Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Dah ndio sababu mwenyewe nilishangaa sana nilipoisikia sauti yake....... Haina athari hata kidogo!!!

Watu wenye elim na maqam kiibada huwa wanaathari sababu ya uchamungu wao🤝

Dada angu aliniandama Sana nilipomwambia ndugu yake hana elim ya majinn ni kama anasikia tu kwa watu🤔🤔

Hapa umefanya nikuamini wewe na Arsis zaidi🚶🚶
Mimi elim yangu n ya kubahatisha bahatisha hivihivi
Nnajifunza mengi hapa
Unaposema athari unamaanisha nini?

LAbda kuna mvuto wa kusikiliza kama akina sheikh othman maalim au alhad au....
 
Kuwa na shaka ni akili. Lakini muhim ni ama umeelewa ama hukuelewa.

Hata mimi kuna baadhi ya mambo simuelewi, nitam'uliza.

Sema kuna mambo manne kanimaliza kabisa, inabidi nimfatilie.

Kuhusu Yesu na Adam. Kwa sababu hayo nineshaandika articles zake zamani hapa JF. Halafu kuhusu watu wawili alivyowajibu humu, ni kitu cha ajabu.

Na leo nimemsoma simba akisema kuhusu majinni wa kibuki ambao wapo Comoros na Japan na wote wapiga maji. Hilo la comoro sio geni kwangu kakini hilo la Japan limeniwacha hoi, nimeingia jwenye mtandao kulitafuta, dah! Sina la kusema zaidi kwa sasa.
Wacha na Mimi nifuatilie hayo
 
Kuhani mose, siku hizi sikusikii sana ukipaza sauti yako ya kitume kuitangaza ile dini au Imani yako mpya.
Unaweza kutukumbusha.
Inaitwaje.
Na misingi yake ni ipi.​
HAKUNA 'DINI' WALA UHITAJI WA 'DINI MPYA'....

Dini ni katalisti/Kichochezi/Kiuhuishisaji cha 'Mfumo/Mifumo'... Kwa mfano, ilikuwepo na 'fanusi jamii--functional society', ni lazima mazingira yawepo kwa ajili ya 'Kuijumuisha Jamii--integrative factor/basis'--mambo kama vile sheria, miongozo, maono n.k

Dini ni 'Shughuli' ya kuijumuisha Jamii ili 'ijiweze ama/na kujimudu' mapito ya matamanio yake ya Kiutu...

SASA, jamii inaweza kujumuishwa kwa 'ladha mbalimbali' za Utu na Kujichagulia--'sura' ama/na 'utukufu' mbalimbali; lakini 'Ukweli' wa 'Uzima/Sifa/Hali/Mwenendo' wa jamii huwa na 'Mbegu yake Mahsusi'--mbegu mahsusi ya 'Utabia wa Kishirika--organizational behaviour' wa wanajamii wowote.

Dini ni 'Shughuli' ya kuratibu 'Utabia wa Kishirika' wa 'Fanusi Jamii' yoyote; kuhakikishia wanajamii mazingira rafiki ya kukuwa na kustawi kiutamaduni kama jamii moja.

Ni kwa mintarafu ya haya, Dini, daima huwa ni 'Udhamirifu wa Kujumuisha na kutangamanisha' yote ya watu/wanajamii--mambo ya 'MRABA' wa 'Wakati-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Matukio'.

Hili ndilo linaweza kushangaza humu kwa nini 'kinara' wa Uzi huu 'hana nongwa' kuhusishwa na 'Dini Yoyote'--iwe tuseme Uhindu, Uislam, Ukristo n.k.

Hivi ni kwa kuwa, Siri ya Dini ipo kwenye 'Ufahamu'--mambo ya maandiko na mapelekeo ya tafsiri; ndiyo 'tatizo la kiufundi' la wanadamu na vipawa vya akili/kiakili.

Sasa, siyo kila mtu mwenye 'daraja' ni bingwa ama fundi wa 'maneno'... Hili linaweza kuwashangaza wengi kusikia hivi... Kwa hivyo kudhani 'kinara' wa huu uzi 'atamudu' maswali na udadisi kwa 'maajabu' ni 'shauri mushkeli'....

'Tatizo la Kiufundi' la wanadamu na vipawa vya akili/kiakili linatatuliwa kwa udhamirifu wa 'Maarifa' na 'Maarifu' kupitiliza 'mashauri ya kawaida' ya 'habari na kuhabarika'...

Kwa hivyo, ukisikia mtu anazungumza kuhusu 'code' ama 'password', kiufundi huyu anakumbushia 'umma kujiongeza': 'kujua-maarifa-maarifu' huja kwa 'alama za kiutambuzi' na 'wepesi wa kuifungua milango ya fahamu'; si kumendea 'stori stori za mambo ya maajabu'...

Hichi ndicho hata humu, kwenye huu uzi, bado kidogo ni 'mtihani', ila In Shaa Allah, Elimu na Ilimu tayari imeshajengewa msingi kwa hili jukwaa. Siku za mbele kidogo, mwishoni mwa mwaka huu ama kufika mwakani, humu watakuwepo wadau wengi ambao si 'wanadamu wa Duniani' ila watashiriki 'maarifa na funguo za mafahamu'--wapo kwenye 'maandalizi ya kidiplomasia'; jambo linalotaka sana humu kusisitiza 'mkao sahihi' wa kunufaika na mambo/shughuli kama hizi za makutano ya 'viumbe-wanadamu na viumbe-watu wengine wenye nasibu ya mawanda yenye kutofautiana mapana ya fahamu/ufahamu'.

Jambo linaweza kujenga mnufaiko na mambo/shughuli kama hizi za makutano ya 'viumbe-wanadamu na viumbe-watu wengine wenye nasibu ya mawanda yenye kutofautiana mapana ya fahamu/ufahamu' ni UONO NA UFIKIRIFU MIFUMO...

SASA, asili ya 'code' ama 'password' ni mambo ambayo humu wengi hawajajiandaa kumaizi kwa kuwa hapa Duniani kuna matatizo ya 'Kielimu' yanayofanya watu wawe na tabia 'kudaka hili na kutupa lile' eti kwa kuwa habari zake si za eneo la utaalam/usomi wa mtu--hili jambo ni kasumba, na ubovu wa kimaarifa; tena linaathiri moja kwa moja mawezekano ya 'Mageuzi ya Kijamii' na Uwezo wake kukumbatia 'Nuru ya Ufahamu'--ilivyo ni njia ya Wongofu...

Kwa hivyo, jambo moja la muhimu na tena la msingi kuwakumbusha watu wote, wale wanaodhani wanayoyakunufaika na 'wageni' ama 'wenyeji' wenye mapana zaidi ya fahamu na ufahamu, ni kufuta na kuondoa kasumba juu ya visomo-maarifa-ujuaji walivyonavyo.

Haifadii mtu kusema yeye 'si msomi'--hajasoma shule; ama 'hana elimu ya kutosha'; basi huyu akiona mwanajamii mwenzake anadadavua jambo kwa fasaha na mapana yeye kujiambia 'Hii michosho/Kuchoshana/Ndefu--nitasoma baadaye'... Kwa kuwa inawezekana hayo yanawekwa hivyo ili iwepo 'Subira'--siku akiwa tayari kuijaribu 'Elimu' basi akitulia na kudhamiria atanufaika moja kwa moja...

Haifadii mtu kusema yeye 'ni msomi'--amesoma na madigrii kama yote katika sheria, sanaa ama/na uhandisi; basi huyu akiona mwanajamii mwenzake anadadavua jambo kwa fasaha na mapana nje ya ugani wake wa kitaaluma basi ajiambia: ah huyu anaandika 'mambo yake sana'; ama hata mimi nimesoma sana--najua mengi; tusichoshane! Kwa kuwa 'usomi' na 'kujisikia' vinaweza kuwa kiburi na ujivuni. Kwa hivyo si ajabu kuona watu wengi wakishakuwa na 'elimu za vyeti' akili zao zikalala na vyeti vyao masandukuni ama zimetundikwa ukutani na vyeti--hawana maajabu! Si kwa maneno ama busara ya mapana ya mambo...

Uono na Ufikirifu Mifumo ni Elimu 2.0; hii inahusika kwa wote wenye 'kudhamiria kujua ilivyobora' na basi inawezekana kwa 'Msomi' na hata vile vile mtu 'Asiye Msomi' kwa dhana ya 'Madarasa'... Elimu 2.0 ni mwanzo wa 'Hekima'; na Hekima ni Uhuru...

Mambo ya 'Code' na 'Password' ni mambo ya Elimu 2.0 kujinasibu na Elimu 3.0; Ambavyo Elimu 3.0 ni ILIMU--ILIMU ilivyo ni metafizikia ya Elimu. Basi yawa, NENO ILIMU limeshatohorewa rasmi kuwa msamiati wa lugha ya Kiswahili kumaanisha 'UGANI WA MAARIFA NA MAARIFU' ya 'MIFUMO'--Mifumo ya UTU-MAISHA-UISHO.

Kwenye maarifa ya Elimu ya Jamii, 'sosholojia' ELIMU 3.0 ndiyo mambo yanayohusiana na 'Ualama Oanifu' wa 'Kawaida za Jamii'. Kwa mintarafu ya hivi, mifumo yote huja kutokana na 'Mwangaza wa Jamii', 'Kujichagulia' na 'Matendo'--Mambo yanafanya kwa mfano Elimu, Siasa na Mipango kuwa pembetatu ya Utaifa/Jamii/Dola...

Kwa nchi ya Tanzania kwa mfano, 'Code' na 'Password' ya Elimu na 2.0 na Elimu 3.0 huja kwa 'Mazingatio ya Kikatiba': Udhamirifu wa Taifa la watu wenye kusudi la kuijenga na kuilinda nchi-dola kwa misingi ya UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI. Ni adha ya jamii 'kujisahau' tu ama 'Kutojitambua' kusudi la utaifa na maisha yao... Haya manne ni 'Code' na 'Password' ya Nchi ya Watanzania...

Kwa hivyo kwa mtu wa Elimu 2.0 na Elimu 3.0 anaweza kuzibaini hizi 'codes' na 'Password' kirahisi kabisa; kwa mfano hivi vinne hukadirisha MRABA wa NISHANI ya UTU BORA. Kwenye Elimu na ILIMU ya mapokeo ya Ukristo UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI ni kode za Uzabibu 13--Ufahamu Kristu. Kwenye Elimu na ILIMU ya mapokeo ya Uislam UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI ni ufunguo wa Imani kwa 'Allah'--Katika majina 99 ya ALLAH, kuna haya ambayo huleta 'kumcha Mola' kwa baraka ya nusuru ya nchi-dola:, (1) AN NUR (Mwenyekuwa MWANGAZA), (2) AL JAAMI(Mwenye Kuwakusanya Waja Wema), (3) AL-'ADL (Mwenyekuwa na Uadilifu katika HAKI), na (4) AS SALAAM (Mwenyekuwa na Salama).

