Sitaki salamu nimevurugwa, naingia kwenye mada moja kwa moja. Nchi hii ina maamuzi ya ovyo na ya kipumbavu sana. Kila kitu kinafanyika ovyo ovyo! Ni juzi tu serikali imeuza nchi kwa warabu wa DP World. Na ni jana tu Rais Samia ameenda India kuwaomba wahindi waje kununua kipande cha nchi...
Polisi
Jeshi la Polisi jijini Maputo limetumia Mabomyu ya Machozi kuwatanya Waandamanaji wa Upinzani huku wengine wakijeruhiwa kutokana na kupinga matokeo ya Uchaguzi uliofanyika Wiki moja iliyopita wakidai Chama Tawala (FRELIMO) kiliiba Kura.
Maandamano hayo yanafuatia uamuzi mwingine wa...
Siku hizi mjini Kuna kasumba ya viongozi wetu wanasiasa, kazi Yao ni kukera wananchi. Nasikitiswa na hivyo vitendo wanavyovifanya.
Kuna serikali ya awamu ya Nne, Tano na Sita. Asilimia 98 ya watendaji ni wale wale, yaani ndio waliotenda hizo awamu zote. Lakini kinachosikitishwa ni kuwa madudu...
Kila ninapopita nakutana na sakata la vijana, jinsi viongozi wanavyowazungumzia ni watu wasiojituma, wasiopenda kufanya kazi, yaani vijana wa Kitanzania wanaonekana hawapendi kazi kuliko vijana wengine duniani.
Viongozi walioajiriwa wanatuambia sisi tujiajiri. Mtu unaweza vipi kujiajiri pasipo...
Habari ndiyo hiyo upumbavu wa kufungua mageti saa nane na huku mkijua mifumo yenu ni slow na niyakizamani mtaleta maafa siku ya ijumaa ! Mtu akitoa pesa yake aheshimiwe ,utapeli wakupiga watu bila sababu tutakuja kutoka na roho ya mtu ! Nimewapa onyo mjifanye wajuaji ,
Tumesikia huko Mbeya madereva na wenye magari wamegoma kusafirisha abiria kati ya Mbeya na Tunduma na kuzua taharuki kwa wananchi wasafiri.
Huo ni utovu wa nidhamu na kiherehere, kama kuongezeka kwa mafuta yameongezeka nchi nzima. Kuna taratibu za kuongeza nauli na LATRA iko kwenye mchakato. Ni...
Lindi na Mtwara ni miongoni mwa mikoa ambayo wananchi wake wana uhakika wa kupata fedha za pamoja tofauti na baadhi ya mikoa.
Kuna msimu wa ufuta, vijana hupata mamilioni, msimu wa korosho wazee pamoja na vijana hupata mamilioni, msimu wa mbaazi pia huwapa mamilioni wakulima baadhi. Ila makazi...
Waziri wa Fedha Olawale Edun, ambaye pia ni Mratibu wa Uchumi, amesema Baraza limetoa baraka hiyo kwa lengo la kufanya marekebisho ya Sera ili kukuza Uchumi ambao umeatajwa kuwa kwenye mdororo kwa miaka kadhaa.
Tangu aigia madarakani, Rais Bola Tinubu amekuwa akibadili sera za Mtangulizi wake...
Hakuna Haja ya Salaam Maana naona kama hili swala halijakaa sawa sana..
Kila nikifungua TV au Redio nasikia nakuona Serikali ikieleza Athari za Mvua ya Elnino na Athari zote zikielekezwa kwa Wananchi..
Na serkali ikifika mpaka kutishia wananchi wanaoishi Bondeni kwamba hakutakuwa na Malipo wala...
Utapeli kwa katika ununuzi wa vitu au upangishaji wa nyuma unazidi mno kwa kipindi hiki hususan katika upangishaji wa nyumba, imefikia hatua Dalali anakuwa na Mwenye Nyumba wa mchongo na akaunti ya benki ya kitapeli kulipia pango. Serikali hebu saidia Wananchi katika hili.
Nakumbuka Lukuvi...
Hawa viongozi tuliowaamini wana mgao! Wao ndo wanapanga fidia kiasi gani! Unakuta mlalamikaji wala hana neno na alishindwa kwenye kesi ya msingi ya kwanza! Sasa wanamwendea na kumlazimisha aifufue hiyo kesi na atashinda kwa fidia (labda tuseme 1 billion).
Hawa watanzania mafisadi wanasema...
Hawa viongozi tuliowaamini wana mgao! Wao ndo wanapanga fidia kiasi gani! Unakuta mlalamikaji wala hana neno na alishindwa kwenye kesi ya msingi ya kwanza! Sasa wanamwendea na kumlazimisha aifufue hiyo kesi na atashinda kwa fidia (labda tuseme 1 billion).
Hawa watanzania mafisadi wanasema...
Leo asubuhi nimesikia kwenye redio kipindi cha kusomewa magazeti kuwa rais ameagiza serikali isimamie na kugharamia maziko ya makada wa CCM huko Njombe waliofariki kwa ajali wakiwa kwenye shughuri za chama chao, kitendo hiki hakitoi haki kwa watamzania wote ambao si wafuasi wa CCM ambao...
Nina kiwanja changu kama nusu eka nilichonunua 2012 maeneo ya Chanika. Nilikizungushia fence ya waya na mara moja moja nilikuwa natuma mtu apasafishe.
Takriban miaka 6 nilikuwa nje ya Dar kikazi. Nimerudi mwisho wa mwezi wa 9 ila ilikuwa sijapata fursa ya kwenda kwenye kiwanja changu.
Jana...
Mfumo mpya wa ulipaji mapato ya Serikali umekuwa ngumu sana kwa Wananchi wa kawaida.
Nitoe mfano, kama Mfanyabiashara anataka kulipia leseni yake kwa mfumo mpya lazima umtafute mtu akusaidie taratibu zote mpaka control number itoke. Mfanyabiashara kwa kazi hii anatozwa mpaka 20,000 kwa kazi...
SERIKALI IMEWATENGA WANAWAKE WA VIJIJINI
Leo dunia inapoadhimisha siku ya wanawake vijijini, hapa nchini Tanzania hali ya wanawake, hasa wa vijijini bado ipo duni. Sensa ya 2022 inaonyesha kati ya wanawake milioni 31.6, wanaoishi mjini ni milioni 11.2 na waliosalia wote wanaishi vijijini wengi...
Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge ametoa siku 14 wasakwe na kukamatwa viongozi 24 wanaotuhumiwa kujihusisha kuwatapeli watu na kuwauzia eneo la shamba la mitamba mali ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi.
Viongozi wanaotafutwa ni pamoja na mabalozi, wenyeviti wa mitaa, watendaji walioshirikiana...
Katazo la Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuhusu matumizi ya mtandao binafsi (VPN) bila kibali maalumu, limewaibua wadau wa mawasiliano na siasa, wakisema hatua hiyo inalenga kubana upatikanaji na utoaji wa habari kidijitali.
Katazo hilo lilitolewa juzi na TCRA kupitia taarifa yake kwa...
Kila ukipita Singida unaona hali ni ileile miaka nenda rudi same applies to Manyara. Na hapa tunapita mjini hata maji ya kunywa shida, ukienda huko wilayani kisha vijijini hali ni mbaya zaidi.
Mkoa wa Kagera ni moja ya mikoa maskini nchini kwa sasa. Pamoja na hali ya hewa nzuri na kuzalisha...
Katika mahojiano yaliyofanyika kwenye Channel ya YouTube ya Simulizi Na Sauti (SNS) kati ya Sky Walker, DJ Smaa na Yericko Nyerere. Nguli wa uchambuzi wa mambo ya Siasa na uchumi wa kivita na ujasusi, Yericko Nyerere amesikika akiishauri Serikali ya Tanzania na Idara ya Usalama wa Taifa (TISS)...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.