Harrison Justine
JF-Expert Member
- Jun 19, 2015
- 1,136
- 559
Mie anipigie tu push up 20 kila day yaani nitafurahi
sura mpya zinahitajika, zisizo na uogaa kabisaa
mr makonda
bulembo
polepole
shonza
kishimba
mkuu kuna kasoro naiona hapa kuna rais na makamu wake ambaye huyu ataitwa msaidizi wa rais ,pale nairobi wana mfumo mzuri rais huambatana na makamu wake katika shughuli za kikazi mfano kukagua ,kutoa maelekezo kweli inapendeza hapa kwetu hali ipo tofauti hili mkuu tuliweke sawaRais ndio huyo tena ameshaapishwa, waliomtaka na wasiomtaka ila wote hawa ndio rais wao wa awamu ya tano.
Je, wewe raia ungependa rais aanze na jambo lipi kulitendea kazi au kulisimamia ambalo unaona ni la muhimu na kwa sababu zipi?
Wote ondoa ila prof.muhongo muache
. Ni mtu makini, mkali, anunuliki, msomi na anaogopeka uliza mameneja wa Tanesco, watakuambia. Huwa hana utani, ni the strongest candidate.
Mi ni ukawa pure
Pamoja na kwamba sina imani na chama chako, ila naomba unishawishi wewe binafsi katika serikali yako.
Kama ulivyojinaji kuwa serikali yako, yani Tanzania ya Magufuli itakuwa KAZI TU, basi naomba udhihirishe hivyo katika baraza lako la mawaziri.
Kabla hata sijataka kujua waziri mkuu ambaye ataendana na sura ya kauli mbiu yako, lakini nataka usituletee watu hawa ambao walikuwa mzigo kwa taifa na waliolifikisha nchi hapa ilipo chini ya aliyekutangulia pamoja na waziri mkuu wake.
1. Sopteter Muhongo.
Huyu pamoja na kwamba tunaambiwa hakuhusika moja kwa moja kwenye kashfa xa escrow lakini alikuwa kinara wa utetezi katika sakata hili. Pia ni miongoni mwa waziri wenye elimu kubwa lkn hakuwa na mkakati bunifu wa kutatua tatizo la umeme nchini zaidi ya kuiacha tanesco kwenye deni kubwa. Pia ni miongoni mwa viongozi ambao hawathamini wawekezaji wa ndani, anaamini nchi itajengwa na wazungu au wachina.
2. Lazaro Nyalandu.
Huyu ni miongoni mwa mawaziri ambao tumeshuhudia tembo wakiuliwa kwa wingi, na twiga wetu wakisafirishwa kwenda nje, hafai katika serikali yako, kwani atafanya kazi ya mazoeaa ya serikali ya awamu ya 4.
3. Mwigulu Nchemba.
Pamoja na kwamba hakukaa kwenye wizara ya fedha kwa mda mrefu, lkn ni miongoni mwa vijana ambao hawana adabu katika taifa hili. Ni mmoja wa wanasiasa wachanga ambao hajali matamshi yake mbele ya umma, haangalii baada ya hapa athari zake zitanipeleka wapi, sio mstaarabu.
4. Willium Lukuvi.
Huyu kwa mwendo wa kasi inayohitajika nchini hatufai, utendaji wake hauto tofautiana na wa awamu ya 4, hana jipya ndani ya serikali yako.
5. Shukuru Kawambwa
Huyu ni moja ya mawaziri walioshusha thamani ya elimu yetu. Sio mbunifu. Fedha za fidia za rada mpaka leo hatujui matumizi yake yalienda wapi, hatufai kabisaa.
6.Hawa Ghasia.
Huyu mama bado uchama umemkaa kichwani kuliko maslai ya taifa. Hayupo active katika utendaji wake.
7. Jumanne Maghembe.
Huyu ni moja ya mawaziri ambao ndio chanzo cha huduma mbovu za elimu na maji. Elimu yake ni kubwa lkn haina msaada kwetu.
8.Harrison Mwakyembe.
Huyu kinachompa sifa ni lile sakata la richmond ambalo tunamwona kama shujaa. Lakini kiukweli hafai hata kuwa mwenyekiti wa kijiji. Sijaona mafanikio yake katika wizara alizozisimamia, ni mzigo ana asili ya mtandao ambao ni chanzo cha utendaji mbovu nchini. Ni mafya wa kisiasa
9. Magreth Sitta
Mama huyu tangu zama ni outdated, haendani na kasi ya dunia, yupo nyuma na mda, hafai katika serikali yako.
10. Sofia Simba
Hana tofauti na Mama sitta, tena huyu uchama na mtandao wa uongozi umemjaa kichwani, hafai katika serikali yako.
11. Andwer Chenge
Najua huyu unamfahamu vema
12. Anna Tibaijuka
Najua unamfahamu vizur
13. Willium Ngeleja
Najua wamfahamu vzr
NB.
1. Mheshimiwa Rais kuna vijana wengi ambao naamini katika utendaji wao lkn siamini kundi lake, na mmoja wao ni Januari Makamba. Huyu binafsi namwamini kiutendaji, ubunifu lakini kinachomsumbua ni kutaka madaraka makubwa, kundi lake lililo nyuma yake, Huyu badala ya kuchapa kazi atakuwa anawaza urais baada yako kustaafu. Kwa mtazamo wangu ungemweka kando kwa mda baada ya miaka miwili ndo uumpe majukumu.
2. Kwa kukusaidia mh Rais ni vema ukachagua mawaziri wachache ambao wengi wao hawakuwa mawaziri, sio viongozi katika chama, vijana, wenye elimu isiyo na shaka. Hawa ndio wataileta tanzania mpya ya HAPA KAZI TU.
Mh Rais ukikosea kwenye baraza la mawaziri basi jua umeuwa nchi, na hapo tutadhibitisha kuwa hakuna cha Magufuli 4 change itakuwa ccm ni ile ile.
Asantee.
Tueleze ni kwanini wanafaa?Muhongo, Mwigulu, mwakyembe wanafaa sana kuwepo hao wengine hawafai wote
Kabla hata sijataka kujua waziri mkuu ambaye ataendana na sura ya kauli mbiu yako, lakini nataka usituletee watu hawa ambao walikuwa mzigo kwa taifa na waliolifikisha nchi hapa ilipo chini ya aliyekutangulia pamoja na waziri mkuu wake.
2. Lazaro Nyalandu.
Huyu ni miongoni mwa mawaziri ambao tumeshuhudia tembo wakiuliwa kwa wingi, na twiga wetu wakisafirishwa kwenda nje, hafai katika serikali yako, kwani atafanya kazi ya mazoeaa ya serikali ya awamu ya 4.
Mimi namkubali Prof Muhongo kwa sababu ni mtu wa facts, anaongea kitu ambacho kipo direct. Kuhusu kuthamini wawekezaji wa ndani sio kwamba hawathamini ila ni ukweli ulio wazi kwamba sekta ya nishati na madini inahitahi wawekezaji ambao wako full competent. Mfano kipindi cha mzozo wa vitalu vya gesi alitaja technical and financial requirements ambazo mwekezaji anatakiwa kua nazo ili apate kitalu.. Akasema anayeona ana qualify basi aende ofisini. Na kuhusu kutetea, ni kawaida waziri yupo upande wa serikali na lazima atetee serikali yake.
Muhongo kichwa aliingizwa chaka nA wabongo, huyu arudi tena kwenye nishati alisimamia vema tanesco
Wachezaji walewale endapo watabailishiwa kocha na kuletewa mzuri watafanya vizuri!
Je? La kuhamia Dodoma limo?
Mwambie arudishe pesa za umma kwanza (Esclow) then ndo urudi hapa kumpigia chapuo ya uwaziri