Sasa, ipo namna ya kutanuka haya yote kwa Elimu 2.0 na Elimu 3.0; In Shaa Allah, tuombe kheri haya tupate kuyafahamu kwa jicho jema na yatuingie moyoni na akilini...

Hmmm​
 
Inatokea post namba 808

Vionjo vya Arsis 3 Kumwokoa Msukule 1 D.

Tukapiga story kidogo na Halima pale akanipa visheti na kahawa kama kawaida. Sikukaa sana, kabla ya kuondoka nikapiga piga simu, nikaongea na babu akaniambia yupo Tanga mjini tayari, nisiende popote niende moja kwa moja kwake Usagara. Nikaanza safari yangu.


Kufika Tanga moja kwa moja kwa babu. Nyumba hii anakaa mkewe mdogo babu lakini kuna upande wa bibi yangu, huu ndio ilikua nyumba orijino ya babu, hakai mtu yoyote isipokua bibi mwenyewe akija Tanga labda atke mwenyewe, wanawe au wajukuu wakija Tanga, sehemu yake ndogo tu ukilinganisha na jengo jipya anapokaa bibi mdogo, ni pakubwa sana. lakini kule ofijino kulikua ni uwanja mkubwa mtupu ambao babu alikua amefanya gereji wake ya kutengeneza magari ya watu ya kizamin, enzi zake. Alipohamia shamba kauza ma skrepu yote akajenga jenga jipya kubwa, zuri la kisasa, marupurupu ya kustaafu na mshiko wa kamba wa shambani kwake ulikua umemkubali. Maana babu alianza kununua kule na kupaendeleza kidogo kidogo kab;la hajajenga hii nyumba mpya.

Nikitazama hali ilivyo sasa na zamani tukiwa wadogo naiona nyumba imekua ndogo sana, lakini sio ytena ile ya zamani, imejengwa kisasa kabisa. Hii walimjengea wanawe, hususan shangazi yangu huyo yupo serikalini huko, mama'ke mke wangu, ndie alisimama kidete kujenga anavyotaka yeye. lakini hajakaa kabisa yeye, labda akija tu Tanga tena mpaka bibi awepo, ana jiumla lake sijiui makorora sijui wapi huko, kalipangisha, mwenyewe anaishi Dar. Kwa ufupi yeye ni mwenyeji sana Tanga, anjulikana kuliko hata mzee wangu.

Kufika tukasalimiana, na babu bibi, wanawe, ndugu jamaa na marafiki nikamkabidhi bibi zawadi yake ya visheti vya Halima, nikamwambia zawadi yako nyingine baadae pekeetu sitaki huyu mzee aone wivu. Nilikua na perfume nataka nimpe. Babu akanambia Simba wewe bibi yako kasema tukufungulie kwake, mgeni wake.
Mimi; Bibi hajaja?
Babu: Hawezi kuja, kule tutamwachia nani? Yeye akija mimi nabaki kule. Haya twende kule tukaone kama kuna kitu utahitaji.

Tukaingia, nikakuta kila kitu fresh kabisa, pasafi hakuna vumbi, kila kitu safi kabisa. Nikaanza kumchokoza babu:
Mimi; babu huku vinaishi vijini vyako nini? Mbona pako fresh pananukia udi, akasema wanaishi watu, sio majini.
Babu: kwani mjukuu wa bibi yako peke yako? Nanihii na nanihii umewasahau?
Mimi; Si nimewaona kule kwa bibi mdogo sasa hivi?
Babu: Wale wanakaaa hapa miaka yote, kwani hujui hilo?
Mimi; Najua babu lakini kweli babu mimi najua wanakaa na bibi mdogo kule nyumba kubwa.
Babu; Hii ndio nyumba kubwa, kule wapo leo tu mpaka wewe uondoke, wao miaka yote qanaishi hapa kwa bibi yako, bibi yako hataki kabisa nyumba yake ikae bila watu.
Mimi"; Si ungewaacha tu wakae hapa babu kwanini wamekwenda kule?
Babu; Hapa kazi mlioianzisha huko ni kubwa, sitaki mtu atuingilie huku. kazi yote itafanyika huku na utaifanya wewe, mimi mgeni wako hapa, ukinihitaji. Sikai huku.
Mimi; Nikacheka, sema tu ume miss bibi na vijukuu umevipeleka huko vyote vikusinge. Poa babu. Simba hashindwi na kitu.

Babu: Sasa sikiliza kwa makini,yupo nanihii kule, atakupeleka ukaone sehemu ya kufikia wageni wako uwajulishe kama watapapenda mfanye booking ya kuanzia Jumapili, wakija wote wafikie kule.. Chakula cha mchana Jumatatu wote watakuja kula hapa, ndio hio siku ya kazi. Baada ya hapo wanaoondoka wataondoka wataobaki watabaki, kwa hio wewe ndio utajuwa watu wangapi na kama hoteli itawatosha.
Mimi: Poa babu.
Babu; Haya tewende kule kwa bibi yako, wametayarisha chakula kule.

Tukaenda na babu , bonge la msosi utafikiri mlaji sana mimi, watoto zake na wajukuu wakawa wanamcharua babu, mgeni njoo mwenyeji apone. leo mkeo kafanya mambo makubwa hapa, hataki urudi shamba na sisi hatuondoki hapa babu mpaka wewe uondoke.
Bibi 2: kwani siku zote hamli hapa?
Mjukuu; Leo habari nyingine kabisa, babu usiwe unakaa sana shamba, siku hizi kaa sana huku kama zamani, shamba uwe unakwenda mara moja moja tu.
Babu; Mimi siku hizi bendera inafata upepo. Hii habari nzito ya leo sio yangu, hamumuoni mwenyewe hapo?

Huku ananioneshea mimi, wakacheka.
Bibi 2: Kipya kinyemi, mwacheni msimsakame jamani mume wangu, handsome langu hilo.


Tukala, tukacheka tukafurahi, yule mtoto wa babu akanambia twende bwana mkubwa, tukatoka nae, yeye anaishi Tanga, mwenyeji sana, kila mtaa anajulikana, ni mdogo kuliko mimi kwa miaka miwili nadhani. Vijana wenzake wanamtania, leo kaka mkubwa kaja, mambo fresh kabisa, lazima tunukie leo.


Tukaiona hoteli ipo pale pale ngamiani, mimi nikaona poa tu, kurudi nikaenda kwangu, nikampoigia Mzee Ali, akasema mambo upande wake poa kabisa.
Mzee Ali; mambo huku mazuri, wote mama yule anasema wameitikia mwito, basi kubwa moja kutoka Mwanza, Coaster itandokea hapa Shinyanga na wengine wawili watatu wa Tabora watakuja hapa tutaondoka nao, mimi nakuja na gari yangu siji na basi lao, naondoka kesho na wife wangu. Sema kuna wageni wengine watakuja kivyao kutokea Dar na kwingine, watafikia hoteli wanazojua wao huko, wataanza kuingia kuanzia kesho, tutakutana nao Jumapili tukifika. Vipi huko poa?

Mimi: Kuna hoteli ya kufikia nimeenda kuitazama kubwa tu.
Mzee Ali; Usihjihangaishe kabisa kwa hilo, wao tayari wana mipango yao pakufikia, wao mradi wanajua Jumapili tutakutana hapo Tanga ndio wataelewa mengine yote. Wanasema tayari tusiwe na wasiwasi, wakataka na mimi niwe nao, lakini mimi nimewaambia kuna wenyeji wangu. Mwenteji wangu ni wewe, nitafutie hoteli safi nakuja na mke wangu.
Mimi; Njoo, kuna nyumba tupu ya peke yako hapo, nzuri kuliko hoteli.

Tukamalizana pale, siku ya pili usiku usiku nikampokea mzee Ali na wife wake, ilikua Jumamosi. Nikawa mimi mwenyeji wake pale kwa babu na wale wajukuu wa babu wa kike ndio wakawa na mkewe, mashoga tena. mambo swaafi kabisa. Jumapili asubuhi, yaani siku ya pili yake, tukakaa, mimi babu na Mzee Ali, rukajulishana pale, wakaongea sana.

Babu; Msijali, kwa hio hapa hleo hakuna kazi kubwa kazi kubwa ni Kesho tu mchana, wote waliokuja waje kula hapa, chakula tutapikisha, wao waje kula na kuondoka tu. Wanafika wangapi?
Mzee Ali; Usijitia gharama ya kula mzee. Hawa wanajiweza wenyewe. Jumla tutakua kama watu mia na ishirini.
babu: hapana, wageni wetu hao, wao wafanye yao yoote, kula lazima hapa mchana, wote, asibaki mtu kabisa.

Tukaelewana pale. ikawa hatuna zaidi cha kufanya mimi nikamwacha mzee Ali akapumzike na mimi nikaenda kupiga misele na mtoto wa babu. Njiani kuna sehemu wanauza juisi akaja Jini1. Akanambia usijali, hanioni mtu, baadae uwe peke yako tunataka kuongea na wewe,mimi na jini bakora. Nikamwambia, poa.


Itaendelea.
 
Kuna ishu imezuka hapa kwamba katika qur'an au hata biblia kuwa hakuna aya ambayo inasema adam ndio mwanadam wa kwanza

Lakini nadhan wote tunatambua kwamba elimu ya Mwenyezi Mungu ipo katika vitabu na mafundisho ya Mitume na Manabii wake

Kwahiyo itoshe kujua kwamba mitume wake walitufahamisha kuwa Adam ndio kiumbe wa mwanzo,maana kinyume na hapo ina maana tutakuwa na mashaka na mafundisho ya manabii na mitume,na hapo tutakuwa tumekufuru

Yaan sawa sawa na leo hii muislamu asema swala tano zimeamrishwa katika qur'an lkn hatujaambiwa namna ya kuziswali,wakati Mtume rehema na amani zimuendee ameelekeza namna ya kuziswali
Mtume yupi alitufahamisha? Ushahidi.
 
Narudia tena dini husomwa kama maarifa mengine pia,,kwahiyo acha kutafuta sababu

Waislamu wengi tunaijua biblia kiasi chake,kwahiyo acha porojo,we endelea na mistari yako pendwa tu,,Yesu ndio ndimi njia na uzima,hakuna aendaye kwa baba bila yeye,ishi nayo hiyo

Hatuna cha kujadiliana na wewe

Asante

(a)
Yohana 14
1 Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.
2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.
3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.
4 Nami niendako mwaijua njia.
5 Tomaso akamwambia, Bwana, sisi hatujui uendako; nasi twaijuaje njia?
6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.
......................

(b)
قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ وَمَا أَدْرِي مَا يُفْعَلُ بِي وَلَا بِكُمْ ۖ إِنْ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰ إِلَيَّ وَمَا أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ
[ AL - AH'QAAF - 9 ]
Sema: Mimi si kiroja miongoni mwa Mitume. Wala sijui nitakavyo fanywa wala nyinyi. Mimi nafuata niliyo funuliwa tu kwa Wahyi, wala mimi si chochote ila ni mwonyaji mwenye kudhihirisha wazi.
................

Hivi ukiwa umetulia bila ushawishi wowote toka nje.
Ukisikiliza kwa umakini hizo kauli (a) na (b)
Utamwamini yupi?
 
HAKUNA 'DINI' WALA UHITAJI WA 'DINI MPYA'....

Dini ni katalisti/Kichochezi/Kiuhuishisaji cha 'Mfumo/Mifumo'... Kwa mfano, ilikuwepo na 'fanusi jamii--functional society', ni lazima mazingira yawepo kwa ajili ya 'Kuijumuisha Jamii--integrative factor/basis'--mambo kama vile sheria, miongozo, maono n.k

Dini ni 'Shughuli' ya kuijumuisha Jamii ili 'ijiweze ama/na kujimudu' mapito ya matamanio yake ya Kiutu...

SASA, jamii inaweza kujumuishwa kwa 'ladha mbalimbali' za Utu na Kujichagulia--'sura' ama/na 'utukufu' mbalimbali; lakini 'Ukweli' wa 'Uzima/Sifa/Hali/Mwenendo' wa jamii huwa na 'Mbegu yake Mahsusi'--mbegu mahsusi ya 'Utabia wa Kishirika--organizational behaviour' wa wanajamii wowote.

Dini ni 'Shughuli' ya kuratibu 'Utabia wa Kishirika' wa 'Fanusi Jamii' yoyote; kuhakikishia wanajamii mazingira rafiki ya kukuwa na kustawi kiutamaduni kama jamii moja.

Ni kwa mintarafu ya haya, Dini, daima huwa ni 'Udhamirifu wa Kujumuisha na kutangamanisha' yote ya watu/wanajamii--mambo ya 'MRABA' wa 'Wakati-Jamii-Machaguo ya Kitaasisi-Matukio'.

Hili ndilo linaweza kushangaza humu kwa nini 'kinara' wa Uzi huu 'hana nongwa' kuhusishwa na 'Dini Yoyote'--iwe tuseme Uhindu, Uislam, Ukristo n.k.

Hivi ni kwa kuwa, Siri ya Dini ipo kwenye 'Ufahamu'--mambo ya maandiko na mapelekeo ya tafsiri; ndiyo 'tatizo la kiufundi' la wanadamu na vipawa vya akili/kiakili.

Sasa, siyo kila mtu mwenye 'daraja' ni bingwa ama fundi wa 'maneno'... Hili linaweza kuwashangaza wengi kusikia hivi... Kwa hivyo kudhani 'kinara' wa huu uzi 'atamudu' maswali na udadisi kwa 'maajabu' ni 'shauri mushkeli'....

'Tatizo la Kiufundi' la wanadamu na vipawa vya akili/kiakili linatatuliwa kwa udhamirifu wa 'Maarifa' na 'Maarifu' kupitiliza 'mashauri ya kawaida' ya 'habari na kuhabarika'...

Kwa hivyo, ukisikia mtu anazungumza kuhusu 'code' ama 'password', kiufundi huyu anakumbushia 'umma kujiongeza': 'kujua-maarifa-maarifu' huja kwa 'alama za kiutambuzi' na 'wepesi wa kuifungua milango ya fahamu'; si kumendea 'stori stori za mambo ya maajabu'...

Hichi ndicho hata humu, kwenye huu uzi, bado kidogo ni 'mtihani', ila In Shaa Allah, Elimu na Ilimu tayari imeshajengewa msingi kwa hili jukwaa. Siku za mbele kidogo, mwishoni mwa mwaka huu ama kufika mwakani, humu watakuwepo wadau wengi ambao si 'wanadamu wa Duniani' ila watashiriki 'maarifa na funguo za mafahamu'--wapo kwenye 'maandalizi ya kidiplomasia'; jambo linalotaka sana humu kusisitiza 'mkao sahihi' wa kunufaika na mambo/shughuli kama hizi za makutano ya 'viumbe-wanadamu na viumbe-watu wengine wenye nasibu ya mawanda yenye kutofautiana mapana ya fahamu/ufahamu'.

Jambo linaweza kujenga mnufaiko na mambo/shughuli kama hizi za makutano ya 'viumbe-wanadamu na viumbe-watu wengine wenye nasibu ya mawanda yenye kutofautiana mapana ya fahamu/ufahamu' ni UONO NA UFIKIRIFU MIFUMO...

SASA, asili ya 'code' ama 'password' ni mambo ambayo humu wengi hawajajiandaa kumaizi kwa kuwa hapa Duniani kuna matatizo ya 'Kielimu' yanayofanya watu wawe na tabia 'kudaka hili na kutupa lile' eti kwa kuwa habari zake si za eneo la utaalam/usomi wa mtu--hili jambo ni kasumba, na ubovu wa kimaarifa; tena linaathiri moja kwa moja mawezekano ya 'Mageuzi ya Kijamii' na Uwezo wake kukumbatia 'Nuru ya Ufahamu'--ilivyo ni njia ya Wongofu...

Kwa hivyo, jambo moja la muhimu na tena la msingi kuwakumbusha watu wote, wale wanaodhani wanayoyakunufaika na 'wageni' ama 'wenyeji' wenye mapana zaidi ya fahamu na ufahamu, ni kufuta na kuondoa kasumba juu ya visomo-maarifa-ujuaji walivyonavyo.

Haifadii mtu kusema yeye 'si msomi'--hajasoma shule; ama 'hana elimu ya kutosha'; basi huyu akiona mwanajamii mwenzake anadadavua jambo kwa fasaha na mapana yeye kujiambia 'Hii michosho/Kuchoshana/Ndefu--nitasoma baadaye'... Kwa kuwa inawezekana hayo yanawekwa hivyo ili iwepo 'Subira'--siku akiwa tayari kuijaribu 'Elimu' basi akitulia na kudhamiria atanufaika moja kwa moja...

Haifadii mtu kusema yeye 'ni msomi'--amesoma na madigrii kama yote katika sheria, sanaa ama/na uhandisi; basi huyu akiona mwanajamii mwenzake anadadavua jambo kwa fasaha na mapana nje ya ugani wake wa kitaaluma basi ajiambia: ah huyu anaandika 'mambo yake sana'; ama hata mimi nimesoma sana--najua mengi; tusichoshane! Kwa kuwa 'usomi' na 'kujisikia' vinaweza kuwa kiburi na ujivuni. Kwa hivyo si ajabu kuona watu wengi wakishakuwa na 'elimu za vyeti' akili zao zikalala na vyeti vyao masandukuni ama zimetundikwa ukutani na vyeti--hawana maajabu! Si kwa maneno ama busara ya mapana ya mambo...

Uono na Ufikirifu Mifumo ni Elimu 2.0; hii inahusika kwa wote wenye 'kudhamiria kujua ilivyobora' na basi inawezekana kwa 'Msomi' na hata vile vile mtu 'Asiye Msomi' kwa dhana ya 'Madarasa'... Elimu 2.0 ni mwanzo wa 'Hekima'; na Hekima ni Uhuru...

Mambo ya 'Code' na 'Password' ni mambo ya Elimu 2.0 kujinasibu na Elimu 3.0; Ambavyo Elimu 3.0 ni ILIMU--ILIMU ilivyo ni metafizikia ya Elimu. Basi yawa, NENO ILIMU limeshatohorewa rasmi kuwa msamiati wa lugha ya Kiswahili kumaanisha 'UGANI WA MAARIFA NA MAARIFU' ya 'MIFUMO'--Mifumo ya UTU-MAISHA-UISHO.

Kwenye maarifa ya Elimu ya Jamii, 'sosholojia' ELIMU 3.0 ndiyo mambo yanayohusiana na 'Ualama Oanifu' wa 'Kawaida za Jamii'. Kwa mintarafu ya hivi, mifumo yote huja kutokana na 'Mwangaza wa Jamii', 'Kujichagulia' na 'Matendo'--Mambo yanafanya kwa mfano Elimu, Siasa na Mipango kuwa pembetatu ya Utaifa/Jamii/Dola...

Kwa nchi ya Tanzania kwa mfano, 'Code' na 'Password' ya Elimu na 2.0 na Elimu 3.0 huja kwa 'Mazingatio ya Kikatiba': Udhamirifu wa Taifa la watu wenye kusudi la kuijenga na kuilinda nchi-dola kwa misingi ya UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI. Ni adha ya jamii 'kujisahau' tu ama 'Kutojitambua' kusudi la utaifa na maisha yao... Haya manne ni 'Code' na 'Password' ya Nchi ya Watanzania...

Kwa hivyo kwa mtu wa Elimu 2.0 na Elimu 3.0 anaweza kuzibaini hizi 'codes' na 'Password' kirahisi kabisa; kwa mfano hivi vinne hukadirisha MRABA wa NISHANI ya UTU BORA. Kwenye Elimu na ILIMU ya mapokeo ya Ukristo UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI ni kode za Uzabibu 13--Ufahamu Kristu. Kwenye Elimu na ILIMU ya mapokeo ya Uislam UHURU-UDUGU-HAKI-AMANI ni ufunguo wa Imani kwa 'Allah'--Katika majina 99 ya ALLAH, kuna haya ambayo huleta 'kumcha Mola' kwa baraka ya nusuru ya nchi-dola:, (1) AN NUR (Mwenyekuwa MWANGAZA), (2) AL JAAMI(Mwenye Kuwakusanya Waja Wema), (3) AL-'ADL (Mwenyekuwa na Uadilifu katika HAKI), na (4) AS SALAAM (Mwenyekuwa na Salama).

