Ramadhan Special Thread
Hutuba ya Ijumaa: Malezi ya Familia Katika Uislamu

Khutbah ya Kwanza:

Alhamdulillah, tunamshukuru Allah Subhanahu Wata'ala kwa kutupa uhai, afya na neema ya Uislamu. Tunamswalia Mtume wetu Muhammad (ﷺ), maswahaba zake na familia yake.

Enyi waumini!
Leo tutazungumzia malezi ya familia – jukumu tukufu ambalo linabeba uzito mbele ya Allah.

Allah amesema:
"Enyi mlioamini! Jilindeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto..." (At-Tahrim: 6)
Hii ni amri ya moja kwa moja ya kuhakikisha kuwa familia zetu zinaongozwa kwa maadili ya Kiislamu.

Baba na mama ni walimu wa kwanza.
Watoto hujifunza kwa kuona, si kusikia tu. Ukimfundisha mtoto kuswali lakini wewe huswali, hautamjenga. Uimara wa familia huanza na wazazi kuishi wanayoyasema.

Mtume (ﷺ) alisema:
"Kila mmoja wenu ni mchungaji, na kila mmoja ataulizwa kuhusu wale aliowachunga." (Bukhari & Muslim)

Malezi bora ni pamoja na:
  • Kufundisha watoto kuswali mapema.
  • Kuwafundisha adabu na huruma.
  • Kuepuka ugomvi mbele ya watoto.
  • Kuwalea kwa mazungumzo mema, si kelele na dharau.

---

Khutbah ya Pili:

Tunamshukuru Allah kwa kutufikisha Ijumaa hii. Malezi ya familia ni ibada – na kama ibada nyingine, huhitaji subira, hekima na dua.

Tujiulize:
  • Je, tunawafundisha watoto wetu Qur'an?
  • Je, tunaswali pamoja kama familia?
  • Je, nyumba zetu ni sehemu ya utulivu au vurugu?

Tujirekebishe. Tuombe msamaha kwa Allah na tuanzie leo, hata kwa hatua ndogo – dua ya pamoja, kusoma aya moja kwa siku, au kusali jamaa na watoto wetu.

Mtume alisema:
"Mtu bora ni yule aliye bora kwa familia yake." (Tirmidhi)

Hitimisho:
Tuwe wazazi wa mfano. Tuwalee watoto kuwa waumini, wenye maadili na heshima. Dunia itabadilika ikiwa familia zetu zitakua katika misingi ya dini na maadili mema.

Wa akhiru da'wana, Alhamdulillahi Rabbil ‘Aalamin.
 
Kesho ni siku ya funga ya Ashura ndugu zangu, fadhila zake ni kusamehewa madhambi ya mwaka mmoja uliopita

Je nani miongoni mwetu hana madhambi nikiwemo mimi ninayeandika hapa

Basi hii ofa huja mara moja kwa mwaka,huenda tusiipate Ashura nyingine mwakani tukawa ndani ya tumbo la ardhi

Basi tufunge hiyo kesho inshaAllah
 
Mume Amezini Nami Nimechukia Nifanye Nini?
Maswali: Zinaa-Liwati

SWALI:

MUME WANGU AMEZINI NA MKE WA MTU BAADA YA KUGUNDUA MAANA NIMEPATA MASHTAKA KUTOKA KWA MTOTO WANGU WA KIUME KUA ALIMFUNGIA NDANI YAYA NILIVYOMUULIZA AKAPINGA SANA LAKINI NILIVYOMWAMBIA KUHUSU HUYO MWANAMKE AKUBALI KUA KWELI AMEZINI NA KUSEMA KUA NI IBILISI.NIKIFIKIRIA ROHO INANIUMA SANA MPAKA INAFIKIA NAHISI NAMCHUKIA KWA KUNIHUNI JE NIFANYE NINI?







JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Tumepokea Swali lako kwa masikitiko ya hayo yaliyokusibu kuhusu mumeo.

Nasiha yetu ni kuwa kwanza mumeo alitakiwa afiche siri ya maasi aliyofanya kwa sababu Muislamu haimpasi kutaja siri ya maasi yake. Anatakiwa anapofanya maasi ni kujisitiri na kutubia kwa Mola Wake.

Tunafahamu kuwa jambo kama hilo ni la kumchukiza sana mtu na linatia ghadhabu kubwa. Lakini kama alivyokiri mwenyewe kuwa ni ibilisi aliyemchezea hadi akafika kufanya maasi hayo, na hivyo ni kawaida yake ibilisi kumtumbukiza mtu katika maasi. Kumbuka dada yetu kuwa baba yetu Adam ('alayhis-salaam) alishindiwa na ibilisi, alimhadaa hadi akamsababisha kuingia katika kumuasi Mola wake na ikawa ni sababu ya kutolewa Peponi. Naye Adam alirudi kwa Mola wake akatubu na Allaah Alimsamehe madhambi yake.

Hivyo ikiwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasamehe waja Wake Aliowaumba na kuwaruzuku kila jema, iwe vipi sisi binaadamu tusiwe wenye kusamehe wenzetu?

Imekuwa ni kazi nyepesi kwa ibilisi kuwatumbukiza wanaume katika maasi haya ya kuzini kwa vile wao ni dhaifu sana mbele ya wanawake. Ndio maana Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amewaruhusu wao waoe wake wanne wanapohitaji. Na wanawake ni fitna kubwa kwao. Na Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alionya:

عن أسامة بن زيد رضي الله عنهما : عن النبي صلى الله عليه وسلم قال : ((ما تركت بعدي فتنة أضر على الرجال من النساء)) . رواه البخاري ومسلم .


Kutoka kwa Usaamah bin Zayd (Radhiya Allahu 'anhuma) kwamba Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Sijakuachieni baada yangu fitna iliyo na madhara kwa wanaume kama wanawake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika kutaja mapambo na matamanio mengi ya binaadamu (wanaume), Ametaja kwanza ni huba ya kupenda wanawake:

((زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ الشَّهَوَاتِ مِنَ النِّسَاء وَالْبَنِينَ وَالْقَنَاطِيرِ الْمُقَنطَرَةِ مِنَ الذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ وَالْخَيْلِ الْمُسَوَّمَةِ وَالأَنْعَامِ وَالْحَرْثِ ذَلِكَ مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَاللّهُ عِندَهُ حُسْنُ الْمَآبِ))

((Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake, na wana, na mirundi ya dhahabu na fedha, na farasi asili, na mifugo, na mashamba. Hayo ni starehe ya maisha ya duniani; na kwa Allah ndio kwenye marejeo mema)) [Al-'Imraan:14]

Udhaifu huu wao mbele ya wanawake umemfanya ibilisi iwe rahisi kwake kuwahadai wanaume katika maasi ya zinaa.

Kwa hiyo, unatakiwa uwe na moyo wa msamaha na umsamehe mumeo madamu amekiri makosa yake. Kufanya hivyo utarudisha mapenzi yenu na muweze kuendelea na maisha yenu bila ya kuyaharibu. Kufanya hivyo naye atakuthamini zaidi na atachukua tahadhari zaidi ya kutokuingia katika maasi tena kama hayo.

Kumbuka vile vile kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Humpa mtu mwenye kuzuia ghadhabu na kusamehe daraja ya muhsiniyn (Wenye kufanya wema). Na daraja hii sio kila mtu anaweza kuipata kwa wepesi ila wenye moyo mkubwa wa kufanya hivyo, na bila ya shaka dada yetu nawe utakuwa ni miongoni mwa wenye sifa hii.

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

((ألَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي السَّرَّاء وَالضَّرَّاء وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ))

((Ambao hutoa wanapokuwa na wasaa na wanapokuwa na dhiki, na wanajizuia ghadhabu, na wasamehevu kwa watu; na Allah Huwapenda wafanyao wema)) [Al-'Imraan:134]



Yanayompasa mume kufanya na Nasiha zetu kwake:

Anatakiwa atubie kwa Mola wake Tawba ya kweli, kwa kuazimia kuacha kutenda maasi hayo. Atambue kuwa maasi ya zina ni jambo Alilolikemea sana Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) bali Ametuonya hata tusikaribie zina. Hivyo inampasa akhofu kurudia kufanya maasi hayo. Asome mada zinazohusu uovu wa maasi hayo na adhabu zake, ili apate kinaa ya kuacha kutenda.

Vile vile amuombe msamaha mkewe na arudie kwake na aridhike na mkewe na ampe haki zake sawa sawa kama inavyompasa.

Vile vile jitahidi wewe umridhishe mumeo daima na uhakikishe kuwa huweki kasoro katika kutimiza wajibu wako kwake kwa kujiweka katika hali ya kupendeza kila mara na kumstarehesha ili asipate matamanio kwa mwengine zaidi yako. Bila shaka utakuwa unafanya hivyo, lakini tunakukumbusha uzidi kuongeza mapambo katika ndoa yako, kwa kujipamba mwili wako, na nyumba yako pia.

Kisha kaa naye uzungumze naye kwa uwazi bila ya hamaki kwa hayo yaliyotokea. Mjadiliane kwa vizuri ili mpate kutatua yaliyo baina yenu.

Kisha someni mada katika viungo vifuatavyo huenda mkapata nukta za kukumbusheni kuzidisha mapambo ya ndoa yenu.


Jinsi Ya Kumfurahisha Mumeo
Jinsi Ya Kumfurahisha Mkeo


Tunakuombea ndoa ya furaha, amani na mapenzi baada ya hayo yaliyotokea.

Na Allah Anajua zaidi
 
Mume Anamtaka Ajimai Naye Njia Isiyo Ya Halali
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:

Asalamu aleikum warahmatullahi wabarakatu.

kwanza kabisa mimi nimeolewa nina miaka 16, lakini kwenye ndoa yangu nina matatizo na mume wangu na ni kuhusu ya kwamba huwa ana tabia ya kutaka kuniingilia sehemu ambayo haijahalalishwa kidini na ni haraam na kila ninapojaribu kumueleza hayo anaapa na kusema kuwa hatorudia lakini hakuna faida ana rudia haya daima sasa sijui nifanyeje. Naomba munipe nasiha itakayo nifaa mpaka Kesho Akhera.

Asalamu aleiykum.




JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), ahli zake, Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka siku ya Mwisho.

Haya ni baadhi ya matatizo ambayo dada zetu wanakumbana nayo katika unyumba. Hili tatizo hutokea kwa sababu ya malezi kwa mwanamme au mwanamke na pia kutofundishwa wajibu wa kisheria kwa wote wawili. Hivyo mume mara nyingi anakuwa hajui wajibu wake na haki yake katika ndoa na vile vile mwanamke. Hii hupelekea mmoja wao kuangukia katika haramu au kutotekeleza wajibu wake. Mara nyingi haya matatizo hutokea kwa sababu wazazi hawakuchunguza kwa kina kabla harusi.

Kumuingilia mwanamke kwa njia ya nyuma ni haramu, bali amuingilie katika njia iliyohalalishwa kama ilivyo katika kauli ya Allaah سبحانه وتعالى:

((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ))


((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223]

Kama tunavyoona katika hiyo aayah, Mwenyeezi Mungu katolea mfano shamba akionyesha kuwa ni mahali panapolimwa, na penye kulimwa panawezwa kulimwa kwa njia nyingi ingawa lengo ni kutatarajiwa kutoa mazao, na makusudio hapa kwa mwanamke, ni pahali anapoingiliwa mwanamke ambapo ni sehemu anayozaliwa mtoto. Kwa hiyo mtu kapewa ruhusa ya kumuingilia mkewe kwa mitindo mbalimbali lakini kwa sharti pawe sehemu ya mbele ambayo ndiyo inayotoa mazao ambayo ni mtoto. Na kumuingia mke kwa njia ya nyuma kunakwenda kinyume na fitrah (asili ya maumbile ya binaadamu). Vile vile mwanamke atakuwa amedhulumika kwa kupata sehemu yake ya kustarehe na mumewe na sehemu ya nyuma ni sehemu inayotoa uchafu na pia kitendo ni kitendo ambacho kimeharamishwa na Mola Mtukufu.

