President of China
JF-Expert Member
- Dec 6, 2018
- 31,772
- 89,799
Nimekupatia hoja tano naona unaleta blah blah. Vitu unavyoongea ni utoto. Labda issue za watoto wa shule siyo mambo ya nchi. Narudia hoja hizi hapa zijibu hoja kwa hoja zipo tano. TUELEZE NA COST ZA KUREKEBISHE HIZO ISSUESIssue ya kupishana haina mantiki maana hata hao wanaofunga hivyo vichwa sio kwamba wanakuwa na njia toshelezi za kupishana ila train Zinakuwa na ratiba zake.
Mfano train inatoka dar na behewa 100 ila unajua kabisa sehemu kama Moro kuna njia zaid ya 4 za kufanya shunting , hivyo wanachofanya ikifika Moro wanavifungua kama kupanga ili treni nyinge iweze pita kwa njia kuu.
Kuna sehemu kama Australia watu wanafunga mabehewa mpaka 600 zaid ya km 10, hupati shunting ya 10km ila pale inapotokea kuna kupishana lazima itafutwe sehemu ya kupangua.
Sasa kwa ujenzi wa sasa unahisi hata hiyo mgr itakosa sehemu ya kupangulia mabehewa
Dpu huwa ni mfumo ambao unafanyiwa installation kwenye vichwa vya train kwahiyo sio kigezo Cha kusema haiwezekaniki na huo mfumo upo kwenye baadhi ya vichwa vipya vya mgr
Ukisema hivyo basi unamaanisha hata sasa hivi hatuwez tembeza behewa 40 kwa pamoja kitu ambacho si kweli trc huwa kuna muda inafunga mpaka behewa 50 kwa vichwa viwili .
1. MGR ya Tanzania imejengwa kushikilia mzigo mdogo (16–18 tons/axle)
2. Vituo vingi vya MGR Tanzania havina uwezo wa kupokea au kupisha treni zenye urefu wa mabehewa 100 – ni hatari na huchelewesha operesheni.
3. MGR ina kona nyingi na milima (hasa kati ya Morogoro na Tabora) – treni ndefu hupata matatizo ya braking, coupling stress, na kusababisha derailment.
4. Hakuna mfumo wa kisasa wa DPU (Distributed Power Units) wa kuratibu injini mbele, katikati na nyuma kama SGR au reli za Marekani.
5. Treni ndefu zinahitaji braking system yenye akili – MGR ya Tanzania ina mfumo wa zamani (pneumatic brakes) ambao huchelewa kuhimili treni ndefu.