Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo tarehe 03 April, 2024 jijini Dar Es Salaam, katika kikao chake maalum, chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na masuala mengine, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, imefanya mabadiliko madogo ya Sekreteriet ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuwachagua wajumbe kama ifuatavyo:
  • Ndugu John Mongella kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, akichukua nafasi ya Anamringi Macha ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga,
  • Ndugu Amos Gabriel Makalla kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, akichukua nafasi ya Ndugu Paul Makonda ambaye ameteulia kuwa Mkuu wa Mkoa Arusha.
  • Ndugu Ally Salum Hapi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania, akichukua nafasi ya Ndugu Gilbert Kalima ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga,
  • Ndugu Jokate Urban Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM akichukua nafasi ya Ndugu Fakii Raphael Lulandala ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.
Aidha katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi, ambaye pia ni Mwenye kiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kazi kubwa na nzuri ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 – 2025.

IMETOLEWA NA IDARA YA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO 03 APRIL, 2024
Hapo safi, wenye akili tulijua. Makala ni kichwa, siyo mazuzu ya kutuharibia nchi
 
434646079_336971659378324_6770927706532979371_n.jpg
 
Same ‘ol same ‘ol!

It’s the same damn party and the same damn people.

There’s nothing to expect but the continuation of incompetence and ineptitude.

After several months there will be another recycling and fools will be out here felicitating Samia for a ‘job well done’.

So stupid.
 
Ndugu zangu Watanzania,

CCM Ni Chama ambacho huwezi ukakitabilia juu ya maamuzi yake,ni chama ambacho kinakwenda na mahitaji ya wakati ,ni chama ambacho kinawapa watanzania Radha tofauti tofauti.hii ndio sababu hakikauki midomoni mwao Watanzania wala kupungua upendo mioyoni mwa watanzania wala kushuka ushawishi wake kwa watanzania.

Sasa leo kimemteua mwana Dada maarufu na mahili na aliyeisomea siasa darasani Mheshimiwa Jokate Mwegelo kuwa katibu mkuu wa UVCCM ,ambapo unaweza kusema ni Nguli wa sayansi ya siasa kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam mahali alipopikwa akapikika.

Jokate anaifahamu vyema sana UVCCM kwani huko ndiko alikotokea ,unaweza kusema maji yamerejea katika mkondo wake na asili yake. Sasa jumuiya inakwenda kuwaka moto na kutikisa hapa nchini,hii ndio nguzo ya chama,ni tanuri la kuwapika viongozi wa kesho serikalini na ndani ya chama. Nilishamtabiria humu jukwaani jokate kuwa atafika mbali sana na kwamba mwakani lazima aingie mjengoni.Hongera sana Mheshimiwa Jokate kwa uteuzi huo.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Na huu mkeka umekuacha! Kazi ipo.

Usichoke kuweka namba hapo chini, iweke tafadhali. Kukata tamaa ni dhambi.
 
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) iliyokutana leo tarehe 03 April, 2024 jijini Dar Es Salaam, katika kikao chake maalum, chini ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na masuala mengine, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, imefanya mabadiliko madogo ya Sekreteriet ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kuwachagua wajumbe kama ifuatavyo:
  • Ndugu John Mongella kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, akichukua nafasi ya Anamringi Macha ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Shinyanga,
  • Ndugu Amos Gabriel Makalla kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, akichukua nafasi ya Ndugu Paul Makonda ambaye ameteulia kuwa Mkuu wa Mkoa Arusha.
  • Ndugu Ally Salum Hapi kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wazazi Tanzania, akichukua nafasi ya Ndugu Gilbert Kalima ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga,
  • Ndugu Jokate Urban Mwegelo kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM akichukua nafasi ya Ndugu Fakii Raphael Lulandala ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro.
Aidha katika kikao hicho, Halmashauri Kuu ya CCM Taifa imezipongeza Serikali zake zote mbili, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, chini ya Rais Dkt. Hussein Mwinyi, ambaye pia ni Mwenye kiti wa Baraza la Mapinduzi, kwa kazi kubwa na nzuri ya kuendelea kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2020 – 2025.

IMETOLEWA NA IDARA YA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO 03 APRIL, 2024
Makalla safari ya utambulisho akaanzie Arusha itapendeza zaidi
 
Back
Top Bottom