Luhaga Mpina: Serikali inaingia Mikataba Mibovu na ya Siri, Rasilimali zetu zinanufaisha Wageni

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
20240114_135619.jpg
"Licha ya Mafanikio makubwa tuliyoyapata katika kipindi cha miaka 62 ya Uhuru na miaka 60 ya Mapinduzi bado atujafanikiwa kuwapiga na kuwashinda maadui hawa Ujinga, Maradhi na Umasikini kwa asilimia 100.

Nitataja baadhi ya changamoto ambazo zinarudisha nyuma jitihada za nchi yetu kukuza uchumi na kujiletea maendeleo kama ifuatavyo;

(i) Raslimali za Taifa Ardhi, Gesi, mafuta, madini, misitu, Bandari, wanyama, mazao ya uvuvi nk, kulinufaisha Taifa kwa kiwango kidogo sana kutokana na mikataba mibovu inayoingiwa na Serikali, kuingia mikataba ya siri na baadhi ya raslimali za nchi kukabidhiwa wageni kwa mlango wa nyuma kwa kisingizio cha uwekezaji hali hii inaifanya nchi yetu kukosa mapato ya kutosha kugharamia shughuli za maendeleo na kukuza uchumi wa nchi huku raslimali zake zikinufaisha Mataifa na Makampuni ya kigeni" -Mpina

Luhaga Mpina ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kisesa (CCM) amezungumza hayo alipokutana na Wanahabari kwenye Uwanja wa New Amani Complex, Zanzibar wakati wa maadhimisho ya miaka Sitini (60) ya Mapinduzi ya Zanzibar
 
Back
Top Bottom