President of China
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 34,057
- 93,451
Hiyo hoja umeshindwa kuitolea maelezo naona uemanza kujificha kama panya 🤣 🤣 🤣 🤣Huna hoja no kupoteza muda
Nashukuru kwa majibu yako, ingawa hayajajibu hoja niliyoweka. Lakini kwa manufaa ya wasomaji wengine wa mjadala huu, nitaeleza kwa kifupi tena ili iwe wazi:
Urefu wa Treni na Passing Loops kwenye MGR:
Vituo (passing loops) vya MGR Tanzania vimejengwa kwa treni za kawaida zenye mabehewa 20–30 tu.
Treni yenye mabehewa 100 inaweza kuwa na urefu wa zaidi ya mita 1,000–1,200, kulingana na aina ya behewa.
Hoja iko wazi: Miundombinu ya MGR Tanzania haijasanifiwa kupokea au kupisha treni za mabehewa 100 bila mabadiliko makubwa. Hili si wazo la kubuni, ni uhalisia wa kijiinjinia (engineering constraint).