Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Depal yeye jana kashinda 4 bila leo kafungwa 7 kwa 2, huko aliko anafanya kalukulesheni itakuwa 7 kwa 6 hivyo haimuumi sana, goal dıff ni 1 tukama alivyofungwa Sheffield tuila nyie wengine sasa
Depal alienda mbele hatua nne akarudi nyuma hatua saba😂😂😂 hii yote ni kutokutulia na clab bora anakimbilia utopolo kama huu
 
Timu ikifungwa shabiki yeyote hua ghafla anajua kumzidi kocha.

Watu wanasema eti Adrian shati. Adrian kawapa kikombe mmecheza mechi nne au tatu kama sikosei yeye akiwa golini na mkashinda. By that time Adrian alikua analindwa na beki pamoja na kiungo Henderson, Fabinho na Gini ilikua ngumu mtu kupata chansi ya kushut kama hivi.

Jamaa mmoja humu nilibishana naye kipindi fulani yeye alikua analalamika kwanini Henderson hatoi assisst kama KDB nikamuelewesha kua usitarajie assisst kutoka kwa Henderson kwakua ni DMF. Hata Gini kwa liva ni CMF tofauti na akiwa timu ya taifa. Kile kiungo na defense ndiyo kilikua kinamlinda Adrian.

Mwisho alinitukana yule jamaa.

Kwa jana ulionaje mid na defense ya liva? Ilikua komedi.

Now hizi komedi zilitakiwa zionekane tangu msimu uanze. Msimu umeanza virgil amefanya makosa 3 ambayo yote yamepelekea magoli so huyu jamaa dalili tangu mwanzo zilishaonyesha ni wapi alipofikia. Mtu anamlaumu Adrian eti shati, unabaki unajiuliza huyu kaangalia mpira kweli au kasoma matokeo livescore? Magoli aliyofungwa Adrian kipa yeyote anafungwa. magoli ya deflection? Yeyote anafungwa, goli la Barkley si ndiyo kama hilo kafungwa Ederson na Maddison juzi tu?

Kuna eneo mchezaji akikaa kipa inabidi ajaze upande fulani mchezaji akimanage kupiga upande kipa hajajaa hua ni goli. Haina mjadala. Kasave one vs one ambayo ilitakiwa isome 7.

Watu wote mnaachana na ukweli wa kujua kua defense na mid hazikua na ushirikiano zigo la lawama mnataka kumpa Adrian.

Haya wengine wanadai eti liva wabahili. Hivi kabla ya maguire beki ghali alikua nani? Aliyeanzisha mchezo wa kununua mabeki hela nyingi nani? Mid ya liva ina thamani ya zaidi ya 130M wakati mid ya timu inayoongoza ligi ni chini ya 70M pesa ambayo kwa liva ilinunua beki mmoja tu. Na kama haitoshi liva ndiye ina mchezai wa kiafrika anayelipwa kuliko wote duniani.

Ubahili uko wapi hapo?

Mwingine analalamikia high defensive line. Liva inakabia gegenpress. Mpinzani akipata mpira wachezaji watatu wa liva wataufata mpira aggressively wanauretrieve fasta na kuutoa kwa winger Mane au Salah. Ili ukabe hivi huwezi kua defensive line nyuma ni lazima ipande, hii system ya kukaba ni nzuri kama mid ipo strong na defense strong. Mid ya jana ilikuaje? Je defense? Kwahiyo Klopp alitaka kufanyia majaribio ya mid kwa Villa.

Kuna mtu anadai 7 kwa 2 ila kwa tabu kwakua wao ndiyo wamemiliki mpira muda wote. Haya uliza City wakati anabugizwa 5 na Leicester alikua na possession ngapi. Hii hoja ya chenga twawala ni hoja mufilisi.

Hiki kikombe mlichonywea hakina lawama isipokua mpinzani alikua vizuri katika kuibeat gegenpress zaidi ya chelsea na Arsenal. Leeds walitakiwa wawe wa kwanza ila penati zikawabeba.

Kama kawaida kiingereza kimepamba moto.
 
I can't believe! Pepoz doing everything to protect Adrian, for what reason?
Jamaa ametuchomesha! Period.
Ebu taja makosa yote ya Adrian
Goli la kwanza lake
Goli la pili counter
Goli la tatu deflection
Goli la nne - poor defending
Goli la tano la Barkley - Deflection
Goli la sita - deflection
Goli la saba la Gomez - poor defending
Kwea ufupi timu jana utadhani haikutokea kwenye mazoezi
Mabeki hawakuwa na compsure ya Liverpool tuliyoizoea hasa Gomez kaiozesha safu nzima ya nyuma, kule mbele Mane ndie huwa anaichangamsha , jana mbele ilipooza mno
Msimtoe kafara Adrian hata kama kiukweli ni kwamba sio kipa mzuri kama Alisson lakini kosa lake jana ni goli la kwanza tu
Hata hivyo Adrian aliokoa baadhi ya counter kama m,bili hivi zingekuwa 9 jana
 
Hahahaha najua Chelsea ipo moyoni ila nahisi Mr wako atakuwa Liverpool hivyo unamsaport kinamna ..lakini piga ua wewe ni Chelsea damu..

Btw leo AstonVilla tuna jambo letu .leo tunachana mikeka ya watu
Tulichana mikeka jana😂😂😂😂😂😂
 
7-2.... Mashabiki wenzangu wa Liverpool maandamano yetu leo yataanzia Mnazi Mmoja mpaka kwa Mkuu wa Mkoa... Yule Adrian wa nini pale ???
 
*Hawa manure fc kimeshakuwa kikundi cha wahuni na siyo timu ya wacheza mpira kabisa*
Hahahaha hichi chenu kikundi cha mateja 😂😂😂..bora manyumbu kidgo afadhali ni wahuni tu hawana mbele wala nyuma😜😜😜😜
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom