Ninaishauri serikali kupunguza majimbo ya uchaguzi

koryo1952

JF-Expert Member
Mar 7, 2023
380
763
Binafsi ninaona Majimbo ya uchaguzi ni mengi mno hivyo ninaishauri Serikali kupunguza majimbo ya uchaguzi kwa ushauri ufuatao:

Jumla ya Halmashauri zote katika nchi hii ni 184 basi kwa mantiki hiyo kila Halmashauri iwe na Wabunge wawili yaani Mwanaume moja na Mwananmke moja.

Majimbo ya sasa ni mengi sana mfano inakuwaje Mji mdogo kama Bunda, Tarime na mengineyo kuwa na Mbunge. Huu ni ufujaji wa fedha za Serikali. Tufuate ushauri alioutoa Warioba katika Rasimu yake.
 
Ni kweli bora wabunge wakae kwa halmashauri wanaume kwa wanamke inatosha kabisa na ni gender balance.
 
Kwahiyo saivi kila kitu kiende kwa Couple? Ndoa za wabunge kama naziona zikitetereka na kuparanganyika😁
 
Back
Top Bottom