Binafsi nilitokea kukichukia Chama changu Cha Mapinduzi yaani CCM tangia nikiwa sekondari. Chuki zangu dhidi ya CCM sikupandikizwa na mtu bali uelewa na upeo wangu mkubwa wa masuala ya kitaifa.
Nakumbuka nikiwa kidato cha kwanza mpaka namaliza kidato cha Sita nilikuwa na ndoto ya kuwa Rais wa Tanzania siku moja..
najua wengi mnacheka ila nilikuwa serious kabisa, na bado nina ndoto ingawa inafifia ila ya Mungu mengi wenda akaiamsha upya.
Mwaka 2015, binafsi nilikuwa mpinzani mkubwa wa MAGUFURI sababu kubwa ilikuwa nampinga MAGUFURI zi yeye bali kuwa mgombea wa CCM iliyokuwa imechakaa sana na hiaijiwezi tena... Hivyo niliamini MAGUFURI atakuwa kama Marais waliomtangulia ukimuondoa mwl. NYERERE.
Msiojua Tanzania vyema na uelewa wa siasa za Tanzania yetu hamuwezi kujua kuwa tulikuwa tunatawaliwa KIFALME. Namanisha tabaka la watu/familia fulani zilijidhatiti kuhakikisha wanatutawala milele. Ila kwa kuwa MUNGU SI ATHUMANI WALA YOHANA siyo nilichokuwa nakiwaza kinafanywa na MH. RAIS MAGUFURI kwa asilimia kama 95% hivi, licha ya dosari ndogo dogo yeye si malaika.
Hivi Karibuni kulitokea udukuaji wa mawasiliano ya baadhi ya MAKADA WA CCM sitapenda kuzungumzia uhalali wa kudukua mawasiliano ya mtu, wanaojinasibu kuwa wao ndiyo CCM ASILIA, nisikitike kusema kuwa hili ni GENGE moja hatari kabisa lenye malengo mahususi ya kuitawala Tanzania kwa msingi ya koo na urafiki wa kifamilia.
Kama umefuatilia maongezi ya mzee YUSUFU MAKAMBA, JANUARY MAKAMBA NA NAPE NAUYE utakuwa ulionote kitu gani hawa jamaa wanapanga, moja kwanza no dhahiri kuwa wao waliamini Wana Hati na haki miliki ya kudumu na kuitawala Tanzania. Mzee MAKAMBA anasikika akimwelekeza NAPE kuwa baba yake NAPE mzee NAUYE na KINGUNGE NGOMBARE MWIRU eti hajawajatambuliwa mchango wao kwa kepewa majina ya mitaa. Hapo ndipo utajua kuwa kuna koo za kiutawala nchii hii.
Pia ndugu, KAMILIUS MEMBE ukimsikiliza hoja zake utagundua kauli zake anakerwa na kitendo cha MH. Rais MAGUFURI kuteuwa watu pasipo kujali hizo koo za kiutawala na hasa kitendo cha kuzibomoa hizo koo tawala.
Kimsingi naomba kumshukru na kumpongeza MH. Rais MAGUFURI kwa jinsi anavyofanya teuzi zake bila kujali hizi koo tawala. Enzi za NYUMA ilikuwa fhahiri kujua nani anaandaliwa kuwa Rais kitu ambacho ni ujinga kwa taifa la watu wapenda demokrasia ingawa Ina ukakadi bado.
Wapinzani niwashauri kitu, kwasasa hamna MTU MBADALA WA QUALITY ya MAGUFURI kusema mkampanishe, ata CCM hawana huyu MEMBE anashida na urais wala shida wala hashira na shida za watanzania. Mkenge wanaouvaa Wapinzani ni kuacha kuzima nyumba yao inayoungua na kujiunga na koo tawala eti lumpinga MAGUFURI.
Movie nyingine inayochezwa na Wapinzani ni UKANDA na UKABILA, hili nimeliona kanda ya kaskazini hasa ARUSHA na Kilimanjaro turufu ya kumpinga MAGUFURI Iliyobakia ni kupandiza UKABILA na UKANDA hii dhambi ya upanguzi inayofanywa na Wapinzani itawatafuna na imeisha anza uwezi amini Upinzani unakufa slowly kaskazini.
Mimi huwa ni mtafiti mzuri sana, vita dhidi ya MAGUFURI inaongozwa na wachaga ila mjue hizi cheap politics huwa hazidumu ni kama upepo zinapita fasta.
Kitendo cha MH. Rais MAGUFURI kuligeuka hili kunditawala/Kootawala Namuona shujaa na jasiri kabisa.
Nimalize na HEKIMA YA MZEE DR. SLAA" Vijana tunavyotaka mageuzi lazima tu tafakari juu ya AINA YA MAGEUZI TUNAYOTAKA na NJIA SAHIHIHI ZA KUYATAFUTA/KUYAPATA.
ViVa MAGUFURI...2020.