Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,047
20,411
Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Loliondo,Benson Ngowi(32) anashikiliwa na jeshi la Polisi katika kituo cha Loliondo,Wasso kwa kosa la kumlawiti kijana mwenye umri wa miaka 29 mkazi wa Wasso wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha.

Hakimu huyo, ambaye pia alifanya kazi ya uwakili kwenye Kampuni ya mawakali[ jina ni la kiswahili ila hapa naandika kwa kingereza wewe utafsiri JUSTICE FIRST ] ni wakili unaweza kumuona kwenye mfumo wa mawakili, ameacha uwakili hivi miaka ya karibuni na kuwa hakimu.

Kwa mujibu wa chanzo cha Habari wilayani humo,tukio hilo limetokea jana majira ya saa tatu na saa nne usiku nyumbani kwa kijana huyo ambaye hufanyakazi ya kuendesha pikipiki maarufu bodaboda katika eneo la Wasso.

Mtoa taarifa alifafanua kwamba Hakimu huyo ambaye hivi karibuni alihamia kikazi,alionekana majira ya mchana akiwa na kijana huyo na baadaye jioni walienda kunywa pombe nyumbani kwa kijana hiyo ambaye ànaishi chumba kimoja na sebule

Alisema ilipofika majira ya usiku kaka yake na kijana aliyelawitiwa (jina linahifadhiwa) alifika katika nyumbani kwa mdogo wake na kumkuta mdogo wake wakiwa na hakimu Benson Ngowi wakiendelea kunywa pombe aina ya Safari huku hakimu ndiye aliyekuwa akimnunulia kijana hiyo kwa mshahara wake wa January.

Taarifa inasema kwamba majira ya saa tatu usiku Hakimu alimtuma kaka yake na huyo kijana kwenda kuchukua chakula na wakati aliporejea alikuta mlango umefungwa na kuamua kugonga.

"Baada ya kugonga Hakimu alienda kufungua mlango lakini chaajabu alionekama sehemu zake za siri zikiwa Imesimama ndipo kaka yake aliposhtuka na kuamua kuingia chumbani kwa mdogo wake kujua kulikoni na kumkuta akiwa amelala kitandani kifudifudi akiwa utupu hajitambui" alisema mtoa taarifa.

Alisema baada ya tukio hilo aliamua kutoa taarifa kwa watu mbalimbali ndipo hakimu Benson Ngowi wenzake na mtuhumiw walifika Eneo la tukio na baadaye polisi walikuja na kumkuta kijana hajitambui kitandani na baada ya kumwamsha na kuzinduka alihisi maumivu sehemu zake za haja kubwa ndipo askari hao walipomtia nguvuni mtuhumiwa.

Kijana huyo alipelekwa katika hospitali ya Wasso kwa matibabu na taarifa za daktari zimethibitisha kuwepo na michubuko sehemu za haja kubwa pamoja na mbegu za kiume.

Taarifa zinadai kwamba hakimu hiyo alikuwa na mazoea na kijana hiyo kutokana na kumtuma mara kwa mara ikiwemo kumsafirisha kutoka eneo moja kwenda jingine kwa kutumia pikipiki yake.

Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Justin Masejo alipotafutwa alisema bado hajapata taarifa ila anafuatilia tukio hilo na atatoa taarifa.

Update 5-2-2024
#Taarifa zinasema Benson Ngowi alikuwa Wakili kwenye kampuni moja Dar es salaam na baadae kuamua kuwa hakimu ambapo alipangiwa Karagwe na kuhamishwa kwa makosa ya kinidhamu kama hili la Arusha.
 
Walikua wapenzi hao....
Mkuu Lusungo,
Kama walikuwa wapenzi sifikirii ingekuwa rahisi kwa mtuhumiwa kumtuma kaka mtu chakula na wakafanyia uchafu huo hapo ndani, wangeogopa kukutwa na wangetafuta sehemu salama zaidi.

Ila pia kama kijana alikutwa ajitambui huenda aliwekewa madawa kwenye kinywaji hicho, sioni sababu ya yote hayo wafanye kama wangekuwa ni watu wanaoelewana.
 
Mmmh
Kwamba alikuywa mpk akazima?
Au alimwekea kitu?
Na km aliofanya hivyo,how come amfungulie kaka mtu kirahisi tu,hakuogopa?
Nina maswali mengi , sielewi 🤷
Mkuu Tayana,

Ulishawahi kufanya kitu halafu baada ya kukifanya unashangaa nimefanyeje hichi kitu mimi?!!

Hufikirii labda kulikuwa na dawa zingine walizotumia ambazo huenda akili isiwe sawa?

Hata mimi nashangaa kwanini alifungua mlango.

Ila kuna situation unaweza kufanya vtu halafu bado unabaki kama umepigwa butwaa imekuwaje
 
Back
Top Bottom