Madela Wa- Madilu
JF-Expert Member
- Mar 24, 2007
- 3,062
- 731
Ukisha sema hujui kwa nini nchi yako ni masikini tayari unakuwa umekwepa maswali million. Kila swali zuri utaendelea kusema hata mimi najiuliza vivyo hivyo. Huo ni Ujanja wa kitoto ambao Rais wa nchi hatakiwi kusema hata siku moja.
Rais alitakiwa kuelezea ndoto yake alo kuwa akiiota kila siku katika kipindi chote cha miaka 10 kabla ya kujiandaa kuwa rais wa nchi.
Unajua nini? Ukienda Ikulu bila mikakati na agedna zako mwenyewe za kuikwamua nchi kiuchumi, Kisiasa na kiutamaduni ukifika huko utapewa KIONGOZI CHA MWALIMU na Mafisadi ili usome majibu ya namna ya kuiongoza nchi.
Mtu aliye jiandaa miaka 10 kuwania kiti cha Urais hawezi kusema hajui kwa nini nchi yake ni masikini.Labda tu kama agenda yake ya kuwa rais wa nchi ina uhusiano na Ufisadi.
Mwonekano wa Tanzania na Watanzania wake ni kama tumetoka kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa kutumia mishale,pinde na mundu. Nchi iko hoi bin Taabani halafu Mshenzi Habithi huyu( JAKAYA KIKWETE) anadai hajui kwa nini tuko nyuma?
Kuna majibu yanaudhi hasa Msemaji akiwa ni Rais wa nchi.
Nikimwuliza leo hii ni kipi kina idadi kubwa kati ya vifuatavyo atasema nini.
A Matrekta ya wakulima wote Tanzania.
B Mashangingi ya serikali
Nikimwuliza leo hii kwa nini anatibiwa nchini Ufaransa hata ugonjwa wa mdogo tu wa shibe atasema nini?
Kwa sababu amefanya kila linalo wezekana huko Muhimbili na Muhimbili haijaweza kuwa Sibitali ya hadi yake?
Mfalme wa Japan aliwahi kutembea bila Viatu kwa muda fulani hadi siku nchi yake ilipo tengeza viatu kwa wanchi wake.
Japan enzi hizo walikuwa wakiagiza viatu toka China.
Leo hii sisi ile List ya Mafisadi na Makuadi wao telke ambao hawajatajwa wanashindana na kukogana kwa kuvaa viatu vya Mtaliano halafu majibu yao "Sijui kwa nini Tanzania iko nyuma?" Ya kweli hayo??
Ingekuwa vema kwa rais wa nchi kugoma kutibiwa nje ya nchi mpaka kieleweke pale Muhimbili.
Hivi serikali inashindwa kabisa hata kuanzisha VIP wing ya Muhimbili kwa ajili ya Viongozi wa serikali na kuindeleza hatua kwa hatua kwa kuipanua kila mwaka wa fedha hadi iwe ni Sibitali ya kila Mlalahoi?????
Akili nywele kila mtu ana zake, sasa sijui Mungai na kipara chake bado anaakili?
Mwalimu wangu wa somo la Critical Thinking aliwahi kuniambia njia rahisi ya kutambua matatizo yako na kutafuta masuluhisho yake ni kujiuliza maswali?
Marekani ni chi tajiri na iko dunia ya kwanza. Tanzania ni nchi masikini na iko dunia ya tatu kwa nini?
Marekani wanatengeneza matrekta yao wenyewe Tanzania hatutengenezi matrekta yetu wenyewe kwa nini?
Rais wa marekani hatibiwi Ufaransa au katika nchi nyingine yeyote duniani hata kama ugonjwa ni wa kuhatarisha maisha yake, Rais wa Tanzania anatibiwa nje ya nchi hata kama ugonjwa ni kuvimbiwa vitumbua sukari kwa nini?
Maswali yako mengi ambayo Rais Kikwete alitakiwa kujiuliza kabla ya kujiuliza na kujibu swali la kwa nini Tanzania haiendi mbele KIFISADI.
Kuhusu Mikataba ya kuchimba madini Tanzania.
Si kweli kwamba Kuna kipengere kimoja tu cha kutishia maendeleo yetu ndani ya mikataba hiyo, labda kama alisomewa mkataba huo na wasidizi wake.
Mikataba ya madini na makampuni ya uchimbaji yote ni Batili na lazima ibadirishwe kwa nguvu za wananchi kupitia Bunge lao ambalo litakuwa na 45% wabunge wa SISIEMU ifikapo mwisho wa 2010.
Kwa vile Rais Kikwete alisha shiriki kuingia mikataba ya madini na wachimbaji kwa lugha nyingine ameshiriki kuididimiza nchi kwenye lindi la umasikini.
Kikwete amesoma Political Ecomy pale Mlimani, sijui ni vipi anashindwa kujibu swali la nchi ya Tanzania kuwa masikini.
Akiletewa Balance sheet ya kiingiacho na kitokacho Tanzaniia na kinakwenda katika mfuko wa nani, hata kama yey Kikweteni mjinga wa Accounts kama mimi atajua kwamba Hesabu hazijatukali vizuri sisi watanzania.
Kikwete anaiambia Dunia SISIEMU imefanya kila lililo ndani ya uwezo wake kufuta umasikini Tanzania na sasa imefikia mahala imechanganyikiwa na inajiuliza kwanini kijiwe chao Haki Mix.
Maelezo hayo yana maana moja tu SISIEMU si chama cha kutupeleka kwenye maendeleo ila ni mzingo mzito kwa kila raia wa Tanzania.
Ni lazima tuachane na kundi la mbweha watu hao wajiitao SISIEMU walioishiwa mbinu za kujenga uchumi wa nchi.
Ni lazima tuachane na kundi la mbweha watu hawa wajiitao SISIEMU wasio weza kukiri kushindwa, kukiri kuvurunda na kuwa na shingo ngumu kugeukia uelekeo wa maendeleo.
Lazima tuachane na uongozi wa SISIEMU chama muflisi chenye viongozi wenye macho makubwa kama ya Bundi lakini hayatazami na masikio makubwa mithiri ya yale ya Tembo wa lake Manyara lakini hayasikii hata mlio wa radi.
CCM kama chama kimeshindwa kabisa, kwa hiyo sisi watanzania hatuna haja ya kukipa muda wa kuendelea kushindwa.
Endapo baada ya miaka 46 ya kutawala nchi rais wa awamu ya 4 hajui kwa nini nchi yake ni masikini! Sembuse mwanachama wa SISIEMU mlima Kunde kule kijiji cha Mtulingala Malangali?
Najiandaa kwenda gombea Ubunge mwaka 2010 kupitia chama cha upinzani.
Kama mimi sijitokezi na mtu mwingine mwenye uchungu na usongo na nchi yake hajitokezi basi tutaendelea kuongozwa na Mahabithi,Majuha na Mafisadi washenzi hawa milele.
ALUTA CONTINUA MAPAMBANO NDO KWANZA YANAANZA
Rais alitakiwa kuelezea ndoto yake alo kuwa akiiota kila siku katika kipindi chote cha miaka 10 kabla ya kujiandaa kuwa rais wa nchi.
Unajua nini? Ukienda Ikulu bila mikakati na agedna zako mwenyewe za kuikwamua nchi kiuchumi, Kisiasa na kiutamaduni ukifika huko utapewa KIONGOZI CHA MWALIMU na Mafisadi ili usome majibu ya namna ya kuiongoza nchi.
Mtu aliye jiandaa miaka 10 kuwania kiti cha Urais hawezi kusema hajui kwa nini nchi yake ni masikini.Labda tu kama agenda yake ya kuwa rais wa nchi ina uhusiano na Ufisadi.
Mwonekano wa Tanzania na Watanzania wake ni kama tumetoka kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa kutumia mishale,pinde na mundu. Nchi iko hoi bin Taabani halafu Mshenzi Habithi huyu( JAKAYA KIKWETE) anadai hajui kwa nini tuko nyuma?
Kuna majibu yanaudhi hasa Msemaji akiwa ni Rais wa nchi.
Nikimwuliza leo hii ni kipi kina idadi kubwa kati ya vifuatavyo atasema nini.
A Matrekta ya wakulima wote Tanzania.
B Mashangingi ya serikali
Nikimwuliza leo hii kwa nini anatibiwa nchini Ufaransa hata ugonjwa wa mdogo tu wa shibe atasema nini?
Kwa sababu amefanya kila linalo wezekana huko Muhimbili na Muhimbili haijaweza kuwa Sibitali ya hadi yake?
Mfalme wa Japan aliwahi kutembea bila Viatu kwa muda fulani hadi siku nchi yake ilipo tengeza viatu kwa wanchi wake.
Japan enzi hizo walikuwa wakiagiza viatu toka China.
Leo hii sisi ile List ya Mafisadi na Makuadi wao telke ambao hawajatajwa wanashindana na kukogana kwa kuvaa viatu vya Mtaliano halafu majibu yao "Sijui kwa nini Tanzania iko nyuma?" Ya kweli hayo??
Ingekuwa vema kwa rais wa nchi kugoma kutibiwa nje ya nchi mpaka kieleweke pale Muhimbili.
Hivi serikali inashindwa kabisa hata kuanzisha VIP wing ya Muhimbili kwa ajili ya Viongozi wa serikali na kuindeleza hatua kwa hatua kwa kuipanua kila mwaka wa fedha hadi iwe ni Sibitali ya kila Mlalahoi?????
Akili nywele kila mtu ana zake, sasa sijui Mungai na kipara chake bado anaakili?
Mwalimu wangu wa somo la Critical Thinking aliwahi kuniambia njia rahisi ya kutambua matatizo yako na kutafuta masuluhisho yake ni kujiuliza maswali?
Marekani ni chi tajiri na iko dunia ya kwanza. Tanzania ni nchi masikini na iko dunia ya tatu kwa nini?
Marekani wanatengeneza matrekta yao wenyewe Tanzania hatutengenezi matrekta yetu wenyewe kwa nini?
Rais wa marekani hatibiwi Ufaransa au katika nchi nyingine yeyote duniani hata kama ugonjwa ni wa kuhatarisha maisha yake, Rais wa Tanzania anatibiwa nje ya nchi hata kama ugonjwa ni kuvimbiwa vitumbua sukari kwa nini?
Maswali yako mengi ambayo Rais Kikwete alitakiwa kujiuliza kabla ya kujiuliza na kujibu swali la kwa nini Tanzania haiendi mbele KIFISADI.
Kuhusu Mikataba ya kuchimba madini Tanzania.
Si kweli kwamba Kuna kipengere kimoja tu cha kutishia maendeleo yetu ndani ya mikataba hiyo, labda kama alisomewa mkataba huo na wasidizi wake.
Mikataba ya madini na makampuni ya uchimbaji yote ni Batili na lazima ibadirishwe kwa nguvu za wananchi kupitia Bunge lao ambalo litakuwa na 45% wabunge wa SISIEMU ifikapo mwisho wa 2010.
Kwa vile Rais Kikwete alisha shiriki kuingia mikataba ya madini na wachimbaji kwa lugha nyingine ameshiriki kuididimiza nchi kwenye lindi la umasikini.
Kikwete amesoma Political Ecomy pale Mlimani, sijui ni vipi anashindwa kujibu swali la nchi ya Tanzania kuwa masikini.
Akiletewa Balance sheet ya kiingiacho na kitokacho Tanzaniia na kinakwenda katika mfuko wa nani, hata kama yey Kikweteni mjinga wa Accounts kama mimi atajua kwamba Hesabu hazijatukali vizuri sisi watanzania.
Kikwete anaiambia Dunia SISIEMU imefanya kila lililo ndani ya uwezo wake kufuta umasikini Tanzania na sasa imefikia mahala imechanganyikiwa na inajiuliza kwanini kijiwe chao Haki Mix.
Maelezo hayo yana maana moja tu SISIEMU si chama cha kutupeleka kwenye maendeleo ila ni mzingo mzito kwa kila raia wa Tanzania.
Ni lazima tuachane na kundi la mbweha watu hao wajiitao SISIEMU walioishiwa mbinu za kujenga uchumi wa nchi.
Ni lazima tuachane na kundi la mbweha watu hawa wajiitao SISIEMU wasio weza kukiri kushindwa, kukiri kuvurunda na kuwa na shingo ngumu kugeukia uelekeo wa maendeleo.
Lazima tuachane na uongozi wa SISIEMU chama muflisi chenye viongozi wenye macho makubwa kama ya Bundi lakini hayatazami na masikio makubwa mithiri ya yale ya Tembo wa lake Manyara lakini hayasikii hata mlio wa radi.
CCM kama chama kimeshindwa kabisa, kwa hiyo sisi watanzania hatuna haja ya kukipa muda wa kuendelea kushindwa.
Endapo baada ya miaka 46 ya kutawala nchi rais wa awamu ya 4 hajui kwa nini nchi yake ni masikini! Sembuse mwanachama wa SISIEMU mlima Kunde kule kijiji cha Mtulingala Malangali?
Najiandaa kwenda gombea Ubunge mwaka 2010 kupitia chama cha upinzani.
Kama mimi sijitokezi na mtu mwingine mwenye uchungu na usongo na nchi yake hajitokezi basi tutaendelea kuongozwa na Mahabithi,Majuha na Mafisadi washenzi hawa milele.
ALUTA CONTINUA MAPAMBANO NDO KWANZA YANAANZA