Kaka nimekupatia maelezo kuhusu MGR ya Tanzania naona ume ya ignore ili kufurahisha nafsi yako.
1. MGR ya Tanzania imejengwa kushikilia mzigo mdogo (16–18 tons/axle)
2. Vituo vingi vya MGR Tanzania havina uwezo wa kupokea au kupisha treni zenye urefu wa mabehewa 100 – ni hatari na huchelewesha operesheni.
3. MGR ina kona nyingi na milima (hasa kati ya Morogoro na Tabora) – treni ndefu hupata matatizo ya braking, coupling stress, na kusababisha derailment.
4. Hakuna mfumo wa kisasa wa DPU (Distributed Power Units) wa kuratibu injini mbele, katikati na nyuma kama SGR au reli za Marekani.
5. Treni ndefu zinahitaji braking system yenye akili – MGR ya Tanzania ina mfumo wa zamani (pneumatic brakes) ambao huchelewa kuhimili treni ndefu.
Ki-teknolojia inawezekana, miundombinu yetu ya sasa haiiungi mkono hilo
Naomba uje na utatuzi wa changamoto hizo tano na cost zake.