Kwa jinsi kitendo hichi kilivyokuwa ni kiovu kabisa, tunaona dalili ya kuharamishwa kwake kutoka katika Qur-aan na pia kuna dalili nyingi katika Hadiyth zifuatazo za Mtume صلى الله عليه وآله وسلم za kuharamishwa ambazo zina MAONYO MAKALI kabisa. Hivyo inampasa Muislamu ajiepushe kabisa nacho kitendo hicho ili aepukane na laana, adhabu na ghadhabu za Allaah سبحانه وتعالى :

Hadiyth ya kwanza: Haramu kitendo hiki:

عن خزيمة بن ثابت رضيَ اللَّهُ عنهُ انه قال: قالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم: ((إِتْيَانُ النسَاءِ فِي أَدْبَارِهِنَّ حَرَامٌ)) الألباني في السلسلة الصحيحة

Imetoka kwa Khuzaymah bin Thaabit رضيَ اللَّهُ ambaye amesema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: ((Kuwaingilia wanawake kwa nyuma ni haraam)) [Shaykh Al-Abaaniy katika Silsilatus-Swahiyhah]

Hadiyth ya pili: Allaah سبحانه وتعالى Hatomtazama anayefanya kitendo hiki:

عن ابنِ عَبَّاس رضي الله عنهما قال: قال رسول الله)) لا يَنْظُرُ اللَّهُ إلى رَجُلٍ أَتَى امْرَأَةً في دُبُرِهَا))

صحيح ابن حبان
Imetoka kwa ibn 'Abbaas رضي الله عنهما ambaye amesema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: ((Allah Hatomtazama mwanamume anayemuingilia mwanamke kwa nyuma)) [Swahiyh Ibn Hibbaan]

Hadiyth ya Tatu: Amelaaniwa anayefanya kitendo hiki:

قال النبي صلى الله عليه وسلم : (( ملعون من يأتي النساء في محاشِّهن: أي أدبارهن (( رواه ابن عدي وصححه الألباني في آداب الزفاف

((Amelaaniwa anayewaingilia wanawake kwa njia ya nyuma)) [Imepokelewa na ibn 'Udayy na amesema ni sahiyh Shaykh Al-Albaaniy katika Adaabuz-zafaaf]



Hadiyth ya nne: Amekufuru anayefanya kitendo hiki:

عن أبي هريرة رضي الله عنه ((من أتى حائضا أو امرأة في دبرها أو كاهنا فصدقه بما يقول فقد كفر بما أنزل على محمد)) صحيح ابن ماجه و قال الألباني إسناده صحيح

Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه : ((Atakayemuendea (atakayemuingilia) mwenye hedhi au mwanamke nyuma au atakayemuendea mtabiri akamuamini anayomuambia, atakuwa amekufuru yaliyoteremshwa kwa Muhammad)) [Sahiyh ibn Maajah na kasema Shaykh Al-Albaaniy kuwa isnaad yake ni Sahiyh]



Hadiyth ya tano:

عن ابن عباس رضي الله عنهما قال: جاء عُمَر بن الخطاب إلىٰ رسول الله فقال: يا رسول الله، هلكتُ! قال: (( وما الذي أهلكك؟)) قال: حَوَّلْتُ رَحْلِي الليلة، فلم يردَّ عليه شيئاً، فأُوْحِيَ إلىٰ رسول الله هذه الآيةُ: {نساؤكم حرث لكم فأتوا حرثكم أنىٰ شئتم} يقول: أَقْبِلْ، وأَدْبِرْ، واتقي: الدُّبر، والحَيضة سنن النسائي الكبرى

Imetoka kwa Ibn 'Abbaas رضي الله عنهما ambaye amesema: Alikuja 'Umar ibnul-Khatwaab kwa Mjumbe wa Allah akasema: Ewe Mjumbe wa Allah, Nimeangamia! Akasema: ((Nini kilichokuangamiza?)) Akasema: Nimepindua kipando changu usiku (nimemuingilia mke wangu sehemu ya mbele lakini kwa kumgeuza) Lakini hakumjibu kitu. Akateremshiwa Aayah hii ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo)) Anasema: (unaweza kumuingilia) kwa mbele na kwa kumgeuza na chunga kumuingilia nyuma na wenye hedhi. [Sunnan An-Nasaail-Kubraa]



Hadiyth ya sita

عن أم سلمة قالت: لما قدم المهاجرون المدينة على الأنصار تزوّجوا من نسائهم، وكان المهاجرون يجبون وكانت الأنصار لا تجبي، فأراد رجل من المهاجرين امرأته على ذلك، فأبت عليه حتى تسأل رسول الله صلى الله عليه وسلم، قالت: فأتته فاستحيت أن تسأله، فسألته أم سلمة فنزلت: {نساؤُكُمْ حَرْثٌ لَكُمْ فَأْتُوا حَرْثَكُمْ أَنّى شِئْتُمْ} وقال: «لا إلاّ في صَمَّامٍ واحِدٍ» . : مسند الإمام أحمد

Imetoka kwa Ummu Salamah رضي الله عنها kwamba: Muhaajiriyn walipokuja Madiynah kwa Maanswaar waliwaoa wanawake wao. Wanawake Wa Muhaajiriyn walikuwa wakilala kifudifudi (wakati wa kujimai na waume zao) na wanawake wa Maanswaar hawakuwa wakifanya hivyo. Mwanamume mmoja Muhaajir alitaka mkewe afanye hivyo akakataa. Akaenda kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم lakini aliona haya kumuuliza swali hilo, kwa hiyo Ummu Salamah alimuulizia kisha Aayah ikateremshwa inayosema ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo)) Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Hapana! (Sio kila sehemu upendayo) bali ni mbele tu. [Musnad ya Imaam Ahmad]

Nasaha zetu kwa dada yetu ni kama zifuatazo:-

1. Endelea kumcha Allaah سبحانه وتعالى bila kuyumba yumba.

2. Kuwa na istiqaamah na usimkubalie mumeo kukuingiza katika tendo hilo la haramu.

3. Mfanyie Da‘wah mumeo kwa hekima na mawaidha mazuri huenda akabadilika kutokana na tabia hiyo yake mbovu na mjulishe kuhusu Aayah yenye makatazo hayo katika Qur-aan na Hadiyth

4. Ikiwa imeshindikana kumrekebisha basi itisha kikao baina ya wazazi wako na wazazi wa mume. Na ikishindikana kabisa, bora udai talaka yako uepukane na haraam hiyo.



Tanbihi:

Mume kumuingilia mke kwa nyuma haina maana kwamba mke ameachika (Talaka) moja kwa moja kama wanavyofahamu wengi, bali ana haki mke kudai talaka lakini hakuna dalili kwamba hukumu ya talaka iwe imepita katika kitendo hiki.

Tunakuombea kwa Allaah Akupatie moyo wa kukataa maovu na Akupatie uimara katika kudumu na mazuri. Tunamuomba Allah Amuepushe mumeo na tabia mbaya hiyo na Amrudishe katika njia ya haki. Tunakuombea muafaka katika kutatua tatizo hilo.

Na Allah Anajua zaidi.
 
Mume Anamuingilia Njia Isiyo Ya Halali Kwa Nguvu, Anaogopa Kudai Talaka Asije Kuzini
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:




Assallam allaykum warahmatullah wabarakatu. Napenda kumshukuru muumba aliyenipa uwezo wa kuandika swali hili leo hii. Mimi mume wangu anatabia hiyo ya kuniingilia kinyume na maumbile, humkatalia lakini ananifanya kwa nguvu na pia nilisha jaribu kudai talaka lakini hataki kunipa na pia kinachoniogopesha nisije nikaachwa halafu ikapelekea kufanya maovu eidha kuzini na mengineyo maana sisi wanaadamu hatuko sawa. Pia mume wangu nampenda isie akanipa talaka halafu nikazini nae je nifanye nini? Naomba ushauri wenu. Mungu anajua zaidi.




JIBU:


Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola

i wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.


Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kuingiliana kinyume na maumbile baina ya mume na mke. Kulingana na swali lako ni kuwa wewe hutaki kufanya hivyo lakini ni mume ndio mwenye kukufanya hilo kwa nguvu. Ikiwa hivyo unavyosema ni kweli basi wewe utakuwa huna madhambi na mumeo ndio atakayebeba dhambi la kutekeleza hilo. Tufahamu kuwa jambo hili lina madhambi makubwa na wala tusichukulie mzaha. Katika Hadiyth kadhaa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu 'Alayhi wa aalihi wa sallam) anatuambia yafuatayo:


1. "Allaah Hatomtazama mwanamume mwenye kumuingilia mkewe kwa nyuma" (an-Nasaa'iy na Ibn Hibbaan kwa Isnadi nzuri).




2. "Amelaaniwa mwenye kumuingilia mwanamke kwa nyuma" (Ahmad, Abu Dawuud na Ibn 'Adiy).







3. "Mwenye kumuingia mwenye hedhi au mwanamke kwa nyuma au kumwendea mchawi na kumuamini kwa anayosema basi amekufuru kwa aliyoteremshiwa Muhammad" (Abu Daawuud, at-Tirmidhiy na Ibn Maajah, na Isnadi yake ni Sahihi).




4. "Twaawuus amesema: 'Ibn 'Abbaas aliulizwa kuhusu mtu anayemuingilia mkewe kwa nyuma'. Akasema: 'Huyu ananiuliza kuhusu ukafiri'" (an-Nasaa'iy).



Kwa njia hiyo utakuwa huna budi kukataa kwani Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuhusu hilo ni,

"Hakika utiifu ni katika wema".


Na pia, "Hakuna utiifu kwa kiumbe katika kumuasi Muumba".


Na kwa nini ukhofu kuwa ikiwa utaachwa hutoolewa tena. Muislamu mwenye Imani yake kikamilifu huwa hakhofu katika mas-ala ambayo ni ya kumtii Allaah Aliyetukuka na Mtume Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kwani anajua kuwa hataachwa kuteseka.


Hebu fikiria sana kabla ya kuolewa na mumeo huyo, je, ullijua kuwa yeye ndiye atakayekuwa mumeo?

Na ujue ya kwamba, hutoacha kitu kwa ajili ya Allaah Aliyetukuka isipokuwa utapatiwa badali ambayo ni bora zaidi. Hiyo ndiyo iliyokuwa dhana ya Ummu Salamah (Radhiya Allaahu ‘anha) alipoaga dunia mumewe Abu Salamah (Radhiya Allaahu ‘anhu), yeye alidhania kuwa hatopata mume kama huyo mumewe wa kwanza lakini Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alimwambia aombe kwa Allaah Aliyetukuka Ampe mume bora kuliko aliyeondoka. Du’aa yake ilijibiwa na akawa ni mwenye kuolewa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
Nawe lazima upige moyo konde na utafute njia ya kuepukana naye kwani kukaa naye inaonyesha unaridhia madhambi hayo na huenda ukawa unapata madhambi sawa na mumeo. Msamaha wa Allaah Aliyetukuka hauji ila mtu anapojiondosha katika maasiya.




Yale ambayo unafaa uyafanye ni kama yafuatayo:



1. Uzungumze tena na mumeo kuhusu hilo na kuwa kama Waislamu hamufai kufanya hilo.




2. Ikiwa bado anaendelea itabidi ulifikishe jambo hilo kwa wazee wako na wake na muwe ni wenye kufanya mkutano kuhusu suala hilo na pia umhame katika malazi ili asije akakuingilia kwa nguvu. Ikiwa bado inaonekana kuwa hataki kufuata wasiya wa wazee basi idai talaka ili usiwe tena chini ya amri yake.




3. Ikiwa hakukupatikana ufumbuzi wowote itabidi uende kwa Qaadhi au Shaykh kwenye eneo lako ili asikilize kesi yenu na atoe uamuzi.


Ikiwa anaendelea na hilo utakuwa dada yetu huna budi kuomba talaka kutoka kwake. Inabidi uchague mambo mawili: ima umridhishe yeye au Allaah Aliyetukuka, Muumba wako. Je, wewe umechagua nani kati ya hao wawili? Uchaguzi ni wako wala sisi hatuwezi kukulazimisha, ila tu tunaweza kukunasihi katika njia iliyo bora duniani mwako na Akhera.


Ikiwa kwa hakika utaweza kufanya hivyo basi Imani yako itakuwa ni thabiti na hutoingia kwenye zinaa pia InshaAllaah. Allaah Atakupatia badali ambayo ni bora zaidi na mume aliye bora kabisa kuliko huyo wako wa awali. Huu ni mtihani kwako, je, utaupita? Au utafeli.


Kuweka dhana zako na imani kuwa ukiachwa utatumbukia kwenye zinaa, huo ni udhaifu wa kiimani na kukosa elimu ya ubaya na madhara ya zinaa. Kama utakuwa na elimu nzuri ya ubaya na makatazo na uharamu wake, hatudhani kabisa kama unaweza kulifikiria jambo hilo kabisa.


Soma kuhusu ubaya, madhara na uharamu wa zinaa katika viungo hivi:


Binti Mwenye Kufanya Maasi Ya Zinaa


Pia soma haya hapa chini kuhusiana na Liwati na umpe mumeo asome vilevile ili aone makemeo na laana zilizomo za kitendo hichi kichafu kabisa:


Kuharamishwa Liwati


Mume Wangu Ananitaka Njia Isiyo Ya Halali


Amemuingilia Mkewe Kimakosa Nini Hukmu Yake?


Na Allaah Anajua zaidi
 
Mume Hana Uzazi, Naye Kashika Mimba Ya Zinaa, Amjulishe Mumewe Au Atoe Mimba?
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:

Assalam alaikum,

Namshukuru Mungu Mola wa viumbe vyote.Ama baada ya haya nina tatizo naomba nisaidiwe mimi ni mwanamke mbaye nimeolewa na huu ni mwaka wa 3 lakini sikujaaliwa kupata mtoto na kwa upande wangu sikuwa na tatizo ila mume wangu ndio mwenye tatizo la kizazi lakini anatumia dawa za sunna. Kwa bahati mbaya na kwahamu niliyokuwa nayo ya mtoto nikafanya kosa nikatembea nnje siku 1 na wala sikukusudia kuwa nitakuwa na mimba bilisi tuu kanihadaa,baada ya 2 weeks nikajihisi nina mimba na hivi ni miezi 2.

jamani sasa mtoto wa mume au wa nje nifanyeje,nilipomueleza mume alifurahi sana lakini naogopa nitasema nini mimi kwake na kwa Mungu sasa mnanishauri vipi nifanye. au niitowe pia naogopa dhambi mbili kwa pamoja kuuwa na kuzini nje nisaidieni.natarajia majibu ya kuniongoza mazuri NA MUNGU ATANISAIDIA.



JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalah Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mimba ya zinaa.



Mara nyingi sisi hufanya makosa yaliyo makubwa mbele ya Allaah Aliyetukuka nasi tukawa ni wenye kusema bahati mbaya au Iblisi ndiye aliyekushawishi. Kudhania hivyo halitusaidii sisi na lolote wala chochote bali linatupatia sisi muhula na nafasi ya kufanya mengine na kisha kutoa hoja hizo hizo.



Haiwezekani kuwa ukawa umefanya tendo kama la zinaa kisha useme sikukusudia kwani kitendo hicho kinajumlisha mambo mengi sana. Mwanzo unaanza kumtongoza mwanamme au yeye akutongoze, mzungumze, mpeane miadi na mfanye kitendo chenyewe ambacho ni kibaya sana. Allaah Aliyetukuka na Mtume Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wametuhimiza sana kuwa na subira katika mambo yetu yote. Kutokuwa na subira ndiko kumekutia katika njia panda. Na lau kama ungekuwa ni mwenye kuifikiria ile Aayah ya Suratush Shuuraa (42): 49-50 hungekuwa na tatizo kwani ungefahamu ya kuwa watoto wote wanatoka kwa Allaah. Hivyo, tatizo la ni kuhusu hilo na kuhangaika kutafuta madawa n.k.?



Muislamu hutakiwa na kutarajiwa awe na imani kuwa Allaah Humtunuku Amtakaye watoto na Humfanya Amtakaye tasa kwa rehma na uadilifu Wake kama inavyothibitisha Qur-aan:

"Ufalme wa mbingu na ardhi ni wa Allaah; Anaumba Apendavyo, Anamtunukia Amtakaye watoto wa kike, na Anamtunukia Amtakaye watoto wa kiume. Au Huwachanganya wanaume na wanawake, na Akamfanya Amtakaye tasa. Hakika Yeye ni Mjuzi Mwenye uweza". Ash-Shuraa: 49-50.

Hivyo basi hakuna makisio ya miaka wala muda kuwa ndio muda wa mwisho wa kukata tamaa kwa Muislamu kutunukiwa mtoto; kwani imethibiti kawaida kuwa watu hukaa baada ya kukaa zaidi ya miaka kumi ya ndoa yao na wakaja kutunukiwa watoto baada ya hapo.

Umesema, Kwa bahati mbaya na kwahamu niliyokuwa nayo ya mtoto nikafanya kosa nikatembea nnje

Ndugu yetu, hiyo haikuwa bahati mbaya bali ni malipo kwa asiyekuwa na imani kuwa Alilolikataza Allaah ni vyema tujiepushe nalo na kama ukipingana na hayo basi huenda Akakulipa hapa duniani kwa kukufedhehi kama ulivyofedheheka na hakuna anayekusuduia kushika mimba lakini Ibiliys hukushawishi na kukuhakikishia kuwa mara moja tu hakuna kitachotokea kwani uko na mumeo miaka mingapi na hukushika mimba basi jaribu tu hakuna kitu na sasa rafiki yako Ibiliys kakuacha mkono na anakujia kwa njia nyingine; njia ya kujisitiri na kutoa mimba.

Huyo mtoto uliyezaa nje ya ndoa hatambuliki kisheria, asli mtoto ni wa mwenye kitanda lakini wewe unaelewa vizuri kuwa si wa mumeo bali umemtia katika familia isiyomuhusu na imethibiti katika Hadiyth za Mtume (Swalah Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa:



عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه السلام حين نزلت آية المتلاعنين : ((أيما امرأة أدخلت على قوم من ليس منهم فليست من الله في شيء ولن يدخلها الله جنته وأيما رجل جحد ولده وهو ينظر إليه احتجب الله منه وفضحه على رؤوس الأولين والآخرين))




Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ilipoteremsha Aayah ya waliolaaniwa akasema ((Mwanamke yeyote atakayeingiza katika watu asiyekuwemo katika wao basi hana kitu kwa Allaah na hatoingizwa na Allaah katika pepo Yake, na mwanamume yeyote akimkataa mtoto wake na yeye anamuona, basi Allaah Atamfungia (rehma Zake) na Atamfedhehesha juu ya vichwa vya viumbe kuanzia wa mwanzo mpaka wa mwisho)) [Abu Daawuud, na Haakim kitabu cha Twalaaq, hadiythi namba 2814]



Na wewe bila ya shaka yoyote ile ushamtia katika famila asiyekuwemo yaani umechukua mimba kwa uzinifu na hali unaye mume basi umemuingizia katika familia yake asiyekuwa wake.



Na umesema kuwa ulipomweleza mume wako alifurahi sana, fahamu kuwa ni haki yake kufurahi lakini hukumueleza ukweli kwani mtoto ni wa mtu mwengine na si wa aliyekuoa na hilo ndilo ulilotakiwa kumueleza kama kweli ulikuwa na la kumueleza na kumfurahisha na huna njia ya kumueleza na hilo si tatizo kwani unaweza kuitafuta njia ya kumueleza na kumfahamisha kuwa hiyo mimba si yake bali ya mtu fulani.

Umesema, lakini naogopa nitasema nini mimi kwake na kwa Mungu,

Kumbuka hata rafiki yako (Ibiliys) aliyekuacha mkono baada ya kukutia katika dhambi la zinaa pia hudai kuwa anamuogopa Allaah kama inavyothibitisha Qur-aan kwa kusema:

"… Mimi si pamoja nawe. Hakika mimi namuogopa Allaah, Mola Mlezi wa walimwengu wote." Al-Hashr: 16.

Ushauri tunaoweza kukupa ni kama huu: Umetenda kosa lenye kustahiki adhabu iliyowekwa na Allaah nayo ni kupigwa mawe mpaka ukafa kwani wewe ni mzinifu mwenye mume au aliyeolewa au aliyewahi kuolewa; kwa kuwa hakuna pa kupitishiwa hukumu hiyo, hii haina maana kuwa umesameheka bali utaikuta huko mbele ya Allaah kama hukutubia na kukubaliwa tawbah yako, hivvyo basi njia ya kufanya ni kuomba tawbah, tawbah ya kweli kweli na kujuta kwa tendo hilo.



Kitendo ulichokifanya kimekufikisha katika njia panda na hilo limekufanya wewe uanze kufikiria maovu: Je, nitoe mimba au niseme uongo kwa mume wangu? Kuua kiumbe ni katika dhambi kubwa na kuhusu uongo Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anasema kuwa Muumini hawezi kabisa kusema uongo. Njia iliyobaki ni kumwambia kweli mume wako, upate radhi za Allaah Aliyetukuka kuliko kumwambia uongo ukapata radhi ya mume lakini ukakasirikiwa na Allaah Aliyetukuka. Kisha ukisema uongo utakuwa umefanya dhuluma kwani huenda mkazaa na mumeo watoto kwani hakuna ugonjwa usiokuwa na dawa na hapo anapoaga dunia mtoto wako huyu wa kwanza wa nje ya ndoa akamrithi babake wakati ambapo katika sheria hafai kumrithi.





Ushauri wetu ni kuwa umtake msamaha mumeo na kumuombea kwa Allaah awe na moyo wa kukukubalia na kukusamehe na katika kukusamehe pia anaweza akaamua kukuacha kwani hujaonyesha ikhlaas katika maisha yenu na inaonyesha una fadhilisha dunia mbele ya Aakhirah na hukuwa na elimu ya nani unayemuasi. Lakini huenda



Ama kutoa mamba, ni jambo lisilofaa kabisa na ni madhambi mengine ambayo utakuwa unayatafuta, soma hapa chini suala hilo:

Kutoa Mimba - Hukmu Na Kafara Yake

Pia soma jibu hapa chini linalohusiana na hili swali lako:

Nimekwenda Nje Ya Ndoa, Nimjulishe Mume Wangu?

Hivyo, muombe mume wako msamaha na muombe Allaah tawbah ya kweli na inshaAllaah Yeye ni Mwingi wa kusamehe na Mwingi wa Kurehemu.

Na Allaah Anajua zaidi
 
Mume Mwenye Tabia Chafu Ya Liwati Anafaa Kuwa Imaam? Je, Inafaa Kumuozesha Mke?
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:

Mwanamme anaemuendea kinyume cha maumbile mkewe (sehemu ya haja kubwa), anafaa mume huyu awe imamu? Nimeangalia baadhi ya majibu yaliyotolewa kuhusu mume mwenye sifa hii chafu, lkn sijaona kuhusu uimamu?

Jee jamii imuangalie vipi mwanamme huyu? Jee inafaa kumuozesha mtoto wa mtu mwanamme mwenye tabia hii ya Kaumu Lut?



JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Kwenda kinyume na maumbile/liwaat ni katika madhambi makubwa na ni katika uchafu wenye kupelekea kuharibika kwa maumbile, fitwrah, dini na dunia, bali ni uchafu unaofisidi na kuhariku uhai wote ndio Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Akawaadhibu watu waliozuwa uchafu huo adhabu kali sana kama inavyothibitisha Qur-aan kwa kusema:

“Na tulimtuma Luutw', alipowaambia watu wake: Je, mnafanya uchafu ambao hajakutangulieni yeyote kwa uchafu huo katika viumbe vyote! Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio mkawawacha wanawake? Kumbe nyinyi ni watu wafujaji! Na haikuwa jawabu ya kaumu yake isipokuwa kuambizana: Wafukuzeni katika mji wenu, maana hao ni watu wanaojitakasa. Basi tukamwokoa yeye na watu wake, isipokuwa mkewe, alikuwa miongoni mwa waliobakia nyuma. Na tukawamiminia mvua. Basi tazama jinsi ulivyokuwa mwisho wa wakosefu.” Al-A’raaf: 80-84 na pia tazama Suurat Huud: 77-83.



Basi ni vyema jamii ielimishwe na ielezwe bila ya kuogopa kuwa yaliyowafika wenye tabia chafu ya kwenda kinyume na maumbile, tabia ambayo hata wanyama hawanayo, ni katika mabalaa yanayoweza yakatufika kama hakutokuwa na wenye kusema kuwa haya ni machafu na ni haraam na hatarajiwi yeyote katika wenye kuaminiu Allaah na Siku ya Mwisho na akawa anatarajia malipo kwa Allaah kuthubutu kuruhusu amali kama hii, wachilia mbali kuthubutu kuruhusu nchi yake iwe ndio pahala pa kuhalalisha amali aliyoiharamisha Allaah na kuwaadhibu wahusika kwa adhabu kali kabisa. Na wanaofanya hayo ni miongopni mwa wale waliofadhilisha uhai huu kwa kuuza dini yao kwa kitu kidogo katika dunia kwa kuwakubalia wafadhili wao wahalalishe Alichokiharamisha Allaah na Akatoa adhabu ya kuigeuza nchi juu chini, na kuteremshiwa mvua ya changarawe za udongo mgumu uliokamatana wa Motoni na yaliyowafika wenda kinyume na maumbile/ liwaat hayako mbali na wenye kuihalalisha wachilia mbali wenye kutenda amali hiyo kama hawakutubia, na Allaah Ameijaalia kuwa miongoni mwa Aayah za Qur-aan inayotakiwa kusomwa (sio kusomewa maiti) ili iwe ni funzo na mawaidha kwa jamii na kwa wahusika kama wako katika jamii.

Suala lina utata isipokuwa tu kama muulizaji ni mke wa huyo mume basi hapana kitu kwani huwa anatafuta hukumu ya kisheria; ama ikiwa muulizaji anauliza tu kwa kumdhania mtu fulani Mwanamme anaemuendea kinyume cha maumbile mkewe, bila ya kuwa na ushahidi unaokubalika katika Uislamu; basi ieleweke kuwa yeyote katika wenye kuamini Allaah na Siku ya Mwisho iwe muulizaji wetu na wengine, akitujia na kutupa habari kama hii au yoyote yenye kuhitaji ushahidi na uthibitisho kwa kuwa ina hatari ndani yake madhara ni makubwa kuliko tunavyofikiria kwa jamii kama ulivyogusia ‘anafaa mume huyu awe imamu’ na kwa anaedhaniwa ‘jamii imuangalie vipi mwanamme huyu? hapa kama muulizaji ni mke wa huyo mume basi ni sawa, vyenginevyo patahitajika kufanyika uchunguzi ili kuweza kufikia kuelewa ukweli wake, kwa kuchelea tusije tukawaletea watu madhara, kwa kutojua hali yao tukabakia kujuta. Kama inavyotushauri na kututaka Qur-aan kwa kutuita kwa jina tulipendalo:

“Enyi mlioamini! Akikujieni mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kuto jua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyo yatenda.” Al-Hujuuraat : 6.

Hali ya pili ni kuwa muulizaji kama sio mke wa huyo mume, huenda akawa katika waliotakiwa kujitenga mbali na wingi wa kudhania dhana mbovu kwa watu, kwani katika baadhi ya dhana ni dhambi zinazostahiki adhabu (kama hii ya kwenda kinyume na maumbile ikiwa hakuna ushahidi) na kama jambo hilo lipo basi kwanini usimuaidhi kama wewe ni mke, au ilikuwa vyema upeleke lalamiko lako kwa wazazi au wahusika ili awaidhiwe na afaidike huenda akatubia na kuacha, kwani (kama muulizaji sio mke) kupekuwa na kuchunguza au kuwa na tabia ya kutafuta aibu na kuwatupia Waislamu si jambo linalotakiwa awe nalo Muislamu, kwani unaemsingizia ni ndugu yako Muislamu unaetakiwa umsitiri kwa kumuwaidhi na kumuelimisha; na kama unayosayema hanayo basi kufanya hivyo huwa ni ‘buhtaan’ (kosa kubwa zaidi ya kusengenya) kumzulia na kumsingizia mtu jambo ambalo hana.

Asli katika Uimamu (kuswalisha watu) ni kuwa aswalishe aliye bora katika kusoma Qur-aan: mwenye kusoma Qur-aan vizuri kama inavyotakiwa, kama ilivyothibiti katika Hadiyth kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema

“…itapofikia wakati wa Swalah basi na aadhini mmoja wenu na aswalishe mkubwa wenu -na katika riwaya ya Abu Daawuud- Awaswalishe qawm (watu) aliye mbora wao katika kusoma Qur-aan….” Imepokelewa na Al-Bukhaariy na Abu Daawuud.

Jee jamii imuangalie vipi mwanamme huyu? Kwa kuwa hatuna uwezo wa kupitisha hukumu kwa hali tulizonazo hivi sasa na nchi tunazoishi ambazo hazifuati sheria za Kiislam, lakini hukumu yake Kiislam ni kuuliwa na kulaaniwa kwa yule mfanyaji na mfanywaji kama ilivyothibiti katika Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Yeyote mwenye kufanya dhambi dhahiri shahiri na kueleweka au kuonekana na kila mtu katika jamii au mwenye kujionyesha kwa uchafu wake inavyotakikana ni kuwa jamii iwe na msimamo wake kuhusu watu wa namna hii ambao si msimamo wa kuwatenga au kuwabughudhi kwani wemefitinishwa na waliyonayo, msimamo utaoweza kuwasaidia ili wajing’oe katika tabia yao mbaya iwe kwa kutafuta namna ya kuwatibu kama wanahitaji tiba na hapo hapo kutafuta njia na mbinu au namna ya kuihadharisha jamii na kwa kuhakikisha kuwa watu hawa hawaachiliwi kuingia au kwenda pahala katika jamii bila ya kuwa chini ya ungalizi maalumu wasije kuwaambukiza wengine katika jamii.

Inafaa kumuozesha mtoto wa mtu mwanamme mwenye tabia ya kwenda kinyume na maumbile/ liwaat? Sehemu hii ya suala pia ina utata kwani kikawaida aliyefitinishwa na fitna kama hii huwa hana haja yoyote ile na wanawake isipokuwa kuwa shoga katika shoga zake na hili pia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amelikataza kumruhusu hanithi kuwa na ushoga na mkeo au mwanamke mwenye kuamini Allaah na Siku ya Mwisho, kwani kwa amali hii huweza kufikia akawa hana uwezo wa kumtekelezea mke haki yake ya kindoa (kumuingilia) kwani umuhimu wa mtu kuwa mwanamume na kuoa (sio mali) ni kuwa na uume na kama uume hauko au haufanyi kazi ni mzigo usio faida katika mwili basi ndio janga kubwa.

Tujaalie au tukadirie kuwa mtu mwenye tabia chafu na mbovu kama hii ameoa; nini kunaweza kutokea au nini kinatokea kwa wingi?

Mke huwa ni mhanga ‘dhwahiyyah’ hivyo huwa hana raha wala utulivu na kubwa kuliko hayo huwa hana mapenzi ‘mawaddah’ wala rahmah ambazo ni katika desturi na kawaida za maisha ya mke na mume, hivyo basi uhai wa mke (kama hakulalamika na watu kulishughulikia lalamiko lake) humalizikia kuwa ni adhabu aliyotundikwa nayo; kwani anayumbayumba baina ya huku na huko, huku hayuko na huko hayuko; hayuko katika walioolewa, maana kubwa katika kuolewa ni kupatikana tendo la ndoa na yeye hajapata kulionja toka aolewe wala hakuna njia ya kulipata kwani halipo kwa aliyetarajiwa awe nalo (wala hayuko katika wajane) anatambuliwa na jamii kama ni mke wa Fulani (wala hayuko katika walioachwa) hii ni sababu tosha kwa mwanamke kudai talaka; hivyo kumuoza mtoto mtu mwenye tabia ya kwenda kinyume na maumbile/ liwaat ni kama kumchinja mtoto wako kwa kisu kisicho na makali na kumzika hali ya kuwa hai, kwani huenda akaingia katika zinaa kwa kutamani kupata wanachopata wanawake wenzake kwa waume zao au huenda akatumbukizwa katika jangwa lisilokadirika kwa huyo anayeitwa mume kumtafutia beberu la kumtimizia mkewe mahitaji yake. Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Atuepushe na uchafu huu na Awaepushe dada zetu na waume wenye sifa kama hii.

Na Allaah Anajua zaidi
 
Mwanamke Aliyefanya Maasi Ya Zinaa Anaogopa Kuolewa
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:



Assalaam aleykum.

Kwanza ningependa kutoa shukurani zangu kwa kuweza kutuelimisha kwenye masuala haya ya dini.



suali langu:nini ushauri kwa mwanamke ambaye alifanya zinaa na akajutia na kutorudia tena, na kuzidisha ibada kwa sala, sadaka na kufanya hijja, lakini anaogopa kuolewa (na umri unakwenda) kwa kuhofia kuwa ataonekana hana bikira na labda kuchukiwa na mumewe.



Natanguliza shukrani









JIBU:



Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kuogopa kwa mwanamke aliyefanya uzinzi kuolewa.

Mwanzo tunamuombea kila jema limfikie na kumuombea apate Maghrifah ya kutoka kwa Mola wetu Mlezi. Ikiwa ni kama mlivyosema kuhusu huyo mwanamke basi tunatarajia kuwa atakuwa mahali pema na pazuri Peponi. Hii ni kwa kauli ya Aliyetukuka:

“Na wale wasiomuomba mungu mwingine pamoja na Allaah, wala hawaui nafsi aliyoiharimisha Allaah isipokuwa kwa haki, wala hawazini; na atakayefanya hayo atapata madhara. Na atazidishiwa adhabu Siku ya Qiyaamah na atakaa humo kwa kufedheheka milele. Ila yule atakayetubia na kuamini na kufanya vitendo vizuri; basi hao ndio Allaah Atawabadilishia maovu yao kuwa mema; na Allaah ni Mwingi wa kusamehe na Mwingi wa kurehemu. Na aliyetubia na kufanya mema, basi kwa hakika yeye anatubu kweli kweli kwa Allaah. … Hao ndio watakaolipwa ghorofa za Peponi kwa kuwa walisubiri na watakuta humo heshima na amani. Wakae humo milele: kituo kizuri na mahali pazuri pa kukaa” (Al-Furqaan: 68 – 76).



Ama kwake yeye kukataa kuolewa kwa ajili siri hiyo isije ikafichuka yuko katika usawa na kwa kufanya hivyo Allaah Aliyetukuka Atamfichia Siku ya Qiyaamah pia mbele ya umati wa watu. Njia bora ya yeye kuweza kuingia katika unyumba ni kutokea Muislamu ambaye hatofichua siri hiyo lakini amsitiri katika hali hiyo aliyokuwa nayo huyo dada. Na atakayefanya hivyo basi atakuwa na fungu kubwa mbele ya Muumba wake.



Ikiwa hakutapatikana mwenye kujitokeza kumuoa, hakuna ubaya kwake kukaa bila kuolewa maadam hatoshawishika kuingia kwenye uzinifu. Azidishe ibada sana na funga za Sunnah na Allaah Atamuhifadhi inshaAllaah.



Na Allaah Anajua zaidi
 
Mwanamme Amefanya Liwati Akatubu, Mwanamke Anafanya Mapenzi Lakini Hajaingiliwa, Je, Wanaweza Kuoana?
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:




Asalaam alaykum.



Shukrani kwa kutupatia nafasi adhym ya kujifunza. nauliza kijana wakiume amewahi kufanya liwaat ya kwa mwanaume mwenzake na mwanamke kwa wakati tofauti,akalia sana na kuazimia kutofanya tena, hukonyuma hakuwahi kuzini ila kwa hao wawili. akabahatika kupata mchumba.kwa sharti waish kiislam, kwani mwanamke alikuwa ana mazingira yote ya zinaa anatoka mpaka sannane usiku kwenye starehe kwenye mahoteli na wanaume mbali mbali na wanafanya romance,ila hakuwahi kuingiliwa,nae shart lake kuish kiislam, mahari tayari,ila mwanamke anasema yeye yuko tohara hajawahi kuzini na kamna mwanaume amewahi kuzini, hawafanani akamuo mzinifu mwezake,yeye ni tahara mwanaume amejibu k hakuwahi kuzini ila aliwahi kufikia asilmia tisni ya kuzini. Lakini kweli kila akiingiza tu uume anamaliza kabla ya kufanya, sasa jee hawa watu hawawezi kuona kwasababu mwanaume kasema uongo?







SWALI KALIRUDIA:




Asalaam, alaykum,

ALLAH subnhaana wataala akulipeni kwa kutuelimisha, swali ukawahi kufanya liwaat, halafu ukAjuta na kuazimia kutofanya tena, jee hamfanani kwa kuoana na mwanamke anayefanya mapenzi yote ila haruhusu kuingiliwa. Na pia akawa mwanamke anakwenda kwenye kumbi za starehe na wanaume mbali mbali.haifai kumokoa kwa kumoa na kukubaliana kuishi kwa kufata dini ya kiislam katika maisha yenu,










JIBU:




Sifa zote njema Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema Siku ya Mwisho.




Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mwanamme aliyefanya liwati na mwanamke anayekwenda kwenye nyumba za starehe.

Swali lako linaonyesha kuwa hao watu wameshaoana na unataka kujua kama wanaweza au hawawezi kuoana? Tunashauri mtu awe anauliza jambo kabla hajaingia ndani yake au kabla hajalifanya jambo lenyewe, kuliko kulifanya kasha ndio swali laja.

Hata hivyo, tukijibu swali lako, ni kuwa wote wawili hao wana madhambi japokuwa dhambi la mwanamme ni kubwa zaidi kuliko la mwanamke. Hakika hakuna aliye twahara kati ya hao wawili kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Ameonya:

“Wala msikaribie uzinzi. Hakika huo ni uchafu na njia mbaya” (al-Israa’ 17: 32).

Na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akatumbia:

“Zinaa ya jicho ni kutazama, ya mkono ni kushika, ya masikio ni kusikiliza na ya miguu ni kutembea katika maasiya”.




Hivyo, inatakiwa kila mmoja kati yao atubie kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) toba ya kweli kweli na sawa sawa. Kutubia kikweli kweli ni kutimiza masharti yafuatayo:




1. Kujiondoa katika maasiya.

2. Kujuta kwa kufanya dhambi hilo.

3. Kuazimia kutorudia tena kosa hilo.




Mwenye kutubia kisawa sawa, Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Humsamehe na kwa hiyo huwa hana tena dhambi. Na watu hao Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anawazungumzia:

“Isipokuwa wale waliotubu baada ya hayo na wakatengenea; kwani bila ya shaka Allaah ni Msamehevu, Mwenye kurehemu” (an-Nuur 24: 5).

Na Anasema (Subhaanahu wa Ta’ala) kwa uwazi zaidi:

“Isipokuwa atakayetubu, na akaamini, na akatenda vitendo vyema. Basi hao Allaah Atayabadilisha maovu yao yawe mema. Na Allaah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu. Na aliyetubu na akafanya mema, basi hakika huyo ametubu kweli kweli kwa Allaah” (al-Furqaan 25: 70 – 71).




Kwa kuwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Husamehe madhambi yote (az-Zumar 39: 53), mtu anayetubia huwa hana tena dhambi kwa hivyo anaweza kuoa au kuolewa na mwanamke twahara au mwanamme wa aina hiyo.




Kitu muhimu ni kujaribu kumchunguza kama kweli ameacha maovu hayo na akaanza kufanya mema na mazuri. Ikiwa amebadilika kabisa basi hakuna matatizo kwa ndoa hiyo kufanyika kwa ridhaa za wote wawili. Hakuna atakayelazimishwa kuoa au kuolewa. Ikiwa mwanamke anajiona kuwa yeye ni msafi sana na anahitaji mwanamme ambaye hajazini au kufanya liwati basi ana khiyari ya kukataa na hatolazimishwa. Hata hivyo, akimpata mwanamme kama huyo ambaye hajafanya machafu naye mwanamme huyo anaweza kuweka sharti kuwa lazima awe mwanamke ni kama yeye, hajatembea na mwanamme yeyote. Kwa sharti hilo, mwanamke naye atakuwa hawezi kuolewa na mwanamme huyo yeye tayari amestarehe na wanaume wengi ila tu hakuingiliwa na kustarehe kwenye kunaonyesha kuwa maadili ya mwanamke huyo si mazuri.




Kwa muhtasari ni kuwa, ikiwa kweli wametubia wanaweza kuoana bila ya matatizo yoyote yale.




Bonyeza viungo vifutavyo upate manufaa zaidi:




Mwenye Kufanya Maasi Ya Liwati Anaweza Kurudi Kwa Allah Kutubia?




Ndoa Baada Ya Kutubu Zinaa










Na Allaah Anajua zaidi
 
Mwanamume Aliyetembea Na Mke Wa Mtu vipi Atubie?
Maswali: Zinaa-Liwati
SWALI:







Assalaam aleykum. Mie nilikuwa nauliza jee? Mwanaume akitembea na mke wa mtu vipi atubie.



JIBU:

Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.



Hakika ni kwamba hili ni swali zuri na nyeti na inabidi liwekwe wazi ili watu walipatie umuhimu na uzito unaopaswa kupewa.



Wamesema wanavyuoni: “Toba ni wajibu kwa kila dhambi. Ikiwa dhambi alolifanya mja ni baina yake mja na Allaah Aliyetukuka haliingiliani na haki ya binadamu, litakuwa na sharti tatu:



Ya kwanza: Kuacha maasiya.

Ya pili: Kujuta kwa kufanya hayo maasiya.

Ya tatu: Kuazimia kutorudia tena kosa lile milele. Likikosekana sharti moja katika hizi tatu basi toba haitosihi”.



Na ikiwa dhambi lililofanywa lina mafungamano na mwanadamu sharti za kupata toba zinakuwa ni nne: “Sharti hizi tatu zilizotajwa hapa juu na ya nne ni kuirudishia haki ya yule mtu, ikiwa ni mali au kitu chengine chochote umrudishie. Ikiwa umefanya hiyana kwa kulala au kuzini na mke wa mtu inabidi uombe msamaha kwa mume wa huyo mwanamke ili upate toba kutoka kwa Allaah Aliyetukuka kwa dhambi lako hilo.



Ni wajibu kwa Muislamu kutubu (kuomba msamaha) kwa madhambi yote. Ikiwa atatubia baadhi ya dhambi husihi toba yake kwa dhambi ile na zinabaki zile zilizobakia. Zimedhihiri dalili katika Kitabu na Sunnah na Ijma’ ya Ummah katika uwajibu wa toba.



Allaah aliyetukuka amesema: “Na tubuni nyote kwa Allaah, enyi Waumini, ili mpate kufanikiwa” (24: 31).



Na toba inafaa iwe ya sawa na ya kweli kwani Allaah Aliyetukuka Anasema: “Enyi mlioamini! Tubuni kwa Allaah toba iliyo ya kweli” (66: 8).



Na Allaah Anajua zaidi
 
00-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Na Hakika Wewe Uko Juu Ya Kiwango Adhimu Cha Tabia Njema




Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)


00-Na Hakika Wewe Uko Juu Ya Kiwango Adhimu Cha Tabia Njema



www.alhidaaya.com





Hakuna sentensi itakayoweza kuelezea mazuri aliyokuja nayo Nabiy wetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam); utukufu wake, daraja yake, elimu na Risala aliyokuja nao pamoja na upana wa hikma zake, na sifa na akhlaaq (tabia) zake.



Jina lake pekee linatosha kuelezea tabia zake kwani Muhammad maana yake ni "Mwenye kusifiwa." Kwa hiyo bila shaka anamiliki sifa na tabia njema zilizokamilika ambazo hakuna mtu yeyote mwingine aliyemiliki; ni cheo cha daraja ya juu kabisa hakuna atakayeweza kufikia! Na si mwengine aliyemsifia kiumbe huyu bali ni Mwenyewe Allaah ('Azza wa Jalla) Anayesema:

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ﴿٤﴾

Na hakika wewe uko juu ya kiwango adhimu cha tabia njema. [Al-Qalam: 4]



Swahaba Sa'ad bin Hishaam (Radhwiya Allaahu ‘anhu) alipomuuliza Mama wa Waumini 'Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kuhusu tabia ya Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alijibu:

كان خلقه القرآن. ألست تقرأ القرآن (( وَإِنَّكَ لَعَلى خُلُقٍ عَظِيمٍ )) أبو داود والنسائي

Tabia yake ilikuwa ni Qur-aan, kwani husomi katika Qur-aan )) Na hakika wewe uko juu ya kiwango adhimu cha tabia njema. (( [Abu Daawuwd na An-Nasaaiy]



Naye Nabiy (Swalla Allaahu 'alayh wa aalihi wa sallam) akasema:

((إِنَّمَا بُعِثْتُ لِأُتَمِّمَ صَالِحَ الأَخْلاقِ‏))

((Hakika nimetumwa ili nikamilishe khulqa (tabia) njema)) ‏[Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ameipokea Imaam Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy Swahiyh Al-Jaami’ (2349), Swahiyh Al-Adab Al-Mufrad (207)]



Zitakazofuatia ni baadhi ya sifa na akhlaaq ambazo zinazompelekea Nabiy wetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuchukua nafasi adhimu na ya pekee katika ulimwengu huu, pamoja na kuacha athari zake ambazo zimewasisimua na kuwahamasisha watu wengi mno mpaka makafiri wakaingia Uislamu kwazo, na hazitoweza kubadilika wala kufutika hadi Siku ya mwisho; Swalla Allaahu 'alayh wa aalihi wa sallam.



Wabillaahi At-Tawfiyq
 
Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)



01-Alijulikana Kabla Ya Unabii Kuwa Ni Mkweli Na Mwaminifu



www.alhidaaya.com





Khulqah yake ya Asw-Swaadiq (mkweli) na Al-Amiyn (Mwaminifu) ilijulikana kabla ya kupewa Unabii kutokana na ukweli wake na uaminifu wake hata akapewa jina la “Asw-Swaadiqul-Amiyn” (Mkweli Mwaminifu):



1-Maquraysh wa Makkah walipokuwa wakiijenga upya Al-Ka’bah baada ya kutokea mafuriko makubwa yaliyosababisha maji kuingia ndani ya Msikiti na kubomoka, na pindi walipomaliza kujenga, wakataka kuirudisha Al-Hajar Al-Aswad (Jiwe jeusi) katika kona ya Ka’bah. Makabila manne ya ki-Quraysh yalikaribia kupigana vita vikubwa kwa kuzozana nani kati yao anayepaswa kuliweka jiwe hilo katika kona yake. Mvutano huo ukaendelea takriban masiku manne au matano.

Abuu Umayyah bin Mughiyrah Al-Makhzuwmiy ambaye alikuwa mtu mzima wao, akashauri kuwa liwekwe na mtu wa kwanza atakayeingia katika lango la Msikiti, na wote wakaridhika na rai hiyo. Allaah ('Azza wa Jalla) Akajaalia kuwa ni Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aingie na hapo wote wakapiga ukulele: "Huyu Mwaminifu! Sote tumeridhika naye huyu Muhammad."



Naye Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa hikma aliyojaaliwa na Allaah ('Azza wa Jalla) akaamrisha kiletwe kitambaa (kikubwa) kisha iwekwe Al-Hajar Al-Aswad katikati kisha akawataka viongozi wa makabila yote; kila mmoja wao akamate kona moja ya kitambaa hicho kisha wanyanyue kwa pamoja, na walipofikia mahali pa kuliweka, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akainyanyua Al-Hajar Al-Aswad kwa mikono yake miwili na kuiweka katika kona ya Al-Ka’bah. Mzozo ukamalizika na watu wakaridhika. [Ar-Rahiyq Al-Makhtuwm, Muhammad Rahmatul-Lil-’Aalamiyn]





2-Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alipomteremshia amri hii:



وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

Na onya (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) jamaa zako wa karibu. [Ash-Shu’araa: 214]



Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipapanda juu ya jabali Swafaa akawaita watu wake na kuwaambia: "Enyi Maquraysh (na riwaayah nyingine enyi Banuu Manaaf, Enyi Banuu fulani na fulani). Je, ikiwa nitawaambieni kuwa wapanda farasi wapo nyuma ya jabali hili wakijitayarisha kukushambulieni, mtanisadiki?" Wote kwa pamoja wakamjibu:

"Bila shaka tutakusadiki, kwa sababu hatujapata kusikia kutoka kwako isipokuwa maneno ya kweli." Akasema: "Basi mimi ni mwonyaji kwenu juu ya adhabu kali iliyo mbele yenu. Okoeni nafsi zenu kutokana na moto…" [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo kwa riwaayah tofauti]





3-Kauli ya Abu Jahl:



“Wa-Allaahi mimi najua vilivyo kuwa yeye ni Mkweli….Tulikuwa tukimwita katika ujana wake Asw-Swaadiq Al-Amiyn.” (Mkweli Mwaminifu). [Tafsiyr Al-Qurtwubiy]





4-Imepokelewa kutoka kwa Maswahaba mbali mbali wakihadithia Hadiyth za Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakisema: “Amesema Asw-Swaadiq Al-Maswduwq” (mkweli aliyesadikishwa). Mfano ni Hadiyth ya ‘Abdullah bin Mas’uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu):



عن أبي عبْدِ الرَّحْمن عبدِ الله بنِ مسعودٍ رضي الله عنه قال: حدَّثَنا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم وهُوَ الصَّادقُ المَصْدوق: ((إنَّ أَحَدَكُمْ يُجْمَعُ خَلْقُهُ في بَطْنِ أُمِّه أرْبعينَ يوْماً نُطْفَةً، ثُمَّ يَكُونُ عَلَقَةً مِثْلَ ذلك، ثُمَّ يَكُونُ مُضْغَةً مِثْلَ ذلك، ثُمَّ يُرْسَلُ إليه المَلكُ فَيَنْفخُ فيه الرُّوحَ ويُؤمَرُ بأرْبَعِ كلماتٍ: بِكَتْبِ رِزْقِهِ وأَجَلِهِ وعَمَلِهِ وشَقيٌّ أو سَعيدٌ، فَوَاللهِ الَّذي لا إله غَيْرُهُ إنَّ أَحَدَكُمْ ليَعْمَلُ بعَمَلِ أهْلِ الجَنَّةِ حتى ما يكُونَ بَيْنَهُ وبَيْنَها إلا ذِرَاعٌ، فَيَسْبِقُ عَليْه الكِتابُ فَيَعْمَلُ بعَملِ أَهْلِ النَّارِ فَيَدْخُلُها. وإنَّ أَحَدَكُمْ لَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أَهل النَّارِ حتى ما يَكُونَ بَيْنَهُ وبَيْنَها إلا ذِرَاعٌ، فَيَسْبِقُ عَلَيْهِ الكتابُ، فَيَعْمَلُ بِعَمَلِ أهل الجنَّةِ فَيَدْخُلُها)) رواه البخاري ومسلم



Kutoka kwa Abuu 'Abdir-Rahmaan 'Abdillaah bin Mas‘uwd (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: “Ametusimulia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) ambaye ni mkweli mwenye kuaminiwa: “Hakika kila mmoja wenu hukusanywa umbo lake katika tumbo la mama yake siku arubaini akiwa ni mkusanyiko wa mbegu (za uzazi za mama na baba), kisha arubaini zifuatazo huwa ni donge la damu, kisha arubaini zijazo huwa pande la nyama, kisha Allaah Humtuma Malaika kwake na kumpulizia roho (yake). Na (Malaika huyo) anaamrishwa maneno manne; Kuandika rizki yake, ajali yake (umri atakaoishi duniani), amali zake, mtu muovu au mwema. Wa-Allaahi naapa kwa Yule Ambaye hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Yeye, hakika mmoja wenu huenda afanye ‘amali za watu wa Jannah hadi ikawa baina yake na Jannah ni dhiraa na kile kilichoandikwa kikathibiti akafanya ‘amali ya watu wa motoni akaingia motoni. Na mmoja wenu hufanya ‘amali za watu wa motoni hadi ikawa baina yake na moto ni dhiraa na hapo kile kilichoandikwa kikathibiti akafanya ‘amali ya watu wa Jannah akaingia Jannah)) [Al-Bukhaariy na Muslim]



Pia Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Al-Bukhaariy Kitaab Al-Fitan, na wengineo.





5-Allaah ('Azza wa Jalla) Mwenyewe Amethitibisha kuwa ni Asw-Swaadiq (mkweli) Anaposema:



وَالَّذِي جَاءَ بِالصِّدْقِ وَصَدَّقَ بِهِ ۙ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُتَّقُونَ﴿٣٣﴾

Na yule aliyekuja na ukweli na wakausadikisha - hao ndio wenye taqwa. [Az-Zumar: 33]



Amesema Mujaahid na Qataadah na wengineo kuhusu: “Na yule aliyekuja na ukweli” “Huyo ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)” [Tafsiyr Ibn Kathiyr]
 
Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)


02-Akijali Mno Umma Wake Na Akiwakhofia Adhabu



www.alhidaaya.com







Nabiy wetu Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akijali mno Ummah wake huu wa Kiislamu, akikhofia na kujali Waumini wasipatwe na shari au balaa au adhabu yoyote ile. Hadiyth ifuatayo ni dalili mojawapo ya kujali kwake kwa Ummah huu wa Kiislamu:





عنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ، أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم تَلاَ قَوْلَ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ فِي إِبْرَاهِيم: ((‏رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِنَ النَّاسِ فَمَنْ تَبِعَنِي فَإِنَّهُ مِنِّي)) الآيَةَ‏.‏ وَقَالَ عِيسَى عَلَيْهِ السَّلاَمُ:‏ ((إِنْ تُعَذِّبْهُمْ فَإِنَّهُمْ عِبَادُكَ وَإِنْ تَغْفِرْ لَهُمْ فَإِنَّكَ أَنْتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ‏)) فَرَفَعَ يَدَيْهِ وَقَالَ" ((اللَّهُمَّ أُمَّتِي أُمَّتِي)) وَبَكَى فَقَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: يَا جِبْرِيلُ اذْهَبْ إِلَى مُحَمَّدٍ وَرَبُّكَ أَعْلَمُ فَسَلْهُ مَا يُبْكِيكَ فَأَتَاهُ جِبْرِيلُ عَلَيْهِ الصَّلاَةُ وَالسَّلاَمُ فَسَأَلَهُ فَأَخْبَرَهُ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم بِمَا قَالَ‏.‏ وَهُوَ أَعْلَمُ‏.‏ فَقَالَ اللَّهُ يَا جِبْرِيلُ اذْهَبْ إِلَى مُحَمَّدٍ فَقُلْ إِنَّا سَنُرْضِيكَ فِي أُمَّتِكَ وَلاَ نَسُوءُكَ.‏






Amesimulia ‘Abdullaah bin ‘Amru bin Al-‘Aasw (رضي الله عنه): Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alisoma kauli ya Allaah (عزّ وجلّ) kuhusu Nabiy Ibraahiym:



رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ ۖ فَمَن تَبِعَنِي فَإِنَّهُ مِنِّي ۖ

Rabb wangu! Hakika hao (masanamu) wamepoteza watu wengi. Basi atakayenifuata, huyo yuko nami. [Ibraahiym: 36]



Na amesema ‘Iysaa (عليه السلام):



إِن تُعَذِّبْهُمْ فَإِنَّهُمْ عِبَادُكَ ۖ وَإِن تَغْفِرْ لَهُمْ فَإِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١١٨﴾

Ukiwaadhibu, basi bila shaka hao ni Waja Wako, na Ukiwaghufuria basi hakika Wewe Ndiye Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote [Al-Maaidah: 118]



Akanyanyua mikono yake akisema: “Ee Allaah! Ummah wangu! Ummah Wangu! Akalia, kisha Allaah (عزّ وجلّ) Akasema: “Ee Jibriyl! Nenda kwa Muhammad, na Rabb wako Anajua zaidi, kisha muulize kitu kigani kinachomliza? Basi Jibriyl akamwendea (صلى الله عليه وآله وسلم) akamuuliza (sababu ya kulia kwake), na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamjulisha, na Allaah Anajua zaidi, Hapo Allaah Akasema: “Ee Jibriyl! Nenda kwa Muhammad na mwambie: Hakika Sisi Tutaridhia Ummah wako wala Hatutaudhika nawe.” [Muslim]



Imaam An-Nawawiy (رحمه الله) amesema katika Sharh Muslim: “Hadiyth hii imejumuisha aina za faida zikiwemo: Bainisho kamilifu la huruma zake Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa Ummah wake, na kujali kutunza maslahi yao, na kutilia hima mambo yao. Na hii ni bishara adhimu kwa Ummah huu kwamba Allaah (سبحانه وتعالى) Ameuzidishia (Ummah) Sharaf (taadhima) kutokana na ambayo Allaah (سبحانه وتعالى) Amemuahidi Rasuli Wake (صلى الله عليه وآله وسلم) katika kauli Yake: “Tutaridhia Ummah wako wala Hatutaudhika nawe.” Na hii ni Hadiyth itoayo matarajio makubwa kabisa kwa Ummah huu.
 
Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

03-Alisisitiza Mno Ummah Wake Kuhusu Husnul-Khuluq (Tabia Njema)

www.alhidaaya.com





Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesisitiza mno Husnul-Khuluq (tabia njema) katika Hadiyth nyingi, miongoni mwazo ni ambazo zinabashiria Al-Jannah (Pepo) na pia kuwa karibu naye huko Peponi:





1-Aliye na Husnul-Khuluq ni kipenzi cha Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na atakuwa karibu naye Jannah:



عن جابر رضي اللَّه عنه أَن رسول اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال: (( إِن مِنْ أَحَبِّكُم إِليَّ ، وَأَقْرَبِكُمْ مِنِّي مَجلساً يَومَ القِيَامَةِ، أَحَاسِنَكُم أَخلاقا)) الترمذي حديث حسن



Imetoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika walio vipenzi kwangu na watakaokuwa karibu na mimi siku ya Qiyaamah ni wale wenye tabia njema)) [At-Tirmidhiy – Hadiyth Hasan].





2-Taqwa na Husnul-Khulq ndio sababu kuu ya kumwingiza mtu Jannah:



عن أَبِي هُرَيْرَةَ‏:‏ سُئِلَ رَسُولُ اللهِ صلى الله عليه وسلم‏:‏ مَا أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ الْجَنَّةَ‏؟‏ قَالَ‏:‏ ((تَقْوَى اللهِ، وَحُسْنُ الْخُلُقِ)) قَالَ‏:‏ وَمَا أَكْثَرُ مَا يُدْخِلُ النَّارَ‏؟‏ قَالَ‏:‏ ((الأَجْوَفَانِ‏:‏ الْفَمُ وَالْفَرْجُ‏.))



Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa: “Jambo gani zaidi litakalokuwa ni sababu ya kumwingiza mtu Jannah?” Akasema: ((Taqwa (kumcha Allaah) na Husnul-Khuluq (tabia njema)). Na akulizwa: “Jambo gani zaidi litakalokuwa ni sababu ya kumwingiza mtu Motoni?” Akasema; ((Mdomo na sehemu za siri)) [Al-Adab Al-Mufrad, Swahiyh Ibn Maajah (3443)], Swahiyh At-At-Tirmidhiy (2004)]





3-Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amedhamini Jannah kwa anayeacha mabishano na kusema uongo na mwenye khulqa njema:



عَنْ أَبِي أُمَامَةَ البَاهِلي (رضي الله عنه) قَال: قَال رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((أَنَا زَعِيم بَيْت فِي رَبَض الْجَنَّة لِمَنْ تَرَكَ الْمِرَاء وَإِنْ كَانَ مُحِقًّا، وَبِبَيْتٍ فِي وَسَط الْجَنَّة لِمَنْ تَرَكَ الْكَذِب وَإِنْ كَانَ مَازِحًا، وَبِبَيْتٍ فِي أَعْلَى الْجَنَّة لِمَنْ حَسُنَ خُلُقه)) حديث صحيح رواه أبو داود بإسناد صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abu Umaamah Al-Baahiliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mimi ni mdhamini wa nyumba ya kando ya Jannah kwa anayeacha mabishano [wenye shaka] hata kama ni mwenye haki, na ni mdhamini wa nyumba iliyo katikati ya Jannah kwa anayeacha uongo japo ni kwa mzaha, na mdhamini wa nyumba iliyo mahala pa juu zaidi ya Jannah kwa ambaye tabia yake ni njema)). [Hadiyth Swahiyh ameipokea Abu Daawuwd isnaad yake ni Swahiyh]





4-Husnul-Khuluq (tabia njema) inasababisha Miyzaan ya matendo kuwa nzito Siku ya Qiyaamah:



عَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ، عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: (( مَا مِنْ شَىْءٍ أَثْقَلُ فِي الْمِيزَانِ مِنْ حُسْنِ الْخُلُقِ ‏))



Imepokelewa kutoka kwa Abuu Ad-Dardaai kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakuna kitakachokuwa kizito katika Miyzaan kama Husnul-Khuluq [tabia njema])) [Sunan Abiy Daawuwd, As-Silsilah Asw-Swahiyhah ((2/535), Swahiyh Al-Jaami’ 7=5721, Swahiyh Adab Al-Mufrad (204)]





Na pia:



عنْ أَنَسٍ قَالَ لَقِيَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَبَا ذَرٍّ فَقَالَ: ((يَا أَبَا ذَرٍّ أَلا أَدُلُّكَ عَلَى خَصْلَتَيْنِ هُمَا أَخَفُّ عَلَى الظَّهْرِ وَأَثْقَلُ فِي الْمِيزَانِ مِنْ غَيْرِهِمَا)) قَالَ: بَلَى يَا رَسُولَ اللَّهِ . قَالَ: ((عَلَيْكَ بِحُسْنِ الْخُلُقِ وَطُولِ الصَّمْتِ فَوَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ مَا عَمِلَ الْخَلائِقُ عَمَلا أَحَبَّ إِلَى اللَّهِ مِنْهُمَا))



Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokutana na Abuu Dharr alisema: ((Ee Abuu Dharr; je, nikujulishe sifa mbili ambazo ni nyepesi mgongoni mwako na nzito katika kabisa katika Miyzaan kuliko nyinginezo?)) Akasema: “Ndio Ee Rasuli wa Allaah.” Akasema: ((Shikimana na Husnul-Khuluq (tabia njema) na ukae kimya mda mrefu (usiongee upuuzi), kwani Naapa kwa Ambaye nafsi ya Muhammad imo Mikononi Mwake, hakuna 'amali za viumbe Azipendazo Allaah kama hizo mbili)) [Al-Mu’jam Al-Awsatw (7287), At-Targhiyb wat-Tarhiyb ya Al-Mundiriy (3/355) kwa daraja ya Hadiyth Jayyid wasimulizi ni wenye kuaminika]





5-Husnul-Khuluq inazidisha umri wa mtu:



عن عائشة أم المومنينن رضي الله عنها عن النبي صلى الله عليه وسلم: ((...صِلةُ الرَّحِمِ وحُسنُ الخُلُقِ وحُسنُ الجِوارِ يَعمُرانِ الدِّيارَ، ويَزيدانِ في الأعمارِ))

Imepokelewa kutoka kwa Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Kuunga undugu na Husnul-Khuluq (tabia njema) na kumfanyia wema jirani inaamirisha nyumba na inaongeza umri)) [Ahmad na ameisahihisha Al-Albaaniy katika As-Silsilah Asw-Swahiyhah (519), Swahiyh At-Targhiyb (2524)]





6-Iymaan ya mtu haikamilikii ila kwa Husnul-Khuluq (tabia njema):



عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ (رضي الله عنه) قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: ((أَكْمَلُ الْمُؤْمِنِينَ إِيمَانًا أَحْسَنُهُمْ خُلُقًا وَخِيَارُكُمْ خِيَارُكُمْ لِنِسَائِهِمْ خُلُقًا)) الترمذي وقال: حديث حسن صحيح

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muumin aliyekamilika iymaan ni yule aliye na tabia njema kabisa, na wabora wenu ni wale walio bora kwa wake zao kwa tabia)) [At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth Swahiyh Hasan]





Hizo ni baadhi ya Hadiyth nyingi zenye kusisitiza Husnul-Khuluq baina ya watu kwa ujumla, kwa mke na mume, na hata kwa makafiri.
 
Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)



004-Akidhikika Pindi Waumini Wanapopata Shida,

Akiwajali, Mpole Na Mwenye Huruma Mno



www.alhidaaya.com





Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):



لَقَدْ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِكُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِتُّمْ حَرِيصٌ عَلَيْكُم بِالْمُؤْمِنِينَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ﴿١٢٨﴾

Kwa yakini amekujieni Rasuli anayetokana na nyinyi wenyewe, yanamtia mashaka (na huzuni) yanayokutaabisheni, anakujalini, mwenye huruma kwa Waumini ni mwenye huruma mno, mwenye rahmah. [At-Tawbah: 128]



Imaam As-Sa’diy amesema:

لَقَدْ جَاءَكُمْ رَسُولٌ مِّنْ أَنفُسِكُمْ عَزِيزٌ عَلَيْهِ مَا عَنِتُّمْ

Kwa yakini amekujieni Rasuli anayetokana na nyinyi wenyewe, yanamtia mashaka (na huzuni) yanayokutaabisheni.



Yaani: Wanamjua hali yake na wanajimakinisha kuchukua (ujumbe) kutoka kwake wala hawamwendei kinyume katika utiifu, naye ni (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akiwanasihi nasaha nzuri kabisa na akiwaendea mbio kuwafanikishia maslahi yao. Akidhikika na yale yanayokutieni mashaka na yanayokutaabisheni.

حَرِيصٌ عَلَيْكُم بِالْمُؤْمِنِينَ رَءُوفٌ رَّحِيمٌ

anakujalini, mwenye huruma kwa Waumini ni mwenye huruma mno, mwenye rahmah.



Akikupendeleeni khayr na akifanya juhudi kukufikieni hizo khayr na akitilia hima kuongoka kwenu kufikia iymaan na akichukia shari kukufikieni na akifanya juhudi zisikufikieni shari hizo. Mpole na mwenye huruma mno, akiwahurumia kuliko wazazi wao wanavyowahurumia.

[Tafsiyr Imaam As-Sa'dy]



Katika ambayo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) anayojali na kuyakhofia kwa Waumini ni kuwakinga na moto. Kama ilivyothibiti katika Hadiyth:



عَنْ جَابِرٍ، قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((مَثَلِي وَمَثَلُكُمْ كَمَثَلِ رَجُلٍ أَوْقَدَ نَارًا فَجَعَلَ الْجَنَادِبُ وَالْفَرَاشُ يَقَعْنَ فِيهَا وَهُوَ يَذُبُّهُنَّ عَنْهَا وَأَنَا آخِذٌ بِحُجَزِكُمْ عَنِ النَّارِ وَأَنْتُمْ تَفَلَّتُونَ مِنْ يَدِي)) مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mfano wangu na mfano wenu ni kama mtu ambaye anayewasha moto kisha wadudu na nondo wala nguo wakawa wanaanguka humo kisha yeye (huyo mtu) anajaribu kuwatoa humo nami huku nawazuia migongo yao isiangukie katika moto lakini mnateleza mikononi mwangu)) [Muslim]
 
Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)



05-Akiwapendelea Waumini Yaliyo Mepesi Katika ‘Amali Zao Na Katika Da’wah



www.alhidaaya.com





Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliwapendelea Maswahaba kutenda yaliyo mepesi na hakuwatakia wataabike katika ‘amali zao wala katika kutaamuli na watu katika Da’wah. Hadiyth ya Mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amesema:



كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِذَا أَمَرَهُمْ أَمَرَهُمْ مِنَ الأَعْمَالِ بِمَا يُطِيقُونَ قَالُوا: ((إِنَّا لَسْنَا كَهَيْئَتِكَ يَا رَسُولَ اللَّهِ، إِنَّ اللَّهَ قَدْ غَفَرَ لَكَ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ‏.‏ فَيَغْضَبُ حَتَّى يُعْرَفَ الْغَضَبُ فِي وَجْهِهِ ثُمَّ يَقُولُ: ((إِنَّ أَتْقَاكُمْ وَأَعْلَمَكُمْ بِاللَّهِ أَنَا))



Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa anapowaamrisha (Waumini) jambo katika 'amali aliwaamrisha (mepesi) ambayo walikuwa na uwezo nao wakawa wanasema: “Sisi si kama wewe, Allaah Amekughufuria madhambi yako yaliyotangulia na ya baadae.” Akaghadhibika mpaka ghadhabu ikadhihirika usoni mwake kisha akasema: ((Mimi ni mwenye taqwa zaidi yenu, na namjua zaidi Allaah kulikoni nyinyi)) [Al-Bukhaariy]





Na katika Da’wah (ulinganiaji):



عَنْ أَنَسِ (رضي الله عنه) عَنْ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَسِّرُوا وَلاَ تُعَسِّرُوا وَبَشِّرُوا ولاَ تُنَفِّرُوا)) متفق عليه



Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Sahilisheni wala msifanye uzito, wapendekezeni watu khayr na muwabashirie wala msiwakimbize)). [Al-Bukhaariy na Muslim]





Na katika ‘Ibaadah: Hadiyth ya ‘Abdullaah Ibn ‘Amru Ibn Al-‘Aasw:



كُنْتُ أَصُومُ الدَّهْرَ وَأَقْرَأُ الْقُرْآنَ كُلَّ لَيْلَةٍ - قَالَ - فَإِمَّا ذُكِرْتُ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم وَإِمَّا أَرْسَلَ إِلَىَّ فَأَتَيْتُهُ فَقَالَ لِي‏"‏أَلَمْ أُخْبَرْ أَنَّكَ تَصُومُ الدَّهْرَ وَتَقْرَأُ الْقُرْآنَ كُلَّ لَيْلَةٍ‏"‏‏.‏ قُلْتُ بَلَى يَا نَبِيَّ اللَّهِ وَلَمْ أُرِدْ بِذَلِكَ إِلاَّ الْخَيْرَ.‏ قَالَ ‏"‏فَإِنَّ بِحَسْبِكَ أَنْ تَصُومَ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ ثَلاَثَةَ أَيَّامٍ ‏"‏.‏ قُلْتُ يَا نَبِيَّ اللَّهِ إِنِّي أُطِيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ ‏.‏ قَالَ ‏"‏ فَإِنَّ لِزَوْجِكَ عَلَيْكَ حَقًّا وَلِزَوْرِكَ عَلَيْكَ حَقًّا وَلِجَسَدِكَ عَلَيْكَ حَقًّا - قَالَ - فَصُمْ صَوْمَ دَاوُدَ نَبِيِّ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَإِنَّهُ كَانَ أَعْبَدَ النَّاسِ"‏‏.‏ قَالَ قُلْتُ يَا نَبِيَّ اللَّهِ وَمَا صَوْمُ دَاوُدَ قَالَ ‏"‏كَانَ يَصُومُ يَوْمًا وَيُفْطِرُ يَوْمًا‏"‏.‏ قَالَ ‏"‏وَاقْرَإِ الْقُرْآنَ فِي كُلِّ شَهْرٍ‏"‏ ‏.‏ قَالَ قُلْتُ يَا نَبِيَّ اللَّهِ إِنِّي أُطِيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ قَالَ ‏"‏ فَاقْرَأْهُ فِي كُلِّ عِشْرِينَ "‏‏.‏ قَالَ قُلْتُ يَا نَبِيَّ اللَّهِ إِنِّي أُطِيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ قَالَ ‏"‏فَاقْرَأْهُ فِي كُلِّ عَشْرٍ‏"‏ ‏.‏ قَالَ قُلْتُ يَا نَبِيَّ اللَّهِ إِنِّي أُطِيقُ أَفْضَلَ مِنْ ذَلِكَ ‏.‏ قَالَ ‏"‏ فَاقْرَأْهُ فِي كُلِّ سَبْعٍ وَلاَ تَزِدْ عَلَى ذَلِكَ ‏.‏ فَإِنَّ لِزَوْجِكَ عَلَيْكَ حَقًّا وَلِزَوْرِكَ عَلَيْكَ حَقًّا وَلِجَسَدِكَ عَلَيْكَ حَقًّا"‏.‏ قَالَ فَشَدَّدْتُ فَشُدِّدَ عَلَىَّ.‏ قَالَ وَقَالَ لِيَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏"‏إِنَّكَ لاَ تَدْرِي لَعَلَّكَ يَطُولُ بِكَ عُمْرٌ"‏.‏ قَالَ فَصِرْتُ إِلَى الَّذِي قَالَ لِيَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا كَبِرْتُ وَدِدْتُ أَنِّي كُنْتُ قَبِلْتُ رُخْصَةَ نَبِيِّ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم.‏



“Nilikuwa nikifunga mwaka mzima, na nikisoma Qur-aan kila usiku. Alipojulishwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniita kwake nikaenda. Akasema: ((Nimesikia kwamba unafunga (Swawm) mwaka mzima na unasoma (unakhitimisha) Qur-aan kila usiku?)) Nikasema: Ndio ee Rasuli wa Allaah. Wala sitaki lolote ila khayr tu. Akasema: ((Inakutosheleza ukifunga katika kila mwezi siku tatu…)) Kisha akasema: ((Na usome Qur-aan (ukhitimishe) kila mwezi)). Akasema: Nikasema: Ee Rasuli wa Allaah, mimi hakika naweza kufanya vizuri zaidi ya hivyo. Akasema: ((Basi soma katika siku saba na usizidishe juu ya hivyo, kwani mke wako ana haki na wewe, na wageni wako wana haki kwako, na mwili wako una haki kwako)). Akasema: Kila nikimkazania (nizidishe ‘ibaadah) alikuwa akinikazania (nipunguze). Akasema: Akaniambia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Huenda umri ukawa mrefu kwako)) Nikaendeleza (‘ibaadah) kama alivyoniambia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Nilipokuwa mkubwa kiumri nilipendelea kufuata rukhsa aliyonipa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo]
 

06-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Miongoni Mwa Hayaa Zake Alimsitahi Allaah Alipofaradhisha Swalaah Tano​

sifa_akhlaq_nabiy.png

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
06-Miongoni Mwa Hayaa Zake Alimsitahi Allaah Alipofaradhisha Swalaah Tano
www.alhidaaya.com


Pindi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipopandishwa mbinguni siku ya Israa Wal-Mi’raaj ambako ndipo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Alimfaradhishia nguzo ya Swalaah kwa Waislamu, na wakati alipopewa amri hiyo ya Swalaah akiwa anarejea, Nabiy Muwsaa ('Alayhis-Salaam) akamtaka arudi kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ili zipunguzwe hizo Swalaah tano, lakini Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimstahi Rabb wake (‘Azza wa Jalla). Hadiyth ifuatayo imethibitisha:

أَنَسُ بْنُ مَالِكٍ وَابْنُ حَزْمٍ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((فَرَضَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ عَلَى أُمَّتِي خَمْسِينَ صَلاَةً فَرَجَعْتُ بِذَلِكَ حَتَّى أَمُرَّ بِمُوسَى عَلَيْهِ السَّلاَمُ فَقَالَ: مَا فَرَضَ رَبُّكَ عَلَى أُمَّتِكَ؟ قُلْتُ فَرَضَ عَلَيْهِمْ خَمْسِينَ صَلاَةً‏.‏ قَالَ لِي مُوسَى: فَرَاجِعْ رَبَّكَ عَزَّ وَجَلَّ فَإِنَّ أُمَّتَكَ لاَ تُطِيقُ ذَلِكَ‏.‏ فَرَاجَعْتُ رَبِّي عَزَّ وَجَلَّ فَوَضَعَ شَطْرَهَا فَرَجَعْتُ إِلَى مُوسَى فَأَخْبَرْتُهُ فَقَالَ: رَاجِعْ رَبَّكَ فَإِنَّ أُمَّتَكَ لاَ تُطِيقُ ذَلِكَ.‏ فَرَاجَعْتُ رَبِّي عَزَّ وَجَلَّ فَقَالَ: هِيَ خَمْسٌ وَهِيَ خَمْسُونَ لاَ يُبَدَّلُ الْقَوْلُ لَدَىَّ‏.‏ فَرَجَعْتُ إِلَى مُوسَى فَقَالَ رَاجِعْ رَبَّكَ فَقُلْتُ قَدِ اسْتَحْيَيْتُ مِنْ رَبِّي عَزَّ وَجَلَّ))

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik na Ibn Hazm kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Allaah ('Azza wa Jalla) Alifaradhisha Swalaah khamsini kwa Ummah wangu, nikazikubali na nikarejea hadi nilipopita kwa Muwsaa ('Alayhis-Salaam) ambaye alisema: Je, Rabb wako Amekufaradhishia nini kwa Ummah wako? Nikasema: Amewafaridhisha Swalaah khamsini. Muwsaa akaniambia: Rudi kwa Rabb wako ‘Azza wa Jalla kwani ummah wako hawatoziweza hizo. Nikamrejea Rabb wangu Allaah ('Azza wa Jalla) Naye Akanipunguzia idadi zake, nikarudi kwa Muwsaa nikamwelezea akasema: Rudi kwa Rabb wako kwani ummah wako hawatoziweza hizo. Nikarudi kwa Rabb wangu Allaah ('Azza wa Jalla) Akasema: Hizo (Swalaah) ni tano lakini ni thawabu khamisini na Kauli Yangu haibadiliki. Nikarudi kwa Muwsa akasema: Rudi kwa Rabb wako. Nikasema: Hakika namstahi Rabb wangu Allaah 'Azza wa Jalla)) [A-Nasaaiy, Ibn Maajah na katika riwaayah ndefu ya Al-Bukhaariy]
 

07-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Miongoni Mwa Hayaa Zake: Alikuwa Akiwastahi Maswahaba Zake Kuwaambia Waondoke Nyumbani Kwake​


sifa_akhlaq_nabiy.png

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

07-Miongoni Mwa Hayaa Zake:
Alikuwa Akiwastahi Maswahaba Zake Kuwaambia Waondoke Nyumbani Kwake

www.alhidaaya.com


Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mwenye kustahi na kuona hayaa mno na amethibitisha hayo Swahaba wake mtukufu:
عَنْ أَبِي سَعِيدٍ الْخُدْرِيِّ رضى الله عنه قَالَ كَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم أَشَدَّ حَيَاءً مِنَ الْعَذْرَاءِ فِي خِدْرِهَا‏.‏
Abuu Sa’iyd Al-Khudriyy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: “Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mwenye kuona hayaa mno kuliko msichana asiyevunja ungo.” [Al-Bukhaariy, na Muslim]


Alisitahi na kuona hayaa kuwataka Maswahaba waondoke siku ya Nikaah yake na Mama wa Waumini Zaynab bint Jahsh, siku ambayo palikuwa na karamu nyumbani kwake. Maelezo kama yalivyokuja katika Hadiyth kwenye Al-Bukhaariy:

عَنْ أَنَسٍ رضى الله عنه قَالَ: "بُنِيَ عَلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم بِزَيْنَبَ ابْنَةِ جَحْشٍ بِخُبْزٍ وَلَحْمٍ فَأُرْسِلْتُ عَلَى الطَّعَامِ دَاعِيًا فَيَجِيءُ قَوْمٌ فَيَأْكُلُونَ وَيَخْرُجُونَ، ثُمَّ يَجِيءُ قَوْمٌ فَيَأْكُلُونَ وَيَخْرُجُونَ، فَدَعَوْتُ حَتَّى مَا أَجِدُ أَحَدًا أَدْعُو فَقُلْتُ: يَا نَبِيَّ اللَّهِ مَا أَجِدُ أَحَدًا أَدْعُوهُ، قَالَ: ((ارْفَعُوا طَعَامَكُمْ)) وَبَقِيَ ثَلاَثَةُ رَهْطٍ يَتَحَدَّثُونَ فِي الْبَيْتِ، فَخَرَجَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم فَانْطَلَقَ إِلَى حُجْرَةِ عَائِشَةَ فَقَالَ: ((السَّلاَمُ عَلَيْكُمْ أَهْلَ الْبَيْتِ وَرَحْمَةُ اللَّهِ)) فَقَالَتْ: وَعَلَيْكَ السَّلاَمُ وَرَحْمَةُ اللَّهِ، كَيْفَ وَجَدْتَ أَهْلَكَ بَارَكَ اللَّهُ لَكَ؟ فَتَقَرَّى حُجَرَ نِسَائِهِ كُلِّهِنَّ، يَقُولُ لَهُنَّ كَمَا يَقُولُ لِعَائِشَةَ، وَيَقُلْنَ لَهُ كَمَا قَالَتْ عَائِشَةُ، ثُمَّ رَجَعَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم فَإِذَا ثَلاَثَةُ رَهْطٍ فِي الْبَيْتِ يَتَحَدَّثُونَ، وَكَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم شَدِيدَ الْحَيَاءِ، فَخَرَجَ مُنْطَلِقًا نَحْوَ حُجْرَةِ عَائِشَةَ فَمَا أَدْرِي آخْبَرْتُهُ أَوْ أُخْبِرَ أَنَّ الْقَوْمَ خَرَجُوا، فَرَجَعَ حَتَّى إِذَا وَضَعَ رِجْلَهُ فِي أُسْكُفَّةِ الْبَابِ دَاخِلَةً وَأُخْرَى خَارِجَةً أَرْخَى السِّتْرَ بَيْنِي وَبَيْنَهُ، وَأُنْزِلَتْ آيَةُ الْحِجَابِ" البخاري

Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba iliandaliwa karamu ya mkate kwa nyama siku ya Nikaah ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Zaynab bint Jahsh, nikatumwa kualika watu (wahudhurie karamu), basi watu wakaanza kuhudhuria (kwa makundi). Wakawa wanakula na kuondoka. Kundi lingine likawa linahudhuria kula na kuondoka. Nikaendelea kualika watu mpaka nikakosa tena watu wa kuwaalika. Nikasema: Ee Nabiy wa Allaah! Sipati tena watu wa kuwaalika! Akasema: ((Chukua chakula kilichobakia)). Kisha kundi la watu watatu wakawa wamebakia nyumbani kwake wakipiga gumzo. Nabiy wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaondoka kwenda chumbani kwa ‘Aaishah akasema: ((Assalaamu ‘Alaykum Ahlal-Bayt wa RahmatuLLaah)). Akajibu: “Wa ‘Alaykas-Salaam wa RahmatuLLaah. Je, umemkutaje mke wako Baaraka Allaahu Laka?” Kisha akaingia vyumbani mwa wake zake wote na akawaambia vile vile kama alivyomwambia ‘Aaishah nao wakasema vile vile kama alivyosema ‘Aaishah. Kisha Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akarudi na kukuta kundi la wale watu watatu bado wangaliko wakiwa wanapiga gumzo. Nabiy wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa ni mtu mwenye kuona hayaa mno basi akatoka nje (kwa mara ya pili) kisha akaingia chumbani mwa ‘Aaishah. Sikumbuki kama nilimjulisha kuwa watu wameshaondoka. Akarudi na pindi alipofikia tu mlangoni, akavuta pazia baina yangu na yake, hapo Aayah ya hijaab ikateremshwa.” [Al-Bukhaariy]

Aayah hizo ziloteremshwa ni:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتَ النَّبِيِّ إِلَّا أَن يُؤْذَنَ لَكُمْ إِلَىٰ طَعَامٍ غَيْرَ نَاظِرِينَ إِنَاهُ وَلَـٰكِنْ إِذَا دُعِيتُمْ فَادْخُلُوا فَإِذَا طَعِمْتُمْ فَانتَشِرُوا وَلَا مُسْتَأْنِسِينَ لِحَدِيثٍ ۚ إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ يُؤْذِي النَّبِيَّ فَيَسْتَحْيِي مِنكُمْ ۖ وَاللَّـهُ لَا يَسْتَحْيِي مِنَ الْحَقِّ ۚ وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ۚ ذَٰلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ ۚ وَمَا كَانَ لَكُمْ أَن تُؤْذُوا رَسُولَ اللَّـهِ وَلَا أَن تَنكِحُوا أَزْوَاجَهُ مِن بَعْدِهِ أَبَدًا ۚ إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمًا ﴿٥٣﴾
Enyi walioamini! Msiingie nyumba za Nabiy isipokuwa mkipewa idhini ya kwenda kula si kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni, na mkimaliza kula, tawanyikeni, na wala msikae kujiliwaza kwa mazungumzo. Hakika hiyo ilikuwa inamuudhi Nabiy, naye anakustahini, lakini Allaah Hasitahi (kubainisha) haki. Na mnapowauliza wake zake haja, waulizeni nyuma ya pazia. Hivyo ni utwaharifu zaidi kwa nyoyo zenu na nyoyo zao. Na haipasi kwenu kumuudhi Rasuli wa Allaah. Na wala kuwaoa wake zake baada yake abadani. Hakika jambo hilo mbele ya Allaah ni kubwa mno.

إِن تُبْدُوا شَيْئًا أَوْ تُخْفُوهُ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴿٥٤﴾
Mkidhihirisha kitu chochote au mkikificha, basi hakika Allaah daima ni Mjuzi wa kila kitu.

لَّا جُنَاحَ عَلَيْهِنَّ فِي آبَائِهِنَّ وَلَا أَبْنَائِهِنَّ وَلَا إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ أَخَوَاتِهِنَّ وَلَا نِسَائِهِنَّ وَلَا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ ۗ وَاتَّقِينَ اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدًا ﴿٥٥﴾
Si dhambi juu yao wanawake kuonana na baba zao, na wala watoto wao wa kiume, na wala kaka zao, na wala watoto wa kiume wa kaka zao, na wala watoto wa kiume wa dada zao, na wala wanawake wenzao (wa Kiislamu), na wala iliyowamiliki mikono yao ya kulia. Na mcheni Allaah. Hakika Allaah daima ni Mwenye kushuhudia kila kitu.
[Al-Ahzaab: 53-55]
 
Skip to main content
slogan_mobile.png

Ukurasa Wa Kwanza

Search form​




Ukurasa Wa Kwanza /Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Kwa Ujumla /08-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Miongoni Mwa Hayaa Zake Alistahi Maswahaabiyaat Katika Kuwaelekeza Jinsi Ya Kutwaharisha Hedhi

08-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Miongoni Mwa Hayaa Zake Alistahi Maswahaabiyaat Katika Kuwaelekeza Jinsi Ya Kutwaharisha Hedhi​

sifa_akhlaq_nabiy.png

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

00-Miongoni Mwa Hayaa Zake Alistahi Maswahaabiyaat
Katika Kuwaelekeza Jinsi Ya Kutwaharisha Hedhi

www.alhidaaya.com



Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alimstahi mwanamke aliyemjia kumuuliza swala la hedhi yake, basi kwa kusitahi, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alifunika uso wake baada ya kumjibu mwanamke huyo. Hadiyth inaelezea:

عَنْ عَائِشَةَ، قَالَتْ سَأَلَتِ امْرَأَةٌ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَيْفَ تَغْتَسِلُ مِنْ حَيْضَتِهَا قَالَ فَذَكَرَتْ أَنَّهُ عَلَّمَهَا كَيْفَ تَغْتَسِلُ ثُمَّ تَأْخُذُ فِرْصَةً مِنْ مِسْكٍ فَتَطَهَّرُ بِهَا ‏.‏ قَالَتْ كَيْفَ أَتَطَهَّرُ بِهَا قَالَ: ((تَطَهَّرِي بِهَا ‏.‏ سُبْحَانَ اللَّهِ)) ‏.‏ وَاسْتَتَرَ - وَأَشَارَ لَنَا سُفْيَانُ بْنُ عُيَيْنَةَ بِيَدِهِ عَلَى وَجْهِهِ قَالَ: قَالَتْ عَائِشَةُ وَاجْتَذَبْتُهَا إِلَىَّ وَعَرَفْتُ مَا أَرَادَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم فَقُلْتُ تَتَبَّعِي بِهَا أَثَرَ الدَّمِ ‏.‏ وَقَالَ ابْنُ أَبِي عُمَرَ فِي رِوَايَتِهِ فَقُلْتُ تَتَبَّعِي بِهَا آثَارَ الدَّمِ ‏.‏
Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) ambaye amesema: Mwanamke alimuuliza Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) vipi kuoga kujitwaharisha baada ya kumaliza hedhi yake. Akataja kuwa alimfundisha vipi kuoga kisha akamwambia achukue kipande cha pamba aweke misk kwa ajili ya kujitwaharisha. Aksema: Vipi nijitwaharishe nacho? Akasema: ((Jitwaharishe nacho Subhaana Allaah!)) (Nabiy Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akajifunika uso wake. Sufyaan bin ‘Uyaynah akaonyesha jinsi alivyojifunika uso wake. Akasema ‘Aaishah: Nikamvuta mwanamke kwangu kwani nilifahamu alivyokusudia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), nikasema: Pakaza pamba hiyo katika sehemu zenye athari ya damu. Na Ibn ‘Umar katika Hadiyth yake (ametaja maneno ya ‘Aaishah) Pakaza katika sehemu zenye athari ya damu. [Muslim]
 

09-Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Mtu Bora Kabisa, Mkarimu Mno Na Shujaa​

Sifa Na Akhlaaq Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
09-Mtu Bora Kabisa, Mkarimu Mno Na Shujaa
www.alhidaaya.com


عَنْ أَنَسٍ، رضى الله عنه قَالَ كَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم أَحْسَنَ النَّاسِ وَأَشْجَعَ النَّاسِ وَأَجْوَدَ النَّاسِ، وَلَقَدْ فَزِعَ أَهْلُ الْمَدِينَةِ، فَكَانَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم سَبَقَهُمْ عَلَى فَرَسٍ، وَقَالَ: ((وَجَدْنَاهُ بَحْرًا))
Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa mtu bora kabisa, shujaa kabisa na mkarimo mno kuliko watu wengineo. Pindi watu wa Madiyna walipofazaika (kwa khofu), Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipanda farasi akatangulia mbele yao na akasema: ((Tumempata farasi huyu haraka kabisa)) [Al-Bukhaariy]

Na katika Hadiyth nyengine:

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَحْسَنَ النَّاسِ وَكَانَ أَجْوَدَ النَّاسِ وَكَانَ أَشْجَعَ النَّاسِ وَلَقَدْ فَزِعَ أَهْلُ الْمَدِينَةِ ذَاتَ لَيْلَةٍ فَانْطَلَقَ نَاسٌ قِبَلَ الصَّوْتِ فَتَلَقَّاهُمْ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ رَاجِعًا وَقَدْ سَبَقَهُمْ إِلَى الصَّوْتِ وَهُوَ عَلَى فَرَسٍ لِأَبِي طَلْحَةَ عُرْيٍ فِي عُنُقِهِ السَّيْفُ وَهُوَ يَقُولُ" ((لَمْ تُرَاعُوا لَمْ تُرَاعُوا)) قَالَ: ((وَجَدْنَاهُ بَحْرًا)) أَوْ ((إِنَّهُ لَبَحْرٌ)) .‏ قَالَ: وَكَانَ فَرَسًا يُبَطَّأُ مسلم

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa mtu bora kabisa, na mkarimu mno kuliko watu wengineo, na shujaa kabisa. Usiku mmoja, watu wa Madiynah walifazaika kwa khofu (ya mshindo wa sauti). Wakatoka watu kuelekea mshindo wa sauti lakini Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alishafika kabla yao sehemu ya sauti hiyo, akakutana nao akasema: ((Msikhofu! Msikhofu!)) Naye alikuwa amepanda farasi wa Abuu Twalhah, farasi huyo alikuwa hana tandiko lake na shingoni mwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kulikuwa na panga akasema: ((Nimeshampata farasi kwa haraka kama (kasi ya mawimbi ya) bahari)) Au ((Hakika hiyo (sauti ya mshindo) ni (mfoko wa) bahari)) [Al-Bukhaariy]
 
Back
Top Bottom