Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Liverpool FC (The Reds) | Special Thread

Inauma sana tena sana mimi kwa kiasi kikubwa namlaumu Gomez na Arnold, poor defending sisemi kama wachezaji wabaya ila kwa jana hapana na pia VVD hakusimama kama kiongozi wakati jahazi linazama. viuongo wametuangusha sana wamepoteza mipira mingi sehemu mbaya makosa makubwa huku kipa sitaki kusema maana wote tunajuwa msimu ukianza hatutegemei kama atacheza lakini ndio hivyo. sio kwamba tulizidiwa hapana ila makosa mengi sana wamefanya Villa waonekani kama Bayern. Kufungwa kunauma hata yule Maguire wa Man u baada ya mechi yetu kasahauliwa anaonekana mzuri tu .......
 
Ok naona mnataka epl na uefa tu ,lakin hivo vikombe vinawakataa mapema sana



Labda mnajiandaa kutoka empty this season
 
Nashindwa kuwalaumu sana misimu mi 3 mmepiga mpira wa nguvu sna na kikosi kilikuwa finyu all in all mpira una maajabu yake ukinaswa ndio hivyo tena mara wiki mara 6 mara 5 za city
Ahaha mkuu Hii ligi mwaka huu imekuwa na maajabu sana unaeza shangaa EPL ikachukuliwa na midtable team.

Ila bado saba nyingi aise
 
Sioni wa kutupiga pale EPL labda timu zikijitahidi zipate droo. EPL inarudi Anfield
Duh kweli mzee si tumeona kwa matokeo ya jana
IMG-20201004-WA0212.jpg
 
Goli 7 unasema wameshinda kwa taabu.visingizio havikosekani.wewe kubali kuwa mmefungwa kwa uhalali sio tena unaanza kusema mara hao kwa taabu
Liverpool hawana deep squad. Kukosekana kwa mane mbele imekuwa butu. Kukosekana kwa Alisson golini kumeonekana jana
Siku akiongezeka na VVD yaani VVD, MAne na Alisson wote wakawa majeruhi, Liverpool ni ya kujipigia tu. Ombeni Mungu hili ninalolisema lisitokee
 
Hakuna,

Mimi nimecheki game alfa na omega, goli 4 ni deflection wamemuuza mabeki, na hayo mengine mawili counter mabeki wamechomesha, moja penați, tena amesave 1 against 1 kama mbili hivi, ambazo leo hii tungekuwa tunazungumzia 9 kwa 2,

Kipa kajitahidi sana tena sana
Hata kama ingekuwa Alisson, zile deflections asingeweza kuzizuia, labda angepunguza magoli kutoka 7 kwenda 5 hivi
 
Kampeni ni nzito ila kipigo chenu mlichokipata nikizito sana kiufupi ni cha kiada na ziada .
 
Nasikia jogoo amegongwa na bodaboda barabarani,mnaambiwa muwafungie kuku hamsikii.
 
Ndugu kimewakumba nini? Yan jana nikajisemea game yenu hata siangalii nikaamua kujikita kwenye shughuli ya kijamii walau nimalize weekend vizuri. Daah kumbe nimekosa burudani na utamu mwanana kuliko hata huo wa kijamii.

Daah roho inaniuma sana. Kwanini mimi nisimuliwe huu mkasa!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom