NKNS
Vitabu vya
Dolores Cannon labda?
Huyu mama ameandika mengi hasa kuhusu haya yote--kwa kweli; wengi tu huko Magharibi na
Mashariki ya Mbali wameandika 'habari za ajabu' za mtu, watu na maisha.
Mazoezi !, mazoezi !--maarifa ni pamoja ujuzi na uwezo wa matumizi bora ya lugha na maneno; hili linakuja kwa nidhamu na udhamirifu wa fasaha na miundo ya semi/udadavuaji...
Maarifa yana 'Mbegu ya Ujuaji', siyo porojo tu na kuhorojoka. Ukifanyika uwezo ndani yako wa kuzibaini 'mbegu za ujuaji uliobora' basi unaweza kusoma mashauri yoyote na juu ya kisomo chochote--ilihali uwasilisho wake umesukika kiufundi.
Kwa hivyo yapo mengi humu, katika huu uzi, yanoyohitaji 'Kunyooshwa'--kutengenezewa koherensia ya ufikirifu; lakini hili linakuja kulingana na 'chachu' ya washiriki na uwezekano wa manufaa katika kuingiliakati mazungumzo.
In Shaa Allah, kadiri inavyofaa, kidogo kidogo 'tutayapatia sura rasmi' yote yanayohusiana na 'Ulimwengu wa Kiroho' kwa lugha yetu ya Kiswahili; kwa manufaa ya wale wote wenyebidii ya visomo na pia udhamirifu wa jitihada/ufundi wa uwasilishaji wa habari za maisha na maajabu ya maisha/uisho...
Hili siyo suala la starehe tu, hili ni suala la Utamaduni na Umahiri wa mambo... Kwenye 'kujichagulia ilivyobora', 'hakuna kazi nyepesi'...
Kila mtu anaubeba mzigo wake.
Hmmm