Kwasababu umeshindwa kujifunza,kuelewa na kuchambua.
Unajua huu mzunguko woote umeanzia kwenye kujibu swali la akili ni nini?
Sijapenda hili jibu lako kwangu lakini hainisumbui kwa sababu sielewi kiwango cha uelewa wako wa mambo.
Kwa kuwa tu sijajibu unavyotaka wewe haimaanishi sijakuelewa au sina akili ambayo haujaielezea ni kitu gani.
Kwanza, naweka wazi msimamo wangu binafsi kuhusu uwepo wa Mungu, mimi ni muumini mzuri tu kwamba yupo.
Pili, vitabu vinavyomuongelea Mungu (namaanisha Biblia takatifu) vimeweka bayana kwamba hatua ya kwanza kabisa, lazima uwe na Imani. Nje ya hapo utakuwa sahihi kusema hayupo.
Biblia imeeleza kwa upande wake uweza, mamlaka na sifa za Mungu, leo anakuja mtu kusema hapana, anatakiwa athibitishwe kwa aina anayotaka yeye, haiendi hivyo. Nnaweza kuwa tajiri na nikatoa msaada kwa namna nnayotaka mimi au nisitoe kabisa, haitamaanisha mimi sio tajiri.
Mara nyingi sipendi kubishana sana kuhusu hili jambo kwa sababu kuu moja tu. Huyo Mungu mie sio kazi yangu kumthibitisha wala kuutetea uungu wake, atafanya hivyo kwa namna yake.
Mwisho, naheshimu maoni ya watu wote, nisichokipenda ni ile upande mmoja kuona wengine kama wamepungukiwa akili au wana tatizo flani kutokana na msimamo wao kiimani iwe uwepo wa Mungu au kutokuwepo. Wote mnaamini vitu tofauti, wote mnakufa, mna ubitaji wa mambo muhimu kama chakula, hewa maji n.k. wote mnasoma shule, mnahitimu mnaajiriwa nyadhifa tofautitofauti, kila mmoja anaendesha maisha yake. Sasa hapo dharau ya mtu wa imani nyingine inakuongezea au kukupunguzia nini?
Au kuna utafiti uliwahi kuonyesha kuhusu mafanikio ya maisha ya wanaoamini na wasioamini uwiano ukoje? Ntafurahi na ningependa niusome huo utafiti, kama upo na uliwahi kufanyika.