Kiukweli mimi napenda sana nizungumzie ama nichangie kulingana na Dini yangu kwani waislamu huwa tunaaambiwa na Mola wetu kwamba:
وَمَا اخْتَلَفْتُمْ فِيهِ مِن شَيْءٍ فَحُكْمُهُ إِلَى اللَّهِ
"Na mkikhitalifiana katika jambo lolote, basi hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu". [Ash-shuraa aya ya 10]
Pili niseme kwamba mwanaume yyte wa kiislamu anaemruhusu mkewe kufanya kazi hizi za Saloon huyo ni Muislamu Jina sio Muislamu anaeijua dini. Mtume (Swallah Allaahu alayhi wasallam) anasema: "Al-Mar'at Khawra" kwa maana "mwanamke ni Uchi".
Na Allaah akasema:
زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ الشَّهَوَاتِ مِنَ النِّسَاءِ
"Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake......" [Al-Imraan aya ya 14].
Mwanamke ni pambo la mume sio la kila mtu wewe mwanamke wa kiislamu unaejiheshimu utakwendaje saloon ukaanza kuwapapasa wanaume, je wajua kwamba jinsi gani wanavyojihisi. Na ndio maana unakuta wengine vichwa vyao pengine para ila watakwenda kwa ajili ya Massage tu basi.
Tuelewe dada zangu na mama zangu haya yanatakiwa afanyiwe mume ndani huna mume wacha usijitie madhambi. Duniani tunapita hatupo hapa kuridhisha watu ama kutafuta mamali na kujiridhisha tuna mali kiasi gani. Mungu yupo siku zote sio kwamba yupo pale muda unapopatwa na tatizo ama kufiwa na kipenzi chako.
Tambueni "AHADI PEKEE AMBAYO HAINA RATIBA NI KIFO" Hujui muda gani na wapi kitakujia. Allaah mtukufu anasema:-
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّهَ وَلْتَنظُرْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ لِغَدٍ ۖ وَاتَّقُوا اللَّهَ ۚ إِنَّ اللَّهَ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ
"Enyi mlio amini! Mcheni Mwenyezi Mungu, na kila nafsi iangalie inayo yatanguliza kwa ajili ya Kesho. Na mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari ya mnayo yatenda" [Al-Hashr aya ya 18]
Na akasema tena katika Suuratul Taa-Haa aya ya 123 hadi 126
فَإِمَّا يَأْتِيَنَّكُم مِّنِّي هُدًى فَمَنِ اتَّبَعَ هُدَايَ فَلَا يَضِلُّ وَلَا يَشْقَىٰ
".....Na ukikufikieni uwongofu kutoka kwangu basi atakaye ufuata uwongofu wangu, hatapotea wala hatataabika"
وَمَنْ أَعْرَضَ عَن ذِكْرِي فَإِنَّ لَهُ مَعِيشَةً ضَنكًا وَنَحْشُرُهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَعْمَىٰ
"Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu".
Huyu atakaefufuliwa kipofu atasema kumwambia Allaah azza wajallah.
قَالَ رَبِّ لِمَ حَشَرْتَنِي أَعْمَىٰ وَقَدْ كُنتُ بَصِيرًا
"Aseme: Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona umenifufua kipofu, nami nilikuwa nikiona?"
Na Allaah mtukufu atamjibu
قَالَ كَذَٰلِكَ أَتَتْكَ آيَاتُنَا فَنَسِيتَهَا ۖ وَكَذَٰلِكَ الْيَوْمَ تُنسَىٰ
"...Ndivyo vivyo hivyo. Zilikufikia ishara zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika leo unasahauliwa".
Kutaabika kwenyew ndio huko mara ndoa zimevunjika, mara unaziniwa na mwanaume huyu kesho huyu, mara akija huyu umemshika hapa siku mbili tatu utamsikia kwamba [HASHTAG]#HEDHI[/HASHTAG] hapati au anapata kwa shida mpaka achomwe [HASHTAG]#MASINDANO[/HASHTAG] haya yote ni kw7bu hatutaki kuenda sambamba na amri za Muumba wetu. Pumzi zinatuhadaa mpaka tunamuona Allaah mtukufu si chochote si lolote. Wengine waliokuwa na imani dhaifu husema hakuna maisha baada ya kufa kwnini wewe ulianza ukiwa maiti tumboni mwa mama yako na sasa unaishi. Usijidanganye. Mwanamke mwema ni yupi?

Mwanamke mwema ni yule anaetulia kwake. Allaah kahimiza haya kwa kusema:
وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ
"Na kaeni majumbani kwenu, wala msijishauwe kwa majishauwo ya kijahilia ya kizamani......."

Mwanamke mwema ni yule anaehifadhi tupu yake ila kwa mume wake tu.

Mwanamke mwema ni yule anaeheshimu mipaka ya ndoa yake na kumtwii muumba wake.
Wengi wa wanawake wataingia Motoni kw7bu ya:

Kukithirisha Mambo ya laana.

Kutokumbuka Ihsaan na Fadhila za waume zao hata wafanyiwe mema kiasi gani.

Kushughulishwa na Starehe za dunia.
Waume majumbani iwapo tutawaachia wake zetu kuyafanya haya tujiandae na moto ambao hata uwe shabbab kiasi gani hutouweza kwni haiwi mvuke wa moto wa duniani wakushinda kuvumilia je Akhera utaweza. Allaah azza wajallah anasema:
( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلَادِكُمْ عَدُوًّا لَّكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ ۚ وَإِن تَعْفُوا وَتَصْفَحُوا وَتَغْفِرُوا فَإِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ )
التغابن (14) At-Taghaabun
"Enyi mlio amini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu wamo maadui zenu. Basi tahadharini nao..."
Maneno haya Allaah mtukufu katwambia sisi wanaume haina maana maadui kw7bu wana silaha lah ila tukishindwa kuwalea wake na watoto wetu katika misingi ambyo Allaah azza wajallah anataka basi akhera watakuwa maadui wakubwa na huenda tukaingia motoni kw7bu yao.
Kiufupi hili suala ni HARAMU na mimi sioni haja mama zetu kwenda saloon wakajidhalilisha. Niseme tu
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ
"Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao fikiri".
Na Allaah Ni Mjuzi Zaidi.
(Al-Kamaalu Lillaah)