Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

Niliyoyashuhudia nilipofunguliwa macho

NKNS

Vitabu vya Dolores Cannon labda?

Huyu mama ameandika mengi hasa kuhusu haya yote--kwa kweli; wengi tu huko Magharibi na Mashariki ya Mbali wameandika 'habari za ajabu' za mtu, watu na maisha.

Mazoezi !, mazoezi !--maarifa ni pamoja ujuzi na uwezo wa matumizi bora ya lugha na maneno; hili linakuja kwa nidhamu na udhamirifu wa fasaha na miundo ya semi/udadavuaji...

Maarifa yana 'Mbegu ya Ujuaji', siyo porojo tu na kuhorojoka. Ukifanyika uwezo ndani yako wa kuzibaini 'mbegu za ujuaji uliobora' basi unaweza kusoma mashauri yoyote na juu ya kisomo chochote--ilihali uwasilisho wake umesukika kiufundi.

Kwa hivyo yapo mengi humu, katika huu uzi, yanoyohitaji 'Kunyooshwa'--kutengenezewa koherensia ya ufikirifu; lakini hili linakuja kulingana na 'chachu' ya washiriki na uwezekano wa manufaa katika kuingiliakati mazungumzo.

In Shaa Allah, kadiri inavyofaa, kidogo kidogo 'tutayapatia sura rasmi' yote yanayohusiana na 'Ulimwengu wa Kiroho' kwa lugha yetu ya Kiswahili; kwa manufaa ya wale wote wenyebidii ya visomo na pia udhamirifu wa jitihada/ufundi wa uwasilishaji wa habari za maisha na maajabu ya maisha/uisho...

Hili siyo suala la starehe tu, hili ni suala la Utamaduni na Umahiri wa mambo... Kwenye 'kujichagulia ilivyobora', 'hakuna kazi nyepesi'...

Kila mtu anaubeba mzigo wake.

Hmmm
Khaaaa......!?
Uandishi wako sijui kati ya wewe na Pro. Shivji nani ni mwalimu wa mwenzie au kama mlisoma shule moja basi nani alifaulu kumzidi mwenzie??

Tuseme mlisoma shule moja au elimu inayofanana sasa nini kiliwapeleka huko na na nani alikipata kati yenu??!!

😂😂😂😂😂😂
 
Dawa ya kigugummizi ni ndogo sana. kama ni Muislam jifundishe "tajweed".

Kama si Muislam imba nyimbo za kumtukuza Mwenyezi mungu. kama huamini Mungu, imba tu upendavyo.
Simba.
😂😂😂😂😂
Wee jamaa una majibu hadi nimeshindwa kuvumilia. Ni kama utani vile lakini ukituliza akili na kutafakari kwa utuo unapata jibu.
Salute kwako!
 
Salaam wana Uzi!
Nini kimetokea mbona kama uzi umesuswa ghafla na kimya kimetanda kwema jamani??

Simba upo??
 
Nikiri kwamba huu ni uzi nilioupenda sana kwa sababu unadadisi upande mwingine wa maisha tofati na tuliyofundishwa shuleni,kanisani na msikitini! Hata hivyo namlaumu mleta uzi huu adhimu kwa sababu ameutelekeza bila kuufunga kwa heshima stahiki zinazoendana na hadhi ya uzi huu

Kama Arsis au Simba utaupata ujumbe wangu huu nakuomba uridhie kwamba uzi wetu huu unahitaji kufikia tamati iliyo na heshima stahiki au kama sio tamati basi dira ya muelekeo wake uwe wazi mara kwa mara ili wanaoufuatilia wote tuwe katika ukurasa mmoja

Binafsi nisikulaumu sana kwa sababu mwanzoni kabisa ulitoa tahadhari kwamba wewe sio mwandishi mzuri sana kwa hiyo mapungufu kama haya ilikua lazima yajitokeze. Hata hivyo sisi tunaofahamu na kupenda uandishi ni jukumu letu kuweka sawa!
 
InshaAllah
Ndugu yangu nimesoma stori yako ushauri wangu shikamana sana na Ibada jitahidi kutoa sadaka kwa wanyama pia kama unaweza fuga paka na njiwa. Achana na uradi wa masharti kuna wengine hutumia elimu yao kuwapa watu matatizo zaidi ili wao wanufaike kutoka kwako.

Uponyaji unatoka kwa Mwenyezi Mungu tu unakumbuka kisa cha Nabii Musa alipoumwa na kichwa na kumuomba Mungu ampe dawa. Mungu alimwambia akachume mti na kutafuna nae alipona. Mara nyengine Nabii Musa alikwenda kuchuma/kukata bila ya kumuomba Mungu na hakupona mpaka alipo muuliza Mungu tena. Kuwa anatumia mtu uleule lakini haponi?. Mungu alimjibu mwanzo uliomba msaada kwangu sasahivi umekwenda bila ya kuniomba mimi. Hapo kuna funzo la kumtegemea sana Mungu sio hawa masheikh wetu wao wenyewe wana madhaifu yao ya nafsi.

Jitahidi sana na Istikhfar,Suratul Nnas na Falaq. Aya mbili za mwisho za Suratul Al-Baqarah pamoja na Ayatul Kursi. Pia fanya uradi wa Subhana Allah,Alhamdulilah na Allahu akbar. Kila wiki jitahidi kutoa sadaka ndugu utaona rehma za Allah, Mwenyezi Mungu amesema humpa mja mtihani kwa uwezo wa huyo mja(Hampi mja mtihani nje ya uwezo wa huyo mja).

Inshallah Mwenyezi Mungu atakufanyia wepesi na aimarishe afya yako zaidi.
 
Assalaam Alaykum Akhii!
Shukran sana kwa ushauri. Kwa upande wangu nafanya ibada Alhamdulillah. Naswali swala tano na nimehifadhi Qur’an yote Alhamdulillah.

Kwenye suala la kuchinja kwa sasa sina uwezo nalo ila sadaqa ninayofanya ni kununua nafaka na kuwalisha ndege pia ningeomba unipe elimu hapo kwenye kufuga paka au njiwa.

Nyiradi pia nafanya sana miaka mingi ila bado sijaona mabadiliko. Nafahamu huu ni mtihani wa Allah ndio napambana nao kuuondoa na Allah atakapoamua yeye ipo siku utaondoka InshaAllah.

Kuhusu suala la kwenda kwa Masheikh hilo nimeachana nalo baada ya kuujua ukweli kuhusu Arsis maana nimeshuhudia mwenyewe kila unapozidi kwenda kwa hawa watu ndio unapozidi kujizolea matatizo. Simuamini hata huyo Arsis kwa sasa na pia utaona kila watu wanapoomba msaada anajibu shortcuts anakwepa maswali maana hilo sio lengo lake hapa Jamii Forums.

Nimefanya research ya kina kuhusu Arsis na kuwauliza watu wenye elimu kama yake nimekuja kupata uhakika kwamba Arsis sio Muislam bali ni Myahudi. Na hii nawapeni kama sadaqa yangu kwenu na kwa wale mliosoma hii story yake mnaweza kuunganisha vipande vya hapa na pale mnaweza kukubaliana na haya ninayoyasema. Kama mtakumbuka Arsis alipoulizwa kama yeye ni Muislam hakutoa jibu la moja kwa moja bali alisema yeye anaamini Taurat na Qur’an lakini Taurat yenyewe haipo tena. Kwa ninavyofahamu Muislam akiulizwa kuhusu dini yake bila kupepesa macho atatoa jibu la moja kwa moja kwamba mimi ni Muislam lakini kwa Arsis haikuwa hivyo.

Swali: Kwa nini Arsis yupo jamii Forums?
Jibu: Arsis yupo jamii forums kwenye mission maalum inayoshirikisha majini na wanadamu hapa duniani kwa lengo la kuitia shaka Qur’an na kuibadilisha Qur’an ifike kama Wayahudi walivyoitoa Injili kuja kuwa biblia. Miongoni mwa wanadamu wanaofanya hivi ni mtu mmoja anaitwa Dr. Hanny na channel yake iliyopo YouTube inayoitwa "Marvellous Qur’an". Wapo kadhaa nawafahamu ila kwa leo tumuangalie huyu Dr. Hanny ila nashauri kama hujapikika vizuri kwenye dini usiangalie hii channel utapotea!

Huyu Arsis, Dr. Hanny wanazungumza kitu kimoja kwamba Adam sio mtu wa kwanza, Maryam hakuwa bikra, dua zote zenye neno la Allahumma zibadilishwe na litumike neno Rabbana, Nabii Nuh hakuishi miaka 950, Aya nyingi ndani ya Qur’an zimekosewa, Salamu tunayoitumia ya Assalamu Alaykum imekosewa bali inatakiwa iwe Salamun Alaykum, yaani ukiwasikiliza unakuja kukuta 75% ya Qur’an imekosewa. Hapa ina maana kwamba Qur’an nayo itakuja kuitwa kwa jina jipya kama ilivyokuwa Injili leo tunaona Biblia.

Mimi nilijaribu kum challenge Dr. Hanny kwenye comments akawa anafuta comments zangu halafu ana network kubwa ya kiyahudi ambapo ukipingana nae followers wake wanakuvamia mmoja baada ya mwingine. Ukitaka kujua kuwa ile ni network chunguza utakuta wale wanao comment ni comments za kumsifia Dr. Hanny na kukubaliana nae kile anachokiongea lakini zile za kupingana nae huzioni na ukiziona zipo chache halafu hazikai muda zinafutwa! Wapo baadhi ya wanazuoni walishindana nae kihoja mpaka wengine wakapelekea kupewa vitisho hapo ndipo utapojua kuwa huu ni mtandao mkubwa hapa duniani.

Dr. Hanny anadai wanazuoni waliopita walikuwa ni traditional scholars na wamewadanganya waislam kwa miaka 1400 hivyo tunatakiwa tuachane na huo upotevu na tufuate modern thinking! Yaani wanazuoni kama kina Imam Shafi, Abu Hanifa, Malik, Hanbal, etc hawa watupiliwe mbali waliwapoteza Waislam na hii ndio thinking ya Arsis indirectly kama mtamchunguza vizuri.