Sasa, ipo namna ya kutanuka haya yote kwa Elimu 2.0 na Elimu 3.0; In Shaa Allah, tuombe kheri haya tupate kuyafahamu kwa jicho jema na yatuingie moyoni na akilini...

Hmmm​
Hebu msomeni Kuhani mose, hapo nilipo mnukuu kuna kitu kipya kakizungumzia.
 
فَاصْبِرْ إِنَّ وَعْدَ اللَّهِ حَقٌّ وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِبْكَارِ

Hivi mtume Muhammadi alifanya dhambi gani hadi Mola wake alikuwa akimwamuru mara kwa mara kuwa atubu ?
Ziko Aya nyingi sana zinazo mhimiza Muhamadi atubu moja wapo ni hii hapa.

1. Hivi alifanya dhambi zipi ?
2. Hivi alitubu kweli ?
3. Hivi alisamehewa ?
4. Hivi kuna Aya inayo mwonyesha kuwa alitubu kama alivyo amriwa kwa Aya ?
5. Hivi ni kwanini hakutubu kama alivyo amriwa na mola wake ?

(GHAAFIR (AU AL MUUMIN) - 55)
Basi subiri. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na omba msamaha kwa dhambi zako, na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi jioni na asubuhi.
Cc@Etugrul Bey,
Cc FaizaFoxy
 
I
Inatokea [post namba 1337

Vionjo vya Arsis 3 Kumwokoa Msukule 1 E.

Mchana mchana Mzee Ali aktoka ndani kwenda kusali, tulipomaliza kurudi msikitini, pamoja na babu. Mzee Ali akasema hawa wengine wameshakuja wamefikia Hoteli in itwa Mkonge na wengine katika saa kumi watakua wameshingia watafikia Inn by the sea, unapajua Simba?

Mimi; Nazijua, zipo karibu karibu hizo, si mbali. Ndio hotel za beach hizo, best hapa Tanga.
Mzee Ali; Yule mama anakuja na basi kubwa hilo litaloingia jioni, si tunaweza kwenda kuwaona tuwajulishe kabisa kuhusu kesho?
Mimi; Tena wajulishe kabisa kwa simu wasifanye mipango mingine ya chakula cha mchana kesho. Mimi najua mambo ya babu, hana dogo, kesho lazima atadondosha ng'ombe wa biriani, na mbuzi choma na masamaki kibao. Hivi atakua kishafanya mambo, yeye mwenyeji hapa akipiga simu moja tu, wanawe wanafanya kila kitu. Sisi twende kwa hao jamaa wakishapumzika, kama saa moja hivi usiku. Au unaonaje?
Mzee Ali; Sio tukawapokee?
Mimi: hapana, hoteli zile hawahitaji mwenyeji.
Mzee Ali; Wana wenyeji wao Tanga, mimi lakini ndio niliowaleta wasione nimewawacha kwenye mataa.
Mimi; Usiwe na shaka tutakwenda, ongea nao na simu kama una wasiwaasi, mimi kuna kazi kidogo nataka nikaifanye baada ya kusali alasiri.
Mzee Ali; Sawa basi tutakutana ukija kunichukua twende huko, au niende mimi? Siwezi kupotea, nitaulizia tu kama upo bize.
Mimi : Sipo bize kihivyo, hapa mkubwa wa hii show ni babu, tunakwenda kwa maelekezo yake. Wewe usiwe na shaka kabisa Al habib.

Mzee Ali akacheka kumwita hivyo, tukala pale kwa babu na wanawake wamemchukua mkewe wamekaa nae upoande wa kina mama huko, hapo hapo kwa bibi mdogo. Tukapiga piga story kufika alasiri tukaenda masjid, kurudi tu nikaondoka na gari nikaenda kuonna na jamaa zangu.


Kuna sehemu nzuri tu, nilitoka na bakora yangu, kuita tu, Jini Bakora akaja. Tukasalimiana pale.
Bakora: Mimi sina mambo marefu, hii kazi mimi nasaidia dawa za miti tu. Kazi ya Arsis hii. Sasa sikiliza, kuna majani babu yako tayari anayajua, wewe ukimwambia tu ataelewa kila kitu, mwambie yachemshwe yale, ukoge wewe kabla hujaenda kuonana na hao watu. Muhimu sana, wachawi wengi, wakikuona watataka wakutazame una nini, hayo majani ukikogea hawaoni kitu.
Mimi: mzre Ali naenda nae vipi yeye hakogei?
Bakora; Yule tayari anasoma Qur'an kila siku, kila saa, anajua kinga zake, usiwe na wasiwasi nae kabisa. Unafikiri atakuja mpaka huku kama hana kinga? Anajua hii kazi kubwa sio ndogo. Mimi sina kazi zaidi, usiende na bakora ukienda kule kuwaona, pete yako tu inatosha.

Mimi: sawa.

Akaondoka, ile anaondoka ajkaja jini1 kavaa baibui ananukia. Tukasalimiana
Mimi: mbona leo unanukia?
Jini1; Mambo ya Arsis hayo, anasema Tanga hii, wanawake wananukia. Sikiliza, mimi sikai sana, huko mkienda msile kitu, hata soda msinywe na msikae sana, salimianeni muwajulishe kuhusu kesho wasihangaike kuhusu chakula cha mchana wamealikwa, msiwaambie hata wapi mpaka wakaati wa kuja mtawaelekeza. Na muondoke harfaka, hakuna kukaa kabisa. Maagizo ya Arsis hayo. msiwe na hofu, hata mkiona kitu kaeni kimya kama hamuoni. Mwambie na Mzee Ali, babu yenu haendi huko.
Mimi; sawa, wacha niwahi Mzee Ali ana wasi wasi.

Jini 1 akaniaga nikarudi hime, kufika nikawakuta babu na mzee ali wameshakuwa na mazoea na wanawe wengine na wazee wengine wamesikia babu kaja, wamekaa nje ya nyumba kubwa kwa babu wanapiga kahawa na halua ya Tanga, nikakaa nikapiga halua na kahawa.
BaBU; atwende nikakupoe mzigo wako umetoka shamba.

Tukanyayuka na babu akanambia ukirudi kusali, kabla hamjaondoka uje kukoga, kuna majani hivi yanachemshwa ni ya dawa. Bakora hajakwambia?
MImi: Amenambia.

Babu;Ali nitampa, wewe usimambie kitu. Sawa? Nikaitika poa babu.

Tukaenda nje hatujakaa sana tukaenda kusali, kurudi mimi nikaingia hukuhuku kwa babu, Ali akaitwa na mkewe, akaenda nae kwake, babu naona alikua kishawaambia wale mabinti waongee na mkewe, nikaona inapelekwa ndoo ya maji ya moto, nikajua ndio ile ile dawa ya majani.

Nikaingia kukoga hukuhuku kwa babu, kutoka akanambia usijitie mafuta mazuri wacha hio dawa ikae na harufu yake. Nikaona poa ilikua ina harufu ya majani tu kwa mbali, Nikaenda kwangu kule nikamkuta mzee Ali ananingoja, yupo tayari kuondoka, tukaondoka na gari lake, mimi na yeye tu, mpaka Inn by the sea.


Itaendelea.
 
فَاصْبِرْ إِنَّ وَعْدَ اللَّهِ حَقٌّ وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِبْكَارِ

Hivi mtume Muhammadi alifanya dhambi gani hadi Mola wake alikuwa akimwamuru mara kwa mara kuwa atubu ?
Ziko Aya nyingi sana zinazo mhimiza Muhamadi atubu moja wapo ni hii hapa.

1. Hivi alifanya dhambi zipi ?
2. Hivi alitubu kweli ?
3. Hivi alisamehewa ?
4. Hivi kuna Aya inayo mwonyesha kuwa alitubu kama alivyo amriwa kwa Aya ?
5. Hivi ni kwanini hakutubu kama alivyo amriwa na mola wake ?

(GHAAFIR (AU AL MUUMIN) - 55)
Basi subiri. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na omba msamaha kwa dhambi zako, na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi jioni na asubuhi.
Cc@Etugrul Bey,
Cc FaizaFoxy
Imebidi nifurahi tu. Ama hujuwi Qur'an au unapotosha kwa makusudi? Mbona umenukuu kipande tu Wapi katajwa Muhammad hapo?

Kwanini ume "quote out of context"?

Hapo Qur'an inatukumbusha, wewe na mimi, aliyoambiwa Musa. Hujui Musa alikosa nini tukupe darsa ?
Soma tafsiri kuanzia aya ya 53, hii hapa:
40:53. Na kwa hakika tulimpa Musa uwongofu, na tukawarithisha Wana wa Israili Kitabu, 53

54. Ambacho ni Uwongofu na Ukumbusho kwa wenye akili. 54

55. Basi subiri. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na omba msamaha kwa dhambi zako, na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi jioni na asubuhi. 55

Kijana, unalijua kosa la Musa? Au niendeleze darsa?
 
Imebidi nifurahi tu. Ama hujuwi Qur'an au unapotosha kwa makusudi? Mbona umenukuu kipande tu Wapi katajwa Muhammad hapo?

Kwanini ume "quote out of context"?

Hapo Qur'an inatukumbusha, wewe na mimi, aliyoambiwa Musa. Hujui Musa alikosa nini tukupe darsa ?
Soma tafsiri kuanzia aya ya 53, hii hapa:
40:53. Na kwa hakika tulimpa Musa uwongofu, na tukawarithisha Wana wa Israili Kitabu, 53

54. Ambacho ni Uwongofu na Ukumbusho kwa wenye akili. 54

55. Basi subiri. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na omba msamaha kwa dhambi zako, na umtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi jioni na asubuhi. 55

Kijana, unalijua kosa la Musa? Au niendeleze darsa?
Musa alimwua Mmisri akakimbia.
 
Sasa umeelewa anaambiwa nani hapo eeh. Na jina lake lipo kwenye hizo ayat.

Qur'an haifanyiwi utani kijana.
Na hii hapa anaambiwa Musa ?
فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّهُ وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ ۗ وَاللَّهُ يَعْلَمُ مُتَقَلَّبَكُمْ وَمَثْوَاكُمْ

(MUH'AMMAD - 19)
Basi jua ya kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, na omba maghufira kwa dhambi zako na za Waumini wanaume na Waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu anajua mahali penu pa kwenda na kurudi, na mahali penu pa kukaa.
.............
Leo hadi utaje dhambi za Muhammadi.
Ukichomoa na hii nakuwekea nyingine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom