, saa hio hio. Babu yangu akmwabia nipe nusu saa nitakupigia. Babu akafanya mamboi yake akanipigia simu, kama saa tano hivi akanieleza alivyopigiwa simu, akanambia fanya hima uende Unguja lakinimwite Arsis uongee nae hili jambo.
Mimi kwa msisitizo wa babu na mamangu yuko kule nikamwita Arsis, ikaja sauti yake tu kama kawaida, akanambia usiwe na waiwasi, sisi na majeshi yapo kule. Wewe nenda kesho mpema usiende leo. Leo usiku tuonane pale mlangoni. Sehemu yetu ya kukutania Arsis alikua aniita mlangoni.
Mimi: Nikamwambia sawa lakini roho hainipi. Nikarudi nyumbani nikaingia ofisini kwangu, nikamwita Jini 1. Hakuchelewa akaja, live, tukasalimiana pale.
Jini1; Mbona una wasiwasi, mambo yapo vizuri.
Mimi; Najua mpaka sasa unafahamu kinachoendelea. Arsis kanambia nisiende leo kwanini?
Jini1; Tena babu yako kishaongea nao Unguja huko, kawaambia waoshe wazike tu leo hii, kama kawaida, wafanye kama hawajui kitu.Yule mama kazuiliwa hukohuko kwa mganahga wake asirudi mazikoni na mganga wake. Kwa hio huko mambo yanaendelea kama kawaoida na leo saa 10 wanazika, mpaka kaburi limeshachimbwa maiti imeshaoshwa watu wapo kama kawaida.
Mimi: Na huyo binti vipi?
Binti: Yupo palepalee kwao kafichw kichawi, hakuna anaemuona lakini yeye anaona kila kitu, leo watakuja kumchukua usiku sana kabla ya alfajiri, ndio watafatwa washikwe wpoyte ili huo ufisadi ukomeshwe, si unajua mambo ya Arsis?
Mimi; Sasa mi si niende leo?
Jini1; Wewe ukienda leo unaweza ukapatwa na hasira utaona kinachoendelea, tuwachie sisi tupo huko, hivi mama yupo huko, Bakora yupo huko na mimi nilikua huko msibani. Niwache niende, wewe mapema sana nenda usiwe na shaka kazi zitakungoja wewe, hakuna wa kuifanya hii kazi kabla wewqe hujafika, kunamajeshi huko si mchezo. Arsis anasisitiza usiku ukaonane nae.
Ikabidi nitulizane, nikawa na mawazo mengi na nanona muda haufiki, nikampoigia mama, akanambia huki maiti imeshaoshwa na watu ni wengi sana wanawake kwa wanaume, wanangoja muda ufike wakazike.
Mimi: Sikuonge mengi, ikabidi nikubali matokeo.
usiku kama kawaida nikaenda mlangoni nikamwita Arsis. Siku nyingi ilikua sijaenda. Nikakuta kuna mabadiliko ya majengo, ujenzi unaendelea, uwanja umejifinya kidogo.
Arsis: Vipi hali simba?
Mimi: Kama ujavyo, mimi niko poa.
Arsis: Usiwe na wasiwasi. SAema.
Mimi; Niseme nini Arsis na wewe ndio umeniita nije hapa?
Arsis: naona una maswali mengi na una hofu.
Mimi; Kawaida tu, hayo mambo ya Unguja vipi?
Arsis: kwanza leo nimekuita kuna viumbe nataka kukujulisha nao, au unaogopa?
Mimi; Niogope nini?
Arsis: Unaona ile miti mwili ipo nyuma yako?
Mimi; Ndiyo.
Arsis; Ile miti ya zamani sana usiione midogo, ile mbegu waliipanda Wajerumani ya kwao huko, ile miti ni shida sana kufa, ikishashika ardhi, inakaa miaka mingi sana na inakua kidogokidogo sana, jhaikatwi na mtu ile kabisa, hata wakijenga hapa, ipo pale na ipo humo ndani Ikulu. Unaijua kazi yake nini?
Nikawa najiuliza huyu Arsis kaniita kunieleza habari ya miti?
Mimi; Siijui kazi yake.
Arsis; kwanza kacheka, kazi yake hio ni alama, alama ya miaka mingi sana ijayo, wamaoijua wanajua alama ipi. Usiwe na wasiwasi, nataka uelewe hilo. sasa tazama kwenye ile miti, unaona nini?
Mimi kutazama nikaona kuna watu wawili, mmoja mrafu kiasi ana mwili mpana mpna sio mnene lakini, na mmoja kavaa tshirt ya mikono mirefu na jeans, nikamweleza Arsis ninachoona.
Arsis; sawasawa, huyo mmoja ni binadam kama wewe na mmoja ni jinni. Nebda kawasalimie ujuane nao. Usiogope.
Mimi: Siogopi kitu.
Arsis; Haya nenda halafu urudi.
Nikaenda nikapeana nao mikono, yule aliyevaa kanzu alikua ana mikono mipana sio kawaida. Yule mewingine alikua kama mimi tu, sema anainesha kazisi umri. Tukasalimiana, yule binge la mtu akasema sisi tunakujua siku nyingi, wewe ndio hujatuona kabla.
Mimi: Nyie kina nani?
Binadam: Sisi wanafunzi wa Arsis kama wewe.
Mimi nikashangaa , kwa sababu Arsis hajawahi kunambia kama ana wanafunzi.
Mimi; Mnaishi wapi?
Jini mubwa; Sisis tunaishi inapotupeleka kazi, sisi wote wanafunzi wa Arsis lakini mimi ni mwanajeshi, huyu mwenzangu ni mwanafunzi w udaktari, sasa hivi anachukua shahada ya juu.
Mimi; Mmesema mnanijua, mona siwajui wala sijawahi kuwasikia?
Jini Mkubwa; Tulikua hatukutakiwa utujue, tulijulishwa tu kua na wewe ni mwanafunzi wa kipekee wa Arsis.
Jini Mkubwa; twende tukatembee, hutaki kwenda Ikulu ndani ukapaone pakoje?
Arsis: Njoo Simba usiende mahali, haya nyie kwaherini, mtakua nae pamoja leo.
Itaendelea.