Sikutegemea kwakweli [emoji3064][emoji3064]
Nilimkuta kapuku, hakuwa na pesa, nikam offer mpaka pesa ya chakula na nauli kutoka kazini kwake kwa miezi miwili, alikuwa ni wa kuniheshimu sana, kiukweli nilimpenda sana
Sasa amepata vicent, anashindwa hata kurudisha fadhira, anahitaji tufanye mapenzi ili anipatie pesa zake alizozitengeneza kwa msingi wangu, najua leo kwangu kesho kwake, kwani nami kipindi cha nyuma nilikuwa hivi?
Mbona penzi nilimpatia bure kabisa? Tena kwa upendo wote? Tena kwangu? Leo hii kumuomba pesa kwa dharura ananipa masharti ya kwenda kwake na jua lote eti tufanye mapenzi kwanza? Kwani kigeni kwake kutoka kwangu ni kipi mpaka awe na tamaa ya ajabu kiasi icho? Kwani haniamini tena? Thamani yangu anaifananisha na nini kwa sasa? Mwanaume pekee niliempenda, nimeacha wangapi mimi mwenzenu, nimekataa wangapi ili kumtunzia heshima? Na ninyi mnafungua midomo yenu kutetea upuuzi?
Sasa napata kuamini kuwa hakuna mwanaume mwaminifu, hata hawa ninaowaona mtaani wakijifanya kuniulizia na kunitupia macho ya tabasamu na bashasha wananidanganya, huenda wamo humuhumu na ndio wachangiaji wakubwa kunitusi na kunikebehi
Nilimpenda bure jamani, hakuwa na kitu, leo hii nakatiliwa namna hii? asante mungu, ipo siku [emoji24][emoji24]