Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linaendelea na uchunguzi wa tukio la mauaji ya kikatili ya mwanafunzi wa Chuo cha IFM, James Rogers Temba, ambaye mwili wake ulikutwa ukielea kwenye maji ya Mto Msimbazi, eneo la Kipawa Ilala ukiwa hauna kichwa, Aprili 30, 2026.
Polisi tayari imewakamata watuhumiwa wanne kuhusiana na tukio hilo, akiwemo Steven Rogers Chaka (31), mkazi wa Bomang’ombe mkoani Kilimanjaro na Afisa Maabara; Anna Frank Lema maarufu kama “Happines” (30), mfanyabiashara mkazi wa Tabata Chang’ombe; Twalibu Khamis maarufu “Mputo” (23) pamoja na Michael John maarufu “Tambali” (26), wote wakazi wa Kigogo Kati.