Ushauri wangu kwa wale wote wanaomuamini Arsis jueni ya kwamba mnachukua elimu kutoka kwa Sheitwani na huyo Arsis si Muislam bali ni Myahudi na yupo hapa katika mission maalum ya kuhakikisha Qur’an inatafsiriwa ndivyo sivyo. Yale mafundisho yake ya Nabii Adam kuwa sio mtu wa kwanza yatupilieni mbali. Kuna mtu mmoja alituonya humu ndani tusichukue elimu kutoka kwa majini kwa kuwa hatuwaoni na wala hatuwajui alikuwa yupo sahihi kabisa! Swali la kufikirisha: kuna wakristo na waislam wachache humu ndani walimpinga vikali Arsis sasa tujitathmini imani zetu na zao zipi zenye mashaka.

Hebu tuangalie Qur’an kidogo:
(Na siku atakayo wakusanya wote, kisha atawaambia Malaika: Je! Hawa walikuwa wakikuabuduni? Qur’an 34:40)

(Waseme: Subhanak, Umetakasika. Wewe ndiye kipenzi chetu si hao. Bali wao walikuwa wakiwaabudu majini; wengi wao wakiwaamini hao. Qur’an: 34:41)

Hapo Qur’an inatuonya ya kwamba wengi katika watu watakuwa wakiwaabudu majini. Swali la kujiuliza katika hao wengi je mimi na wewe tumesalimika vipi hapo?

Huyo Simba ambae ni kiti wake yeye mwenyewe anahitaji Rukya ili aweze kuondokana na huo msiba wa Arsis.

Ndugu zangu mafundisho ya Qur’an yaliyotoka kwa Mtume (saw) yakaenda kwa Maswahaba, ndio hayo hayo yaliyodumu kipindi cha miaka 300 ya mwanzo ya Uislam, ndio hayo hayo yaliyofundishwa na Maimamu wanne, na ndio hayo hayo ambayo yametufikia mpaka leo. Hivi kweli inaingia akilini Allah ashushe kitabu ambacho kisieleweke na kipoteze watu kwa miaka 1400 halafu leo karibu na Kiyama ndio kitabu kieleweke na cha ajabu wanaotoa hayo mafundisho Kiarabu sio lugha yao ya asili.

Lingine tushikamane na sunnah za Mtume (saw) maana kushikamana na sunnah sio jambo dogo. Says Rasulullah (pbuh): "Hold on to the sunnah with your molar teeth"

Na ndio leo hii unaona watu kama kina Arsis na Mayahudi wanapinga hadithi maana hadithi ndio sunnah za Mtume unapozikuta. Bila hadithi utaijuaje biography ya Mtume (saw)? Jina la Mtume limetajwa ndani ya Qur’an mara 4 tu. Mtume aliezungumziwa zaidi kwenye Qur'an ni Nabii Musa (AS). Hapo utaona ujanja wa kina Arsis wa kuwafanya watu wazipuuzie hadithi kwa kuzitia dosari za hapa na pale ili seerah ya Mtume (saw) ipotee. Tumejionea hivi karibuni baadhi ya nchi za Kiislam zimepiga marufuku idadi nyingi ya hadithi. Hii vita ni kubwa kuliko tunavyofikiria.

Msihadaike na Arsis pale anapopewa majibu makali anajifanya kama haumii anayajibu kwa hekima. Sio kwamba haumii bali yeye ni kiumbe kama sisi anaumia ila hiyo ndio silaha yake ya kuwateka nyoyo zenu.

Ndugu zangu hii ni sadaqa yangu kwenu kama kuna mtu nitakuwa nimemkwaza basi ukamilifu ni wa Allah!

Allah atusamehe sote na atuongoze katika njia iliyo sawa.
 
Kama kipi?
Humu Kuna taswira tofauti tofauti za ulimwengu wa kiroho.

Hasa upande wa chini (upande wa majinn na mashetwan wanavyofanya fanya kazi.

Pia uhusiano kati ya binaadam na ulimwengu wa kiroho jinsi ulivyo!!

Kuna vitu kama:
👉 Viumbe wanazidiana nguvu
👉 Viumbe wanakufa pia
👉 viumbe ni waongo saaaana tena saaaaaana

👉Nafasi ya Mungu kwenye maisha ya mwanaadam
👉Elim ya ghaib imefichwa na Mungu wanayoijua ni wachamungu pekeyao,,,,, mpk majinn na maibiris hawaijui ila wanajua juu juu tu.
👉Ukuu wa mwanaadam ni mkubwa kuliko mashetwan na majinn

Hayo yote yamegusiwa humu ndani,,,, japo mengine kwa lugha za picha.
Mengine utayajua baada ya kusoma zaidi elim ambazo hata waleta mada wenyewe hawana.

Kwahyo kufupisha habari, angarau faida ya hapa na pale ipo.....
(Arsis, kajitahidi sana kwa kiasi chake, wacha tumpe maua yake mapema
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom