Huu ugonjwa wa kuomba omba hela inabidi ukemewe. Unazalisha kizazi kibovu. Mimi mara ya mwisho kuomba hela ilikuwa sekondary huko tena kwa wazazi na ndugu wa karibu. Chuoni boom langu lilikuwa linanitosha, wakati wa likizo nilikuwa natafute kazi ili nipate hela ya ziada. Mpaka sasa nikiwa na shida nakopa na kurudisha kwa wakati. Mwanamke unataka kila baada ya wiki 2 usuke hela za elfu 30, huku huna kupato chochote, unategemewa upewe. Wengine wanaishi nyumba za bei wakitegemea wanaume ambao sio waume zao, unafiri maisha ya baadae yatakuwaje? Utaishia kudanga ukiwa kwenye ndoa. Maisha yamebadilika tuditegemee wanaume wanaweza kubeba mzigo wa familia.