ERTUGRUL BEY
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 11,529
- 21,530
Assalaam alaikum warahmatullah wabrakatuh,,
Moja ya haki ambazo tutazipata kwa ALLAH ni kutodhulimiwa kwa jambo lolote lile,hapa duniani haki ya mtu hununuliwa,hubagazwa ,mwenye nacho ndio mwenye kunufaika na haki
Lakini kwa Allah hakika kuna uadilifu mkubwa mno,miongoni mwa uadilifu huo ni mja kutodhulumiwa amali zake au matendo yake,iwe amali za kheri ataziona na ima ni amali za uovu ataziona
Hakika kila nafsi itapata haki yake,hata kama ni amali ndogo mfano wa punje ya mchanga iwe ya kheri au shari mja ataiona kwenye daftari lake,ndio maana tunaambiwa kwenye qur'an na Allah kwamba,kafir au waovu siku hiyo baada ya kupokea madaftar yao,watasema hili daftar lina nini haliachi kubwa wala dogo yote yamehudhurishwa hapo.
Kuna mambo ambayo kwa mtazamo wetu tunayaona ni madogo lakini hakika mbele ya Allah yana uzito wake,na yote hayo yapo kwenye records zetu
Kwahiyo ndugu zangu katika imani tutambue kila kitu tunachofanya kinadhibitiwa,hapa unaposoma andiko hili sasa unarekodiwa,kwahiyo tujue tupo ndani ya uangalizi wa Malaika waandishi ambao kutwa kucha wapo nasi wanapeana zamu tu,wakati wa Al asir inasemwa ndio hubadilishana shift,ndio maana hii swala ya Kati na kati imesisitizwa kuzingatiwa,ripoti zinapandishwa mbinguni kwamba mja wa Allah tumemuacha akiswali.
Allah tuongoze tuwe watu wenye kusikia maneno ya haki na kuyafuata,amiin
Moja ya haki ambazo tutazipata kwa ALLAH ni kutodhulimiwa kwa jambo lolote lile,hapa duniani haki ya mtu hununuliwa,hubagazwa ,mwenye nacho ndio mwenye kunufaika na haki
Lakini kwa Allah hakika kuna uadilifu mkubwa mno,miongoni mwa uadilifu huo ni mja kutodhulumiwa amali zake au matendo yake,iwe amali za kheri ataziona na ima ni amali za uovu ataziona
Hakika kila nafsi itapata haki yake,hata kama ni amali ndogo mfano wa punje ya mchanga iwe ya kheri au shari mja ataiona kwenye daftari lake,ndio maana tunaambiwa kwenye qur'an na Allah kwamba,kafir au waovu siku hiyo baada ya kupokea madaftar yao,watasema hili daftar lina nini haliachi kubwa wala dogo yote yamehudhurishwa hapo.
Kuna mambo ambayo kwa mtazamo wetu tunayaona ni madogo lakini hakika mbele ya Allah yana uzito wake,na yote hayo yapo kwenye records zetu
Kwahiyo ndugu zangu katika imani tutambue kila kitu tunachofanya kinadhibitiwa,hapa unaposoma andiko hili sasa unarekodiwa,kwahiyo tujue tupo ndani ya uangalizi wa Malaika waandishi ambao kutwa kucha wapo nasi wanapeana zamu tu,wakati wa Al asir inasemwa ndio hubadilishana shift,ndio maana hii swala ya Kati na kati imesisitizwa kuzingatiwa,ripoti zinapandishwa mbinguni kwamba mja wa Allah tumemuacha akiswali.
Allah tuongoze tuwe watu wenye kusikia maneno ya haki na kuyafuata,amiin