Hakika huwa namuheshimu sana
Mshana Jr lakini sijajua ni nIini kimempata hata kufikia hatua ya kujidharirisha namna hii mbele ya halaiki hii ya wana jamiiforums. Nimefuatilia kwa kina mjadala huu ila sijaona kitu cha tofauti kilicholetwa na ndugu Mshana zaidi ya porojo zilezile dhaifu ambazo
Kiranga amekuwa akizivuruga vuruga humu.
Sasa hapa Mshana kauliza swali akitaka kujua kama Kiranga ana akili au laa, na Kiranga ameuliza hizo akili ni kitu gani? mjadala ndio umeishia hapo....
Mshana hataki kutoa jibu sababu anajua akitoa tu jibu basi swali lake la mwanzo linakosa mashiko. Mshana bila shaka angejibiwa ndio basi angeuliza unaamini vipi kuwa una akili hali ya kuwa hujawahi kuziona? Na angehitimisha kuwa hata kwa uwepo wa Mungu ni vivyo hivyo kwa maana haonekani ila tunaamini kuwa yupo. Hii hoja dhaifu sana.
Akili sio kitu tangible kama ilivyo figo au ini. Akili ni matokeo ya mchakato fulani unaotendeka ndani ya ubongo ambao kisayansi unaelezeka vizuri tu. Na huu mchakato huweza kuathiriwa na mambo mengi kama mazingira, lishe na mambo mengine. Sasa matokeo ya huu mchakato hubainishwa na tabia za nje za mtu husika hapa inahusu maamuzi, Kauli, muonekano na mambo mengine mengi ambao yakiwa tofauti na matarajio ya wengi tunaweza kuhitimisha kuwa huyu hana akili, yaani mchakato katika ubongo wake umeleta matokeo yasiyotarajiwa yapo chini ya kiwango ila hapa niweke angalizo kwamba huenda huyo anayeonekana hana akili ndiye mwenye akili ila tu akili zake zipo viwango vya juu sana kuliko uwezo wa walio wengi wanaomtazama.
Kulingana na hilo Kiranga ana akili na hili tunalipima kutokana na hoja zake japo sikubaliani nae kwamba hakuna Mungu ila akili zake zimefanya hoja zake ziwe hazijibiki. Mungu yupo ila kuna mapungufu makubwa sana katika hivi vitabu vinavyojaribu kumuelezea. Vinajipinga vyenyewe kabla hata havijapingwa, vinajichanganya. Na hii kusema sijui ili kuvielewa ni lazima kuwa na imani ni sawa na kuwema ili kuvielewa hupaswi kuwa na fikra huru, unapaswa uwe zwazwa kwanza ndipo uvielewe sasa hapo ndipo ninapojiuliza Mungu alitupa uwezo wa kufikiria wa kazi gani kama hataki tuhusishe fikra huru tunapotaka kumuelewa yeye?
Mshana jipange upya maana bado hujafikia uwezo wa kukabiliana na fikra za Kiranga, tukubaliane tu katika hilo mkuu.