President of China
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 31,772
- 89,799
Ukiongeza upana maana yake unatakiwa kununua mabehewa na vichwa cya treni vipya. Kaka imefanyiwa maboresho tu, ni hiyo hiyo MGR. Teknolojia yake imepitwa na wakati ndio maana tumekuja na SGR.Si waliitandua reli na kuiweka nyingine hadi Tabora kama sijakosea na kuifanya kuwa continuous welded wakisema pia wameongeza upana wa gauge?
MGR itasaidia kusogeza mizigo kutoka local na kuleta kwenye SGR. Kwa mfano kwa sasa itabeba mzigo kutoka mpanda kuja Tabora kabla ya SGR haijajengwa.
Tukiongelea mizigo, kuna mizigo mingi sana. Arsuha na Manyara wataleta mizigo Dodoma. Mizigo kutoka Mbeya, Malawi, Zambia, Iringa, Njombe na Ruvuma itachukuliwa Dodoma Ihumwa.
Mizigo ya maparachichi, Chai na Kahawa kutoka nyanda za huu kusini. Zitakusanywa na magari kisha kuletwa Dodoma na kusafirishwa nje ya nchi kwa kutumia Msalato Airport.
Kaka nchi yetu ipo vizuri sana.