Brother unaleta ubishi wa usio na maana. Biashara ya abiria ipo chini sana.
Nakubaliana na wewe kuwa biashara ya treni ni mizigo na hata wakati wanadizaini hii reli walijua abiria ni kidogo sana ndo maana hata makadirio ya abiria ilikuwa ni 1.5 mil kwa mwaka (soma esia) ila leo tunazungumzia 2.3 almost mara mbili, kwa maana ikisimamiwa vizuri Inaweza fikisha mpaka 6mil kwa mwaka.
Tukija kwenye treni hata kama kutakuwa na treni 20 wastan wa behewa 100 na ukawa na treni 15 kwa maono ya sasa abiria watalipa tu .
Itaweza fikia hiyo pesa inayofika ikiwa imefika kwanza na kigoma ila bado hata huko abiria ni wengi sana wa kujaza mpaka treni 30 kwa siku za abiria.
Mimi nawewe tunatofautiana , wewe unaamini kwa ulivyosikia kuwa ni mizigo tu inalipa ila kwangu naamini abiria wakifanyiwa promo kidogo hata hii ya Dodoma tunaweza toa mpaka treni 20 kwa siku kabla ya kufika dom
Biashara ya mizigo ndiyo kazi ya treni. Treni zikianza kuingia bandarini kwa siku zinaweza yoka treni mpaka 10. Kulingana na wingi wa mizigo
Brother unatuaibisha sana watanzania. Vitu kama huvijui ni bora ukae kimya. Tanzania imeagiza mabehewa 1,430 ya mzigo. Bhehewa moja linauwezo wa kubeba 120 ton. Yaliyoingia ni 264 tu. Yaliyoingia loose cargo ni 64, kontena 200. Hakuna behewa hata moja la kontena lililoanza kazi.
Hakuna behewa la tani 120 lilioagizwa maana axel capacity ni tan 35 na mabahewa yote yaliyotangulia ni tan 75 tu.
Treni ya mizigo ndio kwanza imeanza bado hata haijaingia bandarini. Ikisha ingia bandarini. Ikianza kazi mpaka bandarini kwa siku zinaweza kutoka zaidi ya treni 10 za mizigo.
Kumbuka mizigo sio Kila siku .
Hakuna treni ya mizigo itatoka dar mpaka kigoma ikageuza same day ila ya abiria itaweza hata piga trip 3 kwa masaa 24
Treni 10 kila moja ni Tsh 700,000,000.
Per Day unaingiza Tsh 7b. Na hapo ni one way tu. Ukisema mizigo yote inayotoka DRC, Burundi, Uganda na Rwanda na ile ya Tanzania iishie Dodoma na ibebwe kuja dar. Hapo unaongelea Tsh 14b per day.
Ili ubebe mzigo wa 700mil inahitaji mabehewa 163 na si chini ya vichwa vya treni 4 je ushapiga hesabu ya gharama ambatanisho?
Hivi unajua hiyo abiria ikivuta behewa hata nusu ya hiyo kwa siku Inaweza ingiza mara mbili ya
Niambie Treni ya Abiria kwa mwaka inaingiza Tsh 60b kwa mujibu wa maelezo yako. Ndani ya 7 days SGR ya mizigo inaingiza Tsh 98b zaidi ya pesa za SGR ya abiria.
Sasa huoni kama ya mzigo inachelewa kuingiza pesa. Kama kwa sasa ya abiria kwa siku inaingiza 151mil kwa siku 7 si inaingiza 1.bil Tena treni moja sio zote 🤣.
Tukisema tufanye treni zote mbili ni 2bil kwa siku saba . Hiyo hela utazipata kwa treni ngapi A mizigo kwa siku sababu ? Kumbuka kjna kushusha na kupakua
Kaka unatakiwa ujue maisha ya usafirishaji.
Nimekuwa kwenye usafirishaji abiria analipa kuliko lorry, ila abiria anataka heshima na nidhamu .
Unaweza toa lorry dar - songea ukalipwa 5mil ila ukachukua siku tatu
Ukitoa gharama zote ukabaki na 2mil ila kukawa na mtu wa mabasi yeye Kila siku akalaza 1.8 baada gharama nyinginezo . Ndani ya siku tatu kibindoni akawa na 5.4mil na wewe huko ukienda unaweza subiri mzigo